Bernard Membe, aliyekuwa mgombea Urais kupitia ACT Wazalendo kwenye Uchaguzi 2020, ajiondoa kwenye chama hicho

Hivi tangu lini DGIS Mstaafu akanyea kambi?,
zile story za kumbakumba sijui kitu gani,yalikuwa maigizo tu,au ni secrets codes kwa wanaojua,
Mission zao zinakuwaga tofauti,kubadili upepo,au kujua upepo unaelekea wapi,
Baada ya hapo hata Awards zao wont come to light,
 
Huu ndo Upinzani wa Tanzania na tabia zake;

Kupokea makada wakongwe wa CCM Yani wale wa CCM damudamu
Kisha wanawapa vyeo vya juu ndani ya Chama mfano, wajumbe wa kamati kuu na n.k
Wanawapa nafasi za kugombea nafasi za juu kabisa kama Urais.

2015 ilitokea CDM baada ya Mzee mwenye nywele nyeupe kucheza na Akili zao.
2020 ikatokea kwa ACT wazalendo baada ya Jasusi mbobezi kucheza na Akili zao.
2025 tutegemee kada mwingine kwenda kucheza na Akili za Hawa wapinzani wetu.

Hivi nyie vyama vya Upinzani huwa hata hamjiulizi swali Hili; kwanini makada wakongwe wa chama Cha kijani hujifanya kuhamia kwenu wakati wa harakati za kampeni na Uchaguzi tu?
 
mbona collabo ilipigwa ?
 
Hapa mkiwalaumu wapinzani mtakuwa mnawaonea. Upinzani ndio walimtumia na sio vingine. Chadema hawakushughulika nae na ACT-WAZALENDO wakaamua kumuacha mgombea wao na kum support Lissu waziwazi. Na kwa sababu palikuwa na vyama viwili vya upinzani vyenye nguvu ilikuwa vigumu kukabiliana nao.

Amandla...
 
Upinzani Waligundua kwenye sekeseke lile la Airport,
Maigizo yakaanzia pale,ila ilikuwa too late,
Uzuri walioufanya Walisave vifaranga wachache kuliwa na mwewe,if u what i mean
 
Kiukweli kabisa hili ni Joka tuu la Mdimu, hakuna kitu pale!. Tulimshauri hakusikia...

P
 
Membe mnampa kichwa tu, kamwe hajawahi kuwa tishio. This time upinzani ulijua kuwa accommodate watu wa aina yake bila kuleta madhara. Kilichopelekea wasiungane wala siyo Membe bali ni sheria ya vuama iliyotungwa kimkakati.
 
Bado nangoja bao la dakika ya tisini. Wapinzani walimbwaga siku nyiiingi.
 
Tatizo sio Membe bali uwezo wenu wa kuusoma mchezo wa siasa za bongo. Mnapita mule mule!
vyama ya siasa vipo kwa mujibu wa katiba ambayo ndio inayo inachezewa..... mchezo ni kutoheshimika kwa katiba ya nchi wanaichezea mpaka sikukuu ya Uhuru (tunu ya taifa) inakua anasa na kero.... watoto wetu hawata ihitaji tena kwa hili linaloendelea..... katiba yetu ni mchezo mchafu ndio maana haisomeki
 
Ambaye mpaka sasa amecheza kadi zake vema na mnashindwa kumshitukia ni Mwalim Seif (huyu ni CCM kindakindaki)
 
Ametimiza kazi iliyo mpeleka huko
Kamanda 'iliyompeleka' ni neno moja siyo mawili kama ulivyoandika. Nyie ndio mnaandika 'physio the rapist' badala ya physiotherapist πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…