Biashara ya Uchawi Tanzania

Biashara ya Uchawi Tanzania

Mikoa saba nchini Tanzania ndiyo tishio kwa kuwa na nguvu kubwa za uchawi
1. Tanga ndio kinara
2. Lindi unafuatilia
3. Dar es Salaam
4. Mtwara
5. Tabora
6. Kigoma
7. Mwanza

Mikoa yenye wachawi wengi, kwa maana kwamba karibu kila kaya kuna mchawi
1. Sumbawanga (Rukwa) ndio kinara
2. Ruvuma inafuatialia
3. Mbeya
4. Singida

Mikoa ambayo wananchi wake ndio wateja wakuu wa wachawi
1. Kilimanjaro inaongoza
2. Morogoro inafuatilia
3. Kagera

Wateja wengine wa wachawi
1. Wafanyabiashara
2. Wasanii
3. Kina mama wa nyumbani
4. Wanafunzi wa shule za sekondari hasa wa kidato cha pili.


wewe data zako zimezidi kuwa za kufikirika..umewaacha wakinga na mkoa wa iringa?biass wazi wazi kwa mikoa baadhi..
 
Nilikuwa natafuta Mkoa wa IRINGA kule ambako kaburi halihamishiki sijauona.

Kaburi walishalihamisha na hakuna lolote lilitokea, ilikuwa ni stori au imani tu za kipumbavu.
 
Kama wana mahela ya kuchezea, waambie waende pale ustawi wa jamii, kuna watoto yatima, labda hizo hela zitawasaidia!
 
Gambushi huko kwa wasukuma shinyanga mmekusahau? watu washambaaaa lakini wachawi balaaa...kijiji usiku kipo mchana hakionekani..
 
Maji Moto,
Inasemekana kuwa MV Spice ilijaza watu na mizigo kupita kiasi, kiasi kwamba meli ilionekana kabisa kuinamia upande hata kabla ya safari kuanza. Nahodha wake akagoma kuiondoa lakini akatafutwa mwingine ndo akaenda kuwazamisha watu baharini. Sasa hapa nina swali, pamoja na kuiona hatari yote hiyo watu hawakustuka na waling'ang'ania kwenda tu. Je kuna mkono wa ibilisi katika ajali hii? Na kama ni ndiyo kuna suala lolote la kafara la kuhusishwa na hii ajali?
Asante
 
kama sioni wanasiasa na viongozi wa makanisa ya kilokole napinga takwimu hizo
 
kama sioni wanasiasa na viongozi wa makanisa ya kilokole katika wateja wa uchawi napinga takwimu hizo
 
Kaburi walishalihamisha na hakuna lolote lilitokea, ilikuwa ni stori au imani tu za kipumbavu.
<br />
<br />
ni kwl kaburi limeondolewa lakini kwa taarifa nilzo pata nikwmba watu wlio fanya kazi iyo wamekufa.
 
kama sioni wanasiasa na viongozi wa makanisa ya kilokole katika wateja wa uchawi napinga takwimu hizo

Uchawi kwani si kuwanga? Kwa uelewa wangu mdogo,mtu haendi kuuomba uchawi kwa mchawi! Wachawi ndo wanaweza kukushawishi ujiunge nao! Ni tofauti na mambo ya UGANGA ili kufanikisha biashara,mapenzi,kulipwa madeni,kufutwa kesi,n.k. Baadhi[huenda hata na MAJIMOTO naye] huchanganya UCHAWI NA UGANGA!
 
Uchawi kwani si kuwanga? Kwa uelewa wangu mdogo,mtu haendi kuuomba uchawi kwa mchawi! Wachawi ndo wanaweza kukushawishi ujiunge nao! Ni tofauti na mambo ya UGANGA ili kufanikisha biashara,mapenzi,kulipwa madeni,kufutwa kesi,n.k. Baadhi[huenda hata na MAJIMOTO naye] huchanganya UCHAWI NA UGANGA!

Huwezi kuwa mganga wa kienyeji usiwe mchawi.

Waganga wote huongozwa kwa usaidizi na mizimu au majini, mizimu ni roho kamili zinazowekwa ndani ya mwili wa mtu, roho hizi chafu huweza kuona mambo yote katika ulimwengu usionekana. Mganga yeyote awe amevaa suti na ofisi nzuri bado anazo sifa zote za uchawi. Mtoto anapozaliwa mizimu hii huona uwezo wa mtoto katika ulimwengu usionekana, mtoto akiwa na uwezo mkubwa, wachawi/waganga hufanya matambiko na kumchanja mtoto wakimtayarisha kuwa mganga siku atakapokuwa na umri mkubwa. Ndiyo maana baadhi ya waganga wanapokuwa wakubwa hutokewa na mambo ya ajabu ajabu yanayomlazimisha kuacha kazi zao nzuri na kuingia kwenye uganga bila ya hiari yake.

Mganga hawezi kukufanya ufanikiwe kibiashara, kushinda kesi au mafanikio ya aina yeyote bila ya kukupa uwezo wa majini, waganga wanauwezo wa kuyaita majini na yanapokuja huangizwa yafanye mambo yanayoagiwa na mganga, baada ya kupewa damu aidha ya kuku, ya mbuzi, ya ng'ombe jini huwekwa ndani hirizi, matarasimu, ndani ya maji yaliyooshea maiti nk. na mteja hupewa vitu hivyo na kuelekezwa jinsi ya kuvitumia, jini linapokuwa kubwa, ndivyo linavyo nyweshwa damu nyingi. Mafanikio yanakuwa makubwa majini yanaponyweshwa damu ya binadamu, ndiyo maana waganga wengi huweka mitego yao barabarani inayosababisha ajali, zinazowapa kiasi kikubwa cha damu au baharini kupindua meli na kuzamisha abiria majini.

Ili uwe mteja wa kudumu wa mganga, ni lazima wachukue damu yako wanakuchanja kwenye ulimi ili siku zote uwe unawasifia, wanakuchanja miguu, linapotokea tatizo lolote miguu yako inakuwa miepesi kuwakimbilia. Damu yako inakuwa kama remote controll, wakikutaka muda wowote, ni lazima utafunga safari kuwafuata.
 
kama sioni wanasiasa na viongozi wa makanisa ya kilokole katika wateja wa uchawi napinga takwimu hizo

hata mimi napinga kwa sababu hizo. Halafu wazee wa bagamoyo wamesahaulika. Kwa mzee kwenyewe!
 
wanasiasa(Magamba orijino na Magamba B) na viongozi wa vitengo ni noumer kwa kupulizia ndumba! bila kusahau masekretari ili wapendwe na mabosi
 
wanasiasa(Magamba orijino na Magamba B) na viongozi wa vitengo ni noumer kwa kupulizia ndumba! bila kusahau masekretari ili wapendwe na mabosi

Khee! Usiniambie mwenzangu, kumbe mambo ya ofisi ndo hivyo!?
 
LANGO KUU LA KUZIMU LA DAR ES SALAAM

Kuzimu ni shimo la giza lililopo duniani katika ulimwengu usiooneka, hapo ndipo yalipo makao makuu ya shetani katika dunia tunayoishi. Shetani ameshikilia tawala za mataifa mengi, anamiliki utajiri na fahari zake zote na humpa ampendaye kwa sharti ni lazima umsujudie.

Lango kuu la kuingilia kuzimu la Upanga Dar es Salaam linajulikana kwa jina la MUSTALLAH. Ndani ya shimo la Mustallah kuna aina kumi na mbili za majini makatili sana yanayoangamiza jamii ya watu wa jiji la Dar es Salaam. Wachawi wa nchi huenda mara kwa mara shimoni kuongeza nguvu za uchawi wao, kabla ya kuingia shimoni ni lazima ufunge kwa siku tatu. Hapa tunajifunza kuwa shetani naye huwa anafunga.

Tuangalie sasa aina za haya majini ya Mustallah na kazi zao.

1. Ratafari ni jini linalosimamia laana zote za ukoo.
Wapo watu wanasema ukoo wetu unasumbuliwa sana na ugonjwa wa pumu, kisukari, presha, kutokuolewa na mambo mengi ambayo utakuta ukoo unakuwa na tatizo moja linalofanana kwa kila mwanaukoo, hili jini ndilo linasimamia laana hizo zimalize ukoo hadi kifo.

2. Muzaphari ni jini linalozuia mafanikio.
Ukitupiwa hili jini, hutaweza kufanya jambo lolote ukafanikiwa. Ukikopa shs 500,000 bank kwa ajili ya kuanza bishara, utafilisika na kuingia kwenye deni, na dhamana yako uliyoweka bank kuuzwa. Ukitaka kujiendeleza kimasomo yatatokea matatizo mengi yatakayosababisha kusimamisha masomo yako.

3. Latifu hili jini linasimamia mambo matatu, ufukara, mateso, na pesa zako kupotea katika mazingara ya ajabu ajabu.

4. Jujan ni jini linalosababisha watu kula udongo.

5. Jahad ni jini la kutorosha mali
Makarani wa bank ndio hasa wanaoadhirika na hili jini, utakuta karani anafanya kazi kwa uangalifu mkubwa, lakini kila siku ana shoti ya pesa. Pia kwenye maduka ya kawaida na hasa supermarket.

6.Hazinan hili jini linalosimamia pombe, uvutaji wa sigara, madawa ya kulevya na mirungi.

7. Jube ni jini linalosimamia utasa, vipimo vya hospitali vitaonyesha kuwa huna tatizo lakini mtoto kamwe hapatikani.

8. Sifafiru hili ni jini linalosimamia ukahaba. Likimwingia mtu yeyote, kwa siku atatembea na watu zaidi ya watano bila hamu ya mapenzi kumalizika.

9. Subian hili ni jini linalosimamia ajali. Chakula cha hili jini ni damu.
Linasababisha wanawake wasipate siku zao, wengine wanapata maumivu makali sana wakiwa katika hedhi, utasikia tumbo linakata kuanzia kushoto kwenda kulia na hali hiyo huendelea kwa muda hadi unanza kusikia maumivu makali ya mgongo.

10. Sumri jini hili linanyonga watoto wakiwa tumboni kabla ya kujifungua, pia linajihusisha na kuchukua watoto hospitali kichawi.

11. Munsar hili ni jini linalosimamia ndoa ya jinsia moja.
mwanamke kwa mwanamke au mwanamume kwa mwanamume.

12. Waidadat hili jini linasababisha vijana wa kiume kuvaa hereni, kusuka nywele na rasta.

Haya majini yamesumbua familia nyingi kwa kiwango cha kutisha, kuyaondoa ni rahisi sana na kwa muda mfupi.


Waziri mkuu wa Uingereza anasumbuliwa na jini munsar.
 
Back
Top Bottom