Bilioni 286 kujenga uwanja Mpya wa 'Samia Suluhu Hassan Arusha Stadium' Kwa ajili ya AFCON 2027

Bilioni 286 kujenga uwanja Mpya wa 'Samia Suluhu Hassan Arusha Stadium' Kwa ajili ya AFCON 2027

Wajuzi wa mambo kati ya uwanja huu na ule uwanja wa Kenya una ojengwa upi mzuri kimchoro ?!
Japo wa kenya ni mkubwa utabeba watu elfu 60 wamesema.View attachment 2938903
kupanga ni kuchagu,
ya wakenya wang'ang'ane nayo wakenya na waTz tufanye yetu 🐒

Chabo na tamaa zisituzubaishe wala kutuchelewesha...
Kazi uendelee na ikamilike kikamilifu kama ilivyo pangwa na kuamuliwa 🐒
 
Vipi na kuhusu zile Arena 2 walisema wata jenga, moja Dar es salaam na Nyingine Dodoma, zime ishia wapi maana naona kimya hakuna lolote, kwa mnao jua kuhusu hili tafadhali naombeni majibu.
Wa Dodoma unajengwa mkuu...wamezungushia mabati kabisa...upo juu kilimani kama unaenda Ihumwa unakua unaangalia jiji la dodoma kw uzuriii....
 
Serikali imeingia mkataba wa kuanza Ujenzi wa uwanja Mpya Jijini Arusha Maarufu kama Samia Suluhu Hassan Stadium ambao ni Mahsusi Kwa Ajili ya Maandalizi ya AFCON 2027.

Uwanja huo utagharimu zaidi ya Shilingi Bilioni 286.

Kazi iendelee [emoji116][emoji116]

============

Serikali kupitia wizara ya Sanaa ,Utamaduni na Michezo leo Machi 19, 2024 imesaini mkabata wa ujenzi wa Uwanja wa Dokta Samia Suluhu Hassani wenyewe thamani ya shilingi bilioni mia mbili na themanini na Sita ambao utatumika katika michuano ya mataifa Afrika AFCON 2027 inayoandaliwa na nchi za Tanzania, Kenya na Uganda

Akizungumza na waandishi wa habari Waziri wa Michezo Dokta Damasi Ndumbaro amesema Lengo la uwanja huo kujengwa mkoani Arusha ni kuchochea maendeleo ya sekta utalii kupitia michezo.

View attachment 2938864View attachment 2938865View attachment 2938866
Tushachoka na hizo stori benjamin mkapa hadi leo ukarabati haujaisha
 
Kwajinsi nilivyomsikiliza mh waziri,niseme tu kunawakati tunatakiwa kuwa na maamuzi magumu sana(magufuli style) ili tusonge mbele.Hao watu waziri anaosema wanaleta ujanja ujanja Arusha wapo wengi sana.Emu fikiria mradi mkubwa kama huo walikuwa wanataka kufanya yao mbele ya waziri bila kuogopa je ni miradi mingapi tusiyoijuwa au watu wangapi waliofanyiwa mambo kama hayo?Ningekuwa mwenye maamuzi muda huu wangekua wako makwao wanachunga mbuzi watendaji wa aina hiyo.Arusha inaitajika kupitia fagio la kuwaondoa watendaji wasiokuwa na nia ya maendeleo bali mambo yao binafsi.
Bil 286 ni fedha nyingi sana kama zingepelekwa kwenye miradi mingine na kusimamiwa kikamilifu,ila kama serikali imeamua kujenga uwanja inabidi kuwa makini sana katika kusimamia fedha hizo ili zifanye kazi husika iliyokusudiwa.
 
Back
Top Bottom