Bunda: Lissu atangaza kubadili Sheria ya madini, kwamba atajayeyagundua kwenye ardhi yake yatakuwa yake

Bunda: Lissu atangaza kubadili Sheria ya madini, kwamba atajayeyagundua kwenye ardhi yake yatakuwa yake

Sahihi kabisa, Ila madini yapo ardhini na mmiliki wa ardhi ni mwananchi na sio Serikali !! ...... ulaghai huu ulianzia kwa wakoloni na kurithishwa kwa mamlaka zetu za juu.

Kusema ardhi ni mali ya wananchi chini ya usimamizi wa Rais huu ni wizi wa kitaasisi tena mchana kweupe ambao unatakiwa kukomeshwa kupitia katiba mpaya.
 
Sahihi kabisa, Ila madini yapo ardhini na mmiliki wa ardhi ni mwananchi na sio Serikali !! ...... ulaghai huu ulianzia kwa wakoloni na kurithishwa kwa mamlaka zetu za juu.

Kusema ardhi ni mali ya wananchi chini ya usimamizi wa Rais huu ni wizi wa kitaasisi tena mchana kweupe ambao unatakiwa kukomeshwa kupitia katiba mpaya.
Hakika
 
Anafuata sheria za Marekani, sheria inatakiwa ibaki kama zamani. Chamsingi tu kuwe na equal allocation ya hayo madini kwa watanzania wote. Nchini China wanatumia sheria kama yetu.
Lissu ana idea nzuri sana, juzi nilikuwa na angalia Documentary kuhusu ugunduzi wa Gesi huko Papua New Guinea, wale wenye mashamba kwenye eneo lile walipewa share kwenye mapato ya gesi na royalty na Kampuni ya EXXON.

Sisi hapa tumejifungafunga na masheria ya kiroho mbaya.
 
Rais mtarajiwa
Kipaji cha Lisu ni kuwa MWANAHARAKATI!! Hawezi kuwa Rais!! Tutamfaidi vizuri akibakia mwanaharakati!! Chadema watafute mtu mwingine presidential material!! Lisu aje kuwa mwanasheria mkuu wa Serikali huku akiendeleza uanaharakati wake!!
 
Mhuu hili kidogo lina walakini, kwani sheria inasema ardhi ni mali ya Serikali, ukinunua unapewa possession right tu lakini siyo mali yako. Aisee labda kama ataanza kwa kulibadili hilo.
Sheria haisemi ardhi ni Mali ya serikali boss. Sheria ya ardhi na 4 ya mwaka 1999 inasema ardhi ni yote ni ardhi ya UMMA na imewekwa Kwa rais kama mdhamini. (Trustee
 
Nchini Tanzania kwa sheria za sasa , shambani kwako kukikutwa madini , basi haraka sana madini hayo na shamba lako hilo vinageuzwa kuwa mali ya serikali , na baada ya muda mfupi wataletwa wawekezaji wa kiarabu au wa kizungu kuchimba madini hayo , huku wewe ukitimuliwa kwa mijeledi au hata bunduki bila huruma .

Lakini kwenye shamba lako hilo kukikutwa Bangi jua umekwisha , utamilikishwa bangi hiyo na kupigwa pingu .

Sasa leo Tundu Lissu amesema kwamba atakayekuta madini kwenye eneo lake hayo madini yatakuwa yake .mwenyewe , ataamua cha kuyafanya

Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)-Bara, Tundu Lisu ametaja mambo manne yatakayorekebishwa kwenye sheria ya madini pindi chama hicho kitakapoingia madarakani ili kuwanufaisha wachimbaji wadogo nchini.

Lissu amesema hayo leo Jumatano, Septemba 6, 2023 wakati akihutubia mkutano wa hadhara wa Operesheni +255 Katiba mpya, eneo la Kinyambiga, Bunda mkoani Mara.

Amesema licha ya sheria ya madini kusema madini yote nchini ni mali ya umma chini ya udhamini wa Rais kwa niaba ya Watanzania lakini amedai kiuhalisia madini ni mali ya Rais.

Lissu amesema suluhisho la kwanza, Chadema itakapoingia madarakani ni kubadilisha sheria hiyo akidai madini yanatakiwa yawe mali kwanza ya wenye ardhi ambaye ataelewana na atakaye yagundua kwenye ardhi yake.

Pili, sheria iseme machimbo ambayo yanatakiwa yawe kwaajili ya wananchi wa kwetu tu na ukweli ni kwamba sheria ndivyo inavyosema ya sasa lakini shida ni CCM...hizi zinazoitwa PMR remaining licence hizi ni leseni zinazotolewa kwaajili ya watanzania," alisema Lissu akihoji wageni wanakujaje mahali hapo.

Alisema wananchi, vijiji, halmashauri na Serikali kuu wanatakiwa kunufaika na rasilimali ya madini yaliyopo kwenye maeneo yao.

Tatu, linalohitaji mabadiliko ni Serikali inapotoa leseni kwa kampuni kubwa lazima kuwe na mgawanyo wa umiliki na faida zake.

Nne, ni kushugulika na mamlaka ya Rais, akidai Katiba iliyopo sasa siyo tu inamfanya Rais amiliki rasilimali za nchi yakiwemo madini, misitu na wanyama pori bali pia inampa nguvu ya kumiliki nchi na watu wake.
Lissu ni mtu makini sana.
 
Nchini Tanzania kwa sheria za sasa , shambani kwako kukikutwa madini , basi haraka sana madini hayo na shamba lako hilo vinageuzwa kuwa mali ya serikali , na baada ya muda mfupi wataletwa wawekezaji wa kiarabu au wa kizungu kuchimba madini hayo , huku wewe ukitimuliwa kwa mijeledi au hata bunduki bila huruma .

Lakini kwenye shamba lako hilo kukikutwa Bangi jua umekwisha , utamilikishwa bangi hiyo na kupigwa pingu .

Sasa leo Tundu Lissu amesema kwamba atakayekuta madini kwenye eneo lake hayo