Angel Nylon
JF-Expert Member
- Jul 26, 2011
- 9,164
- 18,402
Teller anatakiwa akipokea note bandia toka kwa mteja ai punch pale pale mbele yake, asimrudishie mteja wala asiiweke bila kuitoboa mbele yake mteja kusudi asije akapewa mteja mwengineWahuni sana hao jamaa! Wanatunza noti bandia za kubambikia wateja wao
hazipo kwelisidhani kama utajibuwa jibu la uhakika zaidi ya kupewa siasa kwamba Pesa Bandia Bank hazipo.
..hii ni sawa kabisaUsisahau na hili.ukishtukia umepewa pesa bandia bank usijaribu kuwaambia wamekupa pesa bandia"
Ukifanya hivyo uta pigwa chini ya ulinzi na polisi walinzi na kupewa kesi ya uhujumu uchumi
na si hayo tu pia ni wa choleshaji kwa wale wazee wa front/gun man
kweli, hii sio healthyNi upuuzi wa Baadhi ya matela Kwa nini wasiwaambie waende kwenye dirisha la bulk cash? Huwa Wanaboa sana,unakuja jitu limejaza mabulungutu kwenye begi harafu anakuja kupanga foleni.
Bulk cash, ipo kwenye bundles, either zilofungwa na strips au zile za kwenye nylon from BOT. Kama hizo utahesabu vipi?BANK wana mashine za kuhesabia,wanawalipa watu wana vitendea kazi vyote vya kuhakiki namba.
Halafu ananipa hela nianze tena kuhesabu nadhani huu utaratibu ni wa BANK zinazopatikana TANZANIA TU.
Huwezi mwambia mteja Wa BULK ahesabu hela,nihangaike zitafuta nakuzipokea napo nihangaike zihesabu.
USELESS BANKS, sioni hata maana yao sasa kama unaweza pewa hela pungufu kwa kisingizio makosa ya kibinadamu au sikuhesabu.
20K unatoa kwa teller sio kwenye ATM? Why?Kumbe ndio maana tunao withdraw 20k wanachelewa kutuhudumia na hata wakikupa nikama wanakutupia,Asante Kwa kutufungua mijicho mkuu
Yaani zinatoka kwa mkupuo mmoja? au inabidi kutoa kdg kdg? na makato yake yakoje?Atm inatoa mpka 10m inatokana na uwezo wa card yako...kuna card crdb inatoa 5m,kuna catd inatoa 10m kwenye atm
Na teller nae analazimika kutumia machine maana ndio anaamini ipo accurate na inamsaidia ku detect note fake, hapo chacha!!!NARUDIA TENA NA TENA BANK KUNA WIZI UNAENDELEA KUWENI MAKINI.
Nimeenda kuweka hela kidogo tu Leo, Nikatoa kama kawaida vibunda vitatu vya 10k,5k na 2k
Nimehesabu mara mbili mbili, nikafika kwakua nawajua Teller walivyo nikampa hela dirishani Nikawa makini SANA naangalia siangaliii pembeni namkodolea
Kaweka hela kwenye mashine ikahesabuu fungu la kwanza, Ikahesabu Fungu la Pili na La Tatu.
Akaniambia Bado 5,000 imepelea kwenye lile fungu la 5,000 nikamwambia Rudia kuhesabu,Akachukua zote akaweka Juu ya Mashine zikahesabu kweli imemiss 5000.
Nikamwambia NAOMBA HIZO HELA...
akazichukua hela kafungua Dirisha kanipa Nikazihesabu kwa mkono pale pale Dirishani, Hela zote Zimetimia.
Nikaziweka kama tunavyofunga hela mtaani 5000 moja unaikunja na 5000 mwenzake inakua 10,000
Nikazichukua nikamwambia Chukua HELA hizi hapa Zimekamilika.
Nikagundua WIZI mwingine either ni makusudi au bila kujua Zile mashine kuna Muda zinashika NOTI Mbili zina count kama noti 1.
Usikubali kuhesabiwa HELA kwa mashine akakuonyesha, Chukua Hela zako Hesabu kwa Mkono.
Kama una uhakika 100% hela zako ulizihakiki na yeye anakwambia mashine imehesabu zime miss, Chukua HELA hesabu hapo hapo dirishani kwa Mkono.
BANK wizi hauishi kuna njia nyingi sana wateja tunaumizwa.
Si kamera tuu zinaonesha?Kuhakikisha si rahisi mtu kupata access ya zile records isije punguzwa wala ongezwa kitu,ina faida na madhara yake pia.
No matter what!! Pesa yoyote ninayopewa popote, hata iwe imetoka kwa ATM machine lazima niihesabu. Unless kama imehesabiwa nikiona.Nimekua ni mtu wa kuchukua Pesa mara kwa mara Bank na mara nyingi ni mtu ambae sikuaga na utaratibu wa Kuhesabu Pesa ninazo pewa toka BANK.
Lakini niwahakikishie wale ma teller either ni wao au mtu anaewapa yale maburungutu anakua anapiga hela.
Mara nyingi nikitoa Salio la maburungutu huwa unachukua yakiwa kwenye rubber band unapewa unatia kwenye BAG unasepa.
Kutokana na wingi wake huwezi kuhesabu hizo pesa mara zote huo ndio ukweli.
Haya maburungutu yapo aina mbili kuna yale ya NOTI mpya zinazokua na ki karatasi kushika noti zote (hizo hazina shida)
Kuna Hizi Burungutu ambazo noti zake ni Used unakuta zipo tayari counter pale kwa ajili ya kupewa wateja
[emoji116][emoji116][emoji116]
View attachment 2838836
Hizi burungutu Ndugu zanguni nawambia Ukweli nimejiridhisha kwa asilimia 100 na zaidi kwamba haya maburungutu huwa hayatimiii.
Si yote ila nakuhakikishia Ambae anabisha naomba afanye utafiti wake kisha arudi kunipa mrejesho.
Nimekua na kawaida sana ya kwenda Kuomba chenchi ninapokua nimeishiwa kwenye ofisi zangu.
Kwahyo unaweza PEWA burungutu la 2000,1000 na 5000. Mara nyingi kama mjuavyo biashara si muda wote wateja wapo.
Kuna nyakati wateja hamna mnakaa mnatizamana, Nikaona nijipe kazi ya kupanga Zile Noti za bank kwenye mafungu ya laki (noti za 5000) na 10k kwa (noti za buku na buku mbili)
Nikawa nahesabu hesabu hesabu, mara nyingi nakutaga upungufu kwenye noti za 2000 na 1000 ndio zinapochomolewa pesa.
Kila nikihesabu ni lazima kuna mafungu ntayakuta yamemiss 2000 na kwenye buku inamiss Buku.
Hawachomoi nyingi yani laki ya buku wanatoa buku na Laki ya 2000 wanatoa 2000.
Huwezi shtuka haraka utahisi umejichanganya, kilichonfanya nishtuke ni baada ya kuingia na hela kwenye chumba kisicho na pesa kabisa na begi langu nikamwaga pesa mezani kuhesabu.
Sikuamini nilihisi mazingaombwe kweli hela zimemiss.
Nikiumganisha DOTS nikapata majibu kumbe hawa watu hizi ndio tabia zao.
Unaweza jiuliza Teller anapataje marupurupu ila kumbe njia yao ni hiyo.
Wewe unae waamini BANK kwa kutohesabu pesa wanazokupa ipo siku utapga watoto wako wafanyakazi wako ukisema wamekuibia ila Nakwambia Leo hiii BANK ni WEZI mtapga watu wenu wa karibu mtawahisi na kuwafikiria vibaya lakini ukweli ni kwamba BANK kuna wezi wa kimya kimya.
Kama unaaamini hela bank hawaibi endelea.
Nimemaliza.
Inaelekea sio mnyamaMln 5 hizo si unazi hesabu dakika 3 chap tu mzee
Ova
Alisindikizwa nimemaanisha walimfatilia mara tu alipotoka bank, baada ya kuwashtukia kuwa wanamfatilia ikabidi aingize gari kwenye shule ya umma na jamaa wakazama na pikipiki yao hadi ndani ya shule ila misheni yao haikufanikiwa...Alisindikizwa kwenda wapi?
Sasa aweke kwenye machine zihesabiweSio kwa haya maburungutu mkuuu,huo msemo unakua applied kwa wenye hela za kawaida.
Walitaka kumpora au?Alisindikizwa nimemaanisha walimfatilia mara tu alipotoka bank, baada ya kuwashtukia kuwa wanamfatilia ikabidi aingize gari kwenye shule ya umma na jamaa wakazama na pikipiki yao hadi ndani ya shule ila misheni yao haikufanikiwa...
C ununue machineAtm kutoa laki 4 Mpaka itimie lengo mkuu kibarua chake si haba.
na tunaenda ndani wakat mwingine kwa ajili ya chenchi unatoa 6m unamwambia akupe buku za 500k na 2000 za 500k then 1m akupe 5000 tu, hizo burungutu unazopewa mkuu kusema uzihesabu Njaaa inauma hapo hapo.