Biashara ya Mbao na Miti: Fahamu Uendeshaji, Faida na Changamoto zake

Biashara ya Mbao na Miti: Fahamu Uendeshaji, Faida na Changamoto zake

Funguka mkuu hueleweki au mgeni jukwaani?.watu tunajifunza kitu hapa kama unasema amesema uongo ukweli wako ni upi sasa? ferre tunahitaji mengi kutoka kwako mkuu
Mimi ni mgeni? Umeangalia post zangu na date au unapayuka tu....

Uko sahihi by the way. Mm ni mgeni.
 
Hongera kwa uthubutu,biashara ya mbao ni nzuri sana na ina faida nzuri endapo utaisimamia na kuikubali na kuvumilia.

Mambo ya kuzingatia.

1. Unatakiwa uwe na usajiri(registration) wa kufanya biashara ya mbao hii utaipata ofisi ya misitu ya manispaa uliko japo kua ni shida sana kupata usajiri (naskia imekua deligated to ofisi za misitu za wilaya) usajiri huu ndio utakao kuwezesha kutambulika na serikali km ume ruhusiwa kununua na kuuza mbao pia usajiri ndio utautumia kukata kibari cha kusafirishia mzigo (T.P)

2. Kwa upande wa mtaji inategemea na malengo yako kama.

i} Nataka kununua miti kuchana na kusafirisha mbao mwenyewe au unataka kununua mbao tu kisha una safirisha

ii} Unataka utoe magari mangapi ya mbao kwa wiki/mwezi

iii} usafiri utakao utumia kusafirishia mzigo ni fuso au semi? maana bei ya fuso iko chini zaid ya semi lakini semi inabeba mzigo mkubwa kuanzia pieces 1000-1500 kulingana na size ya mbao.na fuso inabeba pieces 300-400 kulingana na size ya mbao.

*Mbao zina tofautiana kiwango cha bei kulingana na aina ya mti ila kwa iringa(sina uzoefu nako) miti mingi ni pine.kwa ufupi ni kwamba mtaji usiwe chini ya 4 kwa kuanziA.

3. Mbao inauzwa kwa futi au mita,bei ina tofautiana kulingana na size e.g 1x10 ina bei yake,1x8 ina bei yake, 2x6 ina bei yake, 2x4 ina bei yake.kwa hiyo una takiwa uwe makini na vipimo wakati wa kuchana, kununua, na kuuza epuka sana kuchaniwa mbao ambazo ni under size mfano mbao ya 1x10 wakati wa kupima ikawa 1x9 hiyo tayari ni hasara kwa sababu ukienda kuuza bei itapungua.

Eneo hili la vipimbo ndipo panapo umiza I mean hasara na faida ya mbao ipo kwenye vipimo kwa hiyo unapo peleka mzigo sokoni uwe mjanja na makini sna kwenye vipimo ukienda kichwa kichwa unaibiwa bila kujua.

4. Soko la mbao upatikanaji wake ni mgumu kidogo hasa kwa wageni wa hii biashara kwa sababu biashara hii ni ya kimtandao zaidi na mara nyingi wanunuzi wa mbao wana agiza mzigo kwa order hivyo ni juhudi zako binafsi kutafuta wateja na kuuza mbao zako kwa bei ya ushindani, kwa dar mbao zinauzwa tegeta na biguruni.

5. Epuka kununua /kuchana mbao za mti pori kama hauna kibari maalumu hii ni hatari sana kwa mtaji wako na maisha yako serikali iko macho sana japo kua wajanja/wazoefu wanajua wanafanyaje kusafirisha mzigo wa mbao za asili ila ukidakwa ukashindwa kuwatuliza wahusika unataifishiwa mzigo wako na jela juu. Pia zingatia muda wa kusafirishwa mbao ni kuanzia saa 12 asubuhi mpaka 12 jioni zaidi ya hapo ni kujitaftia matatizo.

6. Mbao zina lipiwa ushuru kila mbao ni shilingi 100.

7. Gharama za mbao ni
Hela ya kununulia mti (kama utachana mwenyewe)
Kumlipa fundi wa kuchana mbao,(kama utachana mwenyewe)
Wabebaji na ushuru na kulipia gari

Changamoto kubwa ya biashra ya mbao ni pamoja na

1. Kucheleweshwa kupata hela yako kwa wakati hapa nina maana kwamba unaweza kupeleka mbao sokoni ila unae muuzia asiwe na hela cash aka kuahidi kukulipa hela yako siku fulani but na asikupe hiyo siku husika (kutapeliwa kuna anzia hapa)

2. Mafundi wa mbao kukosa uaminifu na pia wanaweza wasikuchanie mbao kwa wakati kutokana na sababu mbalimbali kama una hasira unaweza kukorofishana na watu wengi sna cha msingi ni uvumilivu tu.

Naamini nime eleza mengi muhimu ambavyo ni msaada tosha kwa kuanzia biashara.

kila la heri.

Chinga One.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Chinga One umeeleza yote tena kwa ufasaha kabisa, bila shaka mleta mada na wadau wengine watashiba maelezo yako. Binafsi nishawahi kujichanganya kwenye biashara hii changamoto ulizoeleza zote nilikumbana nazo at par! mimi nilielewana na mafundi wanichanie mbao za mininga maji n.k aisee walichukua muda mwingi sana kukamilisha mzigo na nyingi zilikuwa undersize, soko lilikuwa bovu sana na licha ya hivyo nilizungushwa malipo mpaka tukazinguana na jamaa mwisho wa siku nilivyozidi kumdai msambaa yule alinipiga na zinga la jiwe kichwani! dah masikini ya Mungu Mpaka Leo Hii Ninakovu kichwani kwajili ya mbao zile!

