Boxer yangu katika chumba cha mpangaji mwenzangu

Boxer yangu katika chumba cha mpangaji mwenzangu

Km wewe kweli ni mwanaume kamili na unajimini ulipaswa kumuitabmwanaume mwenzako na umwambie hali ilivyo

Umwambie uhalisia sababu hamna ukichokufanya na unaogopa kuvunja ndoa ya mwanaume mwenzako bila sababu.

Huwezi kuogopa kusimamia kitu kidogo km hicho.Yeye ndo achague kusuka au kunyoa.
Ni sawa ndugu. Tatizo langu lilikuwa ni hofu iliyonijaa mala baada ya vichapo kutembezwa na kutotokea mpangaji hata mmoja aliyejitokeza kuamulia.
pili, niliingiziwa hofu na wenyeji wangu.
hakika sikuwa na ujasiri wa kulivalia njuga tatizo hilo kwa wakati ule.
 
Kuna ukweli ktk usemalo.
ila sikupenda kuubeba ukweli huo ambao niliusikia ktk majibizano yao.
mimi najihisi kuwa na hatia tu.

Kama ni hivyo
Pale pale bukta ilipoanguka ilikuwa uende kuiomba na kumwambia mshkaji
Oya bukta imedondokea kwako

Ila ukauchuna na kutoa kiti nje na kufurahia movie likiendelea [emoji12]
Ila sitaki kuamini sana hii ya pili
Lakini wapo wa hivyo pia

Dunia Ina mambo hii
 
Kama ni hivyo
Pale pale bukta ilipoanguka ilikuwa uende kuiomba na kumwambia mshkaji
Oya bukta imedondokea kwako

Ila ukauchuna na kutoa kiti nje na kufurahia movie likiendelea [emoji12]
Ila sitaki kuamini sana hii ya pili
Lakini wapo wa hivyo pia

Dunia Ina mambo hii
ni kweli usemalo. ila sikupata solution kwa haraka. Ni kama ganzi tu ilinishika hata nisijue chakufanya kwa haraka.
na haikuchukua hata dakika 5 jamaa akaingia ndani.
hakika nawaza hilo lingetendwa nyumbani kwangu, hata kama ni baba yangu ama kaka yangu nisingelipokea kwa wepesi.
 
Uncle umezingua...ilitakiwa wakati uleule ilipodondoka utoke kuwaeleza wenyeji

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
hakika nimezingua. Ndio maana linanisumbua kwasasa. ningeweza ku mute, tatizo moyo unanisuta.
ni kama nimemgonga mtu kwa gari alafu nikakimbia bila kumpa msaada wowote. amani haipo kabisa.
 
Aisee hata mm nimeshtuka, ila nimeshtuka zaidi boxer yenye maji kuruka kwenye neti kisha ikadunda na kwenda chumba cha pili 🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣
Duh, nimesema kweli ila umeninyima ushirikiano.
hata hivyo nashukuru kwa kustaajabu hilo.
 
Habari wana JF.

Ninaomba ufahamu ili niiokoe ndoa ya watu.
Wiki iliyopita nilimtembelea dada yangu anayeishi Dodoma mjini - Chang'ombe Extension.
Yeye na MR. wake na watoto 2 wana chumba na sebule.

Kwakuwa nilikuwa na majukumu binafsi mbali na kuitembelea familia hii na kutokana na ufinyu wa nyumba yao, ilinilazimu kuchukua room guest.
Siku ya tatu, dada na shemeji yangu wakanitaarifu kuwa kuna chumba kimoja pale kwao ambacho bado hakina mpangaji hivyo nikilipie 20,000/= kwa wiki 2 za kuishi kwangu Dom.

Chumba kilikuwa na changamoto 1 tu, juu palikuwa wazi kabisa.

Tatizo lilitokea siku mbili kabla ya mimi kuondoka Dom. wakati wa usiku wa saa mbili, nimetoka kuoga bafu la nje, wamama wa pembeni mwa chumba changu walikuwa wakiendelea na mapishi jirani na milango yao.

Walizoea kuniita Uncle kwasababu ya vile watoto wa sister wanavyoniita
Nikiwa chumbani nikung'uta bukta niliyotokanayo bafuni, ghafla ile bukta ikagusa kamba ya net na kuniponyoka mkononi na kuangukia chumba cha pili.
Muda si mrefu jamaa wa chumba hicho akawa anaingia ndani kwake na moja kwa moja akaelekea kuwasha TV.

Hapo ndipo alipoikuta bukta yangu nyuma ya TV penye switch ya ukutani. Bukta ya mtu mzima tena bado inamajimaji,,,,,,,,,,,Duh!
Alimuita mkewe aliyekuwa anapika, na hapo ndipo malumbano ya kuwa mwanamke huwa anaingiza wanaume ndani yakakolea.

Kichapo kikatembea,,,,,,hakika moyo uliniuma ila nilikaa kimya.
Kesho yake niliwaeleza wenyeji wangu, ila walinionya nisiingilie wala nisiseme uhalisia. wakiamini kuwa yataisha tu.
Wana miaka 2 ktk mahusino yao ila mdada hajawahi kushika mimba.

ukijumlisha na hili,,,, jamaa kaamua kumuacha mkewe na yuko mbioni kuoa mwingine.
Nimejulishwa kuwa mdada ameanza kwenda kwenye maombi kwaajili ya ndoa yake.
Mimi tayari nimeisha ondoka.
Ila naomba ufahamu kwenu wana JF, jinsi ninavyoweza kuwa msaada wa kurejesha ndoa ya hawa jamaa.
yaani kwa issue yako ilivyo kuwa sensitive hukutakiwa kuchukua muda wa kuomba ushauri...
Ungemuita yule mwanamme huku umevalia taulo yako muombe msamaha kuwa kuna ngua yako imerukia kwake kwa bahati mbaya wakati unaikunguta. Mambo mengine hayataki kuomba ushauri kwani yanataka maamuzi ya haraka; sasa hivi ni vigumu kuaminika...
 
yaani kwa issue yako ilivyo kuwa sensitive hukutakiwa kuchukua muda wa kuomba ushauri...
Ungemuita yule mwanamme huku umevalia taulo yako muombe msamaha kuwa kuna ngua yako imerukia kwake kwa bahati mbaya wakati unaikunguta. Mambo mengine hayataki kuomba ushauri kwani yanataka maamuzi ya haraka; sasa hivi ni vigumu kuaminika...
nilikuwa kama nimebutwaa hivi, na ghafla nikasikia mdada akiitwa na kuulizwa " mala ngapi umekuwa ukifanya uchafu wako humu ndani ya chumba changu na kujifanya mtakatifu.......niambie haraka, hii nguo ni yanani?"
Hapo ndipo hofu iliponishika.
hakika sikuweza kufanya lolote zaidi ya kwenda kuwaeleza wenyeji wangu ambao waliniambia nikae kimya.
 
Iyo bukta yako mkuu nmemuona nayo jamaa kwenye basi la Saratoga sijui anaenda nayo kigoma kukufanyaje

Sent from my SM-G960U1 using JamiiForums mobile app
sijui kama watafanikiwa, maana sikushiriki uchafu wowote zaidi ya kosa hili la ghafla.
mala nyingi ubaya humpata mtu aliyetenda kosa/dhambi kwa makusudi, hasa dhambi ya zinaa huwa haimuachi mtu salama.
 
Back
Top Bottom