Biashara ya mashine ya kusaga na kukoboa nafaka- Fahamu bei zake, uendeshaji wa biashara hii pamoja na faida na hasara zake

Biashara ya mashine ya kusaga na kukoboa nafaka- Fahamu bei zake, uendeshaji wa biashara hii pamoja na faida na hasara zake

Asante nashukuru sana ninaomba unisaidie kwenye mahitaji ya vibali je nako ni leseni ya biashara na tin number au mpaka uwe umefungua kampuni? na je hiyo mota ina maana kama unasaga huwezi kukoboa? NILIWAHI ULIZIA SABA SABA niliambiwa kinu cha kusaga milion mbili na cha kukoboa ilikuwa tatu HAPO SIJAJUA MOTA IPO NJE AU naomba msaada wako mkuu au hata ushauri cost za kuiset mpaka mashine ianze kufanya kazi

Ndio kuitumia kwa muundo niliwekwa Mimi unafanya one thing at a time lakini kumbuka mota ya kusaga ni kubwa kuliko ile ya kukoboa

Bei hizo ziko juu sana lakini haswa tumia za Sido kwa vinu mota ndo uingoe Dukani

sijajua unataka gharama za mashine yenye nini na nini. Kuna umeme hapo? 3Phase? Ongezea nyama nikuelewe mkuu
 
Hakikisha unakuwa na soko la uhakika. Na ikiwezekana muajiri mtu wa 'marketing' kazi yake ni kila siku akuletee mteja wa uhakika wa bidhaa zako.

Hakikisha una 'maintain' ubora wa bidhaa zako, ikiwa ni kupokea 'customers feedback' juu ya kile unachozalisha. Hakikisha na usafi pia.

Hakikisha unakuwa na varieties za bidhaa unazozalisha, usiishie kwenye sembe tu, unaweza kuongeza dona, unga wa dengu, ung wa mihogo, mahindi ya kukoboa nk.

Hakikisha pia unapanua soko nje ya mkoa. Huko ndiko biashara yako inakuwa na kujulikana.


Asante mkuu. Kwa sasa ntaanza na sembe na Dona. Ila business plan yangu ya kukuza nataka niwe natengeneza dona sembe na muhogo ndani ya 3years.Kuna masoko flani nafukuzia nchini India ya muhogo. Tuombeane
 
mkuu siku nyingine, kabla y kuweka uzi, jaribu kutafuta kwanza nyuz za nyuma, utapata watu wameshajadili hayo mambo. so usiwe na akiri kama za ccm

kwi!kwi!kwi!kwi!kwi!!,Wewe inaonyesha ni Mh.Ukawa.Mbona unaichukia hivyo CCM?,Vipi walikuchikulia demu nini???.
 
Mkuu mashine ya kusaga na kukoboa sijaagiza kutoka nje. Hii niliinunua kutoka kwa mstaafu mmoja wa Relwe(TRC) mwaka 2010 nikiwa chuo. Nilinunua kinu cha kukoboa na kinu cha kusaga na mota moja niliyoifunga katikati kwa vinu vyote. Mota yangu ni ya 20hp nilinunua kwa sh.700,000.Hivyo vitu vingine nilinunua kwa milion 2 wakat huo.

Kwa sasa niliagiza mashine ya kupima uzito,kujaza na kufunga mifuko(VFFS) kutoka China. Hii ilinicost mil 4.5 mpk kufika Bongo.Hapo ondoa gharama za shipping kwakua nilipakia katika kontena la mtu.

Natumai nimekujibu.

Mkuu hyo mashine ya VFFS inauwezo wa kufunga mifuko mingapi kwa siku, (kufunga,kujaza, na kupima inafanya kazi kwa wakati Mmoja?
 
Ndio kuitumia kwa muundo niliwekwa Mimi unafanya one thing at a time lakini kumbuka mota ya kusaga ni kubwa kuliko ile ya kukoboa

Bei hizo ziko juu sana lakini haswa tumia za Sido kwa vinu mota ndo uingoe Dukani

sijajua unataka gharama za mashine yenye nini na nini. Kuna umeme hapo? 3Phase? Ongezea nyama nikuelewe mkuu


oh asnte mkuu ngoja nitalifanyia kazi USISITE KUTUVUMILIA TUNAPOKUULIZA MASWALI ZAIDI
 
Ndio kuitumia kwa muundo niliwekwa Mimi unafanya one thing at a time lakini kumbuka mota ya kusaga ni kubwa kuliko ile ya kukoboa

Bei hizo ziko juu sana lakini haswa tumia za Sido kwa vinu mota ndo uingoe Dukani

sijajua unataka gharama za mashine yenye nini na nini. Kuna umeme hapo? 3Phase? Ongezea nyama nikuelewe mkuu

KUHUSU VINU NIMEKUELEWA ASANTE MKUU MIMI NILITAKA HAPO KWENYE MOTA mfano ya 20hpdukani ni 1.2million je nikiwa na vinu vya kukoboa na kusaga utatumia mota moja au mpaka ziwe mbili na ikiwa moja utakuwa unasubiri kusagisha kwanza ndipo uanze kukoboa au unaweza fanya vyote kwa pamoja PIA JE KUSUKA UMEME INAWEZA COST BEI GANI HASA gharama za nyaya
 
Mi nakushauri tembelea hata kiwanda cha kusaga unga cha bakhresa(azam) kuna vitu utapata.

