Bandari ya Bagamoyo Ijengwe au Isijengwe? Soma Makala hii Tujadili

Bandari ya Bagamoyo Ijengwe au Isijengwe? Soma Makala hii Tujadili

Binafsi naona ni vema bandari ijengwe baada ya kupitia yale mapungufu yaliyoonekana kwenye draft proposed agreement na kuyarekebisha. Hii ni sababu naamini hakukuwa na mkataba uliosainiwa bali ilikuwa ni draft ambayo haikuwa imekamilika sababu walikuwa bado kwenye stage ya negotiations.

Jiwe alikurupuka maana ile waliyoleta ni moja ya proposals zao na zilikuwa nyingi sana sio hizi tu, ule ni mkataba mkubwa sana so katika haya machache tufanye mapitio upya ili kuharakisha uwekezaji.

Negotiation mpya zitaturudisha nyuma na gharama zinaongezeka. Negotiation zilifanywa zaidi ya miaka mitatu sasa tukianza upya itakuwa tunarudi upya miaka sita hadi saba nyuma hii sio sawa.

Nashauri pale tulipoona kuna mapungufu ifanyike marekebisho yenye maslahi ya nchi then tusaini mkataba kazi iendelee.
 
Lazma bandari itahamia kule.
Hapo watafunga.
Sidhani kama wataruhusu TENA hapo kuwe na BANDARI
Aibu sana, lakini hiyo hapo itabaki maana ile ya wachina itajengwa kule mbegani. Hiyo ni bandari inahudumia Zanzibar, mafia na visiwa vingine.
 
Lazma bandari itahamia kule.
Hapo watafunga.
Sidhani kama wataruhusu TENA hapo kuwe na BANDARI
Ninachofahamu hiyo bandari inahudumia majahazi ya bidhaa ndogo na mashua za wavuvi wadogo. Huwezi kuhamisha hiyo wakahudumiwe kwenye bandari inayolenga kupokea meli zenye uwezo wa kubeba kontena 10,000 na kuendelea.

Maana katika mkataba pia haizuii sisi kudevelop bandari nyingine. Hiyo bandari ni muhimu.

Ni sawa na pale DSM port unaweza kuona kuna bandari ndogo kwa ajili ya abiria wa boat za visiwani, then kuna Creek kwa ajili ya mizigo ya visiwani then kuna gati za kupokea meli kubwa za nje.

Ni ngumu kupeleka mtumbwi wa samaki kwenye bandari kubwa.
 
hizo JAHAZI za samaki zitabaki kama zilivyo.

Ila kuhusu mizigo ya kutoka bara kwenda Zanzibar.lazma itapitia Bandari hyo MPYA.

na itakuwepo SEHEMU ya bandari ya boat za kwenda Zanzibar,tanga n.k.

Haitoishia kupokea meli kubwa tu.

Ninachofahamu hiyo bandari inahudumia majahazi ya bidhaa ndogo na mashua za wavuvi wadogo. Huwezi kuhamisha hiyo wakahudumiwe kwenye bandari inayolenga kupokea meli zenye uwezo wa kubeba kontena 10,000 na kuendelea...
 
Mkataba unasema bandali ya Bagamoyo ikisha kamilika bandali ya Dar haitaruhusiwa kutumika maana yake ni kwamba mizigo yote ya itapitia bandali ya Bagamoyo na serikali haitaruhusiwa kukusanya hata shilingi moja kwa muda wa miaka 33

Inaweza ikapita hiyo miaka 33 wakasema wamepata hasara iongezwe mingine kiongozi yoyote mwenye akili timamu hawezi kukubali

Kwa nini kusiwe na mgawanyo kati ya wachina na serikali hadi deni lao litakapo isha

Na kama hamjui hiyo miaka 33 hilo eneo la bandali linakua chini ya China na wataweka bendera yao na bendera ya Tanzania haitaruhusiwa kupepea hapo

Wachina wamewekeza star times hadi Leo hawalipi kodi wanasema wanapata hasara wachina sio watu kabisa
 
Ni vema kukawa na mkata mpya wenye tija kwa taifa ,,na si lazima wawe wachina kuwekeza hata wengine wenye uwezo wanaweza kuwekeza ikiwa kunayashwishwi ju ya wachina.

Poa Ni muhimu Sana mkataba huo ukawekwa wazi wananchi tuuone na ujadiliwe!
 
View attachment 1754585
Aliyekuwa Rais waTanzania Hayati John Pombe Magufuli alisema mradi wa bandari ya Bagamoyo ulikuwa na "masharti ya hovyo" ambayo serikali yake isingeweza kuyakubali...
Huu uzi umeurejesha nara ya pili ingawa kichwa cha habari slightly kimerekebishwa. Nami narudia kukujibu kama nilivyoipinga hoja ya kujenga bandari Baganoyo katika hoja ya awali.
Ingawa umeandika analyitically lakini unaupigia debe mradi wa bandari ya Bagamoyo utekelezwe kinyume na maamuzi ya JPM kuwa usitekelezwe. Nami naona nikujibu kiuchambuzi kwa nini usijengwe. Katika uchambuzi huu nitatumia pia hoja za wengine wenye mawazo kama yako.

