Behewa za SGR zaanza kuwasili nchini Tanzania

kwamba hizi behewa kama hivyo zinavyoonekana hatuwezi kuzitengeneza hapa bongo? mbona mabasi wanaunda mabodi? au si kuunda behewa tu tupu halina injini.
Yaani hata mimi nimewaza hivyo
Je tungeagiza chassis tu na body tukaungaunga kwetu tungeshindwa?

Mbona meli tunatengeneza
Hapo tutakuwa tunapigwa kwa kila kitu
Naaona hata shuka na mito inatoka China
 
kwamba hizi behewa kama hivyo zinavyoonekana hatuwezi kuzitengeneza hapa bongo? mbona mabasi wanaunda mabodi? au si kuunda behewa tu tupu halina injini.
Mkuu ata Veta wanaweza kutengeneza bila wasiwasi
 
Halafu muandae watu wa kutosha kusimamia wabongo ndani ya hayo mabehewa!

Maana wengi wamezoea maisha ya kuharibu haribu tu vitu, kutokana na kukosa ile culture of care and maintainance.
Hiyo kazi wapewe Jkt
 
Pascal Mayalla uzi kama hizi huwa yeye ashiriki kujibu hoja huwa ana like tuu nakupotea...
Hapa ninachokisoma na kinachokanushwa ni vitu viwili tofauti, kwanza Watanzania tunapaswa kuambiwa ukweli
1. Taarifa ya TRC inasema vichwa vipya na mabehewa mapya, lakini ukweli ni kuwa ni vichwa mitumba na mabehewa mitumba ya mwaka '1947'!.
2. Mkataba ni wa ukarabati na kutiwa nakshi nakshi kwa vichwa na mabehewa mitumba!, na sio kuundwa kwa vichwa na mabehewa mapya!.
3. Hakuna ubaya nchi kununua vichwa mitumba na mabehewa mitumba, kitu muhimu ni Watanzania tuelezwe ukweli!.
4. Jee hivyo vichwa viliundwa lini, wapi na vimetumika muda gani kabla sisi hatujauziwa?.
5. Mitumba hiyo imenunuliwa kwa bei gani na inakarabatiwa kwa bei gharama gani?.
5. Tufanyiwe comparative analysis, kama tungenunua vichwa vipya na mabehewa mapya, tungetumia gharama kiasi gani, compared na kununua vichwa mitumba na mabehewa mitumba, ili tujue tumeokoa fedha kiasi gani kwa kununua mitumba hiyo?.
6. Japo gharama za kununua vitu vipya ni juu ila maintance cost ni ndogo, unaweza kununua mitumba kwa bei poa kumbe ni mitumba choka mbaya, hivyo maintenance cost ikawa juu.
7. Sii wengi wanajua kazi ya CAG sio kutoa tuu zile ripoti za hesabu za serikali, CAG ni Mdhibiti na Mkaguzi, ufhibiti unafanywa kabla ya manunuzi, jee kulifanyika tathmini yoyote rail worthness report ya vichwa mabehewa hayo mitumba kabla hayajanunuliwa?. Then CAG atufanyie value for money audit, msikute mitumba hiyo tumepewa bure, huku watu wakipiga kubwa tunauziwa kwa bei ya mapya!.
8. Ukiingia mkataba wa manunuzi, mzigo ukanunuliwa, delivery ndio ikachelewa, huwezi kuvunja mkataba huo ukabaki salama, hivyo kesi ikifunguliwa, Tanzania tunashindwa hata kabla kesi haijaanza!.
9. Tulivinja mkataba wa Dowans, watu wakajiapisha "over my dead body", tulishitakiwa, tukashindwa, tukadaiwa tukasema hatulipi!, ukweli ni kuwa tumelipa kwa siri, Watanzania hatukuambiwa!.
10. Tulipo vunja mkataba wa Dowans, Zitto akashauri tuitaifishe mitambo ile, Wabunge wetu wakagoma kuwa Tanzania hatununui mitambo mitumba!.
11. Mitambo ile ikanunuliwa na Simbion, tukaingia nao mkataba ule ule wa Dowans tuliovunja, kwa gharama zile zile na tukawalipa!.
12. JPM alipoingia tukavunja mkataba wa Simbion, tukashitakiwa, tukashindwa, JPM akagoma kulipa!, ila baada tuu ya JPM kuitwa kule, huku nyuma, sio tuu tumelipa, bali pia tumeinunua ile mitambo kwa bei ya ajabu!, sasa mitambo ile tuliosema ni mtumba hatununui, sasa ni mali yetu na malipo yote yaliisha fanyika chap chap!, ila Watanzania hatuambiwi!.

Tuambiwe tuu ukweli!.
P
 




Nauliza tu, kwamba hivi haya mabehewa tunayoletewa toka Korea yana madirisha ya kufunguka, au yamefuata design za huko majuu ambako wao wana uwezo wa kuhakikisha air condition zinatumika na kufanya kazi wakati wote kwenye mabasi na matreni?

Isije tukaua watu kwa joto wakati tumeshindwa ku-mantain hizi air condition kwenye mabehewa, au labda safari kuahirishwa kwa kuwa air condition za mabehewa hazifanyi kazi. Nawaelewa sana Watanzania wenzangu, mambo ya maintance yanatupita kwa mbali sana, ndio maana hadi sasa mabasi yote yanayotumika nchini ni yale ya kufungua madirisha, tofauti na mabasi ya huko majuu.
 
Munataka muanze ingiria dirishani? Hewa inaingia kwa juu. Hayo madirisha kama ya ndege.
 
Mie nipo, hili suala la design ya madirisha nakuambia litakuja kuwa issue, labda kama yanafunguka. Hao watu walio pitisha design sidhani kama walifikiria hilo. Huenda walikuwa wanasiasa sio mainjinia. Yatakarabatiwa kabla hata hayajatumika.
 
hayo ndio yameletwa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…