Bastola iliyoua wawili Sinza ni dili kishirikina, lakini pengine pia imebeba mikosi na laana

Bastola iliyoua wawili Sinza ni dili kishirikina, lakini pengine pia imebeba mikosi na laana

Mshana wakumbushe kuwa kuna ulimwengu wa roho giza na ulimwengu wa roho nuru, ulimwengu wa roho ni halisi na kila jambo linaanzia kwenye ulimwengu wa roho giza au nuru. Tukio lolote linathibitika kakika ulimwengu wa mwili, baada ya kukamilishwa uko rohoni, ulimwengu wa roho giza unamilikiwa na shetani na mawakala wake efeso 6:10-18
 
Hata jamaa wa bongo fleva na bongo muvi wengi Eti wanamiliki vya moto siku hizi.

Master J aliongelea hilo juzi kati Mamlaka husika waliangalie upya kabla ya madhara kama hayo ya kuuana kutokea.

Yani mtu kumiliki silaha ya moto anajikuta kuwa kama tajiri wa dunia namba moja sijui [emoji57][emoji57][emoji57]

Wamejaa viburi !
 
Nashauri kufanyike uhakiki wa wamiliki wa silaha za moto haraka, wengi hawastahili ni mbwembwe tu na kutishia watu maisha mtaani na majidai.

Inasikitisha mtu asiye na hatia kuuawa bila kosa.

Bora angejimaliza yeye mwenyewe peke yake.
 
Halafu huyo muuaji kama ameacha mtoto au watoto watapata tabu sana shauri ya hayo mauaji alofanya baba yao .

Kuna siri kubwa ktk damu na uhai wa mwanadamu zaidi anajua Mungu.

Actually siyo watoto wake tu lakini mpaka wajukuu, vilembwe na vilembwekazi.

Yani hadi kikazi cha 4

Bwana anawapatiliza visasi wana wa uovu.
 
Hahaha Sasa mshana ulitaka kazi ya bunduki iwe kusongea ugali wa dona.

Acheni mawazo potofu Huyo Alex alikuwa kichaa aliemilikishwa silaha na imemuua na kuua. Maisha yataendelea Kama kawaida.
 
Nipe maandiko yanayo sifia pombe hasa yanayo toka katika vitabu takatifu.

Hayasifii bali yanaruhusu unywaji wa kileo.

Kum 12:20‭-‬21 SUV

BWANA, Mungu wako, atakapoongeza mpaka wako, kama alivyokuahidi, nawe utakaposema, Nataka kula nyama, kwa kuwa roho yako yatamani kula nyama; waweza kula nyama, kwa kufuata yote inayotamani roho yako. Na mahali atakapochagua BWANA, Mungu wako, apaweke jina lake, pakiwa mbali nawe mno, ndipo utakapochinja katika kundi lako la ng’ombe na kondoo alilokupa BWANA kama nilivyokuagiza, nawe utakula ndani ya malango yako, kwa kufuata yote inayotamani roho yako.

1 Tim 3:2‭-‬3‭, ‬6 SUV
Basi imempasa askofu awe mtu asiyelaumika, mume wa mke mmoja, mwenye kiasi na busara, mtu wa utaratibu, mkaribishaji, ajuaye kufundisha; si mtu wa kuzoelea ulevi, si mpiga watu; bali awe mpole; si mtu wa kujadiliana, wala asiwe mwenye kupenda fedha; Wala asiwe mtu aliyeongoka karibu, asije akajivuna akaanguka katika hukumu ya Ibilisi.

Kum 14:22‭-‬26 SUV

Usiache kutoa zaka ya fungu la kumi katika maongeo yote ya mbegu zako, yatokayo shamba mwaka baada ya mwaka. Nawe utakula mbele za BWANA, Mungu wako, mahali atakapochagua apakalishe jina lake, zaka ya nafaka zako, na divai yako, na mafuta yako, na wazaliwa wa kwanza wa makundi yako ya ng’ombe na ya kondoo; ili upate kujifunza kumcha BWANA, Mungu wako, daima. Na njia ikiwa ndefu mno nawe, usiweze kuzichukua kwa kuwa mahali ni mbali nawe mno atakapochagua BWANA, Mungu wako, apakalishe jina lake, hapo atakapokubarikia BWANA, Mungu wako; ndipo uzibadili ziwe fedha, na kufunga zile fedha uende nazo mkononi mwako, hata mahali atakapochagua BWANA, Mungu wako; na zile fedha zitumie kwa cho chote itakachotamani roho yako, ng’ombe, au kondoo, au divai, au kileo, au roho yako itakacho kwako cho chote; nawe utakula huko mbele za BWANA, Mungu wako; tena furahi, wewe na nyumba yako;

