Bashiru kusuka au kunyoa - ni baada ya Kinana kuteuliwa kuwa Makamu Mwenyekiti CCM

Bashiru kusuka au kunyoa - ni baada ya Kinana kuteuliwa kuwa Makamu Mwenyekiti CCM

Kinana karudi kwenye system inabidi tuwe macho na tembo wetu tena.
Acheni kuchafua wazee wa watu.
Mzushi mwenyewe (Msigwa) alimuomba radhi mhanga wa uzushi huo (Kinana) na kupelekea kumaliza kesi nje ya mahakama.
Au wewe una ushahidi mpya?
Kama unao ujitokeze bila majina feki tufufue mtanange.
 
Kuna kitu hujakiweka sawa hapo, wananchi unaosema waliishi kwa hofu au kulimia meno kipindi cha JPM je waliendesha maisha yao kwa njia halali au unaongelea wale jamaa wa madawa ya kulevya, wafanyabiashara kanjanja waliokwepa kodi, watumishi waliozoea upigaji serikalini, majambazi sugu na waliofoji vyeti?

Kwani magufuli alifanya kosa gani kudili na huo uozo. Mbona wananchi wa wakawaida na walioendesha maisha yao kwa njia halali hawakuwa na hizo hofu? Siku zote mtu mwenye hofu ni mtu ambaye anaendesha mambo yake kwa njia haramu.
Dikteta alikuwa mtu hatari sn
 
Ila pasipo kushangalia ujio wa kishindo, na kwa namna ile ile ya awali, yaani ujio wa kivingine wa "ari mpya, nguvu mpya, na kasi mpya" slogan iliyoibuliwa na Prof. Mukandala huyu huyu.

Uongozi wa sasa unalazimika kuendeleza na kudumisha mazuri yaliyofanywa na mwendazake. Wananchi wa kada ya chini walimkubali, kumuhusudu na kumwamini.

Wakishindwa kufanya hivyo, utazaliwa upinzani ndani ya CCM, yaani CCM Mpya yenye kumuwakilisha na CCM Maslahi ya hawa wanamtandao na wafanyabiashara wanaokishikilia chama na serikali yake.

Hizi sauti zinazosikika kuhusu haja ya kuwaindoa wahuni waliopo ndani ya chama si za kubeza. Chama kikubwa na kikongwe husambaratika kupitia "its internal weaknesses" na wala siyo kwa kupitia "its external threats"
Well said! Watu wanashadidia kurudi wapigaji wakati bunge zima limejaa wabunge waliosimikwa na Bashiru!
Wasijidanganye kama wamesimama kumbe wamechuchumaa!
 
Mnajichanganya sana. Kwanza Dr Bashiru hajawahi kuwa na interest na siasa! Hana analopoteza zaidi ya maumivu moyoni mwake kwa Watanzania wenye akili ya kiwango chako!

Usimsikitikie Dr Bashiru, kwa levels zake yeye wala watoto wake hawatokuja kupata njaa. Kaa ujifikirie wewe na kizazi chako!
Pumba tupu hapa! Hakuna anayejadili njaa ya Bashiru tunajadili siasa ndani ya CCM!

Usivyo na kumbukumbu ni kwamba Bashiru amekuwa akifundisha siasa miaka yote UDSM na mwanachama wa CUF, amekuwa akiandika makala za siasa na kujadili hadharani mada za kisiasa mpaka amekuwa Katibu mkuu wa CCM na sasa ni Mbunge wa kuteuliwa. Bado akili zako zinakuaminisha kuwa Bashiru hana interest ya siasa!
 
  • Thanks
Reactions: Qwy
Kuna kitu hujakiweka sawa hapo, wananchi unaosema waliishi kwa hofu au kulimia meno kipindi cha JPM je waliendesha maisha yao kwa njia halali au unaongelea wale jamaa wa madawa ya kulevya, wafanyabiashara kanjanja waliokwepa kodi, watumishi waliozoea upigaji serikalini, majambazi sugu na waliofoji vyeti?

Kwani magufuli alifanya kosa gani kudili na huo uozo. Mbona wananchi wa wakawaida na walioendesha maisha yao kwa njia halali hawakuwa na hizo hofu? Siku zote mtu mwenye hofu ni mtu ambaye anaendesha mambo yake kwa njia haramu.
Hii post imejaa pumba kabisa, Ben Saanane alikuwa muuza madawa, vipi kuhusu Lissu.
Extortion walizokuwa wakifanya akina Makonda, Sabaya and the likes kwa wafanyabiashara na industrialists unajua ni kwanini hazikuwa zikiripotiwa or rather unajua ni kwanini habari hizo hazikuwa zikifika mitaani?
Kuwa masikini/mlala hoi siyo sifa na dhana ya kwamba kila tajiri au anayeishi maisha bora ni muuza madawa ya kulevya au muhujumu uchumi ni umasikini wa fikra, watu wana hustle au wengine wanakuja na pesa zao kutoka overseas halafu wanakuja walugaluga wasiojua lolote kwenye maisha zaidi ya kuajiriwa wanawaletea nongwa kisa tu wana maisha mazuri.
Huyo Muhutu Jiwe alikuwa na nongwa mpaka kwa wanaofanya kazi kwenye mashirika ya kimataifa, aliwachukia na kuwaita wafanyakazi wa mabeberu kisa tu hakuwa na uwezo wa kuwa-control.
Tuupige vita umasikini.
 
