Benki ya Dunia yaitangaza Tanzania kuingia rasmi katika orodha ya Nchi zilizo katika uchumi wa kati

Benki ya Dunia yaitangaza Tanzania kuingia rasmi katika orodha ya Nchi zilizo katika uchumi wa kati

Tanzania tupo $ 1,063.Bado sana kufikia Uchumi wenyewe wa kati .Uchumi wa kati ule wenyewe unaanzia $4,046
 
Dah! Ahsante, unajua nilikuwa kimya nikitafuta exact figure kwamba ni ngapi hasa! Sasa kama ndo kwanza $1063, an increase to less than $100, basi kwa speed hii tutafika 2030 lakini bado high middle income ikawa mbali sana kwetu kuifikia!!!
You can change your earlier thoughts I presume.
 
Tangu mwaka 2015 adui wa Tanzania ni

1.Chadema
2.Ujinga
3.Maradhi
4.Umasikini

Kikwete ni ccm kama Magufuli na USD80 za Magufuli zimetosha kuwafanya mabeberu waunge mkono juhudi na kuitangaza Tanzania kuwa sasa ina uchumi wa kati.
 
Uchumi wa kati ni kipato cha wastani wa kuanzia dola 1,036 ambayo ni sawa na shs takribani milioni 2,500,000 kwa mwaka.

Mtanzania wa kawaida mnyonge ni kweli anapata kipato kinachofika takribani shilingi 7,000 kwa siku na kwa mwaka shilingi 2,500,000?

Kufika uchumi wa kati unaotangazwa ni kweli ndio hali halisi au makaratasi yanayopelekwa bemki ya dunia yamedanganya?
Unawabishia WB?!
 
Kumbe na wewe mchawi.
Mimi msema ukweli,acheni kudanganya watu. Kwanza ukilinganisha Gain kipindi cha JK ni kubwa kama mara mbili na robo zaidi ya kipindi cha JPM. Tumieni akili sio kupelekwa pelekwa tu.
 
Mimi msema ukweli,acheni kudanganya watu. Kwanza ukilinganisha Gain kipindi cha JK ni kubwa kama mara mbili na robo zaidi ya kipindi cha JPM. Tumieni akili sio kupelekwa pelekwa tu.
Wewe ufipa tulia, Dkt Magufuli kawekeza zaidi kwenye miundombinu likewise JK ila mianya ya rushwa kwa JK ilikuwa mikubwa
 
Watu bado tuna shadadia sana hata hatuendi kwenye ukweli..uchumi wa kati tuliopo ni lower middle ...daraja la chini ...
Hatujafikia nchi kama India na Brazil ...wapo uchumi wa kati lakn daraja la kwanza.
Hivyo tusipojitahdi tunaweza kurudi tena nyuma ....
 
Wewe ufipa tulia, Dkt Magufuli kawekeza zaidi kwenye miundombinu likewise JK ila mianya ya rushwa kwa JK ilikuwa mikubwa
Angalia 2015 hadi 2018
20200701_205026.jpg
 
ELEWENI 2014, GDP per capita ya #Tanzania ilikuwa $ 1,030 IKASHUKA ikawa $947 2015. Leo tunambiwa tuko $1,090. Tumepanda kwa $40 Kwenye miaka 6. Tunashukuru sana Mh. Rais. Tukiendelea hivi 2025 GDP per capita itafika $1,130. Kwa mwendo HUU tutakuwa tajiri baada ya miaka 150.🙏🏾.

Kwa sasa inaonyesha kila mnyonge wa tanzanai ana uhakika wa kupata shilingi 7000 kwa siku a kwa mwezi zaidi ya shilingi 205,000. Katika pato hilo ndio mtanzania huyo alipe kodi, ada, chakula, umeme, maji, afya na nk

Tujitafakari ni kweli?
 
Kufuatia hatua hiyo, Rais Magufuli amepongeza Watanzania wote!

Sijui wapinzani watatokea wapi safari hii
View attachment 1494549
Serikali itazikubali hizi takwimu? Kuna nyakati WB ikitoa takwimu za kuonyesha kuwa ukuaji wa uchumi wa Tanzania umepungua watu wanapinga na kufura kama kifutu! Utakutwa WB wanaitwa majina kama 'mabeberu' na mengine kama hayo! Kama mnakubali takwimu hizi kubalini pia wanaposema yasiyowaoendeza.
 
Ulishaambiwa kati ya watu wakikwambia kitu usiamini wote wapo ccm na kinara ni kiongozi mkuu
 
Sasa angekuwa amevuruga si ingeshuka??ebu acha ujinga na upumbavu
Kwa takwimu hizo, ni ushahidi tosha kwamba JPM amevuruga uchumi, na JK was far better compared to JPM.

Taarifa hiyo ya Benki ya Dunia inasema kwamba:- Kwa maana nyingine, hatimae ndo tumefika kwenye $1036+!!'

