Biashara ya Michezo ya Video (Video Games): Jifunze Uendeshaji, Changamoto na Faida Zake

Biashara ya Michezo ya Video (Video Games): Jifunze Uendeshaji, Changamoto na Faida Zake

Habari mkuu, nimeanzisha game center nina ps2 na ps3 mbili hapo baadae nina mpango wa kuongeza ps4 ila nasikia ili usisumbuliwe na polisi lazima uende bodi ya game ili upate kibali je kuna ukweli juu ya hili jambo frem nimechukua uswahilini
Biashara inaendaje mkuu
 
Habari mkuu, nimeanzisha game center nina ps2 na ps3 mbili hapo baadae nina mpango wa kuongeza ps4 ila nasikia ili usisumbuliwe na polisi lazima uende bodi ya game ili upate kibali je kuna ukweli juu ya hili jambo frem nimechukua uswahilini
Wengine wanalipia kitambulisho cha ujasiriamali...


Wengine wanalipia kwa wenyeviti sijui hiyo hela knaotwaje ila hawatakaa wakusumbua
 
Wengine wanalipia kitambulisho cha ujasiriamali...


Wengine wanalipia kwa wenyeviti sijui hiyo hela knaotwaje ila hawatakaa wakusumbua
Je ukilipa pesa kwa mwenyekiti wa Serikali za mtaa cheti au kitambulisho anakupa ili wengine wakija ukionyeshe
 
Kuna aliewahi kuagiza mzigo na hawa jamaa??
Screenshot_20220115-171651~2.jpg
 
Nahitaji kufanya hii issue ndani ya huu mwaka.

Sasa huku mkoani hadi tuje dar nauli nayo kubwa inakata sanaa.
 
Magame kama mortal kombat au god of war yana mzuka sana inapelekea mtu kubonyeza zile key mara nyingi na kwa nguvu akihisi ndo inakuwa labda inapga sana.

Kuja kushtuka vile vi raba vya ndani ya pad vimekufa vyote hivo batani kuwa useless au analog kuharibika kabsa.

Pad ya ps3 ni 40k ya mtumba na ps4 ni 120k ya mtumba au 60k mpaka 80k ya dukani.

Wakati ya pc ni 8k na ni ngumu kwakuwa sio kopi
Mkuu vinapatikana wapi vya mtumba?
 
Hii biashara nzuri sana changamoto zake sio kubwa sana ukilinganisha na baadhi ya biashara nyingine mambo yakibuma unasubiri kodi iishe unakusanya vifaa vyako unaenda fungua pengine maisha yanasonga.

Changamoto ni kubwa kwenye kila biashara. Hii nayo haiko nyuma

1) Umeme ndo uti wa mgongo wa hii biashara. Itakulazimu kuwa na Generator ambapo, ili kuingiza faida na kuwa constant itabidi siku Generator linatumika uongeze bei kidogo.
Hii itafanya watu kutega siku zenye umeme ndo wanakuja.

2) kama ushawahi kumiliki ps3/Ps4 na sasa Ps5 unajua kabisa umuhimu wa kua na accesories original. Nazungumzia sana Pas/Controllers/ Joystick inategemea wewe unaziitaje.
Hivi vidubwana kuharibika ni rahisi sana, hii husababishwa na aina ya uchezaji wa mtu na pia yapo magemu ambayo hutumia force nyingi hasa kwenye kurotota Log. Hapa utajikuta kila baada ya muezi miwili unanunua Controller kama tatu.

3) Latest Games. Hamna MTEJA serious atakuja eneo lako leo, umuwekee FIFA 19 alafu kesho arudi. Wengi wanapenda tittle kubwa, tittle recent.
Sikuizi mambo yamekua marahisi kidogo kuna option kadhaa, unaweza cheap console yako, au ukaweka PSN account ukanunua Game alafu ukainstall kwenye Playstation zote (hii ina changamoto kidogo)
Hapa inakufaa uwe mpenzi wa magemu ili uweze kufuatilia kwa ukaribu Game ipi ni mali na ipi sio. Ukiwa umeingia huku kwa sababu tu umeskia kuna 40,000 daily utajikuta unaangukia pua. Wewe utakua mpaka leo una Fifa 18 na wakati watu wanangoja kucheza Fifa 23 miezi kadhaa ijayo.

4) Uwekezaji sahihi. Bila akili kila biashara ni bure. Jaribu kuchunguza kwanza wenzako walioko kwenye hii industry wamefanya kwa kiasi gani? Je mtaa unaofungua hapajawahi kufunguliwa game center? Kama ndio, kwa nini ikafungwa? Je mtaa unaokaa kuna vijana ambao wana passion na hii kitu? Je, kuna kipi cha kuongeza ili kuipa biashara yako heshima?
Hii ni changamoto kubwa sana. Je wateja wako watakaa kwenye benchi la mbao ambalo baada ya mda atachoka makalio? Au utamuwekea sehemu comfortable ya kukaa akitaka kucheza hata masaa kumi na mbili acheze? Hapa ukikosa akili ya ubunifu basi umeumaliza mwendo kijana. Umelala yoooo

5) INTERNET hapa sihitaji kuielezea kwa undani sana. Ila kama biashara yako iko nje ya maeneo ambayo unaweza kupata internet ya fiber ambayo ni unlimited na unapata kwa gharama nafuu mpaka 60,000 tu kwa mwezi andika pain kama unataka kuchezesha kisasa. Kudownload game moja la PS4 huchukua mpaka GB 30 inategemea na tittle. Kucheza online kwa lisaa huchukua wastani wa GB 1-4 inategema na load time. Hapo una console 4, hujakutana na mteja anaecheza kwenye “Party” utajua hujui.

