Zanzibar-ASP
JF-Expert Member
- Nov 28, 2013
- 11,550
- 40,697
Tanzania tupo kwenye mjadala mzito unaohusu bandari na waarabu wa Dubai (DP world), na kiini cha mjadala wote ni kuhusu dosari za kimsingi zinazounguka mkataba wenye.
Jambo moja la wazi linalokubalika na pande zote katika mjadala huu ni kuwa, sote (serikali na wakosoaji) tunakubali kuwa mkataba una dosari za msingi zenye kuhitaji marekebisho kabla ya kwenda hatua yoyote nyingine mbele.
Nikiwa kama mtanzania, mwenye kuipenda nchi yangu na kuwapenda watanzania wenzangu wote, ninatoa pendekezo hili.
Serikali itangaze mara moja kusitisha mkataba wote(makubaliano yote) ili kuanza upya mchakato mzima utaoweza kuzingatia ushauri, maoni na mapendekezo kutoka kwa wadau mbalimbali.
Tuwe wakweli, mjadala kuhusu huu mkataba umetugawa vibaya watanzania, una hatarisha amani yetu, unamchafua rais wetu mpendwa wa Tanzania mama Samia Suluhu, unatupotezea muda sana, unatumia pesa nyingi kujaribu kuutetea au kuukosoa na hautoi taswira njema huko tuendako.
Mkataa pema pabaya panamwita...
Mficha maradhi mauti yatamuumbua....
Heri nusu shari kuliko shari kamili...
Dalili ya mvua ni mawingu...
Samaki mkunje angali mbichi...
Jambo moja la wazi linalokubalika na pande zote katika mjadala huu ni kuwa, sote (serikali na wakosoaji) tunakubali kuwa mkataba una dosari za msingi zenye kuhitaji marekebisho kabla ya kwenda hatua yoyote nyingine mbele.
Nikiwa kama mtanzania, mwenye kuipenda nchi yangu na kuwapenda watanzania wenzangu wote, ninatoa pendekezo hili.
Serikali itangaze mara moja kusitisha mkataba wote(makubaliano yote) ili kuanza upya mchakato mzima utaoweza kuzingatia ushauri, maoni na mapendekezo kutoka kwa wadau mbalimbali.
Tuwe wakweli, mjadala kuhusu huu mkataba umetugawa vibaya watanzania, una hatarisha amani yetu, unamchafua rais wetu mpendwa wa Tanzania mama Samia Suluhu, unatupotezea muda sana, unatumia pesa nyingi kujaribu kuutetea au kuukosoa na hautoi taswira njema huko tuendako.
Mkataa pema pabaya panamwita...
Mficha maradhi mauti yatamuumbua....
Heri nusu shari kuliko shari kamili...
Dalili ya mvua ni mawingu...
Samaki mkunje angali mbichi...