Biashara ya Uchawi Tanzania

Biashara ya Uchawi Tanzania

Hilo la namba 10 lina uhusiano wowote na jina la mabasi ya Sumry?
 
SERIKALI YA MAJINI
Majini wana Utawala wao ambao ni Majini Wakuu na Majini wa Kawaida wanaopewa Kazi za kufanya na Wakuu wao, Katika Serikali yao kuna Wakuu wa Serikali, Wakuu wa Majeshi, Wakuu wa Mahakama na wengineo wengi.

Utawala katika Serikali yao umegawanyika katika sehemu Kuu mbili (2);
  1. Utawala katika Ulimwengu wa Kijini.
  2. Utawala katika Ulimwengu huu wetu wa Kibinadamu.
Majini Wakuu kabisa wapo Watatu (3) ambao Majina yao ni;
  1. Lucifer.................ambae ndio Mfalme wao (Emperor),
  2. Beelzebuth.......... ambae ni Mtoto wa Mfalme (Prince),
  3. Astaroth ..............ambae ni Mtawala Mkuu wa Majimbo (Grand Duke).
Hawa Watawala Wakuu kabisa watatu, iwapo Binadamu anataka kuwaita na kuwatumia inambidi atumie njia Maalum;
Mtu anayewaita anatakiwa achore alama zao kwa kutumia Damu yake mwenyewe, au anaweza pia kutumia Damu ya Kobe wa Baharini (Kasa) katika kuandikia.

Iwapo atashindwa haya yote basi anaweza pia kuwaita kwa kuchora alama za Majini hao kwenye Kito cha Ruby au Emarald; kwani vito hivi vinaendana sana na Majini hasa wale wa Ukoo wa Jua, ambao huwa na Busara, wazuri na Marafiki zaidi kuliko aina nyingine ya Majini.

Alama hizi za Majini zinatakiwa zivaliwe na Mtu ambae anataka kuwaita. Ikiwa muitaji ni Mwanamme, anatakiwa aiweke kwenye Mfuko wake

wa Kulia na iwapo ni Mwanamke, anatakiwa aiweke katikati ya Matiti yake ikielekea upande wa Kushoto.

Alama hizi zinatakiwa ziandikwe katika siku ya Jumanne saa Kumi na mbili (12) mpaka saa moja asubuhi au saa saba mchana mpaka saa nane kwa majini wote.

Majini hawa watatu wana uwezo wa kufanya mambo yote, na kwa Mtu ambae anawaita hawa anatakiwa aheshimu wale tu ambao watamheshimu kwani Majini hawa Wakuu wanawaheshimu wale tu ambao ni Marafiki wao Wakuu na wa karibu, hivyo mtu anaeamua kuwaita anatakiwa ajihadhari kwa lolote ambalo linaweza kutokea.


Utawala wa hawa umegawanyika baina yao wote kwani kila mmoja ana Wasaidizi wake wakuu Wawili ambao nao huwa wanawatuma Majini wengine kuhusu mambo ambayo Mfalme wao Lucifa ameagiza yafanyike Duniani kote.


Wasaidizi walio chini ya Lucifa ni;

Put Satanachia na
Agaliarept;.............Ambao wanaishi Bara la ULAYA na ASIA.
Wasaidizi walio chini ya Beelzebuth ni;
Tarchimache na
Fleurety...................Ambao wanaishi Bara la AFRIKA.
Wasaidizi walio chini ya Astaroth ni;
Sargatanas na
Nebiros.............Ambao wanaishi Bara la AMERIKA.

8. SIRCHADE: Ana uwezo wa kukuonyesha wewe aina zote zile za wanyama katika umbo lolote lile walilonalo.

9. SEGAL: Ana uwezo wa kukuonyesha dhahiri miujiza yeyote iwe ya kawaida au ya kimazingaombwe.


10. HIEPATCH: Ana uwezo wa kukuletea mtu aliye mbali papo hapo.


11. HUMOTS: Ana uwezo wa kusafirisha aina zote za vitabu kwa starehe yake.


12. FRUCIESSEIERE: Ana uwezo wa kuwafufua wafu.


13. GULAND: Ana uwezo wa kusababisha aina yote ya maradhi.


14. SURGAT: Ana uwezo wa kufungua aina zote za Loki.


15. MORAIL: Ana uwezo wa kufanya vitu vyote Duniani visionekane.


16. FRUTIMIERE: Ana uwezo wa kukupa kila aina ya sherehe.


17. HUICTIIGARA: Ana uwezo wa kusababisha kutembea usingizini na kwa wengine kuwakosesha usingizi kabisa.

Satanachia na Satanisie wanawatawala majini 45 au 50 wanne katika hao ni Surgutthy, Heramael, Trimasel na Sustugriel. Wawili wa hawa ni machifu na waliosalia hawana umuhimu wowote.

