Beberu anamtaka sana Iran ajiingize Gaza

Kumbe na Hamas wanaweza kutengeneza propaganda za kitoto hivi na raia wakaamini? πŸ˜„πŸ˜„πŸ˜„πŸ˜„

Usichoelewa ni kuwa Israel alisaidia kuanzishwa HAMAS ili kutengeneza utengano Palestina.

Sera zile zile za CCM na upinzani Tanzania. Kwani CCM inataka umoja wa upinzani?

Israel haikutaka umoja wa akina PLO; HAMAS, PIJ na vikundi vingine ilikuwa Kwa maslahi yake zaidi.
 
Halafu leo hii hao hao hamas waliotengenezwa na Israel wanakujavamia Israel kuua na kuteka raia kisha kuanza kuwaua askali wa Israel walioingia gaza πŸ€”πŸ€”

Bonge moja la movie πŸ˜„πŸ˜„πŸ˜„
 
Mkumbushe pia hata mujahideena (al qaeda) ilitengenezwa na Marekani ili ipambane na USSR ilipovamia Afghanistan.
 

Unaweza kudhani kuwa si Marekani au Israel mwenye kumtaka Iran lakini jiulize:

1. Kwanini kumekuwa na Iran kulaumiwa kwenye mengi kwenye hii vita?

2. Kwanini kila hii vita ikitulia Marekani inatimba Israeli, vita vinarindima upya?

3. Kwanini Marekani ni wajumbe kwenye baraza la vita Israeli?

4. Kwanini kuna vita west bank ambako hakuna HAMAS?

5. Kwanini uwepo huu wa Marekani kwenye Israel na Gaza isiyokuwa na silaha wala usaidizi?

6. Angalia Hapa:

Gaza ni Marekani dhidi ya Palestina si Israel na HAMAS

7. Kumbuka longo longo za Marekani UN kuhusu mzozo huu.

8. Kasi ya Iran hasa kwenye kutaka nuclear ni kitisho kwa mwana mpendwa wa Marekani pale mashariki ya kati.

9. Kama Iraq, Syria au Libya; Iran atakuwa mjinga kutodhani anatafutwa kwa udi na uvumba.
 
Irani hatakuja kuvamiwa kijeshi na taifa lolote maana matokeo ya vita hivyo yatakua mabaya sana sio mashariki ya kati pekee bali dunia nzima kwa ujumla.

1. Tofautisha kumvamia Iran na kumvutia mtegoni akung'utwe.

2. Haipo siri kuwa nguvu za Iran zinaongezeka na hiyo Marekani na Israel ni kitisho kisichopaswa kupuuzwa.
 
Hakuna taifa lolote ulimwengu la kuanzisha vita vya moja kwa moja na Iran au Korea kaskazin
Wataishia kwenye vikwazo na mikwara tuu

1. Kwa maana hiyo hii ni mikwara kumrai Iran asiingie.

Au:

2. Ni kumweka busy Iran asiunge mkono kama anavyofanywa west bank.
 
Siku yake roho ikiondoka tutamuangalia live anaenda kuliwa na mchwa. Hakuna atakaemsaidia.
 
Hivi ISRAEL huwa wanasherehekea krismass kiserikali? , namaanisha je sikukuu ya xmass inatambulika na serikali ya huko.!?
Maana naona ligi za nchi nyingi zinasimama kupisha xmass.

πŸ€”πŸ€”πŸ€”πŸ€”

1. Mayahudi hawakuwahi kumtambua mtoto wa seremala kama Yesu.

2. Kwao Yesu hajazaliwa ..

3. Mayahudi si wakristo.
 
1. Tofautisha kumvamia Iran na kumvutia mtegoni akung'utwe.

2. Haipo siri kuwa nguvu za Iran zinaongezeka na hiyo Marekani na Israel ni kitisho kisichopaswa kupuuzwa.
Ety umvutie mtegoni kwa hizo proxywars Kama Hezbollah na houthi pamoja na teknolojia anayowapa Hamas ya kutengeneza siraha hasa maroketi na maandaki huoni Kama amefanikiwa pakubwa na Hana haja ya kujiingiza huko Ila alishakubali kuwa anawasapoti waziwazi, Sasa kwanini wasimfuate kwake wamkung'ute, 😁 hapo hamna jipya ni danganya toto tu maana wanajua mziki wake.
 

1. Vita sijambo dogo; vinataka uungwaji mkono au uhalali.

2. Tofautisha uhalali au uungwaji mkono kama akijichanganya hapa na kama akifuatwa Kwake.

3. Kungekuwa na azimio la ceasefire UNSC hata Iran angekuwa na pumzi ya kutia mguu Gaza.
 
Irani hatakuja kuvamiwa kijeshi na taifa lolote maana matokeo ya vita hivyo yatakua mabaya sana sio mashariki ya kati pekee bali dunia nzima kwa ujumla.
Kinachowauma wamerekani na israle na kuwaongezea uoga ni kuwa irani imeeekewa vikwazo kila kona na umoja wa ulay ili kumdhoofisha kama walivyofanya kwa sadam lakin jamaa ndo anaimarika kijeshi kila siku , huu na kwa sasa nadhani wameishiwa vikwazo la bda waanzishe vita ambayo itagharim uchumi wa dunia nzima
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…