Balozi Joseph Sokoine ateuliwa kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Balozi Joseph Sokoine ateuliwa kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Hamuoni kama hii ni positive sign?

A very positive move Uhuru na umoja.
 
Usishangae kutokea COVID-19 wakipewa teuzi mbalimbali kuanzia uDC kumaliza giza. Kisha kina Mbowe wataombwa walete listi nyingine rasmi.
Kuhusu Katiba mpya na Tume huru sahau. Labda maigizo yake. CCM hawako tayari kuachia madaraka. Wanaweza kulegeza kamba kidogo ili 2025 CHADEMA waambulie viti kiasi cha kurejea kuwa KUB kama zamani huku fitna zikipandikizwa kwa wingi kuvuruga utangamano ndani ya hicho chama.
CCM ni nani kwa sasa? Je hukohuko ndani ya CCM ni nani ana sauti zaidi ya Mama SSH. Atachotaka kufanyika kitafanyika bila pingamizi lolote lile. Labda wajumbe wa CCM wanaweza toa ushauri tu na si vinginevyo na ushauri wao unaweza kusikilizwa ama husitekelezwe. Usisahau pia, Mama ni Amiri jeshi Mkuu na ana nguvu ya kuamrisha lolote lile atakalo ndani wa uwezo wa mwanadamu na likafanyika liwe ndani ya chama ama ndani ya serikali.
 
Alirudishwa kwa sababu alienda kumtembelea lissu hospitali ubalgiji

Acha uongo wewe

Mheshimiwa balozi Joseph Sokoine, aliteuliwa na hayati Rais Dr John Pombe Joseph Magufuli kuwa naibu katibu mkuu wa ofisi ya makamu wa Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania, kutoka kuwa balozi wa Tanzania nchini Ubelgiji

Kwa taarifa yako, katibu mkuu( Permanent Secretary) / Naibu katibu mkuu( Deputy Permanent Secretary) wa wizara yeyote, ni wakubwa kuliko balozi wa Tanzania anayetuwakulisha kwenye nchi yeyote hapa duniani

Hata kwa majukumu ya kazi, katibu mkuu/ naibu katibu mkuu wa wizara, wana majukuku makubwa zaidi na mazito kuliko balozi

Kwa taarifa yako, balozi ana ripoti kwa mkurugenzi wa idara( eneo husika ambalo nchi ya balozi ipo) kwenye wizara ya mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa

Kwa mfano, balozi wa Tanzania nchini China, ana ripoti kwa mkurugenzi wa idara ya Asia na Australia, kwenye wizara ya mambo ya nchi na ushirikiano wa kimataifa

Na wakurugenzi wa idara wizarani, wapo chini ya katibu mkuu na naibu katibu mkuu

Kwa hiyo balozi Joseph Sokoine kuteuliwa kuwa naibu katibu mkuu, ilikuwa ni promotion na sio demotion

Kws hiyo tuache propaganda za hovyo juu ya hayati Rais Dr John Pombe Joseph Magufuli
 
Ahsante mkuu Ngongo.

Haya, mtu unaweza kusema huyu mama alikuwa anaigiza hapo, kwa ubinaadam huo alioonyesha?

Mtu utaigizaje namna hiyo, tena ukijua kwamba haikuongezei sifa, na pengine kukukosanisha na wabaya waliotaka kuondoa roho ya huyu binaadam mwenzao!

Mama ana roho nzuri, namwombea tu aweke mawazo yake yote wakati wa uongozi wake huu kuwatumikia waTanzania, na kufanya kila awezalo kuwasaidia wainue maisha yao kutoka kwenye umaskini uliokubuhu.

Ni waTanzania pekee watakaojiletea maendeleo ya nchi yao, kwa hiyo uongozi wake auelekeze kwao na sio kwa watu wengine toka nje.
 
Hivi huyu balozi Sokoine si ndio alikuwa anapelekwa kusoma nje na Lowasa maana alikuwa anakubalika sana monduli na Lowasa aliona njia pekee ya kumuweka mbali ni kumpeleka shule nje ya nchi na baada ya hapo akapelekwa ubalozi Washington?
 
Balozi Sokoine mtu wa watu sana, namkumbuka kwenye shughuli za Watanzania DC na New York tangu siku hizo akiwa ofisa wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Tanzania katika ubalozi wa Tanzania Marekani.
 

Balozi Joseph Edward Sokoine alimtembelea Tundu Lissu Hospital Belgian baada ya tukio hili alirejeshwa nyumbani haraka.

Leo Mh Rais Mama Samia Suluhu kamteua kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya nje na ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Pia soma> Tundu Lissu: Balozi Joseph Sokoine alirudishwa Tanzania baada ya kunitembelea Hospitali nchini Ubelgiji
Kitendo cha Balozi Sokoine kurudishwa nyumbani kisa kumtembelea Lissu mgonjwa hospitali ulikuwa ushahidi wa kutosha kuthibitisha uhusika wa magufuli na serikali yake kwenye shambulio ovu dhidi ya Lissu! Mungu amlipe Magu kwa kadri anavyostahili! Moto mkali jehanamu.

Sent from my itel A32F using JamiiForums mobile app
 
Kitendo cha Balozi Sokoine kurudishwa nyumbani kisa kumtembelea Lissu mgonjwa hospitali ulikuwa ushahidi wa kutosha kuthibitisha uhusika wa magufuli na serikali yake kwenye shambulio ovu dhidi ya Lissu! Mungu amlipe Magu kwa kadri anavyostahili! Moto mkali jehanamu.

Sent from my itel A32F using JamiiForums mobile app

Kila mTanzania alisikitika sana.
 
CCM ni nani kwa sasa? Je hukohuko ndani ya CCM ni nani ana sauti zaidi ya Mama SSH. Atachotaka kufanyika kitafanyika bila pingamizi lolote lile. Labda wajumbe wa CCM wanaweza toa ushauri tu na si vinginevyo na ushauri wao unaweza kusikilizwa ama husitekelezwe. Usisahau pia, Mama ni Amiri jeshi Mkuu na ana nguvu ya kuamrisha lolote lile atakalo ndani wa uwezo wa mwanadamu na likafanyika liwe ndani ya chama ama ndani ya serikali.
Sikubishii. Nakukumbusha kwamba huyo Mama ni CCM. Na azma ya CCM ni kubaki madarakani milele huku ikitengeneza sura ya kuwepo kwa taswira ya demokrasia nchini. Atasahihisha makosa aliyofanya Magufuli. Lakini usitarajie afanikishe hatua za kweli kama kutegeneza Katiba ya Taifa inayokubalika na wananchi na kuunda Tume huru ya uchaguzi mambo yatakayopunguza madaraka ya Rais/Mwenyekiti wa CCM na kuwezesha CCM kushindwa uchaguzi. Tarajia janja za kila aina kwenye masuala ya msingi kama haya.
 
Back
Top Bottom