Ukiangalia WB Secondary Data, unakutana na hii kitu (GNI per capita by Atlas Method).
View attachment 1494559

Kumbe, 2015 GNI Per Capita by Atlas Method ilikuwa $980. Kwa maana nyingine, kwa miaka 5 mzima, JPM alikuwa anahangaika kuivusha GNI per capita from $980 to $1036... a difference of ONLY $54.

Kinyume chake, GNI Per capita in 2010 ilikuwa kama ifuatavyo:-
View attachment 1494564

Utaona hapo, in 2010 GNI per capita ilikuwa $720, na kwa maana nyingine, GNI per capita ilipanda from $720 in 2010 to $980 in 2015! Yaani ilipanda kwa $260, wakati miaka 5 ya JPM imepanda around $54+!

On top of that, mwaka 2005 GNI per capita ilikuwa $500, na kwa maana nyingine, miaka yake 5 ya kwanza, Mzee wa Msoga alipandisha GNI per capita from $500 in 2005 to $720 in 2010... yaani $220 wakati JPM miaka 5 yake ya kwanza inaonesha kapandisha for less than $100.

View attachment 1494576

Ama kweli mtaji mkubwa JPM ni Jeshi Kubwa la Wajinga lililopo nyuma yake! And JPM anafanikiwa haya kwa sababu ile ile niliyowahi kuitaja siku za nyuma: Tanzania is full of people with average mind, and many more below the average!
 
  • Thanks
Reactions: Oii
Hii ni hatua nzuri, pongezi kwa watanzania na serikali ya awamu ya tano. Watanzania tusibweteke, ni imani yangu serikali itakayoundwa baada ya uchaguzi itakuwa na watu makini sana ambao watakao tusaidia kusonga mbele zaid.
Kitu kinachotukwamisha ni katiba tu. Sio serikari ya awamu ya nne,tano au awamu ya kumi.tatizo ni katiba tu
 
Mheshimiwa Rais na wataalamu wengine wa masuala ya uchumi, kwa niaba ya Watanzania wote tusio elewa nini maana ya nchi kuwa katika UCHUMI WA KATI tunaomba mtufafanulie ili wote twende sawa.

Leo tumeona mheshimiwa akipongeza kuhusu nchi yetu kuingia kwenye UCHUMI WA KATI ila kwa bahati mbaya watanzania tulio wengi hatujui hili linamaana gani.

Hivyo tunaomba ufafanuzi kidogo wa hicho kinacho itwa uchumi wa kati ndio nini na kinafanya nchi yetu kulingana na nchi zipi za mabeberu kiuchumi?

Ni ngumu kumwambia tu mwanachi wa kawaida huko chini kuwa nchi yetu ipo katika UCHUMI WA KATI wakati huo kila kukicha anaona bora ya jana. Pesa mtaani hakuna, maisha magumu, ajira kwa vijana hakuna hata za huko serikalini hazitoki na mambo mengine kama hayo.

Tunaomba ufafanuzi kidogo ili na sisi tuweze kuwaeleza wananchi kuhusu hilo pindi wanapo tuuliza huku mtaani.

Yote kwa yote hongera Tanzania kwa kufikia UCHUMI WA KATI. View attachment 1494732
Mods msiunganishe huu uzi
Rais muongo huyu. Hapa wajinga watajua tumefika level moja na South Africa yenye GDP ya $6,606 wakati sisi tuna $ 1,063.
 
Tatizo lako ulikuwa unalinganisha kwa miaka 5 ya JPM wakati huna figures za 5 years. I am sure figures za 2019 and 2020 zikitoka kutakuwa na mafanikio mazuri Zaidi, usiwe na haraka yoyote yataonekana tu. Kilicho chini ya jua hakijifichi.
Chifu, nimelinganisha data za miaka mitano mitano!

From 2005 to 2010, From 2010 to 2015, from 2015 to 2020. Mbona hujahoji hiyo ya kuanzia 2005?! Btw, hata hiyo miaka 4 ya JPM kuna nini wakati gni ilishuka from $980 to $970?!

Halafu unadai figures za 2019 na 2020 zikitoka kutakuwa na mafanikio mazuri... figures zipi tena! Hebu shusha pumzi kisha tafakari! WB wamesema low middle income inaanzia 1036, lakini 2018 figure ni 1020! Sasa wameiwekaje kwenye low middle income kama figures za 2019 hazijatoka wakati za 2018 zisingeifanya nchi kuwa kwenye Low Middle?!

Na hapa usisahau kwamba tunazungumzia fiscal year.... kwahiyo figures kuanzia July 2020 zitakuwa accounted kwenye next fiscal year. Za 2019 zimeshatoka na ndizo zimeifanya Tz kutoka kwenye 1020 to Low Middle
 
Back
Top Bottom