Bora kuufuta kwanza mkataba wote wa bandari na DP World kuliko kujaribu kurekebisha chochote ili ufae

Bora kuufuta kwanza mkataba wote wa bandari na DP World kuliko kujaribu kurekebisha chochote ili ufae

Mkataba wa DPW unaipeleka nchi katika utumwa kwa taarifa yako! Ebu nikupe dondoo za mkataba wenyewe kama ulikuwa ufahamu: unahusisha bandari zoote za bahari, maziwa na mito; unahusisha na ardhi zilipo hizo bandari; unahusisha njia za usafirishaji wa mizigo kutoka na kuingia bandari hizo ikiwa na maana SGR, barabara, Meli, na viwanja vya ndege (all transit corridors); inaitaka serikali ihakikishe usalama wa DPW katika nyanja zoote kisiasa, kiulinzi, na kiuchumi bila kumuingilia. Serikali haitakiwi kuhoji uendeshwaji na mapato ya DPW bila ridhaa ya DPW, nk,nk.

Kwa hali hii kama serikali bado haijaufuta na kuuondoa huo mkataba, baasi! Tanganyika ni koloni la DPW! Cha kushangaza DPW sio nchi! Yaani, DPW ni kifupi cha Dubai Port World! Chakushangaza, serikali (Rais, mkuu wa nchi) anaingia Mikataba ya kuuza nchi kwa taasisi (DPW) ambaye mkuu wake sio Rais! Ndo maana tunapigwa na butwaa inakuwaje Rais wa nchi kubwa yenye wasomi na wanasheria wanaenda kuingia mkataba wa kuuza nchi kwa taasisi (sijui kampuni)???
Kwa kifupi maneno ya ndungai yametimia.
 
Tanzania tupo kwenye mjadala mzito unaohusu bandari na waarabu wa Dubai (DP world), na kiini cha mjadala wote ni kuhusu dosari za kimsingi zinazounguka mkataba wenye.

Jambo moja la wazi linalokubalika na pande zote katika mjadala huu ni kuwa, sote (serikali na wakosoaji) tunakubali kuwa mkataba una dosari za msingi zenye kuhitaji marekebisho kabla ya kwenda hatua yoyote nyingine mbele.

Nikiwa kama mtanzania, mwenye kuipenda nchi yangu na kuwapenda watanzania wenzangu wote, ninatoa pendekezo hili.

Serikali itangaze mara moja kusitisha mkataba wote(makubaliano yote) ili kuanza upya mchakato mzima utaoweza kuzingatia ushauri, maoni na mapendekezo kutoka kwa wadau mbalimbali.

Tuwe wakweli, mjadala kuhusu huu mkataba umetugawa vibaya watanzania, una hatarisha amani yetu, unamchafua rais wetu mpendwa wa Tanzania mama Samia Suluhu, unatupotezea muda sana, unatumia pesa nyingi kujaribu kuutetea au kuukosoa na hautoi taswira njema huko tuendako.


Mkataa pema pabaya panamwita...
Mficha maradhi mauti yatamuumbua....
Heri nusu shari kuliko shari kamili...
Dalili ya mvua ni mawingu...
Samaki mkunje angali mbichi...
Kwani aliyetoa saini hakusoma mkataba????
 
Tanzania tupo kwenye mjadala mzito unaohusu bandari na waarabu wa Dubai (DP world), na kiini cha mjadala wote ni kuhusu dosari za kimsingi zinazounguka mkataba wenye.

Jambo moja la wazi linalokubalika na pande zote katika mjadala huu ni kuwa, sote (serikali na wakosoaji) tunakubali kuwa mkataba una dosari za msingi zenye kuhitaji marekebisho kabla ya kwenda hatua yoyote nyingine mbele.

Nikiwa kama mtanzania, mwenye kuipenda nchi yangu na kuwapenda watanzania wenzangu wote, ninatoa pendekezo hili.

Serikali itangaze mara moja kusitisha mkataba wote(makubaliano yote) ili kuanza upya mchakato mzima utaoweza kuzingatia ushauri, maoni na mapendekezo kutoka kwa wadau mbalimbali.

