Biashara ya Uchawi Tanzania

Biashara ya Uchawi Tanzania

Hii sredi nimeivumbua jana make mi si mwenyeji sana JF na nimesoma page zote 1 -25 kusema kweli sina cha kusema ngoja nitafakari angalau wiki nijue pa kuanzia,,, make mimi ni mshabiki mkubwa wa filami za ki Nigeria na kama mnavyojua almost more than 75% ya filamu hizi huonesha mambo ya kishawi,kutokana na fitina, wivu, kutaka utajiri wakatimwingine hata mapenzi na mwisho wake huwa tunaona neno la Mwenyezi mungu linaingilia na kuufunika huo uchawi. kusema kweli hua na nafikiri ni maigizo tu kumbe kuna uhalisia wake sana. kuhusu huyu bwana MAJIMOTO !!!! Duh!!!!!!!!
omba sana mungu uishie kuangalia kwenye move na sio yaje yakupate live hapo ndio utajua dunia kweli inamizunguko miwili
 
mheshimiwa Majimoto kuna tofauti gani kati ya Demon na majini? Kama ni tofauti uhusiano wao na utofauti wao ni nini? Na hayo mafuriko Dar ni moja ya kazi za malango ama??? Freemason wanahusika vipi na malango ya Tanzania? Na kitendo cha rais mstaafu wa Amerika (jina kapuni) na prince wa uingereza (jina kapuni) kufika hapa tanzania na wao pia wamekuja kutafuta uchawi au kuongeza mikoba waliyonayo??? Mbona umepotea sana Majimoto ama umwehamia forum nyingine au umehamisha topic sehemu nyingine niambie. Katika bara la Asia India ni namba ngapi kwa uchawi na wanatumia aina gani ya uchawi?? nasikia ni wabaya ndio wanaofundisha wachawi wa Nigeria. Sikukuu njema. 😛oa
 
Mapepo ndilo jeshi kubwa analolitumia shetani. Kazi ya mapepo ni kuharibu kuuwa na kuteketeza binadamu, mali zake, kuvuruga ndoa, kusimamia maasi nk. Mapepo hutembea kwa makundi makubwa, kundi moja linakuwa na mapepo kati mia tano hadi alfu mmoja, na kama mtaa au kijiji kina watu wengi ndivyo hivyo hivyo idadi ya makundi ya mapepo huwa mengi yakitapakaa juu ya anga ya eneo hilo.

Kwa mfano mapepo yanatumiwa sana na wachawi, hutuma mapepo kwa idadi ya watu walioko ndani ya ibada, mapepo hayo huwafanya karibu watu wote kusinzia mara tu mahubiri yanapoanza.

Wachawi wakitaka damu ya binadamu mapepo hutumwa kwa madereva wa gari linaloelekea Morogoro na mapepo mengine hutumwa kwa dereva anayeelekea Dar, wachawi huchangua eneo la ajali, kwa mfano husema magari haya yakifika Ruvu yapate ajali.
Mapepo haya hukaa mbele ya uso wa kila dereva. Dereva akiangalia mbele anaona magari yanayokuja upande wake yako mbali sana, hivyo dereva huendesha gari bila uangalifu na mara nyingi gari linakuwa katikati ya barabara kwa mwendo wa kasi. Mapepo haya yakiona zimebaki mita chache huondoka mbele ya uso wa kila dereva, na magari yao hugongana na vifo kutokea.

Yapo mapepo ya ukimwi, mtu anapimwa hospitali vipimo vyote vinaonyesha kuwa mtu huyu tayari ameathirika, na huanza clinic ya waathirika, mtu huyu akikutana na mtu akayakemea haya mapepo, hutoka na afya ya mtu kurudi katika hali yake. Akirudi hospitali kupima ukimwi hauonekani tena. Wachawi na waganga wa kishenzi wamesambaza mapepo ya aina hii kwa watu wengi kweli kweli.

