Twin Tower
JF-Expert Member
- Jan 13, 2023
- 2,170
- 3,067
Hapana, hauko hivyo na huu wako wala sio ushauri mwema kwa Benard Membe iwapo angekuomba umpe ushauri wa afanye nini...Mbona hao maaskofu hawakumshauri wakati anatoa matusi. Membe hakuna kusamehe kazia hapo hapo au maaskofu wako upande wake hawafai kuwa wasuluhishi maana anayesuluhisha hastahili kuwa na upande
To every action there's an equal and opposite reaction....Wanabodi,
Huu ni wito wangu na ushauri wangu wa bure kwa Bernard Membe, asibishane na Maaskofu, amsamehe tuu huyu mwana fani mwenzetu, wakati alipofanya makosa yale, hakuwa yeye, alikuwa ni possessed na demons hivyo kuwa kama kichaa kabisa! ni shetani alikuwa akimiliki na akimtumia!, hivyo baada ya kuombewa, mapepo yamemtoka, ametambua makosa yake, ametubu, ameomba msamaha, as a human being, anastahili msamaha, hivyo natoa wito kwa Bernard Membe, amsamehe tuu mtu huyu, hakujua atendalo!, Ila maadam ameombewa msamaha na Maaskofu, Membe ukikaidi maaskofu...
Mimeandika haya, baada ya kusoma mahali humu kuhusu Tetesi: - Membe awakatalia Kardinali Pengo na Askofu Malasusa kumsamehe Musiba.
Duh..., kama mwandishi huyu, ambaye mimi nilimuona kama ni mwandishi kilaza, kanjanja na kichaa kabisa Kichaa mmoja, anaweweseka sana juu ya Zitto, kamtungia uongo, umebuma, Zitto tuko nae hapa Dodoma, anamiliki mali kama hizo!, then huyu jamaa ni kichwa sana!. Ametuheshimisha sana, hivyo najiunga na Maaskofu, Membe amsamehe tuu!.
Kitendo cha Membe kutowatii maaskofu kitamgharimu sana!. Kuna kiongozi fulani aliwahi kuwadharau maaskofu, najua ni nini kilikuja kumtokea, hivyo sitaki Membe yamkute ya kumkuta!. Amsamehe tuu huyu kichaa, ameishajirudi, akili zimemrudia!, amekubali kosa, ametubu dhambi zake kwa viongozi wake wa dini, wanamuomba Membe amsamehe, Membe asamehe tuu.
Kumuombea msamaha kichaa huyu, hakuna maanishi naunga mkono ule ukichaa wake aliokuwa akiufanya!, no!, namuombea msamaha wa kibinaadamu tuu kwa kutambua udhaifu wa binadamu ni viumbe dhaifu na kuna wakati binadamu tunafanya makosa bila kujijua hivyo kujikuta mtu ametenda kosa bila kujua atendalo.
Kila binadamu anastahili a second chance.
Asamehewe.
Paskali
Sawa tu, atalishwa wala usiwe na wasiwasiNaona ni kama vile Membe yupo katikati, asiposamehe uwezekano wa kulipwa kile kiasi chote cha pesa na Musiba ni mdogo, au awe tayari kulipwa kidogo, unless Membe awe alishafanya uchunguzi juu ya mali anazomiliki Musiba.
Kama Musiba akishindwa kulipa bado itabidi Membe amgaramie Musiba akiwa gerezani, hii yote naiona mitego kwa Membe.
Hapana mkuu kinachompa kiburi Musiba ni hivyo vijisenti vyake sasa dawa ni kuuza hivyo vitegauchumi vyake walau robo tatu akabakiza na robo tu, hapo ndo atatia adabu.Hapana, hauko hivyo na huu wako wala sio ushauri mwema kwa Benard Membe iwapo angekuomba umpe ushauri wa afanye nini...
Ndugu zangu hebu tuelewe kuwa, KUSAMEHE ni tendo la roho (sio la mdomoni) na ni jambo moja (la lazima na muhimu sana) na MTU KUWAJIBIKA KWA MATENDO YAKE iwe ni mazuri au mabaya pamoja na matokeo yake ni jambo jingine kabisa...
Mimi naamini Bernad Membe alishamsamehe Cyprian Musiba na kama ni hivyo, basi huyu (Membe), yeye alishafanya wajibu wake..
Cyprian Musiba kwa upande wake anapaswa kuupokea msamaha huo ili kuiponya roho yake na awajibike kwa matendo yake kwa kulipa fidia ya uharibifu na hasara aliyosababisha kwa watu wengine..
Hata Mungu hutusamehe dhambi lakini haondoi makovu ya matokeo ya matendo na makosa yetu yaliyopita. Tunaishi nayo lakini yakiwa hayana maumivu tena Kwa sbb ya nguvu ya msamaha ule...
Hata Cyprian Musiba anapaswa kufanya Kila analopaswa kufanya kama malipizi ya makosa yake kwa furaha na amani moyoni mwake. Kinyume chake, hataweza kubadilika...!!
Labda tunachoweza kumshauri Bernard Membe ni kukaa na nduguye Cyprian Musiba pamoja ili wajafiliane kupunguza kiwango cha malipizi (faini) ikibidi alipe gharama za kesi tu na mambo yaishie hapo. Na Musiba kama ni mtu wa kujifunza, basi atakuwa amepata fundisho muhimu sana ktk maisha yake...
Paskali kaishakula chake toka kwa MusibaMkuu Paskali
NInaona kama Membe anashinikizwa na siyo kushauriwa kupitia hoja yako.
Unaposema asipowatii maaskofu yatamkuta...... je kusamehe ni Lazima au Hiyari ya mtu?
Marehemu baba yangu alinkusia kuwa, ukipewa ushauri una hiyari ya kuupokea na kuutumia ama kuukataa. Lakini kama ushauri huo unashinikizwa sana uufuate ni wazi kuna mushkeli kwenye ushauri huo....
Naunga mkono mawazo yako, watu kama Musiba ni rahisi sana kuingiza nchi kwenye machafuko sababu ya matumbo yao, Rwanda nao walikuwa hivihivi.Paskali, Paskali, Paskali, nimekuita mara tatu, wewe ni muumini mzuri wa Karma. So let's karma ifanye kazi yake. Mbona leo unakuwa kigeugeu, kwani wakati Musiba anatukana watu vibaya, kuwadhalilisha, kuwatisha vibaya, maaskofu hawakuwepo? au walikuwa wamekufa au walikuwa hawaoni? Kwanini hawakukemea wakati wote ule? Maaskofu nao wanafiki wakubwa, hypocrite, walikuwa wapi Musiba akiiumiza watu? Leo ndio wanaibuka baada ya hukumu? Nikisema hao maskofu nao walikuwa upande wa Musiba nakosea?
Bernard Membe, usimsamehe kabisa kabisa kabisaaaa kabisaaaaaaaaaaaaaaa Musiba, asilani usitoe msamaha, Mungu anaona machungu uliopitia Membe, sbb ya Musiba.
Narudia, BM, shikilia hapo hapoooo never ever ever step back and think of forgiveness.. Acha kabisa, Musiba itakuwa funzo kwa watu wengine na vizazi vijavyo.. Tena afilisiwe kabisa, if possible afungwe maisha ndani akishindwa kulipa. Hawa waandishi uchwara ambao wanaotumika kuumiza watu sana, sasa ni zamu yake Musiba, aonje maumivu, what you do to others, it will always come back to you.. Malipo ni hapa hapa duniani, ya Mbinguni tutayakuta huko mbele. Acheni mambo yenu.
Membe alishapeleka malalamiko yake Mahakamani na Mahakama imekuja kuthibitisha kwamba Musiba ni Mkosaji na anahitaji kulipia gharama.[emoji1752][emoji1752]Mkuu Pascal Mayalla heshima yako?
haina haja ya kumshauri Membe amsamehe Musiba hili liko wazi. Na hao Maaskofu wao ndio unapaswa kuwashauri waiheshimu Mahakama na Wasiifundishe nini cha kufanya, ina maana kila mkosaji mwenye hadhi fulani katika jamii yetu awe anaombewa msamaha? Huku ni kuishusha hadhi Mahakama. Membe alishapeleka malalamiko yake Mahakamani na Mahakama imekuja kuthibitisha kwamba Musiba ni Mkosaji na anahitaji kulipia gharama.
Mkuu Yono tayari wako eneo la tukio kwa utekelezaji wa hukumu hiyoKama mahakama imethibitisha pasipo shaka basi jamaaa ahukumiwe ipasavyo...ili iwe fundisho
Musiba lazima awajibike kwa matendo yake. Yono tutangazieni tarehe ya mnada wa vikorokoro vya cyprian musibaHapana, hauko hivyo na huu wako wala sio ushauri mwema kwa Benard Membe iwapo angekuomba umpe ushauri wa afanye nini...
Ndugu zangu hebu tuelewe kuwa, KUSAMEHE ni tendo la roho (sio la mdomoni) na ni jambo moja (la lazima na muhimu sana) na MTU KUWAJIBIKA KWA MATENDO YAKE iwe ni mazuri au mabaya pamoja na matokeo yake ni jambo jingine kabisa...
Mimi naamini Bernad Membe alishamsamehe Cyprian Musiba na kama ni hivyo, basi huyu (Membe), yeye alishafanya wajibu wake..
Cyprian Musiba kwa upande wake anapaswa kuupokea msamaha huo ili kuiponya roho yake na awajibike kwa matendo yake kwa kulipa fidia ya uharibifu na hasara aliyosababisha kwa watu wengine..
Hata Mungu hutusamehe dhambi lakini haondoi makovu ya matokeo ya matendo na makosa yetu yaliyopita. Tunaishi nayo lakini yakiwa hayana maumivu tena Kwa sbb ya nguvu ya msamaha ule...
Hata Cyprian Musiba anapaswa kufanya Kila analopaswa kufanya kama malipizi ya makosa yake kwa furaha na amani moyoni mwake. Kinyume chake, hataweza kubadilika...!!
Labda tunachoweza kumshauri Bernard Membe ni kukaa na nduguye Cyprian Musiba pamoja ili wajafiliane kupunguza kiwango cha malipizi (faini) ikibidi alipe gharama za kesi tu na mambo yaishie hapo. Na Musiba kama ni mtu wa kujifunza, basi atakuwa amepata fundisho muhimu sana ktk maisha yake...
Yeah hata tukiemdaga kuungama Kuna malipizi yanafanyika.Asante,atumie jukwaa like lile awaombe kusamehewa na wote aliowachonganisha,aliowatukana,aliowadhalilisha na akitoa mimacho vile vile,na huenda akasamehewa na Allah na malipizi yawe ni kulipa defamations zote.
Ona huyu mtoto naye.Mimi nigekuwa Musiba ningemlipa tu Membe halafu tuone kama ndio ataupata Urais.
Maaskofu wa mchongo kipindi cha mwendazake walikua wanakula asali tu.Membe hakuna kusameheMaaskofu gani wa hovyo namna hiyo? Walikuwa wanasapoti tawala dhalimu. Kwani hao maaskofu ni nani mpaka membe lazima awasikilize. Membe mpe fundisho.
NonsenseMkuu,
Membe ni aina ya viongozi wenye 'inferiority complex' ndio udhaifu mkuu anaotumia kutafuta huruma. Kiongozi yeyote mwenye visasi kizazi chake chote hufutika kwa visasi pia.
Ukiangalia kawekeza Mtwara badala ya kuwekeza kwanza kwao Lindi hivyo kuufanya mji wa Lindi kama kijiji cha utalii wa majengo ya kijima kama makuti katikati mji.
Mungu akikuonya usilipize kisasi lakini wewe kama binadamu ukang'ang'ania kwa kiburi chako tu lazima nifanye ninavyotaka mwisho wake sio mzuri. Asifikiri anamkomoa Musiba, anajikomoa mwenyewe na wale wanaomhamasisha kumtenda Musiba siku ikifika watamkana