Balozi Joseph Sokoine ateuliwa kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Baada ya tukio lile Joseph Sokoine alirejeshwa nyumbani haraka.

Acha kupotosha wewe, mheshimiwa Balozi Joseph Sokoine, aliteuliwa na Rais hayati Dr John Pombe Joseph Magufuli kuwa naibu katibu mkuu ofisi ya makamu wa Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania kutoka kuwa balozi wa Tanzania nchini Ubelgiji, hapo alifanya kazi na mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan alipokuwa makamu wa Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania, inawezekana ndipo alitambua uwezo wake

Kwa taarifa yako, katibu mkuu/ naibu katibu wa wizara yeyote mkuu ana hadhi kubwa kuliko balozi anayetuwakilisha kwenye taifa lolote

Kwa maana hiyo, hayati Rais Magufuli alimpa promotion kutoka kuwa balozi kwenda kuwa naibu katibu mkuu ofisi ya makamu wa Rais

Na hata alipoteuliwa kuwa naibu katibu mkuu, bado aliendelea kuwa na hadhi yake ya BALOZI

Acheni upotoshaji wa hovyo hovyo
 

Kiswahili kinakupiga chenga naona unademka kweli kweli.
 
Sasa si umwambie arudi nyumbani? Mbaya wake si kafa?

Au kule amenogewa?
 
Mama anazidi tu Kumdhalilisha Mwendazake Kidiplomasia na Kutudhihirishia rasmi kuwa kwa 99% alikuwa hakubaliani na aina ya Uongozi wake sema tu alikuwa hana namna.
 
πŸ˜…πŸ˜…πŸ˜…βœŒβœŒβœŒ
 
Mie bado Mkuu hadi nione wale COVID~19 wamefukuzwa mjengoni na mama kuahidi kwamba lazima katiba mpya na Tume huru ya uchaguzi vipatikane kabla ya 2025.
Usishangae kutokea COVID-19 wakipewa teuzi mbalimbali kuanzia uDC kumaliza giza. Kisha kina Mbowe wataombwa walete listi nyingine rasmi.
Kuhusu Katiba mpya na Tume huru sahau. Labda maigizo yake. CCM hawako tayari kuachia madaraka. Wanaweza kulegeza kamba kidogo ili 2025 CHADEMA waambulie viti kiasi cha kurejea kuwa KUB kama zamani huku fitna zikipandikizwa kwa wingi kuvuruga utangamano ndani ya hicho chama.
 
Mama atapata tabu sana Watanzania wa leo si wa mwaka 47. Kutoa vyeo kama rushwa haitamsaidia chochote katika kupunguza wito wa Watanzania kutaka Katiba mpya na Tume huru ya uchaguzi. Kuzuga ilikuwa mwaka 47 2021 ataula wa chuya na akishupaza shingo muda si mrefu mikono yake itajaa damu ya Watanzania wasio na hatia. Maswala yaKatiba mpya na Tume huru ya uchaguzi HAYAKWEPEKWI kwa namna yoyote ile Watanzania wengi wamechoka kuwa na Wabunge na Madiwani wasiowataka.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…