Kwanza, Ndugai mwanzoni kabisa alisema kuwa Magufuli alishauriwa vibaya. Wote tunamfahamu Magufuli kama mtu makini sana katika kusoma document hata iwe kubwa kiasi gani si rahisi kumchomekea kitu asikione, pili kati ya Ndugai na JPM ambaye anaweza asiwe na access ya document ni Ndugai lakini sio JPM kwa kuzingatia nafasi yake hivyo hoja ya Ndugai kuwa Magufuli alishauriwa vibaya haina mantiki kabisa ila Ndugai aliitumia kama gia ya kutaka kujenga uhalali wa kureverse maamuzi ya Magufuli kuhusu kukataa kujengwa kwa bandari hiyo.

Mnaoupigia debe mradi huo mnadai kuwa bandari ya Bagamoyo ina kina kirefu maji hayajai na kupwa hivyo ndio sehemu inayofaa kujengwa bandari ya kupokea meli hizo kubwa na kuwa bandari ya DSM haiwezi kupanuliwa kuchukua meli kubwa za mita mia tatu au mia nne. Sasa kwa nini mkataba ukataze kujenga bandari ya DSM au nyingine yeyote kuanzia Tanga hadi Mtwara? Hao wawekezaji na nyinyi mnaogopa nini hiyo bandari ya Bagamoyo kushindana na bandari zingine za Tanzania? kwa nini mnaikingia kifua dhidi ya bandari zingine? Busara ya kawaida hapa ni kuwa wao kama wangewekeza (japo mimi napinga) basi wangekuwa tayari kwa ushindani na sio kutaka upendeleo wa kipekee.

Mnadai meli kubwa ndizo zitakuwa zinatia nanga bandari ya Bagamoyo sasa kwanini hamtaki hizo meli mnazoziita ndogo ziendelee kutia nanga katika bandari ya Dsm, Tanga na Mtwara? Kwa nini mnataka kuziua bandari zingine ikiwa lengo ni bandari ya Bagamoyo kuhudumia meli kubwa za mita mia tatu au mia nne?

Pia mnadai kuwa meli kubwa zitaleta mizigo Bagamoyo kisha baada ya kupakuliwa mizigo hiyo itabebwa na meli ndogo kupelekwa sehemu zingine! Uongo ulioje! Hizo sehemu ni zipi? Jiografia ya Tanzania ni kuwa sisi tumezungukwa na nchi sita zisizo na bandari ambazo ni Malawi, Zambia, Congo Mashariki (ingawa atlantic ocean wanayo), Rwanda, Burundi na Uganda. Nchi tatu za mwisho huwa tunashindana na Kenya katika kugombania mizigo yao hivyo wanaotutegemea kabisa ni nchi tatu za mwanzo. Pia hata kwa Zambia huwa tunashindana na bandari ya Durban. Mizigo inapoletwa katika bandari zilizopo hubebwa kwa reli na malori kupelekwa huko katika nchi hizo hivyo suala la meli ndogo ndogo kuichukua mizigo na kuisambaza haina mantiki kabisa, Pia jiografia ya Africa, mizigo inayokwenda Africa kaskazini au Magharibi kutoka Asia ni rahisi kupita Suez canal, mediteranian kisha kwenda huko hivyo haiwezekani mizigo yao ije huku East Africa kisha irudi huku North au west Africa. Hali kadhalika kwa mizigo inayotoka bara la America haiwezi kuletwa huku kwetu kisha ipakiwe tena kwenda West Africa au hata South Africa. Pia mizigo ya Africa Kusini inayotoka Asia haiwezi kuletwa Bagamoyo kisha ipakiwe tena kwenda Africa Kusini. Ni wazi mizigo ya Africa Kusini kutoka Asia moja kwa moja inapelekwa bandari ya Durban ambayo ni bandari kubwa. Hivyo hoja kuwa sisi tutakuwa tunahudumia mizigo ya nchi zenye bahari kama sisi ni hoja mufilisi isiyo na mashiko. Sisi urefu wa Kamba yetu utaendelea kuwa nchi zisizo na bandari zinazotuzunguka tu na ambazo zinahudumiwa vyema na bandari za DSM, Tanga na Mtwara vizuri na kwa ufanisi.

Reli ya kutoka bandari ya Mtwara hadi Mbababay ikikamilika, tutakuwa na uhakika wa kuihudumia Malawi kwa ufanisi zaidi kuliko bandari ya Bagamoyo. Hali kadhalika bandari ya Tanga imepanuliwa na SGR ikikamilika mizigo ya Congo Mashariki, Rwanda, Burundi, Uganda itahudumiwa kwa ufanisi zaidi.

MAPATO

Serikali kupitia mamlaka ya bandari inapata pesa za handling na storage ya mizigo pamoja na kodi/tozo mbali mbali za forodha zinazokusanywa na TRA kutokana na meli zinazotia nanga katika bandari ya DSM, Tanga na Mtwara; lakini bandari ya Bagamoyo ikijengwa mamlaka hizo hazitakusanya mapato huko na wakati huo huo bandari hizo zitakuwa zimeminywa meli zisitie nanga huko, badala yake mapato hayo na mengine ambayo projections zinaonyesha yataendelea kukua yatakuwa yanachukuliwa na wawekezaji hao toka China na Oman kutokana na meli kutia nanga bandari ya Bagamoyo, ujinga ulioje. Tuwe wakweli hata bandari hiyo ya Bagamoyo ikijengwa asilimia kubwa ya meli zitakazokuwa zinatia nanga ni hizi hizi zinazoitwa meli ndogo ambazo kwa sasa zinatia nanga bandari za Dsm, Tanga na Mtwara. Wakina Ndugai wanapigia debe hata haya mapato tunayoyapata sasa kupitia bandari zetu tuyakose badala yake yakusanywe na kuchukuliwa na wachina kwa kisingizio mradi una manufaa. Mbona hawatauambii quantifiable revenue amount ambayo tutakuwa tunapata bandari ya Bagamoyo ikifanya kazi badala yake wamekalia kusema mradi una manufaa sana lakini hawatupi figure?

UJENZI WA VIWANDA

Hoja nyngine ambayo inapigiwa debe na kufungamanishwa na ujenzi wa bandari ni ujenzi wa viwanda katika ukanda huo wa Bagamoyo. Swali rahisi hivi ni lazima mtu akitaka kujenga viwanda lazima ajenge na bandari? Kama hao wawekezaji wana nia ya kujenga hvyo viwanda hawajakatazwa kwani eneo la Bagamoyo ni moja ya meneo yaliyoainishwa kama EPZ, Hivyo wanaweza kuja kupitia TIC na kupewa ruhusa ya kujenga viwanda. Jambo la msingi wajenge viwanda kwa terms zilizo sawa na wawekezaji wengine katika EPZs zingine na wasipewe upendeleo wa kipekee kuliko wawekezaji wengine wanaojenga viwanda. Ukipita barabara ya Kilwa kuelekea Mkuranga, njia ya Chalinze na Tanga, utaona kuna viwanda vya wachina vimejengwa/vinaendelea kujengwa; mbona hao hawakufungamanisha ujenzi wa hivyo viwanda na ujenzi wa bandari ya Bagamoyo?

Ujenzi wa viwanda na ujenzi wa bandari ni vitu viwili tofauti ambavyo mwekezaji hana uhalali wa kulazimisha kuwa lazima afanye vyote. Amekataliwa bandari ajenge hivyo viwanda. Kama atahitaji bandari za kuimport raw materials au export ya bidhaa zake atatumia bandari zilizopo. Hoja kuwa bandari ya Bagamoyo ikijengwa na viwanda 700 vitajengwa haina mashiko kwa sababu hayo mambo mawili siyo lazima yafanyike pamoja.

Hoja yako kuwa China inaitambua Bagamoyo katikampango wake wa Belt and Road sisi haituhusu kwani hiyo ni mikakati yao ya kuitawala na kuinyonya dunia. Kwani hata kama tungeamua kujenga bandari ya Bagamoyo ni lazima wajenge wachina? Hatuwezi kujenga kwa nguvu zetu?

Watu wanapopata nafasi za uongozi wajifunze kuiga uzalendo kama ambavyo viongozi wa mataifa ya Uchina na mengine yaliyoendelea wanavyoweka maslahi ya nchi zao mbele hata kama ni kwa kunyonya nchi zingine.

Bandari ya Baagamoyo ikifanikiwa kujengwa basi itakuwa ni ufisadi kama ufisadi mwingine uliokuwa unafanyika huko
 
Ukitaka kula sharti ukubali na chako pia kiliwe.

Mchina hajatushikia bunduki, kama tunaweza, basi tujenge sisi wenyewe kwani shida iko wapi?
 
Hakuna meli kubwa ya kuja kusambaza mzigo wa Africa hapo Bagamoyo.

Waweke wazi mkataba wote.
 
Swali la kuuliza ni Je Bandari ya Dar inakidhi mahitaji yetu na nchi za jirani?

Kama jibu ndio, hamna haja kujadili bandari Bagamoyo, Tanga , Mtwara nk ila kama jibu hapana swali la pili linakuja. Je ni wapi pako convenient zaidi kuweka bandari kubwa ikiwezekana kuliko ile ya Dar?

Lakini naona mheshimiwa JPM na team yake hawakujibu swali hili wao walijikita sana kuwasema wachina. Sasa kama wachina wanyonyaji si tungejenga kwa pesa zetu wenyewe? Si alisema sisi ni nchi tajiri?

Mbona Ndege tumenunua na zinatia hasara? Mbona bwana tunajenga? Mbona SGR tunaambiwa ni pesa zetu za ndani? Bandari Vs Ndege ni kipi cha muhimu kwetu?
 
Back
Top Bottom