Majini ni daraja la juu na jeshi la shetani, majini nayo yamegawanyika kwa vyeo, kama jeshi lilivyo na vyeo kuanzia cheo cha chini cha kuruta hadi meja majini nayo yako hivyo hivyo. Unapotupiwa jini la meja kazi yake inakuwa ni nzito kulitoa, na uwezo wake wa kufanya uharibifu ndani ya mwili wako au familia yako huwa ni wa haraka na wa ufanisi wa hali ya juu. Majini mengi asili yake ni kutoka bara la Arabia, na ndiyo maana majina mengi ya majini yana asili ya Kiarabu.

Shetani anamtegemea sana jini jike, anayejulikana kama malkia wa anga, hili jini ni katili, katili kweli kweli. Malikia wa anga ndiye anayeratibu majanga yote, majanga yote yanayoikumba dunia kama vimbunga, moto, matetemeko ya nchi, mafuriko, ajali za ndege, ajali za meli. Malkia wa anga ndiye mtawala wa nyota zote, sayari zote, mwezi, jua, mbingu ya kwanza na mbingu ya pili.

Malkia wa anga anazo njia zake anazopita akitoka eneo moja la utawala wake kwenda eneo lingine. Kwa mfano akitoka ndani ya jua akija juu ya dunia yetu, na kwa bahati mbaya akateleza na kutoka sentimita chache nje ya njia yake, basi eneo lote linalozunguka eneo hilo hukumbwa na vimbunga vya pepo kali na matetemeko ya nchi.

Freemason na wachawi wote hupata nguvu ya uchawi wao pamoja na mafunzo ndani ya mashimo ya kuzimu yaliyotapakaa duniani kote, tekinologia ya kisasa inayotumika duniani sasa hivi ni product ya mashimo ya kuzimu. Kama Mungu angefungua macho yako ya ndani kwa muda mchache ungeshangaa, watu usiowatengemea ni wachawi wa kutupa.
 
Mikoa saba nchini Tanzania ndiyo tishio kwa kuwa na nguvu kubwa za uchawi
1. Tanga ndio kinara
2. Lindi unafuatilia
3. Dar es Salaam
4. Mtwara
5. Tabora
6. Kigoma
7. Mwanza

Mikoa yenye wachawi wengi, kwa maana kwamba karibu kila kaya kuna mchawi
1. Sumbawanga (Rukwa) ndio kinara
2. Ruvuma inafuatialia
3. Mbeya
4. Singida

Mikoa ambayo wananchi wake ndio wateja wakuu wa wachawi
1. Kilimanjaro inaongoza
2. Morogoro inafuatilia
3. Kagera

Wateja wengine wa wachawi
1. Wafanyabiashara
2. Wasanii
3. Kina mama wa nyumbani
4. Wanafunzi wa shule za sekondari hasa wa kidato cha pili.

wanasiasa je?
 
ok,majimoto!kijana anapobaleghe huota njoz za mapenz na kumalza haja zake,the same to girls,kwani hayo ni mabadiliko ya kibaiolojia,inakuaje wengne wananasibisha na MAJINIMAHABA?

mkuu BAJABIRI,jina lako naona ni kama inabidi liwe jini la lango la kuzimu,linaloendesha intellijensia ya polisi dhidi ya maandamano ya chadema na vurugu,
 
Mkuu Majimoto asante sana kwa ufafanuzi wako mzuri.

Hizi ajili kubwa zilizotokea hapa nchini kwa mfano MV BUKOBA na ajali za treni zilisababishwa na wachawi ama ni Malkia wa Anga alikuwa anapita offroad?

Kuna aina ngapi za mbingu na imekuwaje mbingu mbili zimechukuliwa na malkia wa anga? Na kuna vita inayoendela kati ya Malaika na Malkia wa Anga na kama ipo inatuadhiri vipi sisi binadamu?

Kuna aina ngapi za Hell? Na kuna malkia wangapi?

Na hizi nchi zilizoendelea mbona zinakimbilia sana kwenda kwenye mwezi na kufanya tafiti mbalimbali kwenye sayari kama vile Mars na uranus na Venus kuna nini huko ambacho sisi hatukifahamu?
 
Watawala wengi wamepata nafasi walizo nazo kwa msaada wa ndumba za wachawi, wachawi ikifika saa 6 usiku ni lazima ahudhurie kwenye madhabahu za kichawi katika mtaa/kitongoji chake. Kila madhabahu ina kiongozi wake na kila madhabahu ni lazima ziwepo kafara. Zipo taratibu za ibada za kishetani, kila mtu ni lazima ajue kucheza ngoma za kichawi, vikao vya kichawi vikianza anakuwepo katibu wa kikao akiandika tariifa za kikao.

