Balozi wa Tanzania nchini Malawi ataacha lini utoto?

Balozi wa Tanzania nchini Malawi ataacha lini utoto?

Hapa nakuunga mkono! This is disgusting indeed! The boy should be punished immediately
Duh kweli maajabu hayaishi duniani..[emoji23] wanasema shetani akizeeka anakuwa malaika
 
Bro hata wewe una starehe au una vitu unapenda kufanya.
Ukiwa kiongozi haikuzuii mambo yako mengine usifanye.
For as long as havunji sheria ya mtu wacha aburudishe nafsi yake.

Mf Mkapa alikuwa rais wa nchi lakini starehe yake kubwa ilikuwa tungi na muziki
Na haikumzuia kuendelea kusakata rhumba na kupiga vyombo.

Kikwete anafahamika KWA kupenda vimwana . Mbona kapita na wengi Sana akiwa presidaaaa

Kuwa kiongozi haiondoi nature yako.
Unamkumbuka balozi Abdul Cisco Mtiro? Alikuwa na kihereni sikioni.......Kuna tofauti kubwa ya kuwa kiongozi na mwananchi wa kawaida
 
Tumeacha ku discuss hoja tumeanza ku discuss watu na maisha yao binafsi ambayo hayana uhusiano wowote na kazi zao.
 
Kuna hali mbili au tatu kwenye makuzi
Kukua kimwili
Kukua kiakili
Kukua kimwili na kiakili
Kuna kukua kiroho pia lakini huku huambata na akili, huwezi kukua kiroho huku akili ikiwa ni ya kitoto

Makuzi ya kawaida ni kuwa na uwiano sawa wa kukua kimwili na kiakili.. Hapa kimwili namaanisha kiumri. Unaposikia fulani ana mambo ya kitoto tambua huyo umri umeenda lakini matendo yake kiakili ni sawa na ya mtoto wa umri fulani.

Ama ukisikia ana mambo ya kikubwa yaani umrí ni mdogo lakini anayofanya yalipaswa kufanywa na mtu wa umri fulani kumzidi

Kuna shida kubwa huko kwenye vetting ya viongozi mbalimbali huko chama chawala, hasa viongozi hawa wa kisiasa. Wengi hawateuliwi kutokana na weledi maarifa, ujuzi na umahiri bali huteuliwa kama asante ama kwa sababu fulani isiyo na tija kwa taifa

Nafasi zinazolalamikiwa sana kwa sasa ni nafasi za uwakilishi wa nchi mbalimbali cheo cha balozi. Wateuliwa wengi hawajui ukubwa, umuhimu na weledi wa hii nafasi.. Wengi wao wanadhani balozi wa nchi ni sawa na balozi wa nyumba kumi

Balozi ni mwakilishi wa nchi pale alipo.. Ana mamlaka kamili na makubwa ya kusimama badala ya mkuu wa nchi..hivyo matendo yake, lugha yake, life style yake ni lazima iendane na nafasi anayoshikilia

Balozi mteule unaposhinda mitandaoni na kufanya vituko wanavyofanya wadogo zetu huko mitandaoni ni wazi kabisa huyo anakuwa hajitambui ama kakua kiumri na kimwili lakini sio kiakili.

Enzi za mwalimu kufanya vituko kama hivi ni automatically umejivua cheo husika hata kabla Mwalimu hajasema
Hebu ona hiki anachofanya huyu barozi wa walawi hapa!

View attachment 2231544
Kwanza amechanja!!!?

Tanzania yangu ina safari ndefu, hicho ndicho alichotumwa kwenda kufanya Malawi!!!
 
Dah. Tunaomba kuona kipengele ya Katiba mpya kuhusu hii issue?
Wala hakuna ulazima wa kuweka kipengele cha kuzuia watu kijirekodi wakicheza.

Mimi naongelea Katiba Mpya itakayoweka misingi ya uteuzi wa watu sahihi na wenye sifa kushika nafasi nyeti katika mifumo ya kiserikali.

Siyo kila mtu ateuliwe tu kwa sababu ni mwanachama wa ccm, au ni rafiki/mtoto/hawala/mke/mume/mchepuko/kunguni, au chawa wa kiongozi fulani. Au kiongoziajisikie tu kumteua mtu, halafu hakuna mamlaka ya kumhoji.
 
Wala hakuna ulazima wa kuweka kipengele cha kuzuia watu kijirekodi wakicheza.

