Binti wa kishua, mwenye shahada toka Marekani amejiajiri kuuza makande, dada zetu maskini wanachagua kazi

Binti wa kishua, mwenye shahada toka Marekani amejiajiri kuuza makande, dada zetu maskini wanachagua kazi

Hivi kwanini watu mliofanikiwa kupata kitu fulani kwenye maisha huwa mnakosa akili na busara? Wengine tulienda shule ili tusiwe wauza karanga au wachoma mahindi,tungetaka kuchoma mahindi au kuuza karanga tungeishia kidato cha nne na kuanza kuuza karanga.....hizi kejeri mnamezeshwa na serikali yenu ya CCM kuwa vijana wajiajiri,mmeshindwa kuzalisha ajira na mmeshindwa kuwawezesha vijana kujiajiri kwa mali au hali,MSITAKE VIJANA TUONEKANE WAVIVU WAKATI TUMEWAKABIDHI HII NCHI ILI MTENGENEZE MWANGA WA MAISHA YA WATANZANIA....narudia tena HAKUNA ASIYEPENDA KUFANYA KAZI WA KULA BURE.
Hata mimi nilikua kama wewe.
Nilikua napenda kulalamika na kuwalaumu watu wengine.
Nilikua nasubiri nifanyiwe ili nije nipate mtaji.
Lakini akili ilipofunguka na kujua hii dunia inataka mtu mwenye akili nyingi, ndipo maisha yangu yalipo badirika.
Nikajua kuwa biashara sio mtaji ila ni wazo.
Wazo la biashara unalipata kulingana na hali yako.

Hakika nakuambia hata leo hii ukipewa mil 100, huwezi ifanyia kitu kama akili yako inadhani biashara ni mtaji
 
Angalia investiment aliyoiweka ndo utajua mtaji nishida.. kuuza makande sio shida lakini unayauza kwenye mazingira gani na kunapika kwenye mazingira yapi?.. Hapo awe mkweli amewekeza shingapi Kama kianzio ndio utajua mtaji ni ishu bablai..

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuuu mi sidhani hata akisema itakusaidia kitu kama umepanga kitu chako haijalishi unamtaji kiasi gani kama uko comited basi hata kwa mtaji wa laki1 utaweza kufanya tu ila ukisema uangalie nani kafanya kwa mtaji gani ndugu utachelewa sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hata mimi nilikua kama wewe.
Nilikua napenda kulalamika na kuwalaumu watu wengine.
Nilikua nasubiri nifanyiwe ili nije nipate mtaji.
Lakini akili ilipofunguka na kujua hii dunia inataka mtu mwenye akili nyingi, ndipo maisha yangu yalipo badirika.
Nikajua kuwa biashara sio mtaji ila ni wazo.
Wazo la biashara unalipata kulingana na hali yako.

Hakika nakuambia hata leo hii ukipewa mil 100, huwezi ifanyia kitu kama akili yako inadhani biashara ni mtaji
Nadhani unaongea vitu vya kwenye vitabu na madaftari,huzungumzii maisha halisi ya hapa Tanzania.
 
Hayo mandhari umeyaangalia lakini yana ghalimu mtaji bei gani au unaongea tu kwa sababu unakula kwa mama wewe dada?
makande yanahitaji mtaji kiasi gani?wabongo kwa visingizio

Sent from my TECNO WX3 using Tapatalk
 
Hongera kwa kujishughulisha lakini kama nchi inabidi kubadili mtazamo naona nchi hii tumeweka malengo chini sana kwa vijana....mtu akifanya kitu kidogo anasifiwa kana kwamba amefanya jambo kubwa wakati jamii ilipaswa iweke matarajio makubwa zaidi kwa vijana....ukiwa na ujuzi wa kupika hata kama darasa la saba ukafanya mama ntilie hupaswi kusifiwa hivyo kwasabu ni kile kinatarajiwa angalau ungeweza kufanya....

Lakini tofauti na majirani nchi hii kijana wa kawaida anatarajiwa kutofanya chochote...akifungua hata banda la juisi basi huyo amefanikiwa....kama taifa yatupasa kutamani makubwa na kuwaza makubwa
 
Hongera sana kwake!!! Na tunakoelekea..... Watajitokeza wengi tu.... Maisha yamekaza hayataki kuremba sasa hivi
Habari wadau...

