Bei ya gesi ya kupikia kupungua bei ili kuchochea Matumizi ya Nishati Safi

Bei ya gesi ya kupikia kupungua bei ili kuchochea Matumizi ya Nishati Safi

Joined
Nov 19, 2024
Posts
94
Reaction score
307
Serikali imejikita kuhakikisha inapunguza bei ya mitungi ya gesi ya kupikia na kutoa ruzuku ya asilimia 20 ya mitungi hiyo Ikiwa ni sehemu ya kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia kwa mwaka 2024-2034.

Naibu Waziri wa Nishati Judith Salvio Kapinga amesema hayo bungeni leo Januari 29 wakati akijibu swali la mbunge wa Viti Maalumu Maryam Azan Mwinyi aliyetaka kujua mkakati wa serikali wa kupunguza bei ya gesi ya matumizi ya nyumbani.

gesi.jpg
 
Serikali imejikita kuhakikisha inapunguza bei ya mitungi ya gesi ya kupikia na kutoa ruzuku ya asilimia 20 ya mitungi hiyo Ikiwa ni sehemu ya kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia kwa mwaka 2024-2034.

Naibu Waziri wa Nishati Judith Salvio Kapinga amesema hayo bungeni leo Januari 29 wakati akijibu swali la mbunge wa Viti Maalumu Maryam Azan Mwinyi aliyetaka kujua mkakati wa serikali wa kupunguza bei ya gesi ya matumizi ya nyumbani.

Inapunguza mitungi ya gas au gas yenyewe?
Watu wanamitungi majumbani mwao imekaa tu.
Ingekuwa na maana kama wangepunguza gesi.
Hivyo vimtungi walivyogawa kwa wananchi, wawatembelee sasa waone kama wanavitumia baada ya gas kuisha.
 
Bei ya gesi ndiyo inatakiwa ipungue siyo mitungi,hata mitungi ikipungua bei kama gesi ikiisha unashindwa kujaza gesi nyingine hilo limtungi utalifungia stoo tu!
 
Labda Mtungi mdogo ukiwa aftatu-3000
Unaofatia ukiwa aftisa
Ule mkubwa uwe afkuminatano


Mtungi ukiuzwa aftatu kwa aftisa ndio watu wataacha kutumia mkaa
 
Uwezo wa Waswahili wengi walau iwe elfu tano na Mswahili asihusike kulipia kasha auziwe gesi tu kilnyume na hapo ni blah blah tu na Waswahili wataendelea kukimbilia kuni tu.
 
Uwezo wa Waswahili wengi walau iwe elfu tano na Mswahili asihusike kulipia kasha auziwe gesi tu kilnyume na hapo ni blah blah tu na Waswahili wataendelea kukimbilia kuni tu.
Afu 2 hio 5 umemtwisha mama kuni kichwani lazima aufyeke ule mwembe wake pale shamba achome mkaa
 
Serikali ili kuchochea matumizi ya gesi asilia inakuja na mkakati wa kutoa ruzuku ya 20%.

Watanzania wengi kulingana na kipato chao wanatumia mitumgi midogo ya kg 6 ambayo hujazwa kwa sh. 23000-25000

Hii tafsiri yake ni kwamba mtungi wa kg 6 unaojazwa kwa sh. 24000 wananchi watajaza kwa takribani sh. 20000. Je, hapa wamefanya nini cha maana?

Hiyo ruzuku itatolewa kwa miaka yote ya uhai wa Mtanzania?

Hiyo pesa ya ruzuku ya miaka yote itatoka kwenye mfuko upi?

Nchi jirani wameweza kuuziana gesi kwa bei ndogo zaidi ya Tanzania, je, ruzuku zimetumika huko mpaka wamefikia hatua hiyo?

Serikali inazunguka zunguka haitaki kusema ukweli kuwa tatizo ni kodi.

Kuna kipindi about 8 months ago nilimsikia Rais akiwaomba wafanyabiashara kupunguza bei ya gesi za majumbani.

Rais anaombaje punguzo kwa wafanyabiashara?

Rais ana options 2 tu kupunguza kodi na option ya pili ni kutumia vyombo vya Sheria na usalama kama wafanyabiashara wamekiuka masharti ya vibali vyao.

Nilitarajia serikali iseme inataka kujenga kiwanda cha kuichakata gesi asili au kumleta mwekezaji achakate gesi hapahapa ndani ya nchi.
 
Hii nchi ina viongozi matahira.
Kwanini wasiite mwekezaji achakate gesi ya ndani?
Kwanini serikali isikope posa na kujenga kiwanda cha kuichakata hapa nchini?
Haya mambo ya kutoa ruzuku ni utapeli na upigaji
Askofu gwajima aliwai ongelea hili swala..

Gwajima ni big brain.

SEMA TATIZO NI CCM anatakiwa apatikane mtu Kama JPM ama TUNDU LISU
 
Tanzania ni ya kwanza nafikiri kwa wingi wa watu wa kulalamika Kila sekunde, Kila dakika na Kila saa na kwa Kila jambo.
 
Back
Top Bottom