Tuwe wakweli, mjadala kuhusu huu mkataba umetugawa vibaya watanzania, una hatarisha amani yetu, unamchafua rais wetu mpendwa wa Tanzania mama Samia Suluhu, unatupotezea muda sana, unatumia pesa nyingi kujaribu kuutetea au kuukosoa na hautoi taswira njema huko tuendako.


Mkataa pema pabaya panamwita...
Mficha maradhi mauti yatamuumbua....
Heri nusu shari kuliko shari kamili...
Dalili ya mvua ni mawingu...
Samaki mkunje angali mbichi...
Ufutwe tu
 
Ule mkataba haufai, na bahati mbaya hata kama wakitaka kuuvunja mwarabu hawezi kukubali tena, zile terms za kinyonyaji zinazomfaidisha vile hawezi kuziachia kirahisi.

Mimi nasema potelea mbali, kama kukosea wameshakosea, afadhali kuwa tayari kulipa fidia ili kulinda heshima yetu, na uhuru wa mipaka yetu, kuliko kuiogopa fidia huku tukuendelea kuwa watumwa ndani ya nchi yetu.
Hakuna fidia yoyote, mkataba uliosainiwa ulikuwa kati ya nchi na nchi wala sio DPW mikataba ya dpw ndio hiyo wanaita HGA, hizo HGA bado kusainiwa labda tu kama wanatuzuga tu kumbe walishamaliza kila kitu, kwahiyo tukijichomoa sasaivi hakuna wakushitaki mwenzio.
 
Hakuna fidia yoyote, mkataba uliosainiwa ulikuwa kati ya nchi na nchi wala sio DPW mikataba ya dpw ndio hiyo wanaita HGA, hizo HGA bado kusainiwa labda tu kama wanatuzuga tu kumbe walishamaliza kila kitu, kwahiyo tukijichomoa sasaivi hakuna wakushitaki mwenzio.
Mkuu usitegemee jambo la maana kwa serikali hii.

Tuhesabu maumivu tu.
 
Uko sahihi kwani maccm yanaweka uchama mbele ili waendelee kutawala badala ya kutanguliza Utaifa kwanza. Bunge hili linakiuka ibara ya 63 (2) ya Katiba ya JMT inayosema :'Sehemu ya pili ya Bunge itakuwa ndicho chombo kikuu cha Jamhuri ya Muungano ambacho kitakuwa na madaraka,kwa niaba ya wananchi, kuisimamia na kuishauri Serikali ya Jamhuri ya Muungano na vyombo vyake vyote katika utekelezaji wa majukumu yake kwa mujibu wa Katiba hii.'

Katika sakata hili tunaona wazi kuwa serikali ndiyo inaliagiza bunge nini cha kufanya. Wabunge wamepelekwa Dubai ili kuandaliwa kuja kupitisha mkataba(wenyewe wanaita makubaliano) wa kimangungo ambao serikali ilishaingia na DP World kitambo sana,kifupi Bunge limetumika kama muhuri tu wa serikali hii. Huu ni uvunjajaji mkubwa wa Katiba yetu hivyo hakuna sababu tena ya kuwaamini watu wanaovunja Katiba ya nchi ili kukidhi njaa ya matumbo yao na matamanio yao ya kuona chama chao kinabaki madarakani milele. Tumeona hata jinsi Spika alivyoendesha kikao kile kishabiki kabisa kama mshabiki oya oya wa Simba au Yanga ambaye yuko tayari kujivua utu wake ili tu kushangilia timu yake hata kama inaboronga.
Hivi Rais akivunja katiba, huwajibishwaje?

Na vyombo vingine kwa mfano Mkuu wa majeshi (Cdf) na Mwanasheria mkuu wa Serikali, pamoja na genge lote linalokula viapo vya kuilinda Katiba wateuliwapo nyadhifa zao kwa viapo vyao vya: ..."Nitailinda, kuihifadhi na kuitumikia katiba ya JMT"... humaanisha kuilinda kwa namna gani, na wakiona imevunjwa ama mtu yeyote anaivunja, hutakiwa kufanyaje ili kuonekana wametekeleza viapo vyao?

Na je wakikaa kimya kumezea uvunjwaji huo, na baadaye kuja kubainika kisheria kuwa Katiba ilivunjwa wakati wao wakiwa kwenye mamlaka, ni hatua gani madhubuti wanazostahili kuchukuliwa?
 
Back
Top Bottom