Nimekutana na habari ya Nancy Lema wa Mwanza nikaona ku-share nanyi wadau mtoe maoni.. je binti yupo sahihi au wrong?

Kafanya Shahada yake St Marys University of Minnesota na masters university of Minnesota huko USA.

Baada ya kumaliza masomo yake akaamua kurudi nyumbani kujiajiri kwa kuuza makande kisasa na kwao ni mambo safi hasa hasa...

Nawaza tu why dada zetu maskini hawapendi kujishughulisha huku washua hawachagui kazi.

Nimemkumbuka na Mercy Kitomari Nelwa Gelato naye ana degree ya U.K ila amerudi Tanzania anauza ice cream tu kisasa



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huko ni kujipa matumaini tu kwa kiwango cha kipuuzi kabisa. Huko ni kwa mtu alieshindwa kutumia nafasi na fursa aliyoipata vizuri.Kama hachagui kazi huo msemo ilitakiwa aitumie akiwa marekani. Kule kuna kazi nyingi za kwenye mashoprite ya kupanga mabox tu,hata kama unasoma,una uwezo wa kutengeneza hela,tena hela sio hizi. Kule unalipwa kwa masaa. Nina mifano miiiiiingi isiyo idadi. Nina familia jirani,huyo mama ni mzee sasa ana watoto wa4,mkubwa yuko uingereza,ndie alianza kwenda kama kusoma,lakini akaanza na kazi hizo za kwenye mashoprite kupanga mabox,baadae alivyomaliza masomo akatafuta kazi huko huko. Kifupi kwenda kusoma ilikuwa gear tu. Baada ya kuseto akampigia pande mdogoake akaenda,akampa michongo mizima. Dogo baada ya muda pale UK,akasepa uswiswi,nae akamvuta dogo mwingine,huyo dogo wa 3 baada ya muda akasepa marekani,baada ya muda nae akamvuta wa 4. Wa 4 yuko Canada. Familia iko njema sana. Mama akiamua kuzunguka kote kwa wanae. Kazi walizoanza nazo ni hizo ambazo wazungu hawazitaki za kupanga mabox wanaziona ni za chini. Lakini zina mshahara wa kukufikisha ukawa milionea ukija huku kwetu. Hata ufanye ndani ya miaka 10 tu wewe ni bilionea ili mradi uwe na malengo,achana na statehe za kwao

Sent using Jamii Forums mobile app
Kama kuna ufara basi huu wako ni wa kiwango cha SGR. so tafsiri yako ya kuishi nje ni mafanikio. Braza kama hujawahi enda huko tulia. Hao wanaoishi nje ni Mungu wao na wao ndo wanajua.
Our mental liberation s pre-requisite to the future prospect

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimejifunza kitu kwa huyu dogo, kwanza kupika ni passion yake hicho ni kitu muhimu kabisa, pili amejua kusudi lake na analifanyia kazi kwa udanisi na furaha (Nanauka anasema tambua kusudi lako) tatu, anafanya biashara ya kuuza chakula na kunasiku maalumu anapika makande, nampa hongera kwa kujua kusudi lake, elimu alikua anapuyanga tu bora angesomea upishi mapema, lakini hajachelewa. So muandishi anasema eti kaamua kupika makande!?!??!?! Halafu tunaanza kulaumiana?!! Wasomi wa nchi hii wako confused kabisa! Jua kusudi lako basi. Sio kudanganyana msomi anapika makande na anatoboa, huyo anafanya biashara ya chakula na kuna siku ya makande, akijiongeza atapika na ugali was mtama. Hongera dogo kwa kujua kusudi lako. Sijapenda heading ya uzi imekaa kibiashara sana
Kwa kuongezea : tatizo nanba moja la watanzania ni kupoteza muda mwingi kusomea vitu visivyo kua na msaada kwenye maisha yao.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tatizo vijana wakishasoma ulaya wamebadilika kabisaa!!! nimewaona wengi wanafanya vibiashara vya ajabu ajabu ona sasa hata mwandiko wake umebadilika anaandika handwriting ya kizungu
 
