Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Ukiambiwa kununua pia unatakiwa ukanunue kwenye duka ambalo linapokea huduma ya bima siyo kulipa cash.
Watu wengi tunatumia makampuni haya kwa kulipiwa na ofisi...
hivyo sometimes wala hatujui hasa mtu unalipa kiasi gani na kama 'value for money'
inazingatiwa....
sasa ningependa kujua kati ya kampunio zoote zilizopo
ipi ni better?
ambayo ni cheap but ni nzuri zaidi?
kwa mtu binafsi anaetaka kujilipia ...aende kampuni ipi?
gharama zikoje?
huduma zikoje?
mfano mtu anatakiwa kutibiwa ugonjwa wenye vipimo gfhali na operesheni kadhaa
aende kampuni ipi?
Metropolitan 20 mil kwa mwaka, ina cover 'some'
strategy ni chee zaidi
ikoje gharama zake?AAR mkuu
ikoje gharama zake?
Mimi nafikiri uangalie zaidi ipi ambayo unaweza kuitumia kwenye hospitali zenye madaktari wazuri na dawa.
Nilifanya research isiyo rasmi kipindi fulani wakati namtafutia kijana wangu na mama yake nikagundua coverage ya AAR ni nzuri,inakubalika hospitali zote kubwa.
Ila bei yao imechangamka,mama na mtoto niliwalipia 2.2M hiyo ni gold membership kwa mwaka,ni international kwa maana popote duniani unatibiwa na wanatibiwa nje ya nchi kama ugonjwa utashindikana tz.
Ila kuna silver na bronze na kama nakumbuka vizuri tofauti ya gharama kati ya packages ilikuwa around laki 3
Mimi nafikiri uangalie zaidi ipi ambayo unaweza kuitumia kwenye hospitali zenye madaktari wazuri na dawa.
Nilifanya research isiyo rasmi kipindi fulani wakati namtafutia kijana wangu na mama yake nikagundua coverage ya AAR ni nzuri,inakubalika hospitali zote kubwa.
Ila bei yao imechangamka,mama na mtoto niliwalipia 2.2M hiyo ni gold membership kwa mwaka,ni international kwa maana popote duniani unatibiwa na wanatibiwa nje ya nchi kama ugonjwa utashindikana tz.
Ila kuna silver na bronze na kama nakumbuka vizuri tofauti ya gharama kati ya packages ilikuwa around laki 3
Wakuu mimi ni mjasiriamali na nahitaji bima ya afya, je utaratibu kuipata ukoje!? Naweza kupata kwenye hospitali ya wilaya? Gharama zake zikoje in comparison!? Nimewahi tumia ya NHIF nikiwa chuo na tulikuwa tunalipia 50000! Sijajua sasa gharama zikoje
Fika kwenye Ofisi yoyote ya Bima ya Afya (NHIF) ilyo karibu nawe watakujuza utaratibu mzima. Kima cha kuchangia kwa mwanachama ambaye si mtumishi wa umma (mjasiliamali) ni Sh. 968,500/= kwa mwaka na watakaonufaika na matibabu ni wewe mchangiaji, mwenza wako (mkeo/mumeo) na watoto wenu wenye umri chini ya miaka 18 au wazazi wenu ilimradi idadi ya wtegemezi wasizidi wanne. Kwa mantiki hiyo wanfaika wasizidi sita. Ukisaliia nausaini mkataba wewe a waegemezi wako mtapwa vitambulisho vitakavyowawezesha upata huduma za matibabu kwenye hospitali yoyote iliyosajiliwa na Bima ya Afya popote ndani ya mpaka ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania.
Aidha huduma zinazogharamiwa na Bima ya Afya ni:- Ada ya uandikihji, wagonhjwa wa nje(Outpatiens) wagonjwa wakulawa (inpatients), vipimovyote viakavyotakiwa na daktari, Dawa zote kwa mujbu wa Orodha ya Taifa ya Dawa, atibabu ya macho(pamoja na mwani ya kusomea kwa mwanchama mchangiaji tu), matibau ya kinywa na meno (isipokuwa meno ya bandia) huduma zaupasuaji kuanziaupasuaji mdogo hadi upasuai mkubwa na wa kitaalau (specialist surgery). Hayonika uchache,maelezozaidi unawe kuyapata kwenye Ofizi za Bima ya Afya ambazo zipo kila Mkoa.