Bondia Mwakinyo hajui anachosimamia! Amegeuka Tena.

Bondia Mwakinyo hajui anachosimamia! Amegeuka Tena.

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Joined
Mar 24, 2018
Posts
28,297
Reaction score
68,017
Habari Wakuu!

Mwakinyoni mpiganaji mzuri lakini moja ya udhaifu wake ni majivuno ambayo hayana manaa yoyote kwenye kazi yake. Kwenye masumbwi yapo majivuno yenye maana katika ubondia lakini Kwa mwakinyo majivuno yake nayaona Kama hayana maana kwani hayamsaidii lolote.

Siku za nyuma Mwakinyo aliwahi kuponda mabondia wenzake akimlenga zaidi Twaha kiduku, Kwa kupigana kisa Gari Aina ya Crown, alisema yeye ni mpiganaji Mkubwa wakimataifa ambaye anapigana kupata mikanda na sio vizawadi mshenzi Kama vigari.
Alijitamba kuwa yeye anamagari mengi na mazuri hiyo hana uhitaji tena wa magari.


Nilimuelewa lakini kama ningeambiwa nimshauri ningemshauri vinginevyo!


Mwakinyo katoka Familia Masikini,
Mwakinyo yupo nchi Masikini!
Mwakinyo yupo kwenye Fani ambayo bado ipo chini na bado inaumasikini Mkubwa wa wafuasi.

Mwakinyo kujishaua na kukataa baadhi ya mapambano ndani ya nchi yake ni Dalili ya kuonyesha hayupo Sirius, na haijui nchi yake, na hajui vizuri watu wa nchi yake.

Hapa Tanzania Sanaa na mchezo wenye wafuasi wengi ni Muziki wa bongo Fleva, Hiphop kidogo na Muziki wa injili.
Mpira nao unawafuasi wengi hasa kwenye timu ya Simba, Yanga, na Azam.

Mchezo wa Masumbwi hauna wafuasi wengi hapa nchini kumaanisha bado sio biashara nzuri Kwa wawekezaji. Hilo lazima mwakinyo alijue.

Kama angekuwa analijua hilo asingejifanya kutaka dau kubwa lisiloendana na uhalisia wa Biashara ya mchezo wa Masumbwi hapa nchini.


Unataka milioni 100 wakati Pambano likiitishwa watu watakaoingia hawafikishi hiyo milioni Mia moja unategemea nini hapo.

Mwakinyo aache kujilinganisha na mabondia wa nchi za nje zilizojijenga katika mchezo huo.

Ni Sawa na Mchezaji wa mpira wa Tanzania achezaye Simba au Yanga stake kulipwa Sawa na mchezaji wa Mpira wa Mamelody ya Afrika Kusini. Hiyo ataonekana hamnazo!

Sasa Mwakinyo amegeuke tena! Anasema Mkanda ni zawadi tuu haumuongezee chochote, baada ya kunyang'anywa, anachotaka ni pesa. Inashangaza Sana.

Mwakinyo ninakushauri, jua umetoka familia Masikini, upo nchi Masikini, na upo kwenye mchezo wenye umasikini WA wafuasi.
Kiufupi wewe na wenzako bado mnajenga msingi wa mchezo wa masumbwi hivyo msitarajie makuuubwa Sana kama wenzenu wa BongoFleva!

Lazima muongeze wafuasi katika mchezo wenu huo ili ifikie hatua Pambano likitangazwa basi uwanja wa taifa unajaa au nusu ya uwanja kukaa!

Embu jiulize Mwakinyo, hivi Pambano lako likitangazwa unauwezo wa kujaza uwanja wa taifa au nusu yake?
Au hata vile viwanja vya mpira vya jamhuri Kama Morogoro, CCM kirumba ya Mwanza, au Sokoine ya Mbeya?

Jina linaweza kuwa kubwa lakini lisiwe biashara yenye faida kubwa!

