Barua ya mwaliko ili kupata passport

Barua ya mwaliko ili kupata passport

Hii sio sababu ya msingi hata kidogo, kwa hiyo mtu akiwa na Nia ovu ndio atashindwa kuleta hiyo mibarua yao ya mialiko au?

Halafu mbona lipassport letu raia wa kigeni wanalitumia sana tu huko nje?

Kuna wanyarwanda Kibao tu na wakenya wanatumia passport yetu huko nje, na Tena ukiskiliza story zao wanakwambia Wala hata hawakutumia nguvu nyingi kupata hiyo passport...

Hapa Tanzania mtu anayetumia nguvu nyingi hadi anajikatia tamaa kwenye kutafuta passport ni mtanzania wa asili wa kuzaliwa hapa hapa...

Kuna mahindi Kibao tu na mapakistan ambayo hata kiswahili hayakijui ila yakitaka passport ni siku mbili tu yanaipata.

Tunavyosema kwamba nchi hii imeoza na Ina maudhi Kibao tuna sababu za msingi
Sawa na kitambulisho cha NIDA
wageni wanapata kiurahisi ila watz sasa
 
Vipi na sisi ambao tunateseka tukiwa hapa hapa kwenye hii nchi yenu ya Maziwa na asali, mbona hatuoni huo msaada wao???
Huku unaweza kuonana na wajomba, shangazi n.k wakakusaidia ata viazi vya kuchemsha.
Sasa huko ugenini kama huna shughuli ya maana, utaonekana kama uchafu unaotembea na kuchafua mazingira.
 
Roho zinawauma wakiona mtu anataka kutoka wanajua ataenda kutusua wakati wao wanataka watu wateseke hapa hapa Bongo
Hili linaukweli kwa 100% yaani pure facts.

Kikawaida mtanzania ni mtu mwenye roho mbaya sana na si mkarimu kama ambavyo huwa tunajinasibu.... Na mbaya sana hiyo roho mbaya mara nyingi huwa tunaionesha kwa watanzania wenzetu, ila kwa mgeni huwa ni full kujipendekeza.

Umeongea ukweli kabisa, mtanzania huwa anafurahi sana kuona mtanzania mwenzake anaishi kwa taabu wakati huo yeye ana auheni ya maisha.

Wale maafisa uhamiaji huwa wanafurahi sana kuona umekwama kuondoka hapa nchini, maana wanaamini kinachokukimbiza huku ni Hali ngumu ya kimaisha na ukifanikisha kuondoka pengine utaenda kuishi vizuri huko uendako kuliko wao wanavyoisha hapa nchini, hivyo kuondoka kwako roho lazima ziwaume hasa kama destination yako ni first world country.
 
Wqpi nimemwambia adanganye? Huelewi unachokisoma?

Mbona wao wanamdanganya mpaka apeleke barua ya mwaliko?

Lakini kwa JF ya siku hizi, inaweza kuwa mleta mada kajitungia tu.
Sijajitungia ni ukweli
 
Hili linaukweli kwa 100% yaani pure facts.

Kikawaida mtanzania ni mtu mwenye roho mbaya sana na si mkarimu kama ambavyo huwa tunajinasibu.... Na mbaya sana hiyo roho mbaya mara nyingi huwa tunaionesha kwa watanzania wenzetu, ila kwa mgeni huwa ni full kujipendekeza.

Umeongea ukweli kabisa, mtanzania huwa anafurahi sana kuona mtanzania mwenzake anaishi kwa taabu wakati huo yeye ana auheni ya maisha.

Wale maafisa uhamiaji huwa wanafurahi sana kuona umekwama kuondoka hapa nchini, maana wanaamini kinachokukimbiza huku ni Hali ngumu ya kimaisha na ukifanikisha kuondoka pengine utaenda kuishi vizuri huko uendako kuliko wao wanavyoisha hapa nchini, hivyo kuondoka kwako roho lazima ziwaume hasa kama destination yako ni first world country.
Upo sahihi kabisa.
 
huyu jamaa hajawahi kusafiri nje ya nchi hizo mambo za barua ya mwaliko na copy ya passpot ya unaye enda kumtembelea huko nje ya nchi hii ni kwa maombi ya VISA ila mtoa mada kaandika passport badala ya Visa waliomuelewa watamsaidia
Boss, ni ishu ya passport baada ya kulipia 20k inayohitajika ilikupakua form online baada ya kumaliza kujaza taarifa nikaenda ofisini ndio nimekutana na hiyo ishu ikabidi niwe mpole nikarudi na makablasha yangu
 
Kwamba hii ndio sababu kubwa ya wao kuweka hicho kigezo cha ovyo???

Kwamba nikialikwa na mtu ndio siwezi kuzamia huko baada ya muda wangu wa kustay kuwa umeisha au?

