Very interesting,nilifikiri wazungu hawagusiki na uchawi wa kiafrika?
Majimoto unajua lolote kuhusu uchawi katika jamii ya wamarekani weusi??????
Shetani ndiye mtawala wa dunia, ametapakaa kila kona ya dunia, angani yupo, nchi kavu yupo, ndani ya bahari na maziwani yupo. Kila mahali shetani yupo. Shetani kama mtawala wa dunia, anao wasaidizi wake na ana vikosi vya majeshi ya kupigana vita. Madhalani shetani anamtegemea sana shetani anayemiliki anga, huyu ni mwanamke anayejulikana kama malkia wa anga, ni mbaya na katili kwelikweli kuliko wasaidizi wote wa shetani. Malkia wa anga huwa hakai sehemu mmoja huwa anasafiri kuzungukiwa anga yote ya ulimwengu kuanzia dunia yetu sayari zote, nyota zote, hadi mwezini. Huyu malkia ana njia zake kabisa angani anazopita na anatembea kwa kuteleza kwenye ulimwengu usioonekana, huteleza kama wanamichezo wanavyoteleza kwenye michezo ya barafu.
Majanga yote makubwa yanayoikumba dunia husababishwa na malikia wa anga, kama vimbunga, matetemeko ya ardhi n.k.
Shetani anao wasaidizi wengine kama majini na mapepo, na yote yametapakaa dunia yote. Majini yanatumiwa sana na ulimwengu wa Kiaarabu, mapepo nayo yapo kwa wingi sana, kiasi kwamba hapo ulipo sasa hivi umezungukwa na mapepo kati ya 500 hadi 1000 au zaidi kutegemea na hali ya eneo, kama eneo hilo wanateketezwa kwa wingi wa sala ndivyo idadi kubwa ya mapepo hutumwa eneo hilo, kuzuia maombi na sala.
Hao ni baadhi ya wasaidizi wa shetani ambao wako katika ulimwengu usioonekana, kwenye ulimwengu unaoonekana shetani anawatumia wanadamu ndio hawa tunaowaida wachawi au waganga wa kienyeji. Hawa wachawi hutofautiana sana kutoka eneo moja hadi eneo lingine la ulimwengu wetu, tofauti yenyewe hutokea haswa kutokana na maendeleo na kiwango cha elimu ya eneo husika. Kwa mfano mchawi wa Tanzania wengi elimu hawana au ni ndogo sana, mchawi huyu ataloga kila kitu, hataki mtu ajenge nyumba ya bati, ataloga mkorosho, mbuzi, watoto wako yeye uchawi ni kuzuia maendeleo.
Wachawi wa uropa na marekani siyo rahisi kuwatambua, wamesoma na wana nafasi nzuri za biashara na utawala, wengi sasa hivi utawakuta wamening'iniza flash disk shingoni kumbe ni ungo wa kusafiria.
Yapo maeneo ambayo uchawi ni sehemu ya maisha ya kila siku ya watu wa eneo hilo, maeneo yanayoongoza duniani kwa uchawi ni:
a) Bara lote la Asia, Japan ikiwemo
b) Nchi zote za Kiarabu, Iran ikiongoza
c) Bara lote la Afrika, Tanzania ikiongoza
d) Marekani ya Kusini
e) Nchi za Uropa