Biashara ya Mbao na Miti: Fahamu Uendeshaji, Faida na Changamoto zake

Biashara ya Mbao na Miti: Fahamu Uendeshaji, Faida na Changamoto zake

Ndugu, nitakusaidia kukutafutia miti. Ukishapewa ABC na wataalamu ni PM nikufanikishie.
 
JamiiForums katika ubora wake! Katika biashara au uwekezaji wa muda mrefu huu unalipa! nimeona hadi hapa mafinga Wakenya wananunua ardh na kupanda miti Wabongo 2melala 2.
 
Naombeni ufafanuzi kuhusu kodi inayotakiwa kulipwa TRA. Nijuavyo kama ni misitu ya asili kila cubic meter unalipia kama 205,000. Je bado kuna kodi nyingine y a kulipa TRA?
 
KVM vp mrejesho wa hii kitu. Tushirikishe maendeleo yake kaka, wengine ndo tunataka kuanze

Samahani bwana nilikuwa nimesafiri kidogo.

Lakini maendeleo ni mazuri kutosha. Kumbuka tu kwamba mimi nilianza kitambo kidogo na miti yangu mingine naweza
kuipasua muda wowote ule. Nataka kuanza upasuaji rasmi ndani ya miaka miwili ijayo.

Hata hivyo miti ipo kwenye stage mbalimbali kama picha hapo chini zinavyoonyesha.

Kitu cha kufarijika ni kuwa kumekuwepo na muamko mkubwa sana wa upandaji miti. Sasa hivi ukitoka Njombe mjini kuelekea Songea ni takribani kilomita zaidi ya mia moja unachoona ni mashamba ya miti tu kulia na kushoto.

DSC_0583.JPG

DSC_0677.JPG


DSC_0699.JPG

DSC_0769.JPGDSC_0667.JPG

DSC_0710.JPGDSC_0798.JPG
 
Nani anaweza kuandika business plan nzuri kwa ajili ya biashara hii ya miti ili tuweze kumiliki shamba kubwa na kuweza kuvutia wawekezaji?

Kuliko small scale farming ambao wengi wetu tunaifanya

Nawasilisha
 
nani anaweza kuandika business plan nzuri kwa ajili ya biashara hii ya miti ili tuweze kumiliki shamba kubwa na kuweza kuvutia wawekezaji?

Kuliko small scale farming ambao wengi wetu tunaifanya

nawasilisha

Nadhani business plans nzuri za miradi ya kilimo zinaweza kutengenezwa na watu waliomaliza SUA (Agricultural Economics).

Hata hivyo mimi napenda kuwahamasisha zaidi wapandaji wadogo wadogo hasa wa kule vijijini. Wengi wao wana uwezo wa kupanda ekari chache (ekari mbi, tano hadi kumi) lakini impact yake kwenye kijiji walimo inakuwa kubwa sana sana hasa kama kila mwanakijiji atapanda hiyo miti. Hicho ndicho unachokiona kwenye barabara za kutoka Njombe kwenda Songea, Njombe kwenda Makete, na Njombe kwenda Lupembe.
 
Mimi nigependa kuwahamasisha wanJF kupanda miti ya mbao hasa mbao nyeupe (pines and cypress). Miti hii inasitawi sana sehemu za nyanda za juu kusini.

Mimi nilianza kupanda miti hii kama miaka kumi iliyopita. Nimepanda miti mingi kila mwaka bila kukosa. Kwa sasa ninazo ekari nyingi za miti hii. Vile vile miaka ya karibuni nimepanda eucalyptus.

Wakati naanza kupanda miti mche mmoja nilikuwa nanunua kwa Shs 50 na kuupanda kwa Shs 20. Kwa vile napanda miti mingi (zaidi ya laki moja kwa mwaka) baadaye niliamua kuotesha miche mimi mwenyewe ili kupunguza gharama.

Gharama zaidi ya miche na upandaji ni barabara za moto kuzunguka msitu. Hata hivyo nilinunua ngómbe na kuwaweka kwenye shamba ili wale majani yanayozunguka msitu. Wamenisaidia sana.

Unaweza kupanda miti kidogo kidogo kila mwaka kutumia mshahara wako kama nilivyofanya mimi. Baada ya miaka kadhaa utakuwa na miti mingi na utaweza kuwa unauza miti au kupasua mbao kila mwaka.

Hongera sana mkuu!!,muda si mrefu utakuwa bonge la millionea.
 
Jamii forums katika ubora wake! Katika biashara au uwekezaji wa muda mrefu huu unalipa! nimeona hadi hapa mafinga wakenye wananunua ardh na kupanda miti wabongo 2melala 2,

Mkuu sisi wabongo tumelala kisawasawa!!,ngoja Wakenya watuzidi.
 
Nadhani business plans nzuri za miradi ya kilimo zinaweza kutengenezwa na watu waliomaliza SUA (Agricultural Economics).

Hata hivyo mimi napenda kuwahamasisha zaidi wapandaji wadogo wadogo hasa wa kule vijijini. Wengi wao wana uwezo wa kupanda ekari chache (ekari mbi, tano hadi kumi) lakini impact yake kwenye kijiji walimo inakuwa kubwa sana sana hasa kama kila mwanakijiji atapanda hiyo miti. Hicho ndicho unachokiona kwenye barabara za kutoka Njombe kwenda Songea, Njombe kwenda Makete, na Njombe kwenda Lupembe.

Kweli mkuu!,upo Njombe mkuu?
 
Nadhani business plans nzuri za miradi ya kilimo zinaweza kutengenezwa na watu waliomaliza SUA (Agricultural Economics).