Mimi naongelea Katiba Mpya itakayoweka misingi ya uteuzi wa watu sahihi na wenye sifa kushika nafasi nyeti katika mifumo ya kiserikali.

Siyo kila mtu ateuliwe tu kwa sababu ni mwanachama wa ccm, au ni rafiki/mtoto/hawala/mke/mume/mchepuko/kunguni, au chawa wa kiongozi fulani. Au kiongoziajisikie tu kumteua mtu, halafu hakuna mamlaka ya kumhoji.
Good suggestion; kwani Katiba la sasa haina hivyo vipegele? na pengine kwa maoni yako, Katiba mpya kitahakiksha hayo mabadiliko??
 
Wala hakuna ulazima wa kuweka kipengele cha kuzuia watu kijirekodi wakicheza.

Mimi naongelea Katiba Mpya itakayoweka misingi ya uteuzi wa watu sahihi na wenye sifa kushika nafasi nyeti katika mifumo ya kiserikali.

Siyo kila mtu awe na sifa ya kuwa kiongozi kwa sababu tu ni mwanachama wa ccm, au ni rafiki/mtoto/hawala/mke/mume/mchepuko/kunguni, au chawa wa kiongozi fulani.
Tate Mkuu, yote uliyosema ni kweli ila binafsi nafahamu kuwa Komredi Polepole ana sifa za kuwa kiongozi wa juu sana humu nchini, in fact ana uwezo, weledi, akili, maarifa na uzalendo kuliko viongozi wengi saaana kwenye Kabineti ya sasa na hata huko Bungeni.

Hivyo basi, kama uteuzi wake kwenye nafasi ya Ubalozi ni kwa nia njema ya kumpa international exposure kwenye siasa na uongozi ni sahihi; lakini kama ni malice - oriented na driven BASI KUNA SHIDA kwenye uongozi na ushauri!
 
Acha kunifokea. Wengi mnapewa mamlaka makubwa huku wengi wenu mkiwa ni vilaza. Kisa tu mko ccm. Siku ya kufa hiki chama chenu, hakika hii nchi itapiga hatua kubwa sana kimaendeleo.
Mkuu usidhani shida ni chama cha ccm....tatizo ni watu,ikiwa watu ni wale wale then tegemea matokeo Yale Yale. Hao walio ccm saizi wanaweza wakahamia chadema au chama kingine chenye nguvu na wakaunda serikali.

Kitakachokuja kuisaidia hii nchi ni vitu vikuu vitatu:
1. Elimu
2. Uwajibikaji.
3. Siasa safi.

Coz ukijaribu kuangalia mambo kwa mapana yake 2015-2021 akina mwigulu,kigwangala na wengineo walikuwa kwenye bendi ya kumsifu Rais Magufuli....ila kuanzia march 2021 nafikiri unaona mambo yalivyo badilika.
 
It's good to have some fun sometimes ila kwa cheo chake ni kweli hilo tunatafsiri kama ni utoto.

Just imagine kuna kampuni toka malawi linataka kusign deal na Tz, then wanaona video ya mtu ataewaguide ndo huyu, kwa akili ya kawaida tu sio rahisi kuamini kama akili yake iko sawa.
 
Mkuu usidhani shida ni chama cha ccm....tatizo ni watu,ikiwa watu ni wale wale then tegemea matokeo Yale Yale. Hao walio ccm saizi wanaweza wakahamia chadema au chama kingine chenye nguvu na wakaunda serikali.

Kitakachokuja kuisaidia hii nchi ni vitu vikuu vitatu:
1. Elimu
2. Uwajibikaji.
3. Siasa safi.

Coz ukijaribu kuangalia mambo kwa mapana yake 2015-2021 akina mwigulu,kigwangala na wengineo walikuwa kwenye bendi ya kumsifu Rais Magufuli....ila kuanzia march 2021 nafikiri unaona mambo yalivyo badilika.
Kaka pembe, nadhani uko sahihi some where ila ukuyafafanua vizuri. Hao uliwataja na wengine wengi ndani ya CHAMA letu, CCM, niwachumia tumbo tu. Ngoja twende and come 2024 na 2025 utaona mambo na hii picha wazi wazi! Tuombe uhai tu kwa Mungu, Yehova.
 
Tafsiri ni tafsiri tu, kila mtu anayo haki ya kutafsiri apendavyo ILA na wewe usiwatafsirie Wamalawi vile ufikirivyo!
 
Back
Top Bottom