Kinachotokea ni kuwa utakuta viongozi wanataka kuimarisha tawala zao, kama yeye mwenyewe ni mchawi ni lazima ahudhurie vikao vya kichawi, kama siyo mchawi, kiongozi huyo huwaendea waganga wa kishenzi. Mganga ndiye anayemwakilisha kwenye kikao. Kikao kikianza kila mwenye shida hueleza kikao shida yake, kwa mfano mheshimiwa fulani anataka aongezewe ulinzi usioonekana au utawala wa kiongozi fulani umeanza kuishiwa nguvu, kwa maana kuwa ushawishi aliokuwa nao kwa raia umeanza kupoa, hasikilizwi au anashindwa kutoa maamuzi.

Kiongozi wa madhabahu huangalia uzito wa shauri lililoletwa kwenye kikao, kama madhabahu inamudu kushughulikia shida hiyo basi kiongozi wa madhabahu huomba aletewe kafara ya madhabahu, kafara ni lazima iwe damu ya ndege, au ya mnyama au ya binadamu. Huteua kamati ya wachawi kati ya wawili hadi kumi kama shughuli ni kubwa, wachawi hawa kazi yao ni kuhakikisha damu inapatikana au kuhakikisha kuwa wamepindisha maisha ya watu ili kiongozi/mfanyabiashara arudi kwenye nafasi yake.

Kama shughuli ikiwa ni kubwa basi mchawi aliyeleta shida yake hupewa idhini ya kwenda kwenye madhabu kubwa zaidi, madhabahu hizi ni malango ya kuzimu, kuna malango yapo angani, mengine yapo chini ya maji baharini/maziwa/mito mengine yapo chini ya ardhi.

Zipo mbingu tatu, mbingu ya tatu ndiyo anayoishi Mwenyenzi Mungu, Malaika Watakatifu na Makerubi, mbingu ya pili ndiyo aliyokuwa akiishi Lucifer kabla ya kutimuliwa, ambayo sasa inamilikiwa na malkia wa anga pia anamiliki mbingu ya kwanza.

Kimsingi baada ya lucifer kutimuliwa, aliweka kwenye moyo wa dunia (moyo wa dunia ni shimo ndani ya ardhi) wakisubiri hukumu yao. Mwenyenzi Mungu alipomuumba Adam na Eva walikabidhiwa dunia na vitu vyote vilivyopo wavitawale, baada ya Eva na Adam kudanganywa na shetani kwa kutenda dhambi, shetani alichukua utawala wa dunia na vitu vyote vilivyopo Adam akabaki hana madaraka tena, ndiyo maana shetani aliondoka ndani ya shimo na kujieneza ulimwenguni pote kama mtawala.

Vita kati ya Malaika na shetani bado muda wake, siku na saa ya vita hiyo ipo, sijui ni lini.

Malaika ni walinzi wetu, kama upo vizuri na Mwenyenzi Mungu huna sababu ya kununua bastola, bunduki kwa ulinzi binafsi. Waite Malaika wa vita, huwa wanashuka na silaha nzito, anzisha vita na mamlaka zozote zilizoinuka juu yako, malaika wanagojea maelekezo yako, lolote utakalotamka hutekelezwa palepale.

Jehanum ya moto ipo moja tu, lakini mpaka leo bado ipo tupu.
 
Maji moto, swala la ukimwi wa kutupiwa nilishawahi kuona mtu wa aina hiyo lakini baada ya muda alipona na mzima mpaka leo.

Swali- kuna watu wanaishi duniani lakini wana asili ya mizimu walilogwa walipozaliwa au mimba ililogwa hao watu utakuta wanaonekana na watu wachache tu wengine hawawaoni ila wanaishi na wanaendesha maisha yao kama kawaida. inakuwaje hapo?
Kuna watu walikufa zamani lakini bado wapo duniani hii inakuwaje. mimi binafsi kuna mtu alikufa zamani sana mwaka 1994 nikiwa mdogo lakini yupo huwa namuona na anaendesha maisha yake kama kawaida na ni mwanadamu tu kama sisi hii imetokeaje?
 