LENGO LA HII COMMENT SIO KUMTISHA MTU. NI KUWASHA MWANGA GIZANI. ILI UNAPOINGIA KWENYE HII BIASHARA UJUE KABISA PALE PANA SHIMO ACHA NIRUKIE HUKU.

OTHERWISE NI BIASHARA SAFI SANA HASA KAMA UNA PASSION NAYO.

Kwa mawasiliano zaidi kuhusu hii na biashara za aina kama hii
Wasiliana nami PM

(Kwa ushauri tuu, siuzi wala sitoi huduma yeyote kwa malipo. Natoa ushauri tuu)
 
Biashara moja ya kiboss sana.
Tafuta ps3 tatu na ps4 moja na ps2 moja. Then tv 4 za inch 32 kwaajili ya ps3 nanps4 na tv moja inch 22 flat kwaajili ya ps2.
Chukua kibali ambacho ni 20k kwa miaka miwili. Anza kula faida ya 20k j3 hadi j5 then 30k to 40k alhamisi na ijumaa. 50k jmos na jpili.

Eneo gani hilo ambalo watu watakuletea hela kucheza ps2 leo 2022? Embu tufanye research ndogo. Aheei uanze na ps4 mbili itakupa mileage kuliko kuweka ps2.
Hio ps2 yako itakua ni asset ambayo haina maslahi
 
Kutengeneza button moja tu ya pad za PS4 sio chini ya elfu 30.
CD ikisizingua tu, moja sio chini ya 120K OG, ku update mashine sio chini ya 30GBs za internet yenye speed kali.

Mkiongea haya mambo ongeeni kwenye uhalisia wake.

Nafanya hii biashara, usipokuwa makini, watu wavuta analogy joyride kama uoinde wa mshale, utajuta.... Zinameguka, spare elfu 60 [emoji23][emoji23][emoji23]

Hii umeongea point. Ila kuwatoa watu hofu, update ya ps4 haizidi GB 1, update ya ps5 haizi 800Mb. Kinachokula kwenye update ni updates za game(tittle) kuhusu CD ili kukwepa usumbufu huo, nunua online games au fanya ku chip. Hii inasaidia kama una console nne watu hawatapanga foleni kungoja CD moja ya Fifa.
 
Mkuu naomba kujua Kuchipiwa ni nini

Kwa lugha nyepesi ya kihuni ni kusema kutekenya.

Kabla sijaanza kutiririka weka maneno haya kichwani maana nitayatumia sana kwa lugha ya kizungu ili yasikuchanganye maana kiswahili chake kitakua kirefu.

a) GAME CONSOLE - hii ni ile deke yenyewe iwe Ps4/Ps5/Ps3 au hata Xbox

b)GAME TITTLE - hili ndo game lenyewe linalochezwa inaweza kuwa kwenye CD au installed kwenye Game Console. Mfano Fifa 2022


HAYA TUANZE
Kampuni kama Sony (wanaotengeneza gaming Console PlayStation) na Microsoft (wanaotengeneza gaming console Xbox) hawategemei sana mauzo ya Console. Mauzo yao mengi na kipato huja kwa njia ya kuuza Game tittles.
Ili kuhakikisha wanapata faida kubwa, wanaweka ugumu sana kupata game kwa njia rahisi. Official zipo njia mbili za kupata hizi games

1)Kununua CD/DVD ya game tittle husika
2)Online purchase. Kuinunua online na kisha Kuidownload

Hakuna namna official unaweza mpelekea rafiki yako Game tittle kwenye Flash na yeye akacheza kwenye console yake.

Hapa ndipo Chipping inaingia kati. Chipping ni kama kuhack au kuitekenya kama nilivosema mwanzo ili iweze kufungua mlango/mwanya unaoruhusu kufanya haya na mengine mengi.

Chipping itakuruhusu kuwa na magemu yako kwenye External hard drive na kuweza kuyacheza pale unapohitaji
Chipping itakuwezesha kupata games Bureee kabisa. Kazi yako ni kuwa na bundle la kudownload mzigo wa GB 10-60 inategemea na Game lenyewe


HASARA ZA CHIPPING AU CHANGAMOTO
Japo inaonekana raha sana kucheap, hasara zipo pia.

Hutoweza kucheza online games.
Console yako inaweza kuwa banned
Hutopata games update

Kusubiri mda mrefu game mpya zinapotoka kabla ya wewe kuipata

Ikitokea bahati mbaya ume Update game itabidi usubiri tena mpaka hio version yako iweze kuchupiwa

NATUMAI NIMEKUPA MUONGOZO
 
Back
Top Bottom