Hata hivyo mimi napenda kuwahamasisha zaidi wapandaji wadogo wadogo hasa wa kule vijijini. Wengi wao wana uwezo wa kupanda ekari chache (ekari mbi, tano hadi kumi) lakini impact yake kwenye kijiji walimo inakuwa kubwa sana sana hasa kama kila mwanakijiji atapanda hiyo miti. Hicho ndicho unachokiona kwenye barabara za kutoka Njombe kwenda Songea, Njombe kwenda Makete, na Njombe kwenda Lupembe.

Naungana na KVM, wawekezaji wakubwa kwenye misitu wanatosha walioko Mufindi/Kilolo na kwingineko. Ningekuwa na uwezo ningeandika bango pale mwanzoni mwa mkoa wa Njombe ukitoka Iringa, lingesomeka hivi " WAWEKEZAJI KWENYE MISITU TOKA NJE YA TANZANIA WASIJE MKOA WA NJOMBE,MBEYA,RUVUMA NA RUKWA" yaani waishie huko huko kwa wenzetu, hivi hata kazi ya kuotesha miti tunahitaji wawekezaji? watalaam tunao,mbegu tunazo,mvua tunayo,ardhi tunayo, manpower tunayo, soko la ndani tunalo.

Ukitaka kuona impact ya small scale ya misitu ktk jamii nenda Makete, wilaya nzima wananchi waliotesha miti zamani, unakuta kibabu kina vimilioni kadhaa ndani, nyumba nzuri na sasa umeme unasogezwa, mambo yatakuwa vizuri.

Nadhani sisi kama Watz kwa sasa, tuanze kujadiliana namna bora ya kusindika mazao ya misitu hii ili tuongeze thamani. Juzi nimekutana na Wachina kule Mapanda Mufindi wanatafuta miti ya kununua kwa ajili ya fenicha Dodoma, nikahuzunika sana, ila tutafika siku moja.
 
  • Thanks
Reactions: KVM
Wewe upo kijiji gani mkuu?

Ardhi ya kupanda miti kama pines bado ni nyingi sana hasa kwenye karibu ya mkoa wote wa Njombe has kwenye wilaya za Njombe, Ludewa na Makete. Nadhani kuna sehemu za mkoa wa Rukwa na mbeya miti hii hustawi vizuri pia.

Mimi nawatia moyo nyote ambao mnataka kupanda miti kufanya hivyo. siyo lazima uwe na kipato kikubwa sana. Huu ni mradi mzuri kwa wafanyakazi. Mimi nimepanda miti kutumia mshahara wangu tu. Tunaweza kupishana kipato lakini panda angalau eka 10 au 20 kwa mwaka. Ni gharama ndogo tu. Hata mimi mshahara wangu siyo mkubwa sana lakini kwa uvumilivu sana nimeweza kupanda miti ya kutosha.

Kazi ya kupanda inafanyika mwezi wa 12 kwa mikoa ya kusini. Ukishapanda huo mti unasubiri miaka ya kustaafu basi unaanza kuvuna. Ni kiunua mgongo kizuri kwa wafanyakazi. Lakini ukiwa kijana bado ni kipato tosha na cha uhakika kwa kila mwaka. Mbao za Tanzania zinauzwa Kenya, Uganda, South Sudan, Somalia na Uarabuni. Kwa sasa hivi mbao za Tanzania hazitoshi kwa hiyo wapasuaji wanakwenda mpaka Malawi kununua miti huko.

Uzuri mwingine wa kupanda mti ni kuwa unawatia hamasa wenyeji wa eneo utakalopanda miti. Wakati naanza kupanda miti pale kijijini nilikuwa karibu peke yangu tu. Baada ya kuwashauri wanakijiji nao kufanya kile nilichokuwa nafanya nao wakaanza kupanda miti. Leo hii kijiji kimezungukwa na mashamba mengi ya miti ya wanakijiji. Baada ya miaka mitano uchumi wa kile kijiji utapaa sana kwani nitakuwepo kuhakikisha hawalaliwi na walanguzi wa miti.
 
Nipo Wino - Mpakani mwa Ruvuma na Njombe upande wa Ruvuma
 
Mimi nigependa kuwahamasisha wanJF kupanda miti ya mbao hasa mbao nyeupe (pines and cypress). Miti hii inasitawi sana sehemu za nyanda za juu kusini.

Mimi nilianza kupanda miti hii kama miaka kumi iliyopita. Nimepanda miti mingi kila mwaka bila kukosa. Kwa sasa ninazo ekari nyingi za miti hii. Vile vile miaka ya karibuni nimepanda eucalyptus.

Wakati naanza kupanda miti mche mmoja nilikuwa nanunua kwa Shs 50 na kuupanda kwa Shs 20. Kwa vile napanda miti mingi (zaidi ya laki moja kwa mwaka) baadaye niliamua kuotesha miche mimi mwenyewe ili kupunguza gharama.

Gharama zaidi ya miche na upandaji ni barabara za moto kuzunguka msitu. Hata hivyo nilinunua ngómbe na kuwaweka kwenye shamba ili wale majani yanayozunguka msitu. Wamenisaidia sana.

Unaweza kupanda miti kidogo kidogo kila mwaka kutumia mshahara wako kama nilivyofanya mimi. Baada ya miaka kadhaa utakuwa na miti mingi na utaweza kuwa unauza miti au kupasua mbao kila mwaka.

KVM,

Hapo pekundu imebidi na mimi nifanye kwangu.
 
Habarini watu wa Mungu, mimi ninavutiwa kufanya biashara ya kuuza mbao Nairobi, mtaji kwangu suo tatizo sana, msaada ninaohitaji kwenu ni process za kupata kibali, kama kuna mtu anafaham utaratibu mzima wa kibali au taratibu nyingine zinazohusiana anisaidie tafadhali.

Asanteni sana
 
Back
Top Bottom