Kuna mtu aliniambia kuna watu wa zamani sana wapo duniani(hawaonekani na watu wengi) wana mawasiliano na Mungu, wanaongea naye kabisa ni kweli?
 
Maji moto, swala la ukimwi wa kutupiwa nilishawahi kuona mtu wa aina hiyo lakini baada ya muda alipona na mzima mpaka leo.

Swali- kuna watu wanaishi duniani lakini wana asili ya mizimu walilogwa walipozaliwa au mimba ililogwa hao watu utakuta wanaonekana na watu wachache tu wengine hawawaoni ila wanaishi na wanaendesha maisha yao kama kawaida. inakuwaje hapo?
Kuna watu walikufa zamani lakini bado wapo duniani hii inakuwaje. mimi binafsi kuna mtu alikufa zamani sana mwaka 1994 nikiwa mdogo lakini yupo huwa namuona na anaendesha maisha yake kama kawaida na ni mwanadamu tu kama sisi hii imetokeaje?

Watu wasionekana ni wengi, wengi mno. Katika kila mazishi ya maiti 70 kwa mia za vijana na watoto uliyowahi kushiriki, mlizika majeneza yakiwa na migomba au magogo. Wapo watu wengi wanaotafuta wafanyakazi, na watu hao huwa wanataka mtu watakayemdhibiti siku zote za uhai wake. Kwa mfano mtu anataka kuanzisha kazi ya uvuvi, huwaendea wachawi wamtafutie vijana wenye uzoefu wa kuogelea na wenye nguvu. Wachawi hutuma watu wao maeneo ya kando ya bahari au maziwa ambapo vijana wengi hupenda kukaa na kuogelea kama cocoa beach au feri. Watu hawa wanapokuwa kwenye mawindo yao, huwa wana uwezo wa kurusha mishale ya kichawi kwa kutumia macho yao.

Kinachofanyika ni kuwa wakimwona kijana mwenye bidii ya kuogelea na kupiga mbizi huwa wanamfuata na kusalimiana naye macho ya hawa wachawi yanapoangaliana na macho ya huyo kijana, hurusha mishale ya kichawi na kuingia ndani ya macho ya hawa vijana bila ya vijana kuhisi kitu chochote. Mishale hiyo inakuwa ni alama, hata akisafiri kwenda mkoa gani bado anakuwa akionekana kwenye vioo vya kichawi, hivyo mipango ya kumchukua huandaliwa, kwa sababu kila kifo ni lazima kiwe na sababu , wachawi huandaa kifo rahisi kwa mazingara yao kama ajali ya gari, ajali ya kuzama ndani ya maji, kuumwa na nyoka au ugonjwa wa ghafula hasa kichwa kuuma sana mbele ya paji la uso kwa muda mfupi.

Ajali ikitokea wenyewe huwepo eneo hilo hilo la ajali, wanachofanya wanakupiga kofi la mgogoni na kuondoka nawe ukiwa mzima mzima, hugeuza mgomba au gogo linafanana sawasawa na mwili wa huyo kijana/mtoto. Ndugu zako wakija wanalitambua kuwa ni maiti ya ndugu yao. Wanakupulizia madawa ya kichawi kuondoa ufahamu wako na kupakwa madawa fulani usiweze kuonekana na watu, kisha wanakata ulimi usiweze kupiga kelele au kuongea.

Watu hawa huhifadhiwa juu ya dari za nyumba, chini ya mivungu wa kitanda, ndani ya makabati ya nguo, ndani ya makabati ya vyombo na wengine huwekwa maporini.

Viwanda vingi pugu road wapo wengi sana watu hawa, wavuvi wengi huwatumia kushusha nyavu chini ya bahari, maduka mengi huwatumia kwenda kuiba mali kwenye maduka mengine, wapo watoto wengi wamechuliwa kulea watoto wadogo kwenye nyumba nyingi sana, wapo wengi wapo mashambani wakilima, wapo wengi ni madereva wa mabasi na malori, wengi wapo maporini wakipasua mbao na kuchoma mkaa, wengi wapo mahotelini wakipika na kutoa huduma za vyumba. Viongozi wengi wanao watu hao kuimarisha nafasi zao za kazi au utawala. N.k.

