Bado tupo utumwani? kwanini tunasita kubadili jina la jiji kubwa zaidi Afrika mashariki

Bado tupo utumwani? kwanini tunasita kubadili jina la jiji kubwa zaidi Afrika mashariki

kamuite mtoto wako "abeed" jina lililotumika kuwaita watumwa weusi,

Tuna matatizo ya muhimu kama maji, jina lolote linaweza kumfaa mwanao
Wewe unashida mahali ebu nenda kamuone daktari kwa ushauri zaidi😀

Ukute bado unalala kwenye kibanda chako cha mbavu za mbwa badala ya kupambana na kuleta mada za kuwepo na unafuu wa maisha ili uwe na maisha bora unaleta mada za kutetea jina Mzizima😂😂😂😂.

Wewe kama unawachukia waarabu utajua mwenyewe.Tafuta njia ya kutoa chuki zako.Babu zako akina TAMBAZA ndio waliwakaribisha waarabu wa OMAN na kuwauzia pwani ya Tanganyika.

Nenda ukagarauke kwenye kaburi la TAMBAZA huku ukibubujikwa na machozi.
 
Mkuu mimi nimeuliza legacy ya Sultan Majjid kuonyesha alifanya cha maana Dar Es Salaam kuweza kuchukuliwa kama mwanzilishi wa mji, hata Ikulu yenyewe haiwezi kuwa legacy ya maana. Wakoloni wazungu tunaona walianzisha mipango miji, administrative structures, ujenzi wa miondombinu(majengo, bandari na reli), shule n.k Sultan yeye legacy yake ilikuwa ni nini kusema ameanzisha mji wa Dar es Salaam??
Mkuu,

Nimeweka kitabu kizima kinazungumzia legacy ya Sultan Majjid.

Sultani ndiye kaanzisha mji, wewe unazungumzia legacy gani? Legacy kubwa kabisa ni mji kuwapo mpaka leo.

Kuna wakati baada ya Sultan kuanzisha mji kilipiga kimbunga hapo Dar mji ukawa kama umekufa.

Sultan akaendelea kujenga mji.

That was perseverence.

Bila ile perseverence pengine Dar isingekuwapo leo.

Soma kitabu hicho nimekiweka hapa.
 
Tukiangalia majina karibia yote ya mikoa yana asili ya hapa kwetu iweje jiji kubwa nchini na Africa Mashariki tubaki kungangania jina la kikoloni lenye historia ya kitumwa ?

Jina la jiji kubwa zaidi Afrika Mashariki "Dar Es Salaam" lilipewa na Sultani Majid bin Said

Kabla ya hapo, eneo hilo lilikuwa kijiji kidogo cha wavuvi kilichoitwa Mzizima, neno lenye maana ya "mji wenye afya."

Sultani Majid alikuwa akifanya biashara ya kikatili ya utumwa iliyomtajirisha, Bandari aliyotumia aliisifia kwa kuiita Dar Es Salaam, kwa tafsiri ya kiswahili ni bandari salama, alisafirisha babu na bibi bila bugudha ndio maana akapaita Dar Es salaam, sehemu ambazo babu zetu walifikia wamechapwa sana mijeredi, wamelimishwa sana mashambani, walioenda nchi walizotokea masultan hali ilikuwa mbaya walikatwa viungo vya uzazi ndio maana ni ngumu kukuta wajukuu zao, utaowakuta ni waafrika waliohamia kuanzia miaka ya 70s

View attachment 3250594

Itapendeza zaidi paitwe MZIZIMA
hivi wewe jina lako la kwanza unaitwa nani?
 
Tukiangalia majina karibia yote ya mikoa yana asili ya hapa kwetu iweje jiji kubwa nchini na Africa Mashariki tubaki kungangania jina la kikoloni lenye historia ya kitumwa ?

Jina la jiji kubwa zaidi Afrika Mashariki "Dar Es Salaam" lilipewa na Sultani Majid bin Said

Kabla ya hapo, eneo hilo lilikuwa kijiji kidogo cha wavuvi kilichoitwa Mzizima, neno lenye maana ya "mji wenye afya."

