Uchaguzi 2020 Barua ya Wazi kwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kuhusu Mwenendo wa Kampeni za Uchaguzi Mkuu (2020) za Mheshimiwa Tundu Lissu

Uchaguzi 2020 Barua ya Wazi kwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kuhusu Mwenendo wa Kampeni za Uchaguzi Mkuu (2020) za Mheshimiwa Tundu Lissu

Ndugu mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC),

Ninachukua fursa hii kukupongeza wewe na timu yako kwa kazi ngumu mnayoifanya. Mnafanya kazi zenu kwa weledi na kwa mujibu wa sheria. Hongereni sana.

Kama inavyofahamika, nchi yetu hufanya uchaguzi mkuu wa Rais, wabunge na madiwani kila baada ya Miaka mitano. Hii ni kwa mujibu wa sheria za nchi yetu ambayo ni nchi inayofuata demokrasia ya vyama vingi.

Ndugu mwenyekiti, mwaka huu, 2020 Tanzania itafanya Uchaguzi mkuu wa Rais, wabunge na madiwani. Tayari kampeni za uchaguzi zimeanza kote nchini huku vyama mbalimbali vikizunguka kunadi ilani zao za uchaguzi.

Itakumbukwa kuwa lengo la kampeni hizo Ni kunadi sera za chama husika ili wananchi waweze kufanya maamuzi sahihi siku ya kupiga kura. Kampeni hizi zinatawaliwa na kanuni, sheria na taratibu pamoja na utamaduni wetu Kama watanzania. Hivyo, haitarajiwi kampeni hizi kutumika Kama sehemu ya kuwagawa Watanzania.

Hivi karibuni tumeshuhudia vitendo kadhaa vya uvunjifu wa amani ambavyo mara zote hufanywa na chama kimoja tuu, CHADEMA. Kabla ya kuanza kampeni, tulimsikia Tundu Lissu, mgombea urais wa Tanzania kupitia tiketi ya CHADEMA akiweka wazi kuwa atawaingiza watanzania barabarani Kama hatatangazwa mshindi. Tuliahihudia waandishi wa TBC wakifukuzwa kwenye uzinduzi wa kampeni za CHADEMA pale mbagala kwenye viwanja vya zakhiem.

Tundu Lissu akiwa jijini Mbeya aliendeleza mashambulizi kwa viongozi wa nchi kuwa itawaka Moto usiozimika. Huku akijua kabisa analengo gani, anaweza hoja za kuwa atadhuriwa huku akijenga hoja "kijanja" na kuwatumbukiza viongozi wa nchi ili wananchi wakoae imani na viongozi hao.

Kubwa kuliko Ni kauli yake aliyoyafanya Zanzibar akisema Hayati mzee Karume alilazimishwa kusaini makubaliano ya Muungano kinyume na mapenzi yake. Aliunda mbali zaidi kuwaambia ndugu zetu wazanzibar wanachaguliwa viongozi wao na Tanganyika huku akijua fika kuwa vikao hufanyika Dodoma kwasababu ndio makao makuu ya chama cha Mapinduzi.

Kauli hizi anazitoa sio kwa bahati mbaya kwani Mheshimiwa Lissu ni wakili msomi mwenye weledi mkubwa wa masuala ya kisheria. Anafanya hivi kwa makusudi akitumia utaalamu wake wa kisheria kuwashawishi watanzania kuamini uongo ambao unaweza kupelekea uvunjifu wa amani.

Ninaomba nikiwa Kama mtanzania mzalendo ninayeipenda nchi yangu kuwa Mheshimiwa Lissu aonywe na aelekezwe kujikita kwenye kueneza sera za chama chake. Ni muhimu Mheshimiwa Lissu akumbushwe kuwa Kuna maisha baada ya Uchaguzi. Mimi na yeye tunaweza tusiwepo, Ila watanzania amvao Ni ndugu, rafiki na watoto wetu wayendelea kuwepo. Hawa wanastahili kesho bora zaidi.

Ni vema Mheshimiwa Lissu akakumbushwa kuwa viongozi wa kisiasa Kama yeye ni watu wenye ushawishi kwa wafuasi wao na kuwa maneno yao yanaweza kuleta Faraja au huzuni, kilio au furaha, upendo au chuki, umoja au utengano zaidi sana kifo au maisha.