Watu hawa chakula chao siku zote ni pumba za nafaka zilizolowekwa kwenye maji, na siku moja moja damu za watu. Siku wanapokula nyama, ni wakati mmoja wao anapofariki, mwili wake hukatwakatwa vipande vipande na kupewa kula pamoja na pumba za nafaka.
 
Hao kweli wanaweza kujiokoa kutoka mikononi mwao na kurudi katika maisha ya kawaida? Lingine ni kwamba watu hawa wakifa, roho zao zinakwenda wapi?
 
Majimoto umenifanya nifikiri sana juu ya walofariki na uwezekano wa kuwa hai, utajuaje kama umezika migomba na sio watu na vipi uwezekano wa kuwarudisha kama watu wa kawaida?
 
Happy new year.

Mkuu majimoto asante kwa ufafanuzi wako. Mkuu majimoto sasa kama unamjua adui yako na kila siku anakufanyia vituko leo hichi kesho kile na unasamehe kila siku kama Mungu alivyosema lakini bado anakuwa kichwa ngumu anaendelea. Sasa Mkuu nitawaitaje Malaika na kuwaambia wakampatie kipigo?

Kama wachawi wanakuwa na mikutano yao ya kila siku na wanapangiana kazi za kufanya kwa nini wachawi wa mtaa mmoja wanauana?

Mkuu kuna testimony nyingi za watu wanaosema kwama walipelekwa Jehanam na Yesu na wakaona watu wakipata mateso yasiyokifani sasa hawa ni waongo ama kuna sehemu nyingine ambayo watendeji dhambi wanapelekwa kabla ya Jehanam na ambao hawana dhambi wanaenda wapi?

Hayo Joyceline aliongelea yameshamtokea rafiki yangu mmoja nilipokuwa mdogo alikuwa anatuambia anakuja kuchukuliwa shuleni na kurudishwa nyumbani na mmoja wa rafiki za mama yake ambaye alikuwa ameshafariki.Siku moja mama yake akamuuliza unarudishwa na nani nyumbani, akamwambia ni yule rafiki yako wa pale madukani mama yake akamwambia yule mama alishafariki siku nyingi lakini binti alibisha sana ikabidi siku hiyo mama yake aje shuleni kumchukua ili aone kama atakutana na huyo rafiki yake lakini hakumuona na wala huyo rafiki yake hakutokea mpaka hivi leo.

Ina maana misukule wanaendelea kusaidia watu wanaowajua kama wakikutana nao? Ama alikuwa anampangia nini huyo mtoto?
 
Happy new year.
Mkuu majimoto asante kwa ufafanuzi wako. Mkuu majimoto sasa kama unamjua adui yako na kila siku anakufanyia vituko leo hichi kesho kile na unasamehe kila siku kama Mungu alivyosema lakini bado anakuwa kichwa ngumu anaendelea. Sasa Mkuu nitawaitaje Malaika na kuwaambia wakampatie kipigo? Kama wachawi wanakuwa na mikutano yao ya kila siku na wanapangiana kazi za kufanya kwa nini wachawi wa mtaa mmoja wanauana?

Mkuu kuna testimony nyingi za watu wanaosema kwama walipelekwa Jehanam na Yesu na wakaona watu wakipata mateso yasiyokifani sasa hawa ni waongo ama kuna sehemu nyingine ambayo watendeji dhambi wanapelekwa kabla ya Jehanam na ambao hawana dhambi wanaenda wapi?

Hayo Joyceline aliongelea yameshamtokea rafiki yangu mmoja nilipokuwa mdogo alikuwa anatuambia anakuja kuchukuliwa shuleni na kurudishwa nyumbani na mmoja wa rafiki za mama yake ambaye alikuwa ameshafariki.Siku moja mama yake akamuuliza unarudishwa na nani nyumbani, akamwambia ni yule rafiki yako wa pale madukani mama yake akamwambia yule mama alishafariki siku nyingi lakini binti alibisha sana ikabidi siku hiyo mama yake aje shuleni kumchukua ili aone kama atakutana na huyo rafiki yake lakini hakumuona na wala huyo rafiki yake hakutokea mpaka hivi leo. Ina maana misukule wanaendelea kusaidia watu wanaowajua kama wakikutana nao? Ama alikuwa anampangia nini huyo mtoto?