Hawa ni Majini watumikao kwa binadamu kwa urahisi na haraka lau ikiwa wanaelewana na anaemuita,

Serguthy ana uwezo juu ya wake za watu na wanawali
Heramael anafundisha elimu ya madawa na anatoa na ujuzi kamili wa magonjwa yote, tiba zake sahihi, anafundisha aina ya mimea yote,

sehemu mimea hiyo inapatikana, nyakati nzuri ya kuipata, umuhimu wa mimea hiyo na namna ya kuchanganya mimea hiyo ili kupata dawa sahihi kwa maradhi ya aina yeyote ile.

Trimasel na Sustugriel hawa wawili ni Machifu na wanatoa elimu ya kichawi kwa wale wanaowapenda.

Agalierept na Tarihimal wanamtawala Elelogap, ambae nguvu zake zipo juu ya Maji.

Nebirots Wawili wawatawala Hael na Sergulath.
Hael anatoa maelezo juu ya Usanii wa kuandika kila aina ya Barua, anampa Mtu uwezo wa kuongea mara moja kila aina ya Lugha na anaelezea na kufumbua vitu vyote vya siri.
Sergulath ana uwezo wa Kufundisha Mtu njia mbalimbali za kuvunja pande ambazo hazielewani.

Hawa wana Wasaidizi wao Wanane (8) wenye nguvu


1. Proculo ambae ana uwezo wa kumpatia Mtu usingizi kwa muda wa masaa manane huku akiwa anafahamu yanayotokea usingizini.


2. Haristum ambae anampa Mtu uwezo wa Kupita kwenye Moto bila ya kuungua.


3. Brulefer, ambae ana uwezo wa Kumfanya Mtu apendwe na Wanawake.

4. Pentagnony, ambae anawapa Watu uwezo wa Kutokuonekana (Invisible), pia anapendwa sana na Watawala Wakuu
5. Aglasis, ana uwezo wa Kumsafirisha Mtu kwenda sehemu yeyote ile Duniani.
6. Sidragrosam, anawafanya Wanawake wacheze Uchi.
7. Minoson, ana uwezo wa Kumhakikishia Mtu kushinda katika Michezo yeyote ukiwepo wa Kamari.
8. Bucon ambae ana Uwezo wa kuanzisha Chuki na Wivu kati ya Jinsia mbili (Wanaume na Wanawake).


 
Hivi mwenge wa uhuru unaokimbizwa nchi nzima hauna uhusiano wowote na uchawi? Naomba kufahamishwa.
 
mambo Majimoto daah hebu niambie hizo dvd za ushuhuda wa mwisilamu (mchawi) aliyeokoka na za Malango makuu ya kuzimu nitazipata wapi? Na mimi nipate kujua mabo ya dunia.
 
Mary Chuwa, Zamani wazee wetu walikuwa wakifanya matambiko ya aina mbalimbali kwa mizimu, matambiko hayo shabaha yake ilikuwa ni kuomba ulinzi wa mizimu iwalindie ukoo, ilinde watoto au mizimu isadie mvua zinyeshe kipindi ambacho kiangazi kimepitiliza sana na mvua kuchelewa kunyesha au kama kuna jambo lolote lisilokuwa la kawaida limetokea kwenye ukoo au familia, matambiko haya yalikuwa yanafanywa kuomba msaada wa mizimu, matambiko haya bado yanaendela kufanywa na familia nyingi.

Mizimu ni nini? Watu wengi wanafikiri mizimu ni ndugu wa ukoo waliofariki miaka mingi sana (mababu na mabibi). Mara nyingi utakuta ukoo au familia zina Mzee wa ukoo, ambaye ndiye anayeratibu taratibu zote za kufanya matambiko. Kimsingi hakuna uhusiano wowote ule kati ya mizimu na mwanadamu. Mara nyingi matambiko hufanyika kwa kuchinja wanyama na damu ya mnyama hutumika kuomba dua kwa mizimu iwatendee mambo yote wanayoyataka yafanyike, kisha hufuatiwa na viapo vya ukoo kwa mizimu kuwa watafuata yale yote mizimu itakayo sema wayafanye.