Amani Msumari
Tanga

Nakala:
Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania
Msajili wa Vyama vya Siasa Tanzania
Katibu Mkuu - CHADEMA
Katibu Mkuu - CCM

Naona umetumwa wewe...... Pumbaf....!!
CCM mtaweweseka Sana Uchaguzi wa mwaka huu! Toto Tundu amewashika pabaya...!!! Na bado mpaka Jiwe aje ayaite maji 'mma'!
 
Uzuri moja wale mliokuwa mnawategemea kuwasemea (mabeberu) wamepigwa pini ya hali ya juu. Hawawezi kusema lolote lile maana walifikiri Tanzania haikujipanga. Mwaka huu tumejipanga na namba mnaisoma bado mapema. Safi sana, mmebaki kupiga zumari tu humu JF, CCM ni mbele kwa mbele.

Ukijitambua na wewe utaandika kitabu chako ukijutia ulioyafanya
 
Sema yote lakini uadilifu wa Rais Magufuli sio wa kutiliwa shaka hata kidogo.
Ana makando kando kibao including kuwa mshukiww wa kwanz wa wasiojilikana. Ni mtu wa kutilia shaka ktk kila angle ya uhalifu tangu ashike madaraka.
 
Huko ilitokea kwasababu viongozi walilazimisha kubakia madarakani kinyume na matakwa ya wananchi. Hilo silioni Tanzania kwani tunawependa viongozi tulionao na katika uchaguzi huu tutawaweka viongozi tuwatakao kwa kupitia sanduku la kura na si vinginevyo.
Kama ni hivo basi tulia
 
Vyombo vya habari vinamuonyesha yeye tu huoni jambo hilo halipendezi?japo ndio linazidi kuwapa credit wa upande wa pili na ujue watu wengi wana hamu zaidi ya kuwasikiliza wale waliokua kimya kwa miaka mitano iliyoita
Nimeongelea suala la kuhatarisha amani ya nchi na kupelekea machafuko
 
Unaona kibanzi cha Lissu pasi na kuona li boritiii kuubwa upande unaoutetea.
 
Hajatishia usalama wa taifa letu hata mara moja
Rubbish
Peleka nakala hata mbinguni na ahera
Lissu anawanyima usingizi
Usitutishe buaana
Tz yetu sote
Kelele za mpangaji malizia......
Usalama wa Taifa my....
 
umeandika utopolo na utaona wanautopolo wanzako wanakuunga mkono
 
Ndugu mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC),

Ninachukua fursa hii kukupongeza wewe na timu yako kwa kazi ngumu mnayoifanya. Mnafanya kazi zenu kwa weledi na kwa mujibu wa sheria. Hongereni sana.

Kama inavyofahamika, nchi yetu hufanya uchaguzi mkuu wa Rais, wabunge na madiwani kila baada ya Miaka mitano. Hii ni kwa mujibu wa sheria za nchi yetu ambayo ni nchi inayofuata demokrasia ya vyama vingi.

Ndugu mwenyekiti, mwaka huu, 2020 Tanzania itafanya Uchaguzi mkuu wa Rais, wabunge na madiwani. Tayari kampeni za uchaguzi zimeanza kote nchini huku vyama mbalimbali vikizunguka kunadi ilani zao za uchaguzi.

Itakumbukwa kuwa lengo la kampeni hizo Ni kunadi sera za chama husika ili wananchi waweze kufanya maamuzi sahihi siku ya kupiga kura. Kampeni hizi zinatawaliwa na kanuni, sheria na taratibu pamoja na utamaduni wetu Kama watanzania. Hivyo, haitarajiwi kampeni hizi kutumika Kama sehemu ya kuwagawa Watanzania.

Hivi karibuni tumeshuhudia vitendo kadhaa vya uvunjifu wa amani ambavyo mara zote hufanywa na chama kimoja tuu, CHADEMA. Kabla ya kuanza kampeni, tulimsikia Tundu Lissu, mgombea urais wa Tanzania kupitia tiketi ya CHADEMA akiweka wazi kuwa atawaingiza watanzania barabarani Kama hatatangazwa mshindi. Tuliahihudia waandishi wa TBC wakifukuzwa kwenye uzinduzi wa kampeni za CHADEMA pale mbagala kwenye viwanja vya zakhiem.