Naungana na mkuu Safari_ni_Safari kwamba uselemala na biashara ya mbao ni shughuri zilizolaaniwa!
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Chinga One umeeleza yote tena kwa ufasaha kabisa, bila shaka mleta mada na wadau wengine watashiba maelezo yako. Binafsi nishawahi kujichanganya kwenye biashara hii changamoto ulizoeleza zote nilikumbana nazo at par! mimi nilielewana na mafundi wanichanie mbao za mininga maji n.k aisee walichukua muda mwingi sana kukamilisha mzigo na nyingi zilikuwa undersize, soko lilikuwa bovu sana na licha ya hivyo nilizungushwa malipo mpaka tukazinguana na jamaa mwisho wa siku nilivyozidi kumdai msambaa yule alinipiga na zinga la jiwe kichwani! dah masikini ya Mungu Mpaka Leo Hii Ninakovu kichwani kwajili ya mbao zile!!
Naungana na mkuu Safari_ni_Safari kwamba uselemala na biashara ya mbao ni shughuri zilizolaaniwa!

Mkuu pole sana,biashara hii unaweza kuloga hivi hivi mtu ana kaa na hela yako miezi mitatu unategemea nini hapo kama sio kutapeliwa tu.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu pole sana,biashara hii unaweza kuloga hivi hivi mtu ana kaa na hela yako miezi mitatu unategemea nini hapo kama sio kutapeliwa tu.

Asante sana mkuu. Kuna mengi sana nimejifunza kwenye hizi purukushani za kusaka tonge huku uraiani, over 95% ya unaodeal nao ktk kila issue ni shule ndogo na ustaarabu kwao sio ishu. Usipokuwa makini watakukamua mpaka tone la mwisho.

Ndo hivyo tena vijana wa bongo tunakomaa kama watoto wa bata n dats why inachua muda sana kuyaona mafanikio.
 
Niko kwenye hii biashara mwaka wa pili sasa mkuu Chinga One ume maliza kila kitu!Cha kuongezea tu hii biashara ina matapeli wengi sana ni bora biashara ya nguzo za umeme!
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Chinga one nimekuelewa hakika changamoto ni kubwa my interest ni kununua mbao, sio kuchana maana zinahitaji usimamizi sana wasikupige na sumbufu nyingine nyingi.
 
Niko kwenye hii biashara mwaka wa pili sasa mkuu Chinga One ume maliza kila kitu!Cha kuongezea tu hii biashara ina matapeli wengi sana ni bora biashara ya nguzo za umeme!

Mkuu...naww unaweza kufunguka zaidi khs hiyo Biashara ya NGUZO? karibu sana....
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Malila nime ku PM naomba mniunge katika kupata mashamba ya miti ya mbao maeneo mliyokua nayo na mimi niwekeze.

Asante sana mkuu
 
Wakuu bado tunaendelea kupokea ODA zenu! Kumbuka, hatuuzi magogo. Ni mbao zenye ukubwa(size) wa
(i) Inch 1 kwa inch 8 (1*8), urefu wa futi 10 (Mita 3)
(ii) Inch 2 kwa inch 6 (2*6), urefu wa futi 10 (Mita 3)
(iii) Inch 2 kwa inch 5 (2*5), urefu wa futi 10 (Mita 3)
(iv) Inch 1 kwa inch 5 (1*5), urefu wa futi 10 (Mita 3), n.k

Mbao ni za aina mbalimbali, kulingana na mahitaji yako!

NB: Kwa wale msiopenda usumbufu wa kusafiri hadi kufika katika ofisi yetu, wilaya ya Urambo, mkoa wa Tabora. Mnaweza kututumia barua pepe zenu (e-mail), kupitia namba zetu za simu ama barua pepe zetu;

Simu: 0784 324 102 / 0755 732 981 / 0784 667 480

Barua pepe: info@mihambos.com / sales@mihambos.com

Na tutakutumia MKATABA WA MAUZO/ MANUNUZI mara moja, ili taratibu nyinginezo ziweze kuendelea!


Karibuni sana.
 
KVM vp mrejesho wa hii kitu. Tushirikishe maendeleo yake kaka, wengine ndo tunataka kuanze
 
Katika mkoa wa iringa mbao zinapatika mafinga;makambako na njombe ambayo sasa ni mkoa;kila size ya mbao ipo ni wewe tu;mzigo wa kujaza gari kubwa yaan semi trailer unagarimu takriban milion 16;na mzigo wa kawaida ni milion kumi;kwasasa masoko mazuri ya mbao yanapatikana mwanza na dodoma;dsm yapo ila kwa unayeanza siyo mazuri sana;kwahiyo kama una mtaji ni vyema uanze kutafuta masoko kisha uanze kununua na kuuza:
Asantee sana kwa kunipa mwanga mzuri. Nilipenda sana niaze kufanya biashara iyo ya mbao. sasa kwa mtaji wa milioni kumi. Naweza kuazia wapiii. Yaani kupakiaa mzigo na kwendaa kufanyia biashARA. Kwa mtaji wa milion kumi.
 
Mwenye uelewa juu ya biashara ya mbao anisaidie. Nafikiria kufanya biashara hii, nataka kujua faida na changamoto zake, pia minimum capital ni kiasi gani?
 
Mwenye uelewa juu ya biashara ya mbao anisaidie. Nafikiria kufanya biashara hii, nataka kujua faida na changamoto zake, pia minimum capital ni kiasi gani?

Mimi nina uzoefu wa miaka 15 katika biashara ya mbao.

1435042295309.jpg
 
Back
Top Bottom