Kuzimu ni sebule (sitting room) ya shetani, watu wote wanaokufa wakiwa wateja wa shetani hukaa mkono wa kuume wa shetani ndani ya sebule yake. Shetani anawatumikisha apendavyo, kwa suluba na vipigo vya kutisha, kimsingi mtu yeyote anayekufa, kinachokufa ni mwili wake, endapo utaingia kuzimu, kifo chako cha pili cha roho yako ni lazima, siku ya siku ikifika roho yako itaondolewa kuzimu na kutupwa jehanam na hiyo ndiyo itakuwa mauti yako ya pili.

Watu waliopelekwa kuzimu wanaweza kabisa kutolewa na kurudi tena duniani.

Maduka mengi katika jiji la Dsm yanaendeshwa kwa juju. Usishangae mwanao aliyekufa siku chache zilizopita yuko ndani ya nyumba ya jirani yako au ndugu yako akitumikishwa. Jambo moja ambalo napenda kulisema tena, hakuna kijana yeyote aliyekufa ghafula kwa ugonjwa au kwa ajali na kuzikwa, mwili wake ukabaki ndani ya kaburi, hakuna. Lipo andiko langu nilisema tekinologia yote inayotumika sasa hivi duniani chanzo chake ni kuzimu, nitaelezea hili siku nyingine. Vijana wenye nguvu na walioelimika wanatafutwa kama dhahabu ya mwadui huko kuzimu na vifo vya ghafula huhamisha mamia ya hawa vijana kila mwaka toka maisha ya kidunia na kuwashusha kuzimu kutumikishwa.
 
Hakika yule atakayeng'ang'ana na Bwana Mungu aliye hai hakika tutapona na janga hili:

Ninachoweza kusema ni moja tu!

Hakika watakaomtegemea MUNGU kupitia jina la mwanae aliyemleta hapa dunia na akateswa kwa sababu ya Mimi na Wewe na si mwingine ni YESU KIRSTO pekee hakika nawaambia ya kwamba ndio watakao pona janga hili la shetani pepo mchafuu!

Nina IMANI ya kutosha ya kutosha kwa kusema vijana wakimrudia MWOKOZI hakika hata haka kashetani mjaribu watu wa MUNGU hatadhubutu kupenza uso wake hapa kwa watu wa MUNGU.

Hakika vijana wemetekwa na Dunia yenye kila anasa lakini ni KHERI makanisa waendelee kujaza vijana Imani na siku mtu anapojaribiwa na akutwe ktk hali ya Ushindi ktk KIRSTO YESU BWANA wetu na mtetesi wetu!

Amen!!!!
 
Kuzimu ni sebule (sitting room) ya shetani, watu wote wanaokufa wakiwa wateja wa shetani hukaa mkono wa kuume wa shetani ndani ya sebule yake. Shetani anawatumikisha apendavyo, kwa suluba na vipigo vya kutisha, kimsingi mtu yeyote anayekufa, kinachokufa ni mwili wake, endapo utaingia kuzimu, kifo chako cha pili cha roho yako ni lazima, siku ya siku ikifika roho yako itaondolewa kuzimu na kutupwa jehanam na hiyo ndiyo itakuwa mauti yako ya pili.

Watu waliopelekwa kuzimu wanaweza kabisa kutolewa na kurudi tena duniani.

Maduka mengi katika jiji la Dsm yanaendeshwa kwa juju. Usishangae mwanao aliyekufa siku chache zilizopita yuko ndani ya nyumba ya jirani yako au ndugu yako akitumikishwa. Jambo moja ambalo napenda kulisema tena, hakuna kijana yeyote aliyekufa ghafula kwa ugonjwa au kwa ajali na kuzikwa, mwili wake ukabaki ndani ya kaburi, hakuna. Lipo andiko langu nilisema tekinologia yote inayotumika sasa hivi duniani chanzo chake ni kuzimu, nitaelezea hili siku nyingine. Vijana wenye nguvu na walioelimika wanatafutwa kama dhahabu ya mwadui huko kuzimu na vifo vya ghafula huhamisha mamia ya hawa vijana kila mwaka toka maisha ya kidunia na kuwashusha kuzimu kutumikishwa.