Mwingine aliyenyolewa bila maji na wembe wa Bashiru ni Benard Membe hadi akahamia ACT Wazalendo.
Nionavyo ni kama huyu alinyolewa kwa kipande cha chupa bila maji wala sabuni
 
ila jamaa toka mwendazake aondoke yupo kimya sana hajawahi kuongea anajua msala wake
Huoni hata mtendaji mkuu nae yupo kimya siku hizi?
Waliyoyapigania yamekatishwa na msiba ule mkuu. So wamekosa nguvu, wamekosa support, kiufupi wameparaganyika na yanayoendelea sasa.
 
Itakumbukwa mwaka 2019 aliyekuwa Katibu mkuu wa CCM Bw. Bashiru aliwapuuza na kuwafananisha na mpira wa chandimu makatibu wakuu waliomtangulia Makamba na Kinana. Aidha aliwaambia wahamie upinzani kama hawawezi kwenda na kasi ya CCM mpya.

Haya yalitokea baada ya Wazee hawa kulalamika kuwa simu zao zimedukuliwa na wafuasi wa Magufuli aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM. Wengine ambao Bashiru aliwashughulikia ni January Makamba na Nape Nauye ambao wote hivi sasa ni mawaziri katika serikali ya Samia.

Mwingine aliyenyolewa bila maji na wembe wa Bashiru ni Benard Membe hadi akahamia ACT Wazalendo.
Leo wastaafu wameula tena!!! Wamerudi kwa mlango wa mbele wala si wa nyuma!!!Tusubiri tu ligi.
 
Dunia ni sehemu ya wote hata

Cheo ni dhamana ya muda tu

Ishi na wote kwa upendo
Hapana! huwezi kuishi na wote kwa upendo. Wengine ni wahuni. Binadamu wasio na utu! Angalia watu waliowahi kuhisiwa kuuza meno ya tembo wanavyorudishwa kwenye mfumo. Huyo anayewarudisha ana lengo gani? Unaweka baraza la mawaziri la vijana, unarundika wezi wazoefu wazee kwenye chama ili kuwasimamia vijana.
 
Leo wastaafu wameula tena!!! Wamerudi kwa mlango wa mbele wala si wa nyuma!!!Tusubiri tu ligi.
Timu mwendazake wanacheki kwa mbaaali!😁😁😁
 
Itakumbukwa mwaka 2019 aliyekuwa Katibu mkuu wa CCM Bw. Bashiru aliwapuuza na kuwafananisha na mpira wa chandimu makatibu wakuu waliomtangulia Makamba na Kinana. Aidha aliwaambia wahamie upinzani kama hawawezi kwenda na kasi ya CCM mpya.

Haya yalitokea baada ya Wazee hawa kulalamika kuwa simu zao zimedukuliwa na wafuasi wa Magufuli aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM. Wengine ambao Bashiru aliwashughulikia ni January Makamba na Nape Nauye ambao wote hivi sasa ni mawaziri katika serikali ya Samia.

Mwingine aliyenyolewa bila maji na wembe wa Bashiru ni Benard Membe hadi akahamia ACT Wazalendo.
Watajuana wenyewe bwana. Sisi hayatuhusu tunafatilia vita ya Ukraine na Urusi tu.
 
Itakumbukwa mwaka 2019 aliyekuwa Katibu mkuu wa CCM Bw. Bashiru aliwapuuza na kuwafananisha na mpira wa chandimu makatibu wakuu waliomtangulia Makamba na Kinana. Aidha aliwaambia wahamie upinzani kama hawawezi kwenda na kasi ya CCM mpya.

Haya yalitokea baada ya Wazee hawa kulalamika kuwa simu zao zimedukuliwa na wafuasi wa Magufuli aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM. Wengine ambao Bashiru aliwashughulikia ni January Makamba na Nape Nauye ambao wote hivi sasa ni mawaziri katika serikali ya Samia.

Mwingine aliyenyolewa bila maji na wembe wa Bashiru ni Benard Membe hadi akahamia ACT Wazalendo.
Ukipewa nafasi fanya kwa masirahi mapana kwa hyo wewe alitaka awaache hao mafisadi? tena hilo lichama linaenda kumalizikia tena ngoja muone badala ya kumshukuru Magufuli, Bashiru na Polepole mnawadharau hili lichama mnaenda kulizika rasimi , yaani mzee wa Twiga Qatar mnamrudisha saaaaawaa
 
Ukipewa nafasi fanya kwa masirahi mapana kwa hyo wewe alitaka awaache hao mafisadi? tena hilo lichama linaenda kumalizikia tena ngoja muone badala ya kumshukuru Magufuli, Bashiru na Polepole mnawadharau hili lichama mnaenda kulizika rasimi , yaani mzee wa Twiga Qatar mnamrudisha saaaaawa
Sasa mimi nahusikaje?
 
Itakuaje sasa mtu aliyehojiwa na kamati ya maadili leo anaenda kuwa makamu mwenyekiti wa chama hii balaa kwa wale sukuma gang...
 
Back
Top Bottom