Sultani Majid alikuwa akifanya biashara ya kikatili ya utumwa iliyomtajirisha, Bandari aliyotumia aliisifia kwa kuiita Dar Es Salaam, kwa tafsiri ya kiswahili ni bandari salama, alisafirisha babu na bibi bila bugudha ndio maana akapaita Dar Es salaam, sehemu ambazo babu zetu walifikia wamechapwa sana mijeredi, wamelimishwa sana mashambani, walioenda nchi walizotokea masultan hali ilikuwa mbaya walikatwa viungo vya uzazi ndio maana ni ngumu kukuta wajukuu zao, utaowakuta ni waafrika waliohamia kuanzia miaka ya 70s

View attachment 3250594

Itapendeza zaidi paitwe MZIZIMA
Naam mlifanyie kazi
 
Bombay ilibadilishwa kuwa Mumbai,
Harare zamani ilikuwa Fort Saalisbury
Instanbul zamani ilikuwa Constantinople
Gold Coast ilibadilishwa kuwa Ghana
Toronto ilikuwa York zamani
Ongezea Tanganyika Sasa hivi inaitwa Tanzania! Maana kule Zanzibar wakija bara,huwa wanasema wanakuja Tanzania.
 
Jiji la hovyo sana .mpangilio wa makazi ni hovyo.Tunazidiwa na jiji zuri la Kigali na Bunjumbula
Mi ndio nimeshangaa mtoa mada alivyo lipamba mwanzoni nikahisi analizungumzia NEW YORK CITY ila nikashangaa anazungumzia Dar es salaam. Huyu jamaa amekosa exposure na usikute katokea mkoani huko
 
Hayo majina mengi uliyoweka yana asili ya hapa kwetu nakuongezea na Mbeya ilikuwa inaitwa Ibheya, maana yake mji wenye chumvi, Nairobi hapo kenya neno la kimasai lenye maana Maji baridi,

Majina mengine ni Carrier Corps sisi tuliita kariakoo,

Shida ni hio Dar es salaam, mtu alipaita kwasababu palikuwa ni salama kwa biashara zake za kuumiza babu na bibi zetu, ni sawa na muuza viungo anaisifia bandari fulani ni salama kwasbabu hapati bugudha.
Mbona Hinyanga kwa sasa Shinyanga napo walipaita hivo sababu ya kuwa walikuwa wanakutana hapo kwenye mnyaa mkubwa. Hinyanga maana yake kwenye mnyaa.

Sijajua shida yako ni nini. Tufute yale yaliyoitwa na wakoloni turudishe ya kiasili au tuite majina mapya. Sioni lojiki ya unachokitafuta zaidi. Utafika mahali useme hata majina ya Saidi, Lazaro, Asha, Mariamu nayo tuyaache tuitane chaurembo, Taabu, Misori, Ngegemkeni, Mapunda.
 
Sultan Majjid alinunua kipande hicho cja kutoka Magogoni mpaka Aga Khan kutoka kwa famikia ya Tambaza tangu alivyoingia huko 1860s.

Sasa Mjerumani kajenga vipi Ikulu hapo wakati hilo jengo la Ikulu lilikuwapo kabla Mjerumani hajafika hapo?
20250226_214530.jpg

20250226_214509.jpg

Germany Old Boma, Bagamoyo.
Makao makuu ya kwanza ya watawala wa Ujerumani hapa Tanganyika yaliyojengwa na Wajerumani. Iangalie hiyo design, same same na Magogoni.
 
..tunaweza kubadilisha.

..hata majina ya mitaa mbalimbali ya Dsm yalibadilishwa baada ya uhuru.

..barabara ya uhuru nadhani wakati wa Muingereza ilijulikana kama Accacia street/avenue.
Tunabadilisha kwa sababu zingine, siyo kuondoa memory ya utumwa au ukoloni.
 
View attachment 3250910
View attachment 3250911
Germany Old Boma, Bagamoyo.
Makao makuu ya kwanza ya watawala wa Ujerumani hapa Tanganyika yaliyojengwa na Wajerumani. Iangalie hiyo design, same same na Magogoni.
Hii haimaanishi kwamba Wajerumani hawajajenga Ikulu kwenye kiwanja cha Sultani palipokuwa na majengo ya Sultani Majjid hapo Ikulu Dar.

Pia picha hizo hata hazithibitishi kwamba Wajerumani hawajaiga kujenga hivyo kitoka kwa Waarabu.

Hizo picha hazi prove lokote zaidi ya kusema Mjerumani alijenga majengo Bagamoyo.