Matambiko kwa lugha nyingine tunaweza kusema ni kamba za kuzimu, zinazowafunga wanadamu wakiwa duniani. Mizimu ikishafunga ukoo kwa kamba shughuli yake huwa ni pevu kijinasua. Mizimu huifanyia familia jambo lolote ovu jinsi wanavyoamua, na jinsi wapendavyo, hizi kamba za kuzimu ni sawasawa kabisa na unavyotumia remote control ya television kubadilisha vipindi mbalimbali bila kuwepo na waya wa moja kwa moja toka kwenye tv hadi kwenye kitufe cha kuongozea tv. ndivyo hivyo hivyo mizimu inavyoyumbisha maisha ya watu wakiwa kuzimu kwa matatizo na magonjwa ya kila aina.

Familia nyingi zimekuwa mateka wa mizimu, kwa makosa yaliyofanywa na wakale wetu, na mizimu kwa kutumia remote control wameendelea kutaabisha familia nyingi, kiasi kwamba utakuta ukoo karibu wote wanaugua aina moja ya ugonjwa unaofanana kama kichaa, sukari, mapigo ya moyo n.k. au utakuta familia inaanza na maisha mazuri yenye wasomi wazuri na vipato vya kuridhisha, lakini mali hutoweka na huishia katika maisha ya mahangaiko na ufukara wa kutupwa. Familia nyingine utakuta wanawake hawaolewi au wakiolewa ndoa haidumu. Familia nyingine kila mwaka na mwezi unaofanana ni lazima afe mwanaukoo. Familia nyingi zimefungwa na kamba za kuzimu bila ya kijijua, anapozaliwa mtoto mizimu muda huo huo kukifunga kichanga hicho kwa kamba shingoni, na hali hiyo huendelea kizazi kimoja hadi kizazi kingine.

Kila mwanadamu mauti inapomfika ni lazima anapokelewa, familia iliyofungwa kwa kamba za kuzimu anapofariki shughuli yake huwa ni kubwa na kifo chake huwa na mahangaiko yasiyokuwa ya kawaida. Roho ya mwanadamu inapoachana na mwili macho ya kimwili hufunga na macho ya rohoni hufunguka, macho ya rohoni yanapofunguka huwaona wenyeji wake waliokuja kumpokea, wale aliokuwa akiwaita mizimu ya babu na bibi, kumbe ni majoka ya kutisha, yanapokuja kumpokea, yanakuja na vicheko na kumdhihaki na huanza kumshika mgeni wao ili waondoke naye. Mtu wa aina hiyo anakuwa anaongea lugha ya mizimu, ambayo wanaomuguza hawaelewi maana yake, lakini huwa anakataa kuondoka nao, akijaribu kuwafukuza. Wanapoanza kumshika ndiyo maana utakuta mtu aliyefungwa kwa kamba za kuzimu anatupatupa miguu na mikono kila upande ili majoka wasimshike.

Mtu asiyefungamana na kuzimu, roho yake inapoachana na mwili, macho yake ya kiroho hufunguka na huwaona wenyeji wake waliokuja kumpokea, wenyeji wake huwa ni watu waliovaa mavazi meupe kabisa na nyuso zao zinang'aa, anapokelewa kwa nyimbo nzuri ajabu, kinachofanyika kwa mtu huyo, mikono yake huilaza juu ya tumbo lake na anakufa akitabasamu akifurahia nyimbo tamu za wenyeji wake.

Mary uwezo wa kukata kamba za kuzimu zilizoifunga familia yenu ya Chuwa upo mikononi mwako, inawezekana kabisa na ni jambo jepesi.

Majimoto kwa mambo haya dunia naanza kuiogopa.
 
majimoto tuambie nguvu za hawa akina lwakatare na lusekelo ni uweza wa kimungu au ni wa majini?
 
Mheshimiwa Majimoto tafadhali nitumie contacts zako nahitaji kuongea na wewe kirefu kuhusu masuala ya dunia/uchawi/dunia isiyoonekana inaelekea kuna vitu vingi sana ambavyo sijui na ningependa kujua.
 

WARAKA TOKA KUZIMU


THE SAINTS DARKNESS IN THE WORLD
UNDER GROUND DRAGON
SECTION WXXX69

23.05.2011

TO OUR DEAREST SAINTS

TANZANIA; KENYA AND UGANDA

Tunawapa pongezi kwa juhudi zenu juu ya kazi ngumu: tuliyonayo nyakati hizi za mwisho juu ya kuja kwake Adui yetu kulichukua kundi lake.

Tuna Mbinu ambazo kufikia sasa zinaendelea kufaulu nabado zingine zina shida sana upande wetu kuzifanikisha!!

Tungependa kuwaalika rasmi kwenye “kongamano kuu la Africa Mashariki na kati “Mwishoni mwa mwezi 30/07/11.

