Biashara ya Night Club Dar imekufa?

Night clubs zimebaki Nairobi tu...aloo huko ni sio poa. Hizi habari za pubs bongo ndo tumeendekeza na kupigizana makelele usiku kucha kila sehemu, ukigeuka huku kanisa la mabati na maspika yao,ukigeuka huku bar/pub..ndo maana vichaa wanakua wengi. Hata Zanzibar pia bado wanautaratibu mzuri wa night clubs. Kama mkuu wa mkoa mwenyewe anasema ambae hataki makelele ahame Dar unategemea kuna utaratibu kweli hapo?
 
Wabongo wanaziita Lounge. Yaani mtu kaweka maspika, viti mambao mbao, kaunta moja. Wahudumu wenye matako. Anasema JF Lounge.

Nyomi iyoo
 
Nairobi wana mpaka strip clubs. Nilifika pale nikakuta wadada wanacheza uchi wa mnyama
 
Mkuu kila mtaa kuna mabaa makubwa tu, halafu unakuta labda kila jumatano au weekend kuna bendi,open space,mziki upo,na karibu na kwako au mtaani kwako.

Mtu unakaa karibu na maskani ,kufahamiana na usalama wa kutosha .
Bar za mitaani haziwezi kukuza utalii....biashara ya nightclub imeuliwa na SAMIA NI NJAMA YA WAZANZIBAR KUUA UTALII TANGANYIKA ILI WATALII WAENDE ZENJI NINAO USHAHIDI 100% SIYO CLUB TU BALI HATA FUKWE ZINACHAFULIWA NA MCHANGA MWEUPE UNAPELEKWA ZANZIBAR
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…