Dei Gratia Rex
JF-Expert Member
- Sep 13, 2024
- 423
- 696
Na Nairobi ina maanisha nini.
Kwa anaejua.
Kwa anaejua.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Brunei pia inaitwa DarusalaamNini maana ya Dar es Salaam?
Nimeona jina hili linatumika pia kwenye nchi kadhaa duniani hasa za Kiarabu.
Oh kweli ase.Brune pia inaitwa Darusalaam
Sehemu ya Amani
Brunei sorryOh kweli ase.
Utumwa utakuwa kichwani kwako vile unajiona mtumwa na utatenda sawa na watumwa mbele ya waarabu hadi leo.
Jina linabaki kama utambulisho wa mtu au mahali ili watu wapatofautishe na mahali pengine. Nani aliipa jina hiyo sehemu inabaki kuwa historia. Tulikuwa na stendi ya mkoani inaitwa Mbezi Luis sasa hivi ni Magufuli na watu wamekubali jina hilo kuwa ni kituo cha kukutania kwa safari au mambo mengine.
Ukiwa na akili ya kitumwa utawaza kila kitu kwa mtizamo wa kitumwa. Au maskini kwa mtizamo wa kimaskini. Badili mtizamo.
Mfano.
Bwagamoyo........ Bagamoyo.
Watumwa walibwaga mioyo yao wakiingia kwenye boti kwenda utumwani.
Saa Dani...... Saa ndani.
Mwarabu akiishi eneo ilipo hifadhi ya Saadani kwa sasa alikuwa akiwajibu watu wanaomuuliza ni muda gani sasa, yeye anajibu saa dani yaani saa ipo ndani.
Msasani .......... Musa Hasani
Eneo hili akiishi ndugu mmoja akiitwa Musa Hasani. Ndipo pakawa maarufu Msasani.
Mnyamani....... Mwinyi Amani
Soko la Buguruni Mnyamani likipewa jina la mtu maarufu hapo Mwinyi Amani.
Nhobora .......... Tabora
Hinyanga.......... Shinyanga
Ng'wanza ........ Mwanza
Geta ............ Geita
Gahama ....... Kahama
Idodomya...... Dodoma
Ukiangalia yote hayo majina ya upande wa kushoto ya asili yana maana, lakini yalikuja kubadilishwa na wageni kwasababu ya kushindwa kutamka kwa Lugha za wenyeji. Lakini vile wao ndio walikuwa watawala enzi hizo ilibidi vitabu viandikwe kwa kufuata maelekezo yao. Ni sawa na leo flyover ya Ubungo tunaiita Kijazi kwa kuwa watawala waliamua iwe hivo.
Futa utumwa kichwani ufurahie maisha.
Sasa mpaka hapo ushakubali kulikuwa na ngome ya Wajerumani.Hili jengo la sasa la Ikulu inasemwa lilijengwa na British architect John Sinclair baada ya ngome ya Mjerumani kuharibiwa.
Hakuna uthibitisho wa hiyo ikulu kama ilivyo kuwepo hapo kabla ya Wakoloni wa Ujerumani au Uingereza. Hili suala nalichukulia kama ilivyokuwa Ikulu ya Dodoma kabla Magufuli hajajenga hii ya sasa jinsi ilivyo, Chamwino kulikuwa na Ikulu kabla ya Magufuli lakini anayechukuliwa kujenga Ikulu ya Dodoma ni Magufuli.Ukianzia historia ya Dar 1891 kuna miaka karibu 30 ushairuka hapo.
Sultan Majjid alinunua kipande hicho cja kutoka Magogoni mpaka Aga Khan kutoka kwa famikia ya Tambaza tangu alivyoingia huko 1860s.
Sasa Mjerumani kajenga vipi Ikulu hapo wakati hilo jengo la Ikulu lilikuwapo kabla Mjerumani hajafika hapo?
Hii dhana ya kufanya mambo kisa flani alifanya ni namna mufilisi kabisa ya kutetea hoja.Bombay ilibadilishwa kuwa Mumbai,
Harare zamani ilikuwa Fort Saalisbury
Instanbul zamani ilikuwa Constantinople
Gold Coast ilibadilishwa kuwa Ghana
Toronto ilikuwa York zamani
kamuite mtoto wako "abeed" jina lililotumika kuwaita watumwa weusi,Kuacha kuhakikisha vitu vya msingi kama maji kutoka 24/7/365 days na kuongeza barabara za ring road plus kupanga mji ili kulifungua jiji wewe unalilia vitu vya ajabu kama Jina.Sasa ukibadili jina unapata nini wakati mnashida kibao zinawazonga.Waafrika ni lini mtaweza kuadress critical issues na kuachana na INFERIORITY COMPLEX.