Tundu Lissu akiwa jijini Mbeya aliendeleza mashambulizi kwa viongozi wa nchi kuwa itawaka Moto usiozimika. Huku akijua kabisa analengo gani, anaweza hoja za kuwa atadhuriwa huku akijenga hoja "kijanja" na kuwatumbukiza viongozi wa nchi ili wananchi wakoae imani na viongozi hao.

Kubwa kuliko Ni kauli yake aliyoyafanya Zanzibar akisema Hayati mzee Karume alilazimishwa kusaini makubaliano ya Muungano kinyume na mapenzi yake. Aliunda mbali zaidi kuwaambia ndugu zetu wazanzibar wanachaguliwa viongozi wao na Tanganyika huku akijua fika kuwa vikao hufanyika Dodoma kwasababu ndio makao makuu ya chama cha Mapinduzi.

Kauli hizi anazitoa sio kwa bahati mbaya kwani Mheshimiwa Lissu ni wakili msomi mwenye weledi mkubwa wa masuala ya kisheria. Anafanya hivi kwa makusudi akitumia utaalamu wake wa kisheria kuwashawishi watanzania kuamini uongo ambao unaweza kupelekea uvunjifu wa amani.

Ninaomba nikiwa Kama mtanzania mzalendo ninayeipenda nchi yangu kuwa Mheshimiwa Lissu aonywe na aelekezwe kujikita kwenye kueneza sera za chama chake. Ni muhimu Mheshimiwa Lissu akumbushwe kuwa Kuna maisha baada ya Uchaguzi. Mimi na yeye tunaweza tusiwepo, Ila watanzania amvao Ni ndugu, rafiki na watoto wetu wayendelea kuwepo. Hawa wanastahili kesho bora zaidi.

Ni vema Mheshimiwa Lissu akakumbushwa kuwa viongozi wa kisiasa Kama yeye ni watu wenye ushawishi kwa wafuasi wao na kuwa maneno yao yanaweza kuleta Faraja au huzuni, kilio au furaha, upendo au chuki, umoja au utengano zaidi sana kifo au maisha.

Amani Msumari
Tanga

Nakala:
Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania
Msajili wa Vyama vya Siasa Tanzania
Katibu Mkuu - CHADEMA
Katibu Mkuu - CCM
Wewe kachume chai haya unayosemea yako juu ya uwezo wako wa utambuzi, vinega kama wewe ni wa kupuuzwa tu.
 
Vyombo vya habari vinamuonyesha yeye tu huoni jambo hilo halipendezi?japo ndio linazidi kuwapa credit wa upande wa pili na ujue watu wengi wana hamu zaidi ya kuwasikiliza wale waliokua kimya kwa miaka mitano iliyoita
Sawa. Chombo cha habari cha umma ni TBC ambao mliwafukuza na kuwahatarishia maisha. Nashukuru kuwa Sasa mmepatanishwa.

Kuhusu vyombo vingine binafsi, nyie pambaneni muoneshwe. Hilo la vyombo binafsi ni lenu, lipo ndani ya uwezo wenu.

Ila pia ukweli utabaki kuwa ukweli, CHADEMA mwaka huu hamkujipanga vizuri kwenye eneo hilo. Jifunzeni kwa ACT-Wazalendo
 
Maneno anayotamka yako wazi. Huyu jamaa amejipanga kumwaga damu

Kwa hiyo ulitaka asemeje, kwa mfano, kama kutakuwa na uthibitisho kuwa ‘jecha’ amefanya uchakachuaji tena! Watu washangilie na kusifu? Kwamba Magu ashinde kwa hila halafu tushangilie!
Amka! Watanzania wa leo si ‘wadanganyika’!
 
Lissu ndie atakayemwaga damu? Kivipi ebu tufafanulie maana nyie uvccm mnapoint cheap sana

Sent from my SM-J250F using JamiiForums mobile app
Amesema ataingiza watu barabarani ilihali akijua fika njia hiyo ni njia mbaya. Akiona ameonewa, zipo njia za kufuata. Kama vipi anione, nitamshauri bureee email
 
Sasa hivi ni kipindi cha kampeni, haivumiliki kuongea uongo ambao unaweza kuleta madhara makubwa kwenye umoja, amani na mshikamano wetu Kama taifa.

Tindu Antipas Lissu akataliweeeeeee

Kuna mtu anazingumza uongo kama hilo ‘jiwe’ lenu! We hewa sana aisee!
 
Back
Top Bottom