Bodaboda za CCM zenye "chata" ya Samia ziko mtaani

Bodaboda za CCM zenye "chata" ya Samia ziko mtaani

Kampeni kama Kampeni, baada ya kuona mabango nchi nzima hayana impact naona kahamia kwenye boda boda Sasa.

CCM wapo kwenye "Panic Mode" naona maji ya moto sana! Anyway mfadhili wa bodaboda anafahamika tu, yeye atalipwaje na atalipwa na nani Kwa "fadhila" hizo ndio swali la msingi Kwa Sasa.View attachment 2695863
Wananchi (wakiwemo wanaCCM) tumeshasema, boda boda yenye picha au chata ya mama Samia hatutaipanda au kuikodisha. Huu ni msimamo rasmi nchi nzima.
Yaani Samia awape bure waarabu bandari zetu zote halafu raia tumshobokee, hapana.
 
Hayati Benjamin Mkapa alisema uaminifu ni kitu Muhimu sana wakati anawaasa vijana.

Alisema, kwa ufafanuzi usio rasmi, kuwa kijana ukishakamtwa kwa kuiba ukiwa umeajiriwa, Hata ukitubu mara ngapi, mwajiri wako hatakaaakuamini Tena...! Unaweza kuendelea na ajira lakini hutaaminika Tena kwa 100%.

Kwa hiyo tulinde uaminifu tunapopata nafasi za kutoa huduma sehemu yoyote.

Zidumu fikra sahihi za kuliendeleza Taifa la Tanzania.
 
Mbinu ya huyu mama ni kushika boda boda, kushika timu za mipira, na kushika waarabu.
Ili kipindi cha kampeni atumie washabiki wa timu kumpatia huruma ya ushindi.

2. Kushika boda boda ili wamuonee huruma wakati wa kampeni.

3. Waarabu wamwagwe pesa..

Watanganyika kuweni makini na huyu mama, ndiye anayejua kilichompata Jiwe.
Huyu tokea mwanzo, aliporithi kiti hakuchelewa kuanza kampeni, ila sasa naona kama anajihisi kuwa amechelewa, ndiyo maana anahangaika sana.

Alianza na kundi la "WASANII"..., ikawa kama kundi hilo halimsaidii sana.

Kaingia kwenye timu za mpira, nako hana lolote la maana linaloonekana kumsaidia kwenye harakati zake

Kajaribu hadaa za kila namna, kuwafanya akina Mbowe kuwa "MAGAIDI", halafu na kujifanya yeye ndiye mwokozi wao..., hili nalo likafikia mwisho bila ya kumpa heshima yoyote baada ya kuonekana kuwa ni mwigizaji tu ambaye hakuwa na nia thabiti ya kuleta maelewano katika jamii.

Kafanya kila aliloweza, aonekane kuwa yeye ni tofauti na aliyemrithi kwenye kiti hicho, ili avute hisia za waliokuwa wakimsema vibaya Magufuli; huko nako, pamoja na kuwapata watu, lakini akawa anapoteza kundi lililokuwa nyuma ya Magufuli.
Ili kulipoza kundi hilo, na aonekane bado anaye Magufuli, kaigiza "Kazi na iendelee...". Kazi itaendelea vipi wakati unanajisi aliyokuwa akiyasimamia Magufuli?

Kazunguka kila sehemu, aonekane kwa waTanzania kuwa kiongozi mzuri. Lakini kwa bahati mbaya kwake, alipokubali tu kutekwa na kundi/genge la akina Roast..., hapo akawa hana njia tena ya kujifichia

Ni mtu asiyekata tamaa kirahisi, bado anadhani anayo matumaini ya kukoga nyoyo za waTanzania, ndiyo sababu unaona vitendo kama hivi vya mapikipiki, na hii ya juzi ya kuwaingiza watu wa mitandao ya kijamii mbele ya waandishi wa habari. Tegemeo lake sasa ni kuwa, hao 'influencers' watamsaidia kuwavuta waTanzania.
Niseme hapa, huko asiwe na tegemeo kabisa.

Njia ya mwisho ambayo inaanza kujipambanua, ni kutumia nguvu, kama ilivyozoeleka miaka yote kutoka kwa CCM.
Watalazimisha Bandari, na kama baada ya hivyo watakuwa bado wapo madarakani, nguvu zote watazielekeza kunajisi 2024 na 2025.

Hivi kweli Tanzania itabaki salama na mipango ya namna hii safari hii?
Mimi nasema. Hapana. Safari hii CCM watalipata wanalolitafuta siku nyingi.
 
Wananchi (wakiwemo wanaCCM) tumeshasema, boda boda yenye picha au chata ya mama Samia hatutaipanda au kuikodisha. Huu ni msimamo rasmi nchi nzima.
Yaani Samia awape bure waarabu bandari zetu zote halafu raia tumshobokee, hapana.
Hakika Kaka
 
Kajaribu hadaa za kila namna, kuwafanya akina Mbowe kuwa "MAGAIDI", halafu na kujifanya yeye ndiye mwokozi wao..., hili nalo likafikia mwisho bila ya kumpa heshima yoyote baada ya kuonekana kuwa ni mwigizaji tu ambaye hakuwa na nia thabiti ya kuleta maelewano katika jamii.
Jamani si mnasema urais ni Taasisi! Kwa hiyo Taasisi nzima inaonekana inaigiza kweli? Tuheshimu nafasi ya Urais.
 
Mbinu mfu ni misukule tu ndio watamfuata.
Mzimu wa magu unaonekana kila mahali vijijini kwa watu wa kawaida. Mijini pia upo kwenye mitaa choka.
Huu mkataba umekuja kama zimwi ukiunganisha washua na wale wa mzimu wa magu . Mzee, ni utata mtupu kuchomoa yatataka muujiza.
 
Mwarabu kamwaga pesa.

Tutaona na kusikia mengi mwaka huu

HUYU MAMA HAWEZI KUKOMESHA RUSHWA NA UFISADI NCHINI KWANI YEYE NDIO AMEKUWA KINARA WA UOVU HUO!! HAWAWEZI KURUDISHA FEDHA WALIZOHONGWA NA WAARABU ZINGINE NDIO WAMENUNULIA HIZO "TOYO" NDIO MAANA WANAZUNGUKA NCHI NZIMA KUTAFUTA KUHALALISHA HARAMU YAO!!
 
Jamani si mnasema urais ni Taasisi! Kwa hiyo Taasisi nzima inaonekana inaigoza kweli? Tuheshimu nafasi ya Urais.
Hiyo taasisi haina kiongozi wake?

Mkuu 'JITEGEMEE' vipi tena mbona ni kama unajishusha ngazi badala ya kupanda?

"Nafasi ya urais" itaheshimika, kama kiongozi wa taasisi hiyo anao uwezo wa kuiongoza na kufanya mambo ya kuiletea heshima taasisi yenyewe na kiongozi wa taasisi ya urais.

Hao watu walioko kwenye hiyo taasisi hawawezi kuamua na kufanya jambo ambalo kiongozi wa taasisi hiyo halitaki.
 
Ningejua elimu kiwango cha degree hakina thamani hapa Tanganyika nisingeangaika nalo ni ujinga wa kiwango cha lami najuta sana maishani mwangu
 
Back
Top Bottom