Biashara ya madini ni kichaa. Kaka yangu kapoteza milioni 120 mwezi huu nimemkuta ameshaanza kudata

Biashara ya madini ni kichaa. Kaka yangu kapoteza milioni 120 mwezi huu nimemkuta ameshaanza kudata

Wachimbaji wadogo wengi wanafanya kwa kubahatisha, hawafanyi utafiti.

Madini siyo maharage ambayo unapanda sehemu na kuyaona yanavyokua. Kwenye madini, unatafuta kitu ambacho hukuweka wewe wala rafiki yako. Hivyo hatua ya kwanza ni kufanya utafiti, siyo kuchimba. Unachimba baada ya kufanya utafiti, na kujua yako wapi,, kwa kiwango gani.
Usemalo ni kweli ila utafiti wa madini ni gharama kubwa sana mkuu, ndo maana wachimbaji wadogo wanachimba kimungu mungu tu boss.
 
Ya madini nimeivulia kofia aisee kuanzia leo

Wengi wanaingia with unrealistic expectations wanadhani wataenda leo na kuwa matajiri overnight. Never happening.

120M kwenye madini ni hela ndogo sana itakua alisikiliza wachimbaji wadogo wakamjaza matumaini hewa. Hiyo haikutoi hata kwenye level ya uchimbaji mdogo.

Angeuliza wachimbaji wakongwe hapo Chunya wanafanyaje kazi kabla ya kuingiza hela zake.

Screenshot 2025-03-13 085614.png
 
Aisee naandika huu Uzi nikiwa nimekuja kumtembelea kaka yangu hospital hapa Mbeya, aisee hii biashara sio ya kuingilia kichwa kichwa.

Huwezi amini nipo hospitali maana broo kama akili zishaanza kuwehuka, vitu anavyoongea havieleweki aisee, haamini kama kafukia milioni 120.

Nawashauri ndugu zangu wana jamiiforums hii sio biashara ya kufanya, ni kama inauchawi fulani hivi!
Kuna Mpambanaji Huku,Alikuwa Na Duka kubwa La Madawa,nyumba,na Gari akauza vyote akaenda Mgodini Bahati Mbaya Mtaji wote ukakata Mgodini Saivi yupo tu Anajipanga upya
 
Bro wako sio mvumilivu kwenye haya maisha. Nilishawahi poteza 270m, ni kweli iliniuma sana. Nilitulia kiume nikaendelea na maisha.

Nilishasahau na kutengeneza zaidi ya hiyo
Pole,mioyo hutofautiana, wataalamu wa Tabia wanajua hayo kwa ufupi kuna sanguine, melancholy,nk ukizujua Tabia hizi hutosumbuka, Wewe utakuwa sanguine Hawa kwa ufupi hawajali matokeo!
 
hatare sana ndo mambo ya kuchukua risk hayo, kuna kupata na kukosa, ukiwaza kupata tu kisha ukakosa lazima dishi licheze kidogo.

Kuna raia alipoteza mil30 kwenye dhahabu akajifungia ndani miezi sita, huyu wa mil120 simpatii picha
Kapotezaje

Ova
 
Kwahiyo Geita Gold na Barrick nao utumia ulozi??
Bro Biashara ya Madini Matambiko ni lazima Alafu usichokijua Wazungu na Wahindi Ni watu noma Sana Kwenye Hizo mambo".

Ndio maana Hata uwe kigagula kiasi gani Huwezi kuiba benki,au kuiba Madini Mgodini".
 
Akirudia tena atapata mzigo wa maana, dhahabu ndio ilivyo..Ukiwa na moyo mwepesi unafirisika jumla.
 
Tatizo kukosa mahesabu ya elimu ya uchimbaji wa madini pamoja na kuchimba kwa kutegemea mikono ya binadamu!
 
Aisee naandika huu Uzi nikiwa nimekuja kumtembelea kaka yangu hospital hapa Mbeya, aisee hii biashara sio ya kuingilia kichwa kichwa.

Huwezi amini nipo hospitali maana broo kama akili zishaanza kuwehuka, vitu anavyoongea havieleweki aisee, haamini kama kafukia milioni 120.

Nawashauri ndugu zangu wana jamiiforums hii sio biashara ya kufanya, ni kama inauchawi fulani hivi!
Ni bora kubet m 120 angekuwa naweka m1 mechi za Simba au yanga asingekuwa chizi
 
Back
Top Bottom