Jambo hili sio la kawaida kwetu japakuwa itakuwa mwisho wa mwaka. Lakini mambo yetu yanazidi kuharibika kwa upande wetu na baadhi yetu mkashindwa kutekeleza wajibu wenu wengine kukosa nguvu kwa kukawia kutoa sadaka zao.

Kwa usalama wetu acha tukutane nje ya mji katika lango kuu la kuzimu “Mushitara-Dar es Salaam” saa 6.30 usiku hadi saa 9.00 usiku na viti vyetu ni watu; bila kusahau chupa ya lita 5 za damu za watu na mchanga wa kanisani.

Kulingana na lengo letu mambo ambayo tutayazungumzia ni mbinu ambazo tungelifanya ili kuzuia Maombi yao adui zetu na kuvunja amani ya jamii kupitia Migogoro na Migongano ya familia hasa kwa viongozi wakuu wa Makanisa ya Kiroho na kuliwahi kundi lao.

Lengo letu kubwa ni kuhakikisha tunamwangamiza hasa aliyekuwa Mkuu wetu wa uchawi Africa Mashariki na kati ndiye anayezifahamu siri zetu nyingi sana akawa amechukuliwa na adui yetu na kanisa lake linaenda kwa kasi saana wakiwachukua watu wetu maana amefichwa mno.

Kwa kulifanikisha jambo hili na watakieni nguvu kupitia kwa damu yetu DWS-UD na unasema mara sita; ukiwa umesimama na mara sita umechuchumaa, mara sita ukiwa umelala huku ukiwa uchi (666)

AMRI: sasa nendeni kwao ili kuharibu nguvu zao kwa kutumia sheria No. 999 WD ili kujificha (usionekane) unapozidi kuwasogelea na kuwafunga wanaume, wanawake na watoto wao.

Pia kumbukeni Yule M/kiti wetu wa wachawi Africa Mashariki na Kati aliyechukuliwa na adui yetu alipoanza maombi yake mmerudi nyuma sana. Huenda mambo yetu yakawa Mabaya zaidi ndio maana tunawahitaji mkapokee nguvu.

Pasipo kusahau kuwa yupo yule;
URGENT WETU MSALITI WA 1993.

Maeneo hayo tumempa jukumu kupambana naye ni (Madam-mwanamke) wa No 1-11-11-18 ambaye kufikia sasa anaendelea kutafuta njia ya kumnasa na kumharibia mipango yake mungu wao.

Hata hivyo kuna mbinu mpya tunayotaka kuwaelezea watu wa eneo hilo.

Jaribuni kufanya haraka sana ili kutoa kwa mara nyingine sadaka zenu ili kujiwekea ulinzi.

URGENT 1-14-14-18 amekawia tangu alipomtoa mama yake kafara hata sasa hajatoa mwingine akiulizwa anasema atatoa hivi karibuni. Tunawashukuru sana wale wenzake watatu walioshirikiana na kuleta watu wengi kwa ajali.

NOTE: Tumieni mbinu hizi ili kulizuia hili kanisa alilonalo huyu

FORMER URGENT 0-15-15-666

Maana yake anaanza kupanda juu kila kukicha hivi anasikilizwa na ataendelea kusikilizwa kuwaimalisha waliokuwa hawana nguvu amepanga kuwaimarisha kinyume na mambo yetu. Jina la kanisa alipo ni M.D.S Kimekuwa kituo cha uponyaji cha adui yetu akimtumikia.

YAH; NJIA ZA KUWANASA:

Tumieni hii hata kwa makanisa mengine na hata mbali na hilo ili kuweza kufanikiwa:-
  1. Kuzusha magombano baina ya waombezi ili kuwavunja wasiendelee kumtafuta mungu wao.
  2. Sababisheni hadithi kwa wingi wanapoingia ndani ya makanisa yao wakati wa kuja kumwomba mungu wao.
  3. Msiwaruhusu kuomba wakati wa kulala kwao (Janatus) maana hamuwezi kuwaona wakifunikwa na nguvu za mungu wao.
  4. Msiwape nguvu au nafasi ya kusoma Biblia; badala yake wapeni wakati mwingi wa kusoma magazeti, kuangalia Television zao.
  5. Sababisheni ufukara; mateso na pesa zao kupotea bila wao kujua ili wasimtolee mungu wao na walio na pesa roho ya ubahiri ya kutokutoa.
  6. Inueni nguvu za kuzini makanisani kwao baina ya viongozi na washirika wao na vijana kwa wasichana ili kupata nafasi y kuzima nguvu zao.
  7. Ibada zao ziwe baridi kabisa ili Roho wa mungu wao asipate nafasi ya kuongea na kusikia kutoka kwake.
  8. Tumieni ajali maana damu yao tutaitumia katika vikao vyetu.
  9. Akina mama wajawazito wazalishwe kwa operesheni ili kupata damu.
  10. Tumieni ukimwi wa kutengeneza kama pigo kwao ili kuwamaliza na kuwaletea aibu katika vifo vyao.
  11. Vurugeni umoja wa nyumba zao kati ya mke na mume, wazazi na watoto wao ili maombi yasipatikane.
ONYO KALI;
TAFADHALI MUWE NA UANGALIFU SAANA YA KWAMBA MAMBO HAYA YASIJULIKANE NA WAO. MBINU ZINGINE ZA KANISA MTAKUJA KUELEKEZWA KATIKA KIKAO KITAKACHOFANYIKA TAREHE 30/07/2011 “MU”D”

