Bodi ya Mikopo Elimu ya Juu (HESLB) yaja na 'Kampeni ya Fichua' kuwasaka wadaiwa sugu

Bodi ya Mikopo Elimu ya Juu (HESLB) yaja na 'Kampeni ya Fichua' kuwasaka wadaiwa sugu

Yaani mtu uache shughuli zako na uanze kufuatilia fulani alisoma wapi na kama amelipa / hajalipa au alisomeshwa ?

Hii nchi ina mambo ya ajabu sana..., kama tungetumia muda huo kutengeneza sera za maana na rasilimali watu na mali tulizonazo tusingehitaji wala kutoa mikopo bali grants kwa kila mwenye uwezo (after all hawa watu ni nguvu kazi ndio maana sisi walipa kodi tumewasomesha)
 
Kama wanataka pesa ,waje wachukue cheti changu.... Ndio msaada pekee nitakaowasaidia. Kma wanaweza kukibadirisha hiki cheti kuwa pesa hata 100m zote wachuku ziwe zao.
 
yaani ajira wanagawana wao maofisini, wanawekana ndugu kwa ndugu, ukija kwenye miundombinu nayo utakuta wanatengeneza barabara moja ya lami inaenda kwa kiongozi mmoja inaishia hapo..alafu maeneo ya wananchi waliowengi unakuta barabara za vumbi tu hawana habari.
Unakuta viongozi ni wezi, waongo...wanatumia magari ya serikali, wengine wanaiba na mafuta wanayoweka kwenye magari hayo...bado wanatengenezewa barabara za lami hadi majumbani kwao...lakini uswahilini barabara hazipitiki ni vumbi na makorongo......uchaguzi unakuja wanakuja uswahilini wanakwangua barabara wanaacha mavumbi wanataka muwape kura...waje tena wawaibie pesa tena, waibe mafuta ya magari ya serikali, wajichongee barabara za lami hadi majumbani kwao, waendelee kuiba tena..


Wameituma bodi ya mikopo kwenda uswahilini ambako kumechoka, barabara zimechakaa, waende wakadai pesa kwa watu ambao hawataki kuwaajiri wanataka wajiajiri ili hata kidogo wanachopata wawe busy kulipa madeni....na wao waendelee kujineemesha. Jamani jamani!. naamini wangewasaidia wawe wanaajiriwa kwa haki na upendo wangekuwa wanalipa madeni yao wenyewe bila kukumbushwa wala kusukumwa. Wezi wameshindwa kudhibitiwa huko juu, wanalindana na kauli zao za kuwaruhusu wale kwa ulefu wa kamba zao, maana yake hata ajira wawe wanawekana kwa undugu tu hamna shida, taifa langu linaangamia.
Mikopo wanajitahidi wengi wapate ila ajira wanataka ndugu zao tu ndio waendelee kuwekwa humo, kulipa deni anatafutwa yule ambaye hawahitaji kumuajiri ndio awe kipaumbele cha kurejesha deni....sawa kuna siku tutafika wanapopataka...itakuwa too late!!.

wasomi wetu lipeni madeni ya bodi ili watu wasome, waibe, na wajipendelee katika maendeleo yao!!
 
Ianzishwe tozo waajiri na wafanya biashara wawe wanakatwa kwenye mapato yao kwa ajili ya elimu ya juu
Hii kwa lugha ya kitaalamu iitwe UNIV Education Support (UES) hapo vipi wadau
Mnufaika baada ya kuhitimu ana kuwa hadaiwi chochote 😁
 
Mimi nilikula mishahara miwili tu mizuri baada ya hapo bodi wakafanya yao da inaumiza ila tamaliza tu uzuri siku hazigandi.

Ila kuna mshikaji wangu tumeajiriwa mkoa mmojq wilaya tofauti.Bado hajaanza kukatwa sijui nimsanue aise.
 
Ianzishwe tozo waajiri na wafanya biashara wawe wanakatwa kwenye mapato yao kwa ajili ya elimu ya juu
Hii kwa lugha ya kitaalamu iitwe UNIV Education Support (UES) hapo vipi wadau
Mnufaika baada ya kuhitimu ana kuwa hadaiwi chochote 😁
botwana elimu bure nashanga hapo tz mgodi mmoja unaweza somesha wote lkn majambaz yameshika system
 
Katika Tangazo lao wanaweza "Je, unamfahamu mdaiwa wa HESLB mwenye kipato lakini ANAPIGA KIMYA?MFICHUE! Tutumie majina yake kamili, chuo alichosoma, kampuni au taasisi anayofanyia kazi:1. Barua pepe (email): fichua@heslb.go.tz;2. Ujumbe wa WhattsApp: 0739 66 55 33;3. Piga simu: 0736 66 55 33 (Saa 2:00 asubuhi – saa 11 jioni);4. Tembelea http://heslb.go.tz halafu bofya e-Mrejesho; na5. DM (Direct Messages) kwenda kwenda Instagram, X (zamani Twitter) au Facebook kwa jina la ‘HESLB Tanzania’ LILILOTHIBITISHWA na lenye ‘blue tick’.#FichuaKuwaHeroWaMadogo
 

Attachments

  • GRZcgRFacAAsWfo.jpeg
    GRZcgRFacAAsWfo.jpeg
    177 KB · Views: 6
Wanaongea kama mende zilizokunywa sumu
Wadaiwa wengi hawna ajira zinazoeleweka na vipato vyao ni duni sana sasa sijui wtapewa nini hao bodi ya mikopo
 
Back
Top Bottom