Balozi Dkt. Slaa: Hata mimi nimetishiwa, na hata Ubalozi wakitaka wauchukue

Mkuu FaizaFoxy hebu endelea kutueliimisha hapa. Huyu mzee Dr. Slaa anassema kuwa anatishiwa kwa sababu ya kujadili Mkataba unaoihusu DP World. Kwa nini basi vitisho vitumike katika jambo lenye heri kwa nchi? Je maendeleo hususani mashirikiano baina ya nchi na nchi yana nguvu kuliko established governing Laws za nchi?

Kuna picha gani kubwa isiyoonekana kwenye huu Mkataba?
 
Ubalozi alipewa na Magufuli sasa nani atamnyanganya
 
Halafu waandishi wakitoka hapo wanapewa posho?
Au na wao "wazalendo" kama Slaa ?
Wanaenda kuripoti Kwa "uchungu"?😅

Kashafanya mikutano na waandishi mingapi?kashatoa posho ngapi??
Pesa inatoka wapi??
Wakati mwingine unakuja na vioja badala ya hoja... intresting
 
Wauchukue vp wakati kashastaafu.
Ingawa hoja zake zina mashiko
 
Halafu waandishi wakitoka hapo wanapewa posho?
Au na wao "wazalendo" kama Slaa ?
Wanaenda kuripoti Kwa "uchungu"?[emoji28]

Kashafanya mikutano na waandishi mingapi?kashatoa posho ngapi??
Pesa inatoka wapi??
Nawe ulipewa posho kwenye hiyo mikutano ya Dr. Slaa na waandishi wa habari!!??
 
Sisi wana falsafa tunajiridhisha kwa kujibiwa maswali yetu ya msingi sana. na ndipo tunapo anzia kufanya utafiti.

What is UBALOZI ?
And, Why UBALOZI ?
 
Naona kuna mzaha mwingi sana kuhusiana na issue hii. This country is the only country with the key if not the key to most sought African countries. Congo, Zimbabwe, Uganda, C.A.R etc it is geographically at the right spot. Strategically if you have Tanzania give or take you have a reach of 10 or more other countries in Africa easily. Sidhani kwa mwenendo wa "kufungua" nchi Majirani wetu watafurahishwa na zoezi zima la
kubinafsisha Bandari.
 
Balozi yupo makini. Asidharauliwe.
 

"Akizungumzia matumizi mabaya ya fursa ya kujieleza iliyopo nchini kwa sasa, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Masauni alisema: "Tutaendelea kupokea ushauri, maoni na mawazo, lakini bahati mbaya sana kuna baadhi ya Watanzania wenzetu wamekuwa wakitaka kutumia uhuru huo vibaya, kiasi cha kutoa kauli zinazolenga kuhatarisha usalama wa nchi yetu, kuvunia sheria za nchi na kupasua Taifa.

"Kauli hizi haziwezi kukubalika, haiwezekani tutumie kisingizio cha uhuru wa kutoa maoni kavunja sheria za nchi, sheria hizi zitaendelea kubaki kuwa sheria, na tuna wajibu wa kuhakikisha tunasimamia sheria zilizotungwa kwa maslahi ya watu wa nchi hii."

Chanzo: Hujuma nzito bandarini
 
Anaweweseka huyu ndugu yetu Dr.Slaa.....

#MamaAnaupigaMwingi[emoji7]
 
Anaweweseka huyu ndugu yetu Dr.Slaa.....

#MamaAnaupigaMwingi[emoji7]
Dr. Slaa anajidai kuwaponda UWT. Tanzania hii utapewa ubalozi kama haupo kwenye system?

Huyu ana maslahi binafsi, na ni mtu ambae hawezi kufikiri kwa kina. Amesahau kilichomkumba mrema alivyojisahau na kujaribu kuigeuka sysstem iliyomweka madarakani. wakati yeye anajulikana alikuwa pandikizi pale Chadema.
 
Ukosoaji ukijaa kebei na dharau na bezo hugeuza lengo na hoja kupelekea vioja.

Nimekuelewa. Lakini je anayekosea anatishiwa ama kuchukuliwa hatua za kisheria
 
Huu muungano kama vipi uvunjike. Haiwezekani Wazanzibari tuliowakomboa kutoka kwa yule Sultan wao wa Oman mwaka 1964, leo hii wajione kuwa na haki ya kututisha Watanganyika na pia kutuamulia mustakabari wa maisha yetu.
Absolutely !!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…