Azizi Mussa
JF-Expert Member
- May 9, 2012
- 9,186
- 7,492
Sawa mkuuMkuu,
Nakushauri yafuatayo;
Kama una mtaji unaofika 20m, na kuendelea, fungua biashara ya mgahawa wa kisasa, tengeneza chakula kizuri, customer sevice mzuri na usimamizi mzuri. Au kawekeze kwenye ufugaji wa kisasa wa Ng'ombe wa maziwa au mbuzi.
Daladala kwa sasa si biashara salama.
1. Hiace na coater ziko kwenye mchakato wa kuondolewa kwenye ruti nyingi,
2. Faini za barabarani zitakula faida na mtaji
3. Gharama za uendeshaji ni kubwa mno.
4. Risk za kazi ni nyingi sana
5. Madereva watakufanya usiwe na amani katika kipindi chote ambacho unafanya hiyo biashara. Kila simu ikiita moyo utakuwa unaenda mbio.
Nakutakia mafanikio mema ndugu yangu.
Nikweli, ila kuna ile ambayo unaweza icontrol mwenyewe , risk yake ni ndogo, tofauti na ile inayoendeshwa na mtu.Kifupi hakuna biashara isio na changamoto yaani ya mteremko tu,ni sawa na kuwa na uhusiano ulioshwali siku zote,
Ukiwa na mda ukaifanya mwenyewe risk ni ndogo kuliko kumpa MTU akufanyie,Nikweli, ila kuna ile ambayo unaweza icontrol mwenyewe , risk yake ni ndogo, tofauti na ile inayoendeshwa na mtu.
Markach: Ushauri wa bure usifanya biashara ya daladala!!. Mimi nilibahatika kufanya hii biashara miaka ya 1996-1997 na kuna matatizo mawili makubwa (a) Huwezi kupanga bei na bei inapanda polepole kuliko mfumuko wa bei. serikali inapanga bei hivyo ni biashara mbaya sana (2) Huwezi kupanga bei ya mafuta hivyo kama bei ya mafuta ikipanda huwezi kupandisha bei kwasababu bei inapangwa na serikali. Hali hii ilisababisha Isuzu NPR na Costa zishidwe kufanya biashara na hali ya daladala ni ya duni kuliko 1996!!.
Unaweza ukafanya biashara ya tender, fungua kampuni halafu katafute shele zinazohitaji magari halafu ingia mkataba na shule wa kuwapeleka watoto majumbani baada ya shule. Vilevile kama unamagari mazuri peleka card zako balozini ili uweze kuchukuwa wagani mbalimbali wanaokuja na group zinazotoka nje. Hii itakusaidia uhakika wa biashara, kukua kwa biashara na target yako ya watu ni nzuri badala ya kukimbizana na makondakta na matrafiki. Mimi nashauri usiige badilisha kidogo utaona matunda! Huu ni ushauri wangu ndugu
kaka vp?Umuofia kwenu!
Jamani mimi ni employee katika private sector. Katika kufikiria namna ya kujiongezea kipato nimewaza kukopa pesa benki ili niagize hiace na nianze kupiga ruti za Kasulu-kigoma au kasulu-kibondo. Hii Biashara sijawahi kuifanya ila nategemea kuisimamia baada ya kutafuta dereva anayeweza kuaminika.
Ningependa kujua yafuatayo;
1. Hiace aina gani inayofaa?
2. Kwa mazingira ya Kigoma engine gani inafaa? CC zake pia aina ya mafuta (diesel/petrol)
3. Profit margin ya huku ikoje, katika misimu ya mvua na kiangazi?
4. Ningependa kujua pia kuhusu bima ya gari ya Biashara kama hii ya hiace, especially comprehensive/premium ikoje?
5. Kama nimenunua from Japan, gharama ya kuweka viti vya abiria ikoje?
6. Pia ningependa pia kujua chochote kile kinachohusiana na biashara hii kutoka kwa wazoefu/majongwe wa biashara hii.
NB:
Kasulu-kigoma ni 90 km na nauli ni Tsh. 5,000/= na
Kasulu -Kibondo ni 150 km na nauli ni Tsh. 10,000/=.
Barabara zote ni za vumbi na gari linaweza likaenda na kurudi kwa siku bila shida.
Thanks!
Vipi kuhusu noah mimi nataka niingie kwenye business ya noahNami nataka kuhama kutoka kwa noah nihamie kwa hiace
Dumelang