Biashara ya Stationery: Ushauri, Vifaa, Gharama na Mbinu za Uendeshaji

Biashara ya Stationery: Ushauri, Vifaa, Gharama na Mbinu za Uendeshaji

Asante kwa ufafanuzi wako mzuri, naamini mleta mada atakuwa amepata mwanga kwa kiasi flani juu ya biashara hii. Mimi binafsi nimenufaika sana. Kuna jambo ninaomba ufafanuzi wa kina mkuu juu ya idadi ya copy ambazo mashine imeishatoa. Swali langu ni kuna ukomo wa copy ambazo photocopy mashine ikizifikia ndio unakuwa mwisho wake wa kutumika?

THEO,

Asante kwa kushukuru mungu akubariki kwa kutambua msaada wangu,Nami sitasita kutoa msaada wa ushauri kwa kila mtu kama mada iko ndani ya uwezo wangu.

Photocopy haina kikoma cha kutoa copy,Kuna nyingnne zinatoa mpaka copy laki 4 illa bado iko vizuri iinafanya kazi kuna nyingine imeto copy laki 2 unakuta imekufa kabisa.

Na hii isikusumbue kichwa kwasababu hivi ni vifaa vya eletronics havina warranty kuubwa.Na pia inatokana kama ilikuwa inafanyiwa service mara kwa mara,Pia inaweza ikawa imetoa copy nyingi kwa muda mrefu inakuwa safi sana ila kama imeto copy nyingi kwa muda mchache ni rahis kufa mapema.

Nadhani umenipata hapo Theo

MUNGU IBARIKI TANZANIA MUNGU IBARIKI AFRICA

PATRICE LUMUMBA
 
Habari zenu wanajamvi? Nahitaji kufungua stationary mimi naishi Dsm , je ni vifaa gani muhimu napaswa kuwa navyo??

Mchango wenu tafadhari
 
Ni PM nikuuzie vitu vya stationery kwa bei nzuri. Yangu nimeifunga. Niko Dar pia.
 
Ukifanikiwa kufungua nichek nkutafutie muuzaji..anauwezo mzuri wa kusimamia duka na shughuri zote za stationary anazimudu vizuri.
 
Muongo huyo mjimpya. Nimem PM tangu lini cjui kuna vitu nataka yupo kimya adi leo.
 
Hivyo ni vya muhimu ukiwa navyo photocopy mashine,printer,computer(desktop).
 
Habari zenu wapendwa,

Naitaji Msaada na Ushauri Wenu jamani. Nataka nifungue Internet Cafe pamoja na Stationery, Hivyo basi naomba kujua unatakiwa uwe na kiasi gani cha Mtaji. Pia na Mambo mengine ya muhimu kuhusu hiyo project. Kwa wale wanaojihusisha hizo biashara Naombeni Msaada Wenu wa mawazo tafadhari.

Ni hayo tu
Siku Njema
 
Khaa, hii biashara ni ngumu kama vile kuendesha kampuni ya ndege. Nilifungua nikafunga ndani ya mwezi.
Rent 300,000, TTCL bundle Tsh 200,000, umeme 100,000, salary ya mhudumu 150,000, bado ulinzi na gharama nyingine jumla unajikuta unabidi uspend kama 700,000 kama fixed cost. Sasa na vile wateja wa kudunduliza. Bora ufungue mahali amabapo population ya watu ni kubwa, kama wanafunzi wa chuo vile.
daaaahh
 
Wadau,

Nataka nimfungulie mdogo wangu stationary sio kubwa kivile ya kawaida manake amesomea mambo hayo, baada kufanya utafiti nimegundua photocopy machine ndio bei kubwa katika vifaa vinavyohitajika kwa kuanzia. Photocopy machine nzuri ni kampuni ipi na duka lipi linauza hivi vifaa kwa bei nafuu hapa Dar.
 
Photocopy nzuri ni Canon Image Runner 2525 bei 1.5mil, zinapatika Kariakoo. Angalizo: kabla ya kufungua biashara ya stationery fanya utafiti wa eneo la biashara kwanza vinginevyo utaifunga au kugeuza banda la Miamala na Vocha tu.
 
Back
Top Bottom