Asante kwa maelezo haya.
Tusome pia ufunuo wa Yohana 20.
 
Kuzimu ni sebule (sitting room) ya shetani, watu wote wanaokufa wakiwa wateja wa shetani hukaa mkono wa kuume wa shetani ndani ya sebule yake. Shetani anawatumikisha apendavyo, kwa suluba na vipigo vya kutisha, kimsingi mtu yeyote anayekufa, kinachokufa ni mwili wake, endapo utaingia kuzimu, kifo chako cha pili cha roho yako ni lazima, siku ya siku ikifika roho yako itaondolewa kuzimu na kutupwa jehanam na hiyo ndiyo itakuwa mauti yako ya pili.
Bwana Majimoto naona hii ni imani nyingine unayoileta hapa, uchawi, shetani, mapepo, majini, nk hivi vipo lakini unapoingiza swala la wafu na hali zao naona unajichanganya maana ki Kristo wafu wako katika makaburi yao, wala hawamkumbuki Mungu, hawamshukuru, au kumsifu(zaburi 6:4-5, zaburi 115:17) kwa sababu hata mawazo yao yamepotea (zaburi 146:3-4). Walio hai ndio wanojua kuwa watakufa lakini wafu hawajui neno lolote, kumbukumbu lao limesahauliwa, kifo hufananishwa na usingizi (zaburi 13:3), (Ayubu 14:10-12). Yesu aliweka bayana alipomzungumzia Lazaro (Yohana 11:13-15). Hata hivyo biblia inaongelea kufufuliwa kwa waliolala wengine kwa maisha ya milele wengine kwa mauti ya milele (Daniel 12:2, Yohana 5:28-29, Ufunuo 20:14)

Kama ni elimu mpya tofauti na hii ya Kikristo (maana hata signature yako inathibitisha wewe ni mkristo) tuambie mapema kuliko kuelekea kusiko na kupoteza wengi wenye ufahamu kidogo juu ya hali ya wafu.
 
Bwana Majimoto naona hii ni imani nyingine unayoileta hapa, uchawi, shetani, mapepo, majini, nk hivi vipo lakini unapoingiza swala la wafu na hali zao naona unajichanganya maana ki Kristo wafu wako katika makaburi yao, wala hawamkumbuki Mungu, hawamshukuru, au kumsifu(zaburi 6:4-5, zaburi 115:17) kwa sababu hata mawazo yao yamepotea (zaburi 146:3-4). Walio hai ndio wanojua kuwa watakufa lakini wafu hawajui neno lolote, kumbukumbu lao limesahauliwa, kifo hufananishwa na usingizi (zaburi 13:3), (Ayubu 14:10-12). Yesu aliweka bayana alipomzungumzia Lazaro (Yohana 11:13-15). Hata hivyo biblia inaongelea kufufuliwa kwa waliolala wengine kwa maisha ya milele wengine kwa mauti ya milele (Daniel 12:2, Yohana 5:28-29, Ufunuo 20:14)

Kama ni elimu mpya tofauti na hii ya Kikristo (maana hata signature yako inathibitisha wewe ni mkristo) tuambie mapema kuliko kuelekea kusiko na kupoteza wengi wenye ufahamu kidogo juu ya hali ya wafu.

fredmlay, maelezo yangu yako wazi, kila mtu, siku yake inapofika atakufa kama alivyopangiwa na Mungu.

Tatizo langu ni majeneza tunayobeba ndani wameweka mgomba au kipande cha ukuni na macho yenu yakageuzwa kuaminishwa kuwa ndugu yetu aliyefariki ndiye huyu tunayekwenda kumzika, ukisoma maelezo yangu nimesema huyo ndugu aliyechukuliwa kichawi siku yake naye inapofika naye huwa anakufa, tofauti hapa ni kuwa huko aliko huwa hawaziki, bali wanamkatakata vipande vipande na nyama yake huliwa.
 
Back
Top Bottom