Binti (miaka 19) amepotea, naomba msaada kwa atakayemuona

Binti (miaka 19) amepotea, naomba msaada kwa atakayemuona

Pole sana mkuu, ILA hawa police ni piece of shit, why wasubirie 48hrs?,hii sheria ya wapi?nchi hii kweli ni pithole one,mtu akiwa potea, police wanatakiwa waanze muda huo huo kumtafuta, 48 hrs ameshavuka hizi porous borders zetu ndio maana jeshi la police nitalivunja na all above 40 yrs nitawapa marching order, leta vijana wapya wenye ari mpya
mkuu hizi case za teenagers kupotea asilimia kubwa huwa wanarudi wenyewe ndani ya huo muda,na mara nyingi huwa ni mapenzi.
 
Binti yangu wa kazi aliondoka kama hivi na baada ya siku nne akarudi akasema nilikuwa kwa nabii x (hili kanisa lipo dsm) akadai kuanzia sasa atahudumu kanisani.

Akabeba vilivyo vyake akaondoka ila tukamwambia hakufanya sawa na nikamwambia baada ya siku tatu afuate hela yake.

Baada ya siku tatu alikuja akiongozana na vijana wawili ambao alisema anasali nao.

Nimefupisha sana ila tumekaa nae miaka miwili.
 
Habari ndugu zangu.

Ninaomba msaada, binti huyu ninaambatanisha picha zake amepotea tangu tarehe 27/08/2023.

Binti huyu anaitwa Antia Focas, nyumbani walizoea kumuita Nyakato. Ana umri wa miaka 19. Mkazi wa Mkundi Morogoro, japo ana miezi mitatu tu tangu ahamie mkundi, mwanzoni tulikuwa tukiishi Kihonda-Maghorofani. Mimi ni baba yake mdogo, nimekuwa nikiishi naye kwa muda wa miaka mitatu sasa tangu nimtoe kwa wazazi wake.

Niligundua kuwa amepotea tarehe 27/08/2023 muda wa saa 7:30 (saba na nusu) mchana, hii ni kwa sababu alikuwa akimpeleka mtoto shule alafu anapitia kujifunza cherehani, ikifika saa sita na nusu anakwenda shule kumfata mtoto, wanarudi nyumba muda wa saa 7:30. Siku hiyo ilifika muda huo hajarudi, ilipofika saa nane na nusu tukapiga simu shuleni na kugundua kuwa hata mtoto alikuwa hajachukuliwa pale shuleni, shule inaitwa WESLEY.

Tulipopiga simu kwa mtu aliyekuwa akimfundisha cherehani, alisema kuwa alifika tu asubuhi, akaaga kuwa anakwenda saloon, kuosha nywele na kusuka. Tulipofatilia saloon, tukaambiwa kuwa hakufika. Tulitoa taarifa katika kitua cha polisi cha Kihonda, tukaambiwa turudi baada ya masaa 48 kama hajapatikana, tuliporudi tukapewa RB namba na kuambiwa tuendelee kumtafuta.

Bahati mbaya hadi leo hatujampta, alikuwa na simu lakini tangu apotee haipatikani. Pengine ni rahisi kufikiri kuwa labda katoroshwa na mwanaume, lakini mazingira aliyoondoka yatia shaka, kwani hakubeba kitu chochote. Hakubeba hata nguo moja wala mkoba. Naomba msaada wenu kwa atakayemuona.

Simu 0766729127/0688746145.

Asanteni.

View attachment 2735961View attachment 2735963View attachment 2735964View attachment 2735973
Hajatoroshwa na mwanaume, huyo ni mtu mzima kwaiyo ni katoroka na mwanaume. Hapo ni kuomba msaada kwenye kampuni za simu ili kujua watu aliokua anawasiliana nao mara kwa mara.
 
Amesema simu haipatikani, utatrakije simu ambayo haipo hewani?
Lengo la kutrack Huwa sio kujua tu kujua simu Iko eneo gan, simu ikiwa on kinachoongezekaga ni live location tu ila ikiwa imezimwa unaweza kujua alikuwa anazungunza na Nan? Mara ya mwsho kabla ya simu kuzimwa pamoja na kuona jumbe fupi za maneno aliyo tuma na kupokea
 
Habari ndugu zangu.

Ninaomba msaada, binti huyu ninaambatanisha picha zake amepotea tangu tarehe 27/08/2023.

Binti huyu anaitwa Antia Focas, nyumbani walizoea kumuita Nyakato. Ana umri wa miaka 19. Mkazi wa Mkundi Morogoro, japo ana miezi mitatu tu tangu ahamie mkundi, mwanzoni tulikuwa tukiishi Kihonda-Maghorofani. Mimi ni baba yake mdogo, nimekuwa nikiishi naye kwa muda wa miaka mitatu sasa tangu nimtoe kwa wazazi wake.

Niligundua kuwa amepotea tarehe 27/08/2023 muda wa saa 7:30 (saba na nusu) mchana, hii ni kwa sababu alikuwa akimpeleka mtoto shule alafu anapitia kujifunza cherehani, ikifika saa sita na nusu anakwenda shule kumfata mtoto, wanarudi nyumba muda wa saa 7:30. Siku hiyo ilifika muda huo hajarudi, ilipofika saa nane na nusu tukapiga simu shuleni na kugundua kuwa hata mtoto alikuwa hajachukuliwa pale shuleni, shule inaitwa WESLEY.

Tulipopiga simu kwa mtu aliyekuwa akimfundisha cherehani, alisema kuwa alifika tu asubuhi, akaaga kuwa anakwenda saloon, kuosha nywele na kusuka. Tulipofatilia saloon, tukaambiwa kuwa hakufika. Tulitoa taarifa katika kitua cha polisi cha Kihonda, tukaambiwa turudi baada ya masaa 48 kama hajapatikana, tuliporudi tukapewa RB namba na kuambiwa tuendelee kumtafuta.

Bahati mbaya hadi leo hatujampta, alikuwa na simu lakini tangu apotee haipatikani. Pengine ni rahisi kufikiri kuwa labda katoroshwa na mwanaume, lakini mazingira aliyoondoka yatia shaka, kwani hakubeba kitu chochote. Hakubeba hata nguo moja wala mkoba. Naomba msaada wenu kwa atakayemuona.

Simu 0766729127/0688746145.

Asanteni.

View attachment 2735961View attachment 2735963View attachment 2735964View attachment 2735973
Hawa watoto wetu watauwa wazazi kwa presha na sukari wakati mwenyewe kijibinua kwenye tendegu la kitanda. Mtu ametupa hela angalau awe na kaujuzi kwa kumfaa maishani yeye anakimbilia mtalimbo
 
mkuu ulikuwa unaishi nae vizuri kwaupendo kama mwanao wa kumzaa?? yani nikimuangalia huyoo binti namuona kama alikuwa anamanyanyaso anapata.

la msingi ni kuomba Mungu apatikane akiwa buheri wa afya.
 
Back
Top Bottom