CC Mshana Jr
 
The guy was a gun lover
Screenshot_20210719-081903.png
 
Silaha tajwa tayari imeshaondoka na roho mbili na tayari iko mikononi mwa jeshi la polisi.. Haijajulikana kama mmiliki alinunua 'used' au brand new!
Kama kanunua mtumba ni kwamba hapo kabla ilishawahi kutumika mostly ilishauwa.. Wangapi? Haijulikani..labda mpaka kupata historia yake..! Kama kanunua mpya na yeye ndio mtumiaji wa kwanza basi kama sio silaha yenyewe basi pesa iliyotumika haikuwa na baraka.. Ilikuwa na mazonge..Na tayari silaha husika imeshaingia kwenye ulimwengu hasi
Kimsingi hakuna kesi tena ...! Muuaji naye kajimaliza.. Jalada litafunguliwa kisha baada ya muda litafungwa! Hakuna mshtakiwa...kidhibiti kinaweza kuwa huru na kuingizwa kwenye mirathi ama vinginevyo
Kama kitaingizwa kwenye mirathi kitakuja kuuzwa kama mali za marehemu .. Silaha hairithishwi.. Mnunuzi anaweza kutafutwa na ndugu na itauzwa kupitia jeshi la polisi na kitakachopatikana atakabidhiwa msimamizi wa mirathi

Silaha iliyoondoa uhai wa mtu hasa at close range ni dili sana kwa majambazi na wezi wanaotumia silaha kupora ama wauaji wa kukodishwa! Hiyo tayari ina damu kubwa hivyo kafara lake ni rahisi.. Silaha iliyouwa maranyingi zaidi kishirikina ina thamani kubwa zaidi kuliko ile ambayo haijawahi kuondoka na roho hata moja! Hivyo hii silaha ya Sinza inaweza kuwindwa na watu wabaya...!

Kwa upande mwingine ile silaha inawezekana kabida ina nuksi, laana ama imebeba maagano mabaya hasa kama ilikuwa mtumba...! Kuna vitu ni mali ya kuzimu na kazi yake ni kuharibu na kuumiza tuu..Ndio maana kuna watu hawapendi kabisa kununua vitu mtumba..vingi vimebeba nuksi laana na maagano kama nilivyosema hapo juu..!

Tukio limeshatokea na kuzua mijadala mingi mitandaoni.. Pengine kuna watu watawajibishwa hasa kama utaratibu wa kummilikisha mhusika silaha haukufuatwa inavyotakikana
Niandikapo haya kuna familia mbili ziko kwenye msiba mzito.. Wa kuondokewa na baba, kaka mume nknk.. Tayari kuna maisha mapya wanaenda kuyaanza bila mhimili wa familia.. Ni hali ngumu sana..
Haya yote yatasahaulika baada ya muda.. Na itafika mahali kama silaha husika haitateketezwa na jeshi la polisi basi itaingizwa kwenye mirathi na kuuzwa kwa mwingine...

Kuna maroho na mapepo ya kuzimu yapo duniani kuharibu na kutesa na hujipenyeza kwenye vitu na watu... Haya mavitu ya mtumba tunayotumia hatujui huko nyuma yalipitia mikono gani na yalinenewa nini.. Kuna baadhi vimebeba mapepo mapepo na maroho mabaya
Kuna baadhi vimelaaniwa na wamiliki wa kwanza au wa pili nk
Kuna baadhi vimenenewa vibaya
Kuna baadhi vimetumika kwenye madhabahu za kishirikina
Jitahidi unapopata kitu cha mtumba kitakase kwa imani yako

Nimeandika mada hii kwa mtazamo wa kiroho.. Wanaoona ni tukio la kawaida wasione ni kituko kuwaza tofauti na wao..!

View attachment 1858067
Very true..
 
kuna kitu cha kufikirika ktk hili.....ila lililo kuu ni USALAMA WA RAIA POPOTE WALIPO........kile kipind unamaliza six then unaenda JKT.....ilifanya kuwa na asilimia kubwa ya wenye uelewa wa HATARI YA SILAHA za MOTO...........angeweza kudhibitiwa mapema sana......kwa kutoa taarifa kwa vyombo husika.....na tusingepoteza roho 2 @ once........ni tukio la kipumbavu kwa wote waliokuwa pale...wote waliokuwepo WALIRUHUSU muuaji kujifanyia atakavyo.........na ndio kilichotokea......poleni wafiwa....tujilaumu wote...
 
Umeandika 'fact'.

Kuna jamaa yangu alifariki kwa ajali ya kugoga mwembe kwa gari.

Ile sehemu iliyogongwa, walichubua magome yote mpaka wakaokota uvingiri uliosambaa pale chini pamoja na ule 'unga' wa vioo vilivyotapakaa damu, vyote walifagia wakazoa!

Muda wa kubangua hayo magome na kufagia vioo wanaujua wao maana hatukuona mtu akifanya hilo tukio!

Sent using Jamii Forums mobile app
Walifanya kwa usiri mkubwa tena usiku.. Unakumbuka wakati wa Mkapa zile ajali? Kuna yule mzee walimuua baada ya kukutwa eneo la ajali anakusanya úbongo na damu za marehemu na kuweka kwenye rambo yake
 
Ulozi Man, hivi usiku Mara nyingi nasikia mtu anatembea nje,the way anavyotembea hujui anaenda mbele au anarudi nyuma, Mara nyingine nimekaa sebulen mida ya tisa usiku naangalia televihmseni, nikahisi hatua zinatembea kwa muds mrefu dirishani mwangu nkkamute remote nisikilize ghafla hali ikapotea nlivyochungulia dirishani naona tochi inatembea inamulika, mmulikaji haonekani yaweza kua vibaka type au kuna ushirikina involved!?
Hiyo ni michezo ya wanga..hawaendi wala hawarudi wapo tu hapo nje wanagininda
 
Back
Top Bottom