Biblia wanayotumia Wakotoliki na wanayotumia Walutheri pamoja na madhehebu mengine ni tofauti?

Biblia wanayotumia Wakotoliki na wanayotumia Walutheri pamoja na madhehebu mengine ni tofauti?

Kitombise

JF-Expert Member
Joined
Sep 24, 2013
Posts
8,575
Reaction score
25,619
Nayasema haya ni kutokana na kukutana na biblia ya ndugu yangu ambae ni mkatoliki, sasa wakati naisoma nikaona mbona inautofauti.

Utofauti nimeukuta kwenye baadhi ya vifungu ndani ya biblia, japo unakuta maudhui yako sawa ila maneno yanatofautiana.

Mawazo yangu(nikafikiri au ndo zile habari nilizozisoma za Martin Lutter!)

Embu kwa wajuvi wa mambo kujeni mnieleweshe.

Asanteni!
 
Nayasema haya ni kutokana na kukutana na biblia ya ndugu yangu ambae ni mkatoliki, sasa wakati naisoma nikaona mbona inautofauti.

utofauti nimeukuta kwenye baadhi ya vifungu ndani ya biblia, japo unakuta maudhui yako sawa ila maneno yanatofautiana.

mawazo yangu(nikafikiri au ndo zile habari nilizozisoma za Martin Lutter!)

embu kwa wajuvi wa mambo kujeni mnieleweshe.
asanteni..!!
Wakatoliki ina vitabu saba vya ziada

 
Weka ushahidi wa hivyo vifungu hapa,
Kuna vifungu Vingi vimeondolewa kwenye Biblia Matoleo mapya Mengi..
Zaidi ya Vifungu 500
Na vingine vimebadilishwa..
So namuunga Mkono Hoja..

Na hata hivyo kuna Vitabu(Sura) 76 za Biblia ya Roman na kuna Vitabu 66 biblia ya Protestant.. na Orthodox wana vitabu zaodo ya 76 kuanzia 82 na kuendelea

Kama utataka Ninaweza kukuonyesha
 
mkuu ungetoa mfano wa hivo vifungu vilivyo tofauti
Mimi tofauti ambayo nimeiona ni idadi ya vitabu, biblia ya Wakatoliki ina vitabu 72, ya wasio wakatoliki una vutabu 66.

Sijui kwanini wengine wamepunguza na wengine wameongeza wakati biblia hairuhusiwi kuongezwa wala kupunguzwa neno.

Karibuni kwa ufafanuzi.
 
Mmiliki wa biblia na Kanisa Katoliki. Hivyo biblia yake ndio sahihi kuliko zote.
Hivyo kwanza tambua hilo.

Pili biblia ya kwanza iliandikwa kigiriki/kiebrania kisha tafsiri ya lugha zingine. Mfano kiingereza, kifaransa n.k

Sasa biblia nyingi zimefanyiwa tafsiri kutoka lugha ya pili nasio lugha mama. Hivyo kupelekea kupoteza baadhi ya tafsiri halisi.

Nyingine niswaga za makanisa hayo mengine kutaka biblia iendane na matakwa yao.

Viva kanisa katoliki viva wamiliki halisi wa bablia
 
hata hivyo wakatolik, hawaamini katika biblia peke yake, wanaamini pia katika tamaduni,pia wanaweza kutunga jambo lao na ikawa hivo
mfano ubatizo wa watoto wachanga. biblia inasema unatakiwa kuamini kwanza ndo ubatizzwe wao wanasema siyo lazima
.."wanaweza kutunga"..(?)Hili umelitoa wapi?Kawaulize vizuri usijitungie majibu.
 
Kuna vifungu Vingi vimeondolewa kwenye Biblia Matoleo mapya Mengi..
Zaidi ya Vifungu 500
Na vingine vimebadilishwa..
So namuunga Mkono Hoja..

Na hata hivyo kuna Vitabu(Sura) 76 za Biblia ya Roman na kuna Vitabu 66 biblia ya Protestant.. na Orthodox wana vitabu zaodo ya 76 kuanzia 82 na kuendelea

Kama utataka Ninaweza kukuonyesha
Orodhesha unavyovujua, siyo kusema tuu kama unataka.
 
Ni tofauti mkuu wakatoliki walikubali na vitabu vingine ambavyo vinakubaliana na mafundisho yao mengine ya uongo kama kuwaombea wafu, ibada za sanamu, unywaji wa pombe nk ambayo kwenye vitabu vilivyokubaliwa na wengine vile 66 haviyakubali ndiyo utaona biblia yao ina vitabu kama wamakabayo, sira nk
 
Orodhesha unavyovujua, siyo kusema tuu kama unataka.
Screenshot_20240307_123604_Chrome.jpg

Screenshot_20240307_123630_Chrome.jpg

images (27).jpeg


Lakini kama haitoshi unaweza pia ukapitia Hapa kwenye Wikipedia..
 
Orodhesha unavyovujua, siyo kusema tuu kama unataka.
Sikupenda kuorodhesha moja kwa moja maana kuna wengine huwa hawapendi..
Na hiyo ndio sababu nikauliza kwanza..

