Binti mdogo anayemfungia ndani Mama yake mgonjwa aliyepooza kutwa nzima na kwenda kutafuta pesa za kumuhudumia inaumiza wengi mtaani

Ni
Peleka hii habari kwenye vyombo husika, wao ndo wataleta taarifa official nje na hapo ni UTAPELI
Nimeshea hapa nilichokutana nacho pamoja na kutoa wito kwa serikali kuangalia namna ya kuwasiaidia wagonjwa wa muda mrefu kama hawa na wala huyo binti hakunituma hapa kuomba chochote. Binti karidhika na maisha anayoishi
 
Serikali za mtaa, kata wapo wapi wao ndo wapo karibu zaidi na jamii na watakuwa wanalijua hili , wanafanyaje kazi zao?
 
alafu kuna jamaa leo hii ameishaingiza mil 50 na ushee na analalamika maana alitegemea mil 100 nakuendelea, wewe massawe kuja usome hii ujifunze kitu, usijione mungu mtu.
Kila mtu anakula kulingana na kipato chake, maisha lazima yaendelee
 
Hbr za asubuhi. Kwa kuwa nimeona, nachukuwa wajibu wa kuwasiliana na mhusika Ili nijue iwapo kuna hatua za awali zilichukuliwa na kama bado zifanyike ikiwemo za ustawi wa jamii.

Ila baadae nitakuja na kipindi cha elimu kwa jamii kuhusu hatua za kuchukua kimfumo kwa wote wenye changamoto kupitia mamlaka ya Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa kupitia dhana ya ugatuaji madaraka ambapo, huduma zote zimesogezwa Karibu na wananchi kupitia ofisi za wakuu wa wilaya na wakurugenzi wa Halmashauri ambalo, kuna wataalamu wa wizara zote za kisekta wakihudumia wananchi.

Ahsante Sana. Ngoja tumtafute kwa msaada wa haraka, mengine yatafuata.

Shukrani.
 
Itakuwa vema kama utatupa mrejesho humu jambo liliponzia ili nasi tujue kilichoendelea.

Ahsante.
 
Umeongea ukweli mtupu ila sio kwa serikali yetu hii ambayo kila mtu anawamba usawa wake hamuwazii mwingine anachowaza ni yeye tu
 
Hii Dunia ukiwa na shida shida nayo ukiwa na raha rahaa nayo.
Hakuna jipya ishi kulingana na wakati.
 
Nilienda kuiona Hiyo familia na matatizo ya huyo Binti yamenifanya niwe nae karibu kiasi fulani. Na ninatoaga kidogo kilichopo ndani ya uwezo wangu hata kama Mboga basi maisha yanaenda.
Ubarikiwe mno kipenzi ...Mungu akuzidishie maradufu ya ulichotoa
 
Umeongea ukweli mtupu ila sio kwa serikali yetu hii ambayo kila mtu anawamba usawa wake hamuwazii mwingine anachowaza ni yeye tu
Wenye shida ni wengi shida ni taarifa wanaojitokeza wengi wamepata msaada kwa serikali na jamii pia.
Wapo waliopata matibabu,mitaji,
Ukificha shida atajua Nani sasa
 
Bila kuweka majina yao, maeneo wanayoishi na namba za simu bado itatafsiriwa kama hadithi kwa baadhi ya wasomaji
 
Ingependeza ukaweka hata namba yako ili michango ipitie kwako maana kuna baadhi ya wachangiaji humu wanaweza kutumia namba kupeleka application kwa huyo binti
 
Watu wengine hupitishwa ktk magumu ili wewe upate kumshukuru na kumuabudu Mungu
Yaani mtu apitie magumu ili wewe upate kumshukuru na kumuabudu Mungu? Kazi kweli kweli
 
TASAF mradi wa watu wabongo uwape pesa eti wazifikishe sehemu bila kuzichota thubutuu!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…