Maji moto, swala la ukimwi wa kutupiwa nilishawahi kuona mtu wa aina hiyo lakini baada ya muda alipona na mzima mpaka leo.
Swali- kuna watu wanaishi duniani lakini wana asili ya mizimu walilogwa walipozaliwa au mimba ililogwa hao watu utakuta wanaonekana na watu wachache tu wengine hawawaoni ila wanaishi na wanaendesha maisha yao kama kawaida. inakuwaje hapo?
Kuna watu walikufa zamani lakini bado wapo duniani hii inakuwaje. mimi binafsi kuna mtu alikufa zamani sana mwaka 1994 nikiwa mdogo lakini yupo huwa namuona na anaendesha maisha yake kama kawaida na ni mwanadamu tu kama sisi hii imetokeaje?
Watu wasionekana ni wengi, wengi mno. Katika kila mazishi ya maiti 70 kwa mia za vijana na watoto uliyowahi kushiriki, mlizika majeneza yakiwa na migomba au magogo. Wapo watu wengi wanaotafuta wafanyakazi, na watu hao huwa wanataka mtu watakayemdhibiti siku zote za uhai wake. Kwa mfano mtu anataka kuanzisha kazi ya uvuvi, huwaendea wachawi wamtafutie vijana wenye uzoefu wa kuogelea na wenye nguvu. Wachawi hutuma watu wao maeneo ya kando ya bahari au maziwa ambapo vijana wengi hupenda kukaa na kuogelea kama cocoa beach au feri. Watu hawa wanapokuwa kwenye mawindo yao, huwa wana uwezo wa kurusha mishale ya kichawi kwa kutumia macho yao.
Kinachofanyika ni kuwa wakimwona kijana mwenye bidii ya kuogelea na kupiga mbizi huwa wanamfuata na kusalimiana naye macho ya hawa wachawi yanapoangaliana na macho ya huyo kijana, hurusha mishale ya kichawi na kuingia ndani ya macho ya hawa vijana bila ya vijana kuhisi kitu chochote. Mishale hiyo inakuwa ni alama, hata akisafiri kwenda mkoa gani bado anakuwa akionekana kwenye vioo vya kichawi, hivyo mipango ya kumchukua huandaliwa, kwa sababu kila kifo ni lazima kiwe na sababu , wachawi huandaa kifo rahisi kwa mazingara yao kama ajali ya gari, ajali ya kuzama ndani ya maji, kuumwa na nyoka au ugonjwa wa ghafula hasa kichwa kuuma sana mbele ya paji la uso kwa muda mfupi.
Ajali ikitokea wenyewe huwepo eneo hilo hilo la ajali, wanachofanya wanakupiga kofi la mgogoni na kuondoka nawe ukiwa mzima mzima, hugeuza mgomba au gogo linafanana sawasawa na mwili wa huyo kijana/mtoto. Ndugu zako wakija wanalitambua kuwa ni maiti ya ndugu yao. Wanakupulizia madawa ya kichawi kuondoa ufahamu wako na kupakwa madawa fulani usiweze kuonekana na watu, kisha wanakata ulimi usiweze kupiga kelele au kuongea.
Watu hawa huhifadhiwa juu ya dari za nyumba, chini ya mivungu wa kitanda, ndani ya makabati ya nguo, ndani ya makabati ya vyombo na wengine huwekwa maporini.
Viwanda vingi pugu road wapo wengi sana watu hawa, wavuvi wengi huwatumia kushusha nyavu chini ya bahari, maduka mengi huwatumia kwenda kuiba mali kwenye maduka mengine, wapo watoto wengi wamechuliwa kulea watoto wadogo kwenye nyumba nyingi sana, wapo wengi wapo mashambani wakilima, wapo wengi ni madereva wa mabasi na malori, wengi wapo maporini wakipasua mbao na kuchoma mkaa, wengi wapo mahotelini wakipika na kutoa huduma za vyumba. Viongozi wengi wanao watu hao kuimarisha nafasi zao za kazi au utawala. N.k.
Watu hawa chakula chao siku zote ni pumba za nafaka zilizolowekwa kwenye maji, na siku moja moja damu za watu. Siku wanapokula nyama, ni wakati mmoja wao anapofariki, mwili wake hukatwakatwa vipande vipande na kupewa kula pamoja na pumba za nafaka.