Bingwa wa kusilimisha Wakristo ameingia Qatar Wakristo wengi wahofiwa kusilimu. Eneo la FIFA lapambwa kwa maneno ya Mtume Muhammad S.A.W

Bingwa wa kusilimisha Wakristo ameingia Qatar Wakristo wengi wahofiwa kusilimu. Eneo la FIFA lapambwa kwa maneno ya Mtume Muhammad S.A.W

Dini isiyo heshimu dini nyingine mm kwanga hua naiona ni uchafu tu nashukuru sana kuzaliwa mkristo maana naheshimu dini zote maana kama wao wanamuomba Mungu wao na anawajibu kihelehele cha nn ww kujifanya ndo uko sahihi .Mungu sio mnavomfikilia ww jiulize india na china ina watu billion ngapi ina maana Mungu hawataki hao ama hao ndo hawaombi ???mbona mambo yao yako poa tu.
Sasa njoo bongo unakutana mtu amepauka ananuka shida .. kapigika na maisha anajifanya anamjua sana Mungu hua naishia kucheka tu.
 
Watu wanaenda kuangalia mashindano ya kombe la dunia yeye analeta mambo ya mhadhara wa kidini, sio pahala pake.

Na kwenda mbinguni hakuhusiani katu na mambo ya kuslimu, hayo mambo ya kuslimu yanabaki hapa hapa duniani, hizo ni siasa tu religious politics.

uko sahihi mkuu
 
Ana kichaa cha akili na watakaomruhusu kufanya hiyo mihadhara hawajielewi
 
Ni rahisi sana maaskofu nao waombe hadhara hasa wa marekani
 
Kwahyo wana muda na dini inayotangaza mauaji ili kupata mabikra 72 eti ?!
Saana,baada ya 9/11 vitabu vya kiislam vilikua vikihitajika mno kiasi kupotea sokoni,na wazungu wanasilimu Sana,haraka haraka ni Arthur wagna afd,akiwa kiongozi wa chama Cha kupinga German Islamization,aliposoma Qur'an akasilimu akajivua na uanachama
 
Waislamu ni wakarimu na ni watu wanaothamini utu wa mwanadamu, na wanaongozwa na Mwenyezi Mungu na Mtume wake katika kufanya mambo yao kwa uadilifu, hisani na huruma.

Ni kwa kuishi kwa wema, na kujenga uhusiano mwema na wasio Waislamu ndipo Waislamu wanapoweza kufanya Da’awah na kuwalingania wasio Waislamu katika njia ya Haki ya Uislamu.
Wakarimu..??..😅😅😅

Dunia nzima inayumba sababu ya magaidi wa kiislam, kuanzia baba lao IS,Alshabab,Alqaeda, na mengiyo mengi tu....

Hebu mrudie kuwaslimisha hao kwanza ndipo dunia ione ustakharabu wa waislam...
 
Qatar, imemualika mhubiri mkali zaidi duniani, ambaye kwa maneno yake amefanikiwa kusilimisha mamilioni ya Wakristo duniani. Huyu ni bingwa Zakir Naik

Zakir Naik tayari amefika Doha nchini Qatar kabla ya Kombe la Dunia la FIFA 2022, na atatoa mihadhara ya kidini katika muda wote wa mashindano nchini humo. Mamilioni ya Wakristo wahofiwa kusilimu.

View attachment 2422130

Wakati Kombe la Dunia la FIFA la 2022 linaanza saa moja jioni ya leo nchini Qatar, mhubiri maarufu wa Kiislamu mwenye Zakir Naik, tayari amewasili Doha nchini Qatar kabla ya Kombe la Dunia la FIFA 2022, na atatoa mihadhara ya kidini katika muda wote wa michuano hiyo nchini humo.

"Mhubiri Sheikh Zakir Naik yuko Qatar wakati wa Kombe la Dunia na atatoa mihadhara mingi ya kidini wakati wote wa Kombe la Dunia" ndani na nje ya viwanja.

View attachment 2422132
.................

Wakati huo huo Qatar Yaonyesha Hadithi za Mtume Muhammad (s.sa.w) Katika Maeneo ya Kombe la Dunia la FIFA 2022

View attachment 2422135

Wenyeji wa Kombe la Dunia la 2022 Qatar wamepamba kukaribisha ujio wa mashabiki wa soka. Mmoja wao anaonyesha dondoo za hadithi kutoka kwa Mtume Muhammad SAWW kwenye kona tofauti za barabara katika nchi ya Ghuba.

Kulingana na vyombo vya habari kadhaa vya humu nchini, michoro inayoonyeshwa inalenga kuutambulisha Uislamu kwa mashabiki wa soka ambao watakuja kutazama mashindano ya soka yanayofanyika kila baada ya miaka minne.

View attachment 2422136

Nukuu za hadith za Mtume (s.a.w.w.) ina maandishi ya kiarabyu na tafsiri ya Kiingereza. Michoro hiyo ina hadithi kuhusu huruma, hisani, na motisha ambazo zinawahimiza watu daima kufanya mema.

Baadhi ya hadithi ni pamoja na, “Kila jema ni sadaka”, “Asiyekuwa na huruma kwa wengine, hatatendewa huruma”, na “Jilindeni na Moto wa Jahannam”.

Qatar inaonekana kuchukua fursa ya Kombe la Dunia la 2022 kama msukumo wa kushiriki utamaduni na maadili yake na wageni wanaokuja kutoka kote ulimwenguni.

View attachment 2422138

Kombe la Dunia la FIFA 2022 nchini Qatar limebakiwa na masaa machache tu, limeratibiwa kuanza Novemba 20 hadi Desemba 18.

Toleo la mwaka huu litakuwa ni mashindano ya kwanza kuandaliwa Mashariki ya Kati, ya kwanza katika nchi yenye Waislamu wengi, na ya kwanza kufanyika mwishoni mwa mwaka wa kalenda, mwezi Novemba na Desemba.
Ana MACHO YOTE MAWILI ?...kama anayo basi wala hatujali.
 
Anasilimisha wakristo au anaarabisha Waafrika kuingia ujinga wa kiarabu?
Unaonesha hata unachokiandika hukielewi.

Waafrika ni nini? Waarabu ni nini?

Hivi huèlewi kuwa Waarabu wengi duniani ni Waafrika?

Au wewe ni wale wa zile shule zetu?
 
Back
Top Bottom