Mfano, Sanaa ya stand comedy ndio Kwanza ni changa, inavijana wadogo Masikini, kwenye nchi Masikini, yenye umasikini WA wafuasi bao ndio wateja.
Kijana Kama Coy Mzungu ajifanye anataka malipo makubwa ilhali hana wafuasi wengi wanaoweza kutoa pesa kupata Huduma yake.
Ndio maana Coy yeye anapambana kuhakikisha anajenga msingi na kuimarisha wapenzi wa Sanaa hiyo.

Mwakinyo anawadharau Vijana wenzake wanaopigana mapambano mpaka ya Mbuzi asijue wenzake ndio wanajenga msingi wa mchezo wao ndani ya nchi.

Hawawezi kujidanganya kuwa wao ni Masikini Kama ulivyo wewe, wengi wenu elimu zenu ni duni katika nchi Masikini, mchezo wenu bado haujakubalika kivile ndani ya jamii hivyo ni jukumu Lenu kuifanya jamii iukubali. Na sio kulilia maslahi!

Mwisho, Mwakinyo unapaswa ujifunze pia Mazingira zaidi ya mchezo wenu, wafuasi wako, sio uishie kujifunza Kucheza Ringi pekeake!

Kuwa kama Diamond, hajaishia kujikita kwenye kuimba tuu studio na Jukwaani Bali amejifunza Mazingira ya nchi yetu, watu wake wakoje na wanapenda nini hasa Vijana, ambao ndio wateja wake.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Dar es salaam
 
Sema Sasa mtu unayemshauri sijui kama anaweza kufika hili jukwaa na sijui kama anauwezo wakusoma aya zote ulizoandika akaelewa naimani akisoma Aya ya kwanza akifika Aya ya tatu anasahau juu uliandika nini kwaiyo msamehe

Tupeleke watoto shule wapate uelewa japo kipaji kipo, tunaona vijana wanaobahatika kupata umarufu bila kuwa na elimu wanavyokengeuka na umarufu at the end maneno yao yanawacost wanarudi walipotoka
 
Umemshauri vizuri ngoja niu copy huu uzi nimtumie mdogo wake akampe kaka yake akajifunze kitu

Yaani kuna watu wanashangaza mno!

Kwa bongo Bondia kupewa Crown ni zawadi kubwa mno.
Crown bei yake ikiwa mpya zinaanzia 12m kulingana na mwaka.

Na hiyo ni usiku mmoja tuu!

Mabondia wengi hupewa posho tuu! Wengine milioni 2, wengine laki tano, wengine laki 2 basi ilimradi.

Mchezo bado upo chini alafu unataka maslahi makuubwa Kama mtu usiyeelewa biashara. Usiyeelewa nchi yako ipoje bhana
 
huyu jamaa ana maneno maneno ya kiswahili mixer mipasho, sijui ninkwa sababu ni Mtanga

Ashauriwe!

Aambiwe nchi yetu ni masikini,
Asijilinganishe na mabondia wa nchi zingine ambao mapambano Yao unakuta uwanja na Ukumbi uko Full hata pakutemea mate hakuna.

Watu wanatoa pesa ya kutosha.

Hapa bongo mtu kununua tuu ticket ya elfu 10 akaangalie masumbwi ni kipengele.

Kwanza mchezo wenyewe wengi hawaupendi wala kuufuatilia

Mpira kidogo tena ni Simba na Yanga.

Tiki zingine zinalia Kwa uhaba wa mashabiki, wapo marafiki zangu wanalipwa viposho vya laki mbili mpaka elfu 50 katika timu hizi hizi unazozijua
 
Yaani kuna watu wanashangaza mno!

Kwa bongo Bondia kupewa Crown ni zawadi ku apigane kwa crown mtu anashika 3 africabwa mno.
Crown bei yake ikiwa mpya zinaanzia 12m kulingana na mwaka.

Na hiyo ni usiku mmoja tuu!

Mabondia wengi hupewa posho tuu! Wengine milioni 2, wengine laki tano, wengine laki 2 basi ilimradi.