Mawazo mfu, mnawaza kubadilisha majengo na vitu majina baadae mnasifia kuwa mnaleta maendeleo. Wenzenu waliwaza kujenga SGR, Kufufua Air Tanzania, kujenga uwanja wa msalato, kujenga Ikulu mpya Dodoma, kujenga mji wa Serikali Dodoma na JNHEPP. Jina hata wewe unaweza kubadilisha ila halifuti jina la awali kwa wale waliokufahamu tangu awali.Tukiangalia majina karibia yote ya mikoa yana asili ya hapa kwetu iweje ni sehemu moja tu bado tumengangania jina la kikoloni lenye historia ya kitumwa ?
Jina la jiji kubwa zaidi Afrika Mashariki "Dar Es Salaam" lilipewa na Sultani Majid bin Said
Kabla ya hapo, eneo hilo lilikuwa kijiji kidogo cha wavuvi kilichoitwa Mzizima, neno lenye maana ya "mji wenye afya."
Sultani Majid alikuwa akifanya biashara ya kikatili ya utumwa iliyomtajirisha, Bandari aliyotumia aliisifia kwa kuiita Dar Es Salaam, kwa tafsiri ya kiswahili ni bandari salama, alisafirisha babu na bibi bila bugudha ndio maana akapaita Dar Es salaam, sehemu ambazo babu zetu walifikia wamechapwa sana mijeredi, wamelimishwa sana mashambani, walioenda nchi walizotokea masultan hali ilikuwa mbaya walikatwa viungo vya uzazi ndio maana ni ngumu kukuta wajukuu zao, utaowakuta ni waafrika waliohamia kuanzia miaka ya 70s
View attachment 3250594
Itapendeza zaidi paitwe MZIZIMA
Basi Wajerumani walijenga kwa ukubwa na ufahari zaidi kuliko vijengo walivyovikuta hapo ndio maana wanachukuliwa kama wajenzi wa hiyo Ikulu.Sasa mpaka hapo ushakubali kulikuwa na ngome ya Wajerumani.
Na Wajerumani nao walikuta jengo la Waarabu alilojenga Sultan Majjid. Hapo Ikuku Dar palikuwa na jengo la chuo cha kujifunza Uislamu hapo.
Katika uzi wake kuna maneno 11 ya kiarabu aliyoyatumiaVipi na kiswahili?
Tuondoe na maneno yote yaliyoletwa na Hao masultan?
Pathetic
Hiyo Ikulu kama ilivyo leo hata huyo Mjerumani na Muingereza hawajaijenga hivyo.Hakuna uthibitisho wa hiyo ikulu kama ilivyo kuwepo hapo kabla ya Wakoloni wa Ujerumani au Uingereza. Hili suala nalichukulia kama ilivyokuwa Ikulu ya Dodoma kabla Magufuli hajajenga hii sasa jinsi ilivyo, Chamwino kulikuwa na Ikulu kabla ya Magufuli lakini anayechukuliwa kujenga Ikulu ya Dodoma ni Magufuli.
Basi Wajerumani walijenga kwa ukubwa na ufahari zaidi kuliko vijengo walivyovikuta hapo ndio maana wanachukuliws kama wajenzi wa hiyo Ikulu.
Rais gani amejenga Ikulu ya Dodoma?Hiyo Ikulu kama ilivyo leo hata huyo Mjerumani na Muingereza hawajaijenga hivyo.
Hata Nyerere, Mwinyi na Mkapa hawajaijenga hivyo.
So where do you draw the line and how?
Utumwa utakuwa kichwani kwako vile unajiona mtumwa na utatenda sawa na watumwa mbele ya waarabu hadi leo.Jina la jiji kubwa zaidi Afrika Mashariki "Dar Es Salaam" lilipewa na Sultani Majid bin Said, Jina hili linatokana na kiarabu lugha aliyotumia Sultan
Kabla ya hapo, eneo hilo lilikuwa kijiji kidogo cha wavuvi kilichoitwa Mzizima, neno lenye maana ya "mji wenye afya."
Dar es salaam ina maana ya Bandari Salama, kwa muda huo Sultan aliitumia bandari kufanya biashara ya kikatili ya kusafirisha babu zetu kwenda kutumikishwa kitumwa. Bandari aliyotumia haikuwa na bugudha, ilikuwa ni salama kwake na ilimtajirisha zaidi kupitia babu zetu.
Ni sawa na mbakaji anaeteka watoto wanaopita kwenye korongo, sehemu hio ikiwa ni salama kwake ataiita korongo salama, itashangaza sana baada ya mtu huyo kudhibitiwa watu waendelee kupaita korongo salama.
Kuita jiji hili kubwa kwa jina la Sultan kunaambatana na kumbukumbu za historia yetu chungu ya utumwa wa masultan waliokuwa vinara wa biashara ya utumwa, Babu zetu walipelekwa kulimishwa kimabavu mashamba ya Zanzibar, walioenda nchi walizotokea masultan hali ilikuwa mbaya walikatwa viungo vya uzazi ndio maana ni ngumu kukuta wajukuu zao kama Marekani, utaowakuta ni waliohamia kuanzia miaka ya 70s
View attachment 3250594
Itapendeza zaidi paitwe MZIZIMA
Bunjumbula tena mkuuJiji la hovyo sana .mpangilio wa makazi ni hovyo.Tunazidiwa na jiji zuri la Kigali na Bunjumbula
Mkuu mimi nimeuliza legacy ya Sultan Majjid kuonyesha alifanya cha maana Dar Es Salaam kuweza kuchukuliwa kama mwanzilishi wa mji, hata Ikulu yenyewe haiwezi kuwa legacy yenye uzito ya maana. Wakoloni wazungu tunaona walianzisha mipango miji, administrative structures, ujenzi wa miondombinu(majengo, bandari na reli), shule n.k Sultan yeye legacy yake ilikuwa ni nini kusema ameanzisha mji wa Dar es Salaam??Sawa.
Ukikubali point hii utakuwa umekubali pia kuwa Sultan Majjid alikuta kijiji cha Mzizima akajenga kwa ukubwa na ufahari zaidi mji wa Dar es salaam.
Checkmate.
Hayo majina mengi uliyoweka yana asili ya hapa kwetu nakuongezea na Mbeya ilikuwa inaitwa Ibheya, maana yake mji wenye chumvi, Nairobi hapo kenya neno la kimasai lenye maana Maji baridi,Utumwa utakuwa kichwani kwako vile unajiona mtumwa na utatenda sawa na watumwa mbele ya waarabu hadi leo.
Jina linabaki kama utambulisho wa mtu au mahali ili watu wapatofautishe na mahali pengine. Nani aliipa jina hiyo sehemu inabaki kuwa historia. Tulikuwa na stendi ya mkoani inaitwa Mbezi Luis sasa hivi ni Magufuli na watu wamekubali jina hilo kuwa ni kituo cha kukutania kwa safari au mambo mengine.
Ukiwa na akili ya kitumwa utawaza kila kitu kwa mtizamo wa kitumwa. Au maskini kwa mtizamo wa kimaskini. Badili mtizamo.
Mfano.
Bwagamoyo........ Bagamoyo.
Watumwa walibwaga mioyo yao wakiingia kwenye boti kwenda utumwani.
Saa Dani...... Saa ndani.
Mwarabu akiishi eneo ilipo hifadhi ya Saadani kwa sasa alikuwa akiwajibu watu wanaomuuliza ni muda gani sasa, yeye anajibu saa dani yaani saa ipo ndani.
Msasani .......... Musa Hasani
Eneo hili akiishi ndugu mmoja akiitwa Musa Hasani. Ndipo pakawa maarufu Msasani.
Mnyamani....... Mwinyi Amani
Soko la Buguruni Mnyamani likipewa jina la mtu maarufu hapo Mwinyi Amani.
Nhobora .......... Tabora
Hinyanga.......... Shinyanga
Ng'wanza ........ Mwanza
Geta ............ Geita
Gahama ....... Kahama
Idodomya...... Dodoma
Ukiangalia yote hayo majina ya upande wa kushoto ya asili yana maana, lakini yalikuja kubadilishwa na wageni kwasababu ya kushindwa kutamka kwa Lugha za wenyeji. Lakini vile wao ndio walikuwa watawala enzi hizo ilibidi vitabu viandikwe kwa kufuata maelekezo yao. Ni sawa na leo flyover ya Ubungo tunaiita Kijazi kwa kuwa watawala waliamua iwe hivo.
Futa utumwa kichwani ufurahie maisha