Hapa nae kaleta uswahili, ukiwa professional mambo kama haya hayatakiwi, mie nilikiwa namsapoti hili la kugoma kucheza na kiduku, lakini kwa haya maneno ya khanga, wapigane tuone huyu wa milioni 3 na yeye wa dola yupi bora.
Asichokijua mwakinyo au nadhani nae anajua ndio maana anamkwepa kiduku, yeye ile kushinda kule Uingereza ni zali la mtende na ndio kilichomuibua, hii ipo saana kwenye michezo tofauti hadi kwenye mziki kina J.I walibahatisha kidato kimoja kisha kimyaaa, ili uonekane bora inabidi uwe unagonga saana vitu vya maana, yeye mwakinyo kilichompa mpunga ni ile bahat ya Uingereza na ndio anatembea nayo, ila uwezo wake akikutana na kiduku yoyote anawezq poteza na hiki ndio anakikwepa akipigwa na kiduku basi kampa shavu kiduku nae ndio anaweza kuanza kuporomoka.
Katika ndondi kadri unavyofanya vizuri ndio mpunga unaingiza, alivymbahatisha yule mzungu ndio kaanza kula mpunga so anamuogopa kiduku anaweza akaanza kukosa mashavu ikitokea kachezea kipigo.