Ushahidi mwingine ninao kwenye Baadhi ya biblia nimeziweka kama Apps kwenye simu yangu zinatofautiana kwenye baadhi ya Aya
Kuna zingune hazimalizi aya na zingine zinaishia nusu na zingine hazina kabisa hiyo aya
 
Mmiliki wa biblia na Kanisa Katoliki. Hivyo biblia yake ndio sahihi kuliko zote.
Hivyo kwanza tambua hilo.

Pili biblia ya kwanza iliandikwa kigiriki/kiebrania kisha tafsiri ya lugha zingine. Mfano kiingereza, kifaransa n.k

Sasa biblia nyingi zimefanyiwa tafsiri kutoka lugha ya pili nasio lugha mama. Hivyo kupelekea kupoteza baadhi ya tafsiri halisi.

Nyingine niswaga za makanisa hayo mengine kutaka biblia iendane na matakwa yao.

Viva kanisa katoliki viva wamiliki halisi wa bablia
Hebrew Bible, ina vitabu vichache
 
Biblia ni Moja tu yenye Vitabu 73.

Madhehebu Yalianzishwa baadae ndo Yanachagua yaende na Vitabu Gani kukidhi kile Wanachokiamini.

Hapo ndo utawakuta Waliochagua Vitabu 66,Wengine 64, Wengine 53 basi ilimradi kila mtu na biblia yake
 
Ni tofauti mkuu wakatoliki walikubali na vitabu vingine ambavyo vinakubaliana na mafundisho yao mengine ya uongo kama kuwaombea wafu, ibada za sanamu, unywaji wa pombe nk ambayo kwenye vitabu vilivyokubaliwa na wengine vile 66 haviyakubali ndiyo utaona biblia yao ina vitabu kama wamakabayo, sira nk
Kwanini unafikiri Walutheri waliviondoa Hivyo vitabu??
 
Kwa kifupi sana.

Mfalme Constantino wa dola ya rumi (roman) kipindi hiko wakiwa wanatawala dunia, aliwahi kupigana vita na aliweka ishara ya msalaba kama ishara kuu ndani ya jeshi lake. Akashinda ile vita, kwahiyo akatoa agizo dunia nzima kuwe na dini moja tu, ya Kikristo japo mwanzoni dola hiihii ya Rumi ilikuwa ikiipinga mno dini ya Kikristo na hata kuchoma moto maandiko matakatifu yaliyoachwa na waasisi wa imani hiyo, yaani mitume na manabii.

Unfortunately, ndani ya serikali yake, alijali sana kuwaweka Wakristo, matokeo yake dini ikaanza kupoteza ile nguvu ya rohoni na kutoka ktk ile misingi ya mitume na manabii. Tamaduni za kirumi kama kuabudu sanamu, sikukuu n.k vikaanza kuingizwa ndani ya kanisa. Kanisa likafa kabisa rohoni, likabaki jina tu la Ukristo ila rohoni hakukuwa tena na ile nguvu.

Miaka mingi mbele, kwa kufanya utafiti mbalimbali walitokea watu kadhaa wakasema kwamba imani ya Kikristo imepotoshwa na Kanisa Katoriki kwa kufanya ibada za sanamu, kuingiza sikukuu zisizo na maana ndani ya kanisa pamoja na mafundisho manyonge. Watu hawa kwa Historia ya Kanisa wanafahamika kama wana wa uamsho.


Watu hao kuna akina Max, Martin Luther n.k kabla ya Martin Luther walikuwepo watu kadhaa kama watano ambao walichallenge uendeshwaji wa Imani ya Kikristo unaoongozwa na Rumi(Roma) ila tunamtambua Martin Luther sababu yeye aliachana nyaraka nyingi na ndie mwana uamsho mkubwa wa mwisho.

Rumi walihizinisha vitabu 72 na kuundwa Biblia, ndani ya hivyo vitabu 72, Martin Luther King aliviona vitabu 6 havina mafundisho mazuri/umuhimu ktk makuzi ya maisha ya Mkristo kiroho. Ifahamike kuwa Martin Luther alikuwa msomi na Padre ndani ya Kanisa Katoriki.

Baada ya Martin Luther kusigana na viongozi wake, Martin Luther na Katoriki wakatengana, ndipo ukazaliwa uamsho mpya ndani ya Kanisa, hapo ndipo likaja dhehebu la KKKT, lilikuwa na uamsho mkubwa saana kiroho, huduma zote ambazo Yesu aliacha ndani ya Kanisa kupitia Roho Mtakatifu zilionekana, shetani jinsi alivyo na nguvu akapiga kanisa KKKT nalo likatawanyika, hapo sasa ukazaliwa Upentekoste, Pentecoste na KKKT ni kama baba mmoja ila mama tofauti.


Mwisho, tafsiri za Biblia zipo nyingi saana, wala usishtushwe na hizo tafsiri ila kwa sehemu kubwa maana ni ile ile. Ni sawa na kitabu kimoja cha Ushairi kisha kikachambuliwa na maprofessor wa kiswahili, wengine kutoka UDOM, wengine kutoka UDSM na wengine SAUT ila maana ni zile zile.
 
Back
Top Bottom