Mchezo bado upo chini alafu unataka maslahi makuubwa Kama mtu usiyeelewa biashara. Usiyeelewa nchi yako ipoje bhana
ulitaka apiganie crown? Hao wanaopigania crown mazuzu
 
Habari Wakuu!

Mwakinyoni mpiganaji mzuri lakini moja ya udhaifu wake ni majivuno ambayo hayana manaa yoyote kwenye kazi yake. Kwenye masumbwi yapo majivuno yenye maana katika ubondia lakini Kwa mwakinyo majivuno yake nayaona Kama hayana maana kwani hayamsaidii lolote.

Siku za nyuma Mwakinyo aliwahi kuponda mabondia wenzake akimlenga zaidi Twaha kiduku, Kwa kupigana kisa Gari Aina ya Crown, alisema yeye ni mpiganaji Mkubwa wakimataifa ambaye anapigana kupata mikanda na sio vizawadi mshenzi Kama vigari.
Alijitamba kuwa yeye anamagari mengi na mazuri hiyo hana uhitaji tena wa magari.


Nilimuelewa lakini kama ningeambiwa nimshauri ningemshauri vinginevyo!


Mwakinyo katoka Familia Masikini,
Mwakinyo yupo nchi Masikini!
Mwakinyo yupo kwenye Fani ambayo bado ipo chini na bado inaumasikini Mkubwa wa wafuasi.

Mwakinyo kujishaua na kukataa baadhi ya mapambano ndani ya nchi yake ni Dalili ya kuonyesha hayupo Sirius, na haijui nchi yake, na hajui vizuri watu wa nchi yake.

Hapa Tanzania Sanaa na mchezo wenye wafuasi wengi ni Muziki wa bongo Fleva, Hiphop kidogo na Muziki wa injili.
Mpira nao unawafuasi wengi hasa kwenye timu ya Simba, Yanga, na Azam.

Mchezo wa Masumbwi hauna wafuasi wengi hapa nchini kumaanisha bado sio biashara nzuri Kwa wawekezaji. Hilo lazima mwakinyo alijue.

Kama angekuwa analijua hilo asingejifanya kutaka dau kubwa lisiloendana na uhalisia wa Biashara ya mchezo wa Masumbwi hapa nchini.


Unataka milioni 100 wakati Pambano likiitishwa watu watakaoingia hawafikishi hiyo milioni Mia moja unategemea nini hapo.

Mwakinyo aache kujilinganisha na mabondia wa nchi za nje zilizojijenga katika mchezo huo.

Ni Sawa na Mchezaji wa mpira wa Tanzania achezaye Simba au Yanga stake kulipwa Sawa na mchezaji wa Mpira wa Mamelody ya Afrika Kusini. Hiyo ataonekana hamnazo!

Sasa Mwakinyo amegeuke tena! Anasema Mkanda ni zawadi tuu haumuongezee chochote, baada ya kunyang'anywa, anachotaka ni pesa. Inashangaza Sana.

Mwakinyo ninakushauri, jua umetoka familia Masikini, upo nchi Masikini, na upo kwenye mchezo wenye umasikini WA wafuasi.
Kiufupi wewe na wenzako bado mnajenga msingi wa mchezo wa masumbwi hivyo msitarajie makuuubwa Sana kama wenzenu wa BongoFleva!

Lazima muongeze wafuasi katika mchezo wenu huo ili ifikie hatua Pambano likitangazwa basi uwanja wa taifa unajaa au nusu ya uwanja kukaa!

Embu jiulize Mwakinyo, hivi Pambano lako likitangazwa unauwezo wa kujaza uwanja wa taifa au nusu yake?
Au hata vile viwanja vya mpira vya jamhuri Kama Morogoro, CCM kirumba ya Mwanza, au Sokoine ya Mbeya?

Jina linaweza kuwa kubwa lakini lisiwe biashara yenye faida kubwa!