Kitu ambacho hakijabishiwa hapa.
 
Hii haimaanishi kwamba Wajerumani hawajajenga Ikulu kwenye kiwanja cha Sultani palipokuwa na majengo ya Sultani Majjid hapo Ikulu Dar.

Pia picha hizo hata hazithibitishi kwamba Wajerumani hawajaiga kujenga hivyo kitoka kwa Waarabu.

Hizo picha hazi prove lokote zaidi ya kusema Mjerumani alijenga majengo Bagamoyo.

Kitu ambacho hakijabishiwa hapa.
Pia mimi sijabisha Wajerumani walijenga Ikulu yao katika ardhi ya Sultan Majjid/Mzee Tambaza/watu wa pwani ya Dar es Salaam(Wakoloni walichuka ardhi waliyoona inafaa popote Tanganyika kwa matumizi mbalimbali, hili haliwezi kuwa jambo la ajabu au la kipekee sana).

Sijabisha pia labda kulikuwepo na majengo ya Sultan Majjid, sina uhakika na hilo, sijui yalikuwa ya aina gani kama yalikuwepi ila uhakika mkubwa ni kwamba majengo ya Ikulu ya sasa hayakuwa ya Sultan Majjid au Mzee Tambaza bali yalijengwa na Wajerumani.
 
Kule wapo wachache mji mzima hawazidi hata wakazi wa tandika utalinganisha na dar ambayo sawa na wananchi wote nchi nzima
Na Beijing ambayo inawatu zaidi ya milioni 21 lakini imepangwa vizuri na inavutia sana.Au New York city
 
Jina la Dar es salaam tulishalikubali, tulikichukua na kulifanya letu, si la Sultani tena.

Ukishikilia kuwa ni la Sultani, wewe ndiye unampa Sultani umuhimu asiokuwa nao.

Pia, kihistoria Dar es salaam kama mji ni mji ulioanzishwa na Sultani. Hiyo ni historia ambayo haifutiki hata ukibadili jina.
Mkulu unaposema jina la dar..."tumelikubali" una maana ya Watanzania wote au ni kina nani hao ambao wamelikubali?

Je, unataka kusema mleta mada sio Mtanzania?
 
Hii ni sawa na kachumbari tu kwenye pilau, hakuna jambo kubwa sana hapa.
Inawezekana Mjerumani alimpa tu tenda ya kutengeneza milango Mwarabu au Mswahili akajiongeza kuweka mambo yake na Mjerumani akaona ni urembo unaopendezea kwenye mlango.

Huu hapa mlango mmojawapo wa German Old Boma, Bagamoyo
20250226_214450.jpg
 
Hii ni sawa na kachumbari tu kwenye pilau, hakuna jambo kubwa sana hapa.
Inawezekana Mjerumani alimpa tu tenda ya kutengeneza milango Mwarabu au Mswahili akajiongeza kuweka mambo yake na Mjerumani akaona ni urembo unaopendezea kwenye mlango.

Huu hapa mlango mmojawapo wa German Old Boma, Bagamoyo
View attachment 3250942
Sawa.
 
Pia mimi sijabisha Wajerumani walijenga Ikulu yao katika ardhi ya Sultan Majjid/Mzee Tambaza/watu wa pwani ya Dar es Salaam(Wakoloni walichuka ardhi waliyoona inafaa popote Tanganyika kwa matumizi mbalimbali, hili haliwezi kuwa jambo la ajabu au la kipekee sana).

Sijabisha pia labda kulikuwepo na majengo ya Sultan Majjid, sina uhakika na hilo, sijui yalikuwa ya aina gani kama yalikuwepi ila uhakika mkubwa ni kwamba majengo ya Ikulu ya sasa hayakuwa ya Sultan Majjid au Mzee Tambaza bali yalijengwa na Wajerumani.
Hayo majengo yamejengwa kwenye ardhi aliyoinunua Sultan Majjid na yeye alikuwa kashajenga chuo cha kueneza Uislamu hapo.

Maana yake Ikulu ya Dar kuwa hapo leo ni matokeo ya Majjid kujenga hapo.

Angejenga ilipo Aga Khan Hospital leo, inawezekana Ikulu ya Dar leo ingekuwa ilipo Aga Khan Hospital leo.

Huelewi wapi?
 
Back
Top Bottom