Kama kuna ufara basi huu wako ni wa kiwango cha SGR. so tafsiri yako ya kuishi nje ni mafanikio. Braza kama hujawahi enda huko tulia. Hao wanaoishi nje ni Mungu wao na wao ndo wanajua.
Our mental liberation s pre-requisite to the future prospect

Sent using Jamii Forums mobile app
Ufara utakuwa unao wewe,kama umeenda kusoma ulaya halafu ukarudi mikono mitupu,wapo wengine wa aina yako,unaenda ulaya iwe kusoma au vyovyote halafu unaanza kufuata maisha ya wenyeji,ile starehe wanazofanya,na wewe unataka utimize tu kile ulichofuata bila kuangalia fursa zingine nyingi zilizopo kule. Wanaoshindwa kule ni ksbb tu kujifanya nao mabishoo,nao hawataki kazi za chini kama wenyeji japo zina kipato kizuri kuliko huku. Mimi nisingekuwa na maisha yangu ningeenda kule,nakuhakikishia 100% narudi na hela mbayaaa mkuu,sibahatishi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ufara utakuwa unao wewe,kama umeenda kusoma ulaya halafu ukarudi mikono mitupu,wapo wengine wa aina yako,unaenda ulaya iwe kusoma au vyovyote halafu unaanza kufuata maisha ya wenyeji,ile starehe wanazofanya,na wewe unataka utimize tu kile ulichofuata bila kuangalia fursa zingine nyingi zilizopo kule. Wanaoshindwa kule ni ksbb tu kujifanya nao mabishoo,nao hawataki kazi za chini kama wenyeji japo zina kipato kizuri kuliko huku. Mimi nisingekuwa na maisha yangu ningeenda kule,nakuhakikishia 100% narudi na hela mbayaaa mkuu,sibahatishi.

Sent using Jamii Forums mobile app
Then what next ukirudi na hela! Nakuona limbukeni fikra zako ni kuwa kwenda nje ni kuwa na maisha bora. Braza kuna watu wana make mpunga hapa hapa kwa magufuli na sio hizo za kwenda kuosha mbwa wa wazungu. Tuliza kichwa mtaalamu. Kuna mana gani kupata hela kwa kufanya kazi hata ambayo mwenyewe unaona inakushushia utu wako. Wengi wanasema wako nje ila nakuapia ni mahouseboy tu huko.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama kuna ufara basi huu wako ni wa kiwango cha SGR. so tafsiri yako ya kuishi nje ni mafanikio. Braza kama hujawahi enda huko tulia. Hao wanaoishi nje ni Mungu wao na wao ndo wanajua.
Our mental liberation s pre-requisite to the future prospect

Sent using Jamii Forums mobile app
Nina bro tumetoka kijiji kimoja ni afisa wa ubarozi nchi fulani za Scandinavia,yuko huko kikazi kuanzia kipindi cha mkapa. Wakati anaenda kule alikuwa na vijana wawili,halafu kule akaenda kuzaa mtoto mmoja,hao watoto sasa wana uraia wa huko,ni wakubwa sasa. Mafundisho yake kwa watoto ilikuwa ni namna ya kutumia fursa za kuwa kwao kule. Mpaka sasa hao watoto wana akaunti ya pamoja,lakini ina hela ya kutosha. Ksbb wote wakitoka masomoni wanapumzika then wanaingia kazini masaa mengine yasiyo ya masomo na siku zisizo za masomo. Ila kwa nyie mnaoenda mnaiga maisha ya kule badala ya kufikiria na kutumia fursa vizuri hiyo. Mnadharau

Sent using Jamii Forums mobile app
 
mnhhhhh hii ni prove tosha,wazazi wa change mind set zao,nina uhakika huyo binti angesema anaenda kusomea upishi wazazi wangekataa kumsomesha….

Anyway tusidanganyane,huyo binti amecheza na fursa ...ameangalia nini cha kufanya kwa wakati huu..hii haimpunguzii lolote,in the future anaweza kupata kazi inayoendana na kipato chake,cha muhimu ana degree yake under the belt....

Katika nchi yetu,swala la passion halipo,watu wanasoma kutoka na nafasi chache zilizopo katika soko la ajira,mambo ya passion/interests/talents halipo katika nchi yetu…
 
Back
Top Bottom