Mfano, Sanaa ya stand comedy ndio Kwanza ni changa, inavijana wadogo Masikini, kwenye nchi Masikini, yenye umasikini WA wafuasi bao ndio wateja.
Kijana Kama Coy Mzungu ajifanye anataka malipo makubwa ilhali hana wafuasi wengi wanaoweza kutoa pesa kupata Huduma yake.
Ndio maana Coy yeye anapambana kuhakikisha anajenga msingi na kuimarisha wapenzi wa Sanaa hiyo.

Mwakinyo anawadharau Vijana wenzake wanaopigana mapambano mpaka ya Mbuzi asijue wenzake ndio wanajenga msingi wa mchezo wao ndani ya nchi.

Hawawezi kujidanganya kuwa wao ni Masikini Kama ulivyo wewe, wengi wenu elimu zenu ni duni katika nchi Masikini, mchezo wenu bado haujakubalika kivile ndani ya jamii hivyo ni jukumu Lenu kuifanya jamii iukubali. Na sio kulilia maslahi!

Mwisho, Mwakinyo unapaswa ujifunze pia Mazingira zaidi ya mchezo wenu, wafuasi wako, sio uishie kujifunza Kucheza Ringi pekeake!

Kuwa kama Diamond, hajaishia kujikita kwenye kuimba tuu studio na Jukwaani Bali amejifunza Mazingira ya nchi yetu, watu wake wakoje na wanapenda nini hasa Vijana, ambao ndio wateja wake.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Dar es salaam
Mwakinyo aliamka tu asubuhi akaanza kudharau mikanda na hela ndogo? Au kuna kitu alifanywa mpaka akaongea yote hayo.?? Nyie watu mnao ona makosa ya watu jaribuni kuangalia chanzo cha hayo mambo pia. Unajua afande sele alichosema kuhusu mwakinyo na watu wa tanga kwa ujumla baada ya pambano la twaha kiduku ???? Au unaropoka tu kutoa ushauri kwa mwakinyo bila kujua chanzo....? ???? Hizi ni mbinu chafu za vijana wenye bundle kujifanya wajuvi wa mambo ya watu bila kuangalia source na baadae kutoa huku bila kubalance stories......

Pua ......pua.....pua.....pua........
 
mnamchokoza akiwajibu ndio mnasema anadharau hebu acheni uzwazwa,kwa hadhi yake apigane na nani tanzania ni sawa umpambanishe diomond na harmonize

Hadhi yake ni ipi?

Hata Diamond Na Hamornize kwenye muziki wanapambanishwa mbona,

Hivi Kwa akili yako unafikiri Kwa hapa Tanzania hadhi ya Mwakinyo anapaswa alipwe kiasi gani kila akisimama kwenye Pambano?,
 
Habari Wakuu!

Mwakinyoni mpiganaji mzuri lakini moja ya udhaifu wake ni majivuno ambayo hayana manaa yoyote kwenye kazi yake. Kwenye masumbwi yapo majivuno yenye maana katika ubondia lakini Kwa mwakinyo majivuno yake nayaona Kama hayana maana kwani hayamsaidii lolote.

Siku za nyuma Mwakinyo aliwahi kuponda mabondia wenzake akimlenga zaidi Twaha kiduku, Kwa kupigana kisa Gari Aina ya Crown, alisema yeye ni mpiganaji Mkubwa wakimataifa ambaye anapigana kupata mikanda na sio vizawadi mshenzi Kama vigari.
Alijitamba kuwa yeye anamagari mengi na mazuri hiyo hana uhitaji tena wa magari.


Nilimuelewa lakini kama ningeambiwa nimshauri ningemshauri vinginevyo!


Mwakinyo katoka Familia Masikini,
Mwakinyo yupo nchi Masikini!
Mwakinyo yupo kwenye Fani ambayo bado ipo chini na bado inaumasikini Mkubwa wa wafuasi.

Mwakinyo kujishaua na kukataa baadhi ya mapambano ndani ya nchi yake ni Dalili ya kuonyesha hayupo Sirius, na haijui nchi yake, na hajui vizuri watu wa nchi yake.

Hapa Tanzania Sanaa na mchezo wenye wafuasi wengi ni Muziki wa bongo Fleva, Hiphop kidogo na Muziki wa injili.
Mpira nao unawafuasi wengi hasa kwenye timu ya Simba, Yanga, na Azam.

Mchezo wa Masumbwi hauna wafuasi wengi hapa nchini kumaanisha bado sio biashara nzuri Kwa wawekezaji. Hilo lazima mwakinyo alijue.

Kama angekuwa analijua hilo asingejifanya kutaka dau kubwa lisiloendana na uhalisia wa Biashara ya mchezo wa Masumbwi hapa nchini.


Unataka milioni 100 wakati Pambano likiitishwa watu watakaoingia hawafikishi hiyo milioni Mia moja unategemea nini hapo.

Mwakinyo aache kujilinganisha na mabondia wa nchi za nje zilizojijenga katika mchezo huo.

Ni Sawa na Mchezaji wa mpira wa Tanzania achezaye Simba au Yanga stake kulipwa Sawa na mchezaji wa Mpira wa Mamelody ya Afrika Kusini. Hiyo ataonekana hamnazo!

Sasa Mwakinyo amegeuke tena! Anasema Mkanda ni zawadi tuu haumuongezee chochote, baada ya kunyang'anywa, anachotaka ni pesa. Inashangaza Sana.

Mwakinyo ninakushauri, jua umetoka familia Masikini, upo nchi Masikini, na upo kwenye mchezo wenye umasikini WA wafuasi.
Kiufupi wewe na wenzako bado mnajenga msingi wa mchezo wa masumbwi hivyo msitarajie makuuubwa Sana kama wenzenu wa BongoFleva!

Lazima muongeze wafuasi katika mchezo wenu huo ili ifikie hatua Pambano likitangazwa basi uwanja wa taifa unajaa au nusu ya uwanja kukaa!

Embu jiulize Mwakinyo, hivi Pambano lako likitangazwa unauwezo wa kujaza uwanja wa taifa au nusu yake?
Au hata vile viwanja vya mpira vya jamhuri Kama Morogoro, CCM kirumba ya Mwanza, au Sokoine ya Mbeya?

Jina linaweza kuwa kubwa lakini lisiwe biashara yenye faida kubwa!

Mfano, Sanaa ya stand comedy ndio Kwanza ni changa, inavijana wadogo Masikini, kwenye nchi Masikini, yenye umasikini WA wafuasi bao ndio wateja.
Kijana Kama Coy Mzungu ajifanye anataka malipo makubwa ilhali hana wafuasi wengi wanaoweza kutoa pesa kupata Huduma yake.
Ndio maana Coy yeye anapambana kuhakikisha anajenga msingi na kuimarisha wapenzi wa Sanaa hiyo.

Mwakinyo anawadharau Vijana wenzake wanaopigana mapambano mpaka ya Mbuzi asijue wenzake ndio wanajenga msingi wa mchezo wao ndani ya nchi.

Hawawezi kujidanganya kuwa wao ni Masikini Kama ulivyo wewe, wengi wenu elimu zenu ni duni katika nchi Masikini, mchezo wenu bado haujakubalika kivile ndani ya jamii hivyo ni jukumu Lenu kuifanya jamii iukubali. Na sio kulilia maslahi!

Mwisho, Mwakinyo unapaswa ujifunze pia Mazingira zaidi ya mchezo wenu, wafuasi wako, sio uishie kujifunza Kucheza Ringi pekeake!

Kuwa kama Diamond, hajaishia kujikita kwenye kuimba tuu studio na Jukwaani Bali amejifunza Mazingira ya nchi yetu, watu wake wakoje na wanapenda nini hasa Vijana, ambao ndio wateja wake.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Dar es salaam
Dear friend of mine TAIKON, that is what we call poor thinking capacity of Mwakinyo, kama ana akili atakuwa amekuelewa.
 
mnamchokoza akiwajibu ndio mnasema anadharau hebu acheni uzwazwa,kwa hadhi yake apigane na nani tanzania ni sawa umpambanishe diomond na harmonize
Watu sijui wakoje!
Basi apigane na afande Sele au Ndugai!
 
Hadhi yake ni ipi?

Hata Diamond Na Hamornize kwenye muziki wanapambanishwa mbona,

Hivi Kwa akili yako unafikiri Kwa hapa Tanzania hadhi ya Mwakinyo anapaswa alipwe kiasi gani kila akisimama kwenye Pambano?,
Milion 100
 
Ila wabongo kama wana ka wivu hivi kwa Mwakinyo!

Sio wivu!
Anaambiwa ukweli ajirekebishe!
Sasa Taikon atamuonea wivu Mwakinyo Kwa kipi? Hatupo Carrier moja, hatuna ushindani wowote wa kibiashara au kimaslahi.

Ni Kama baadhi ya wanasiasa ambao tulikuwa tunawashauri tunaonekana tunawaonea wivu!

Ingawaje sikatai wapo wanaomuonea wivu Kwa kuleta ushabiki na u-team
 
Go champ mwakinyo.....
Uzuri aliweka wazi hakuna aliyemjua, njia alizopita mpaka anaenda kumpiga Sam pale kwa malkia.
Kwa hiyo wasimpangie, na hataki unafki wetu wabongo...
Wanafki ni hawa hapa wameanza kujitokeza.
Yeye kajipa Value yake, anajijua na anaujua mchezo wa ngumi.
Ni sehemu ya kurisk maisha pia, sio mchezo kama bao kwamba ni burudani tu.
Anacheza mchezo ambao mwili wake ( zingatia hili mwili wake) utakuwa subjected to maumivu na pengine more than maumivu, unaweza kufa pia.

Asa kwanini tunamlazimisha mtu apitie hayo kwa vipimo vyetu sisi, kwamba kwake kupitia hayo ni sawa kwa tsh million 40.
Aliwadunda watu akachukua mikanda ( Huu ni uwezo) ameporwa mkanda sababu hawezi pigana kwa chini ya million 90 ( Anajipa thamani). Kwa kukubali kuachia mkanda hakuna promota atamfuata mwakinyo na hela mbuzi tena.
Huwezi ukaendelea kumuita maskini mtu ambaye anapata ofa za million 40 na anazipiga chini.
Mwacheni mwakinyo aamue anavyoona msimpangie, ni career yake na ana mashabiki wake.
Hongera Champez....
 
Watu sijui wakoje!
Basi apigane na afande Sele au Ndugai!
Halafu huwezi kumlazimisha mtu afanye wanchotaka wao,mabondia wakibongo wanawivu na hatua aliyofikia mwakinyo ndio mana wamemuandama muda wote badala ya kutafuta njia namna gani nchi ifike mbali kwenye mchezo wa ngumi wao,wanamkebehi dogo wa watu akiwajibu wanamchukia
 
Milion 100

Unaona ulivyo vurugwa.

Wewe Kwa akili yako ndogo tuu! Wanaingia pale kwenye kutazama hii michezo ya masumbwi wanafikisha hiyo pesa, hata wanaodhamini matangazo wakati onyesho linaendelea unafikiri ndio itamfanya yeye apewe hizo 100m?

Tatizo Lenu mnadhani bongo ni Ulaya!

Hata nikikuuliza wewe ulishawahi kuingia na kulipia ticket uangalie hayo masumbwi si ajabu hujawahi na huna mpango!

Mchezo wa masumbwi upo chini Sana Kwa wafuasi, sanasana wakilipwa pesa kubwa ni milioni 15
 
Mwakinyo ndiye bondia wa kwanza kujaza uwanja wa taifa kwa mkapa, kujaza pale masaki kwa kiingilio laki moja na kuitwa ikulu na Maghufuri na kupewa uwanja kigamboni,hapo lazima waluguru wa morogoro waone wivu sana
 
Back
Top Bottom