SENIOR URGENT: KUTOKA MAKAO MAKUU:

DW-SU: 13-1-3-18-9-1

Tafadhali tumieni usafiri aina tatu tu! (a) Ungo (b) Kijiko na (c) Kioo

Pia vaeni mapazia rasmi mnapokuja katika mkutano ili kuhifadhi heshima yenu kwa wageni wetu kutoka (hapa kuna maandishi ya kiarabu). UNDERGROUNE

Dugion Canada na ufilipino wakifundisha mbinu mpya za kukabiliana na makanisa pamoja na jamii zao. (Japokuwa: FORMER URGENT 0-15-15-666) anazifahamu!!

Mheshimiwa Majimoto kama yote ulioandika hapa ni kweli na yamefanyika huogopi watakuchukua????? Na binadamu anasafiri vipi na kijiko???????? Jamani Majimoto please reply.
 
Mheshimiwa Majimoto kama yote ulioandika hapa ni kweli na yamefanyika huogopi watakuchukua????? Na binadamu anasafiri vipi na kijiko???????? Jamani Majimoto please reply.

Priya. Binadamu wengi hawajui nguvu na uweza wa kutenda mambo makubwa walio nao. Tenda wema, simama kwenye kweli, fanya ibada bila ya kuchoka utaona matokeo yake, shetani na wasaidizi wake ni LAZIMA ni lazima wakimbie. Mtaani kwangu walikuwepo wachawi/waganga wa kishenzi watatu, viongozi wengi wa serikali walikuwa wakiingia na kutoka tangu asubuhi hadi jioni. Kwa msaada wa Mungu wote wamekimbia mtaa. Mwezi uliopita alifika kijana mmoja akiniomba msaada, nimwelekeze mganga wangu anakopatikana. Mwanzo sikumwelewa, nilimkaribisha ndani, ndipo alinieleza mambo ya kichawi ninayofanyiwa na wakazi wa mtaa wetu ya kuniangamiza, lakini siku zote wanashangaa siku zote nimesimama bila kufikwa na jambo lolote baya. Anasema waliamua kutafuta nguvu maeneo mengine, wakachangishana nauli na walituma ujumbe wa watu wawili kwenda Sumbawanga, ajabu walirudi Dar wakanikuta bado nipo, jambo hilo liliwashangaza sana ndiyo sababu huyu kijana akaamua kunitafuta.

Huyo kijana ninaye na anaendelea vizuri na masomo. Kosa kubwa linalowasumbua watu wengi ni WOGA, woga ni kifo mara moja.

Kusafiri kwa ungo, kusafiri kwa kijiko, kusafiri kwa fagio, ni usafiri wa kutumia majini, nimeeleza kwa kirefu kwenye topic za nyuma.
 
Ndiyo ni uchawi kwa asilimia 100 (%)
Mwenge naweza sema si uchawi bali matokeo yake ni mabaya kupita kiasi sifa za mwenge ni mbaya kwa kila sehemu unapolala kwani kuna maasi mengi mno hutokea kama ulevi uasherati uwizi na ugomvi na kila aina ya mabaya ni bora uachwe ila dhana ya mwenge wa uhuru unamurika bara la africa tuache tufate mazuri na kukimbiza mwenge ni upuuzi tushapata uhuru wetu bandia tosha tuondolewe upuuzi wa mwenge

tufanye kazi tuendelee japo mianya mingi ipo wazi na haina sheria watu wanaiba na kuturudisha nyuma lakini tusikate tamaa tutafika tu tuwe kama ulaya na america
 
majimoto tuambie basi juu ya makanisa kama haya ya akina kakobe,lwakatare,lusekelo, na wengine kama hawa maana tutashindwa hata sehemu ya kwenda kuombewa du!
 
Back
Top Bottom