Mbona sababu ni nyepesi na ya kipuuzi sana?
Sababu zipo nyingi mkuu, lakini hiyo ni mojawapo kuondoa hofu ya uhamiaji haramu. Kuna sababu nyingine kama kuthibitisha safari yako kama ni ishu ya kutembelea familia, charity nk, lakini pia kuthibitisha muda wa kukaa, kuonyesha uhusiano wako na mwenyeji wako kama ni shirika, mtu binafsi nk, kwa kifupi hayo ndio baadhi ninayayafahamu mimi.
 
Tatizo lako uliwaambia unaenda yuropu au amerika
Ungewaambia unaenda Malawi hapo kwenda kuloga walaaa wasingekuomba mwaliko au sababu ya safari.
Sasa katafute mwaliko.
Mkiambiwa muwe mnapitia kwa vishoka muwe waelewa kwani utaepuka kadhia kubwa kubwa kama hizi
Naomba ni pm connection ya kishoka Kama unayo
 
Kwa hiyo kama Sina huo ushaidi wa safari siwezi kupata passport?

Na vipi kama nimeamua tu kutoka nchini kwa recreational purposes na Sina ndugu Wala rafiki huko ninakoenda siruhusiwi kusafiri au?

Kwamba wanatupenda sana na Wana hofu huko tunakokwenda kama hatuna mwenyeji tunaweza tukadhurika ndio maana wameweka mashariti ya namna hiyo au??? Yaani kwamba hii serikali inatupenda sana sisi raia wake?????

Haya Mimi mwakani Nina mpango wa kwenda Morocco kwenye michuano ya AFCON kusapoti taifa Stars, na huko Morocco Sina mwanyeji hata mmoja, je na penyewe wataniambia nitafute mwenyeji wa kuninadikia barua kutoka huko Morocco kabla sijaenda na endapo kama nikikosa mwenyeji huyo hawatoniruhusu kuondoka nchini kwenda kuisapoti taifa Stars??

Nchi hii Ina maudhi mengi sana..
Sasa siuwaambie naenda afcon mambo yasiwe mengi unapewa mbona makampuni kubao yanasafirisha watu kwenda kutizma michuano mbalimbali kimataifa
 
Swali lilikuwa unamtu unakoenda kufikia nikasema ndio, mjamaa akasema basi tuletee barua ya mwaliko na picha ya passport yake ili tuambatanishe
Waambie unaenda msibani. Mimi ilikuwa 2022 hakukuwa na hizo mambo za barua, labda mambo yamebadilika. Je kama wewe huna passport lakini unapata mgeni kutoka huko nje, so atazuiliwa huko atokako kwa sababu wew huna passport? Wanamaanisha mwenyeji naye lazima awe na passport ili kupata mgeni? Invitation letter sawa.
Hizi huwa ni mambo ya kutaka visa
 
Naomba ni pm connection ya kishoka Kama unayo
Ni check mimi pm tuyajenge. Wewe utakaa home tu mpaka siku ya kuja kuweka finger print. Muhimu sana NIDA au Namba yako ya NIDA. Hizo docs nyingine zinapatikana steshenary na pale pale uhamiaji
 
Hili linaukweli kwa 100% yaani pure facts.

Kikawaida mtanzania ni mtu mwenye roho mbaya sana na si mkarimu kama ambavyo huwa tunajinasibu.... Na mbaya sana hiyo roho mbaya mara nyingi huwa tunaionesha kwa watanzania wenzetu, ila kwa mgeni huwa ni full kujipendekeza.

Umeongea ukweli kabisa, mtanzania huwa anafurahi sana kuona mtanzania mwenzake anaishi kwa taabu wakati huo yeye ana auheni ya maisha.

Wale maafisa uhamiaji huwa wanafurahi sana kuona umekwama kuondoka hapa nchini, maana wanaamini kinachokukimbiza huku ni Hali ngumu ya kimaisha na ukifanikisha kuondoka pengine utaenda kuishi vizuri huko uendako kuliko wao wanavyoisha hapa nchini, hivyo kuondoka kwako roho lazima ziwaume hasa kama destination yako ni first world country.
Ila kama unaenda South Sudan, fast unapewa uende ukafe huko
 
Wewe nielimisha hapa hapa japo kwa kifupi tu...

Mimi nimekuwa nikifahamu nchi hii hairuhusu uraia pacha, ila wewe umeni surprise kwamba mtoto wa miaka 18 anaruhusiwa kuwa na urai pacha, Sasa ndio nataka unifahamishe zaidi kuhusiana na Hilo...
Mtoto wa mtanzania aliyezaliwa kwenye nchi inayotoa uraia wa kuzaliwa mara mmoja (bila kujali asili ya wazazi, mfano Marekani), anakuwa na uraia pacha, mpaka atakapofikisha miaka 18. Baada ya hapo, atachagua uraia mmoja anaotaka.
 
Back
Top Bottom