Hili wazo zuri lakini kabla hujafika kwa hao wakubwa fuata kwanza wazalishaji wa mkoani mwako au kwa dar mmoja yupo pale bunju chapa ya unga ni bora nadhani
 
Kama nijuavyo unapoweka unga kwenye mifuko huwa inachukua miezi michache kuharibika tofauti na makampuni makubwa ambapo unga unakaa hata mwaka bila kuharibika
Sasa we utatumia nini kukausha huo unga ili usiwe na moisture?
 
Mimi kwa kuongezea, ningeshauri ufikirie yafuatayo pia kadri biashara itakavyokuwa:
1. Kupata mashine / teknolojia nyepesi ya kukausha pumba. Uzalishaji ukiwa mkubwa ni dhahiri ukaushaji pumba huenda ukakusumbua kutokana na ufinyu wa nafasi ya kuanika au vipindi vya mvua. Hivyo, kuwa na njia ya kukausha pumba kutasaidia pumba kutokuoza au kuungua. Kumbuka, mauzo ya pumba yanasaidia sana kucover gharama za uendeshaji mfano umeme, vibarua, kodi (kama zipo) n.k

2. Fikiria pia kuwa na product ya dona (iliyofungashwa) ili kupata soko la walaji wa dona.

3. Pia, fikiria kuanzisha uongezaji wa virutubishi (zinc, vitamin A, B12 nk) kwenye unga wako wa sembe ili kuufanya kuwa wenye lishe zaidi. Hii kuna kipindi TFDA walitaka kuifanya iwe lazima (sijui iliendaje). Pia, kwa wazalishaji wakubwa wa unga wa ngano nafikiri ni lazima sasa kuongeza virutubishi (tazama mifuko yao utaona "fortified". Kumbuka, utapiamlo ni janga la kitaifa.

Embu ngoja nipate kahawa kidogo labda nitapata vingine vya kuongeza.
 
endelea.mimi niko dodoma nafanya ufugaji.washindani ni wachache ivyo soko linaruhusu ila zingatia zaidi ubora wa bidhaa na huduma na muda.Taasisi za kukopesha pia ni nyingi hata hapa dodoma zipo.mimi pia ninampango wakuamia kwenye kilimo cha biashara soon.
-- ushauri usibase kwenye huduma 1 au biashara 1 tu na hasa kwa mikoa yenye uchumi mdogo na unaoibukia.kimbia na muda tafuta mikopo anza kukamua ba alizeti au wekeza na kwenye biashara nyingine.mikoa kama hii ndo rahisi sana kutusua kwa uwekezaji wakati na mkubwa.
 
Hongera sana, Kuna mtu ameshauri hapo kuhusu kuwa na mtu wa Marketing. Napenda pia kushauri kuwa na watu wa marketing kwa kila mkoa kwa kuanzia angalau DSM, PWANI, sijajua kwa huko mikoani..

Ambao kila kwanza utawapa jukumu la kutengeneza Market Plan iliyoshiba kwa kuelezea na vitendo kuanza haraka juu ya vyanzo vya masoko. Kwa DSM waanze negotiations na shule ya Private, Cafterias za vyuoni mf. DUCE, UDSM, ARDHI, IFM, CBE, DIT, ST JOSEPH, TIA, ST MARK'S, MNMU nk.

Pia kufungua ofisi mbalimbali kwa kila maeneo yenye hizo nafaka. mf. Mbagala, Tabata, Buguruni, Gongolamboto, Temeke, Kigamboni, Mbezi, Kimara, Mwenge, Makumbusho, Magomeni, n.k. Promotion katika vyombo vya habari, kutafuta airtime za mahojiano na TV's au Redio.

Lakini mwisho wa siku kumbuka kutembelea VITUO VYA WATOTO YATIMA angalau kuwapa hizo nafaka. Kumbuka pia promotion nyakati za sikukuu. ALL THE BEST.
 
Habari za jioni wakuu

Ninaombeni mawazo yenu. Niko kwenye mchakato wa kuanzisha kiwanda rasmi cha kusaga na kufungangasha unga wa nafaka mbalimbali. Nina mashine ya kusaga mahindi mkoani Dodoma na nilikua nafunga na kuuza unga kienyeji vijijini. Sasa nimeamua kuifanya iwe rasmi kabisa na Mungu akisaidia January 2016 bidhaa zangu zitakua sokoni. Niliyofanya mpaka sasa?
1. Mashine ya kukoboa na kusaga
Tayari ninayo na inatoa huduma

2. Mashine ya kupima, kufungasha na kufunga niliagiza kutoka China na iko kwenye hatua za mwisho za kuwa installed

3.Nimeshaanza mchakato wa kupata vifungashio kwenye kiwanda kimoja Bagamoyo. Mifuko ya kilo 5, 10 na 25 yenye nembo.

4.Stock ya mahindi ninayo karibia tani 10

5.Niko kwenye hatua za mwisho za kupata kibali cha tbs.

Kwa wazoefu wa biashara hii naomba kama kuna mwenye mchango wa ziada tushauriane mpaka hapo nilipofikia. Na kama kuna kitu kingine chochote kinahitajika.Tunaweza wasiliana hapa kwa michango au anymore business ideas/patnership na masoko zaidi.Au hata kwa PM

Shukran.
Mjasiriamali
Kaka Hiyo n hatua moja nzur sana ktk maendeleo mm nlikua na idea Hiyo nlikua cjui naanzia wap Leo nmepata mwelekeo itakua vzur kama Nkipata mawasiliano yako
 
Hi mwana ifm naomba nije kwako unipe mwongozo mi nimemaliza banda na machine zipo ila sijui pa kununua mahindi lakin pi a na Fundi wa umeme.. 0784800989
 
Tunashukiru kwa kutujuza wengine tunajifunza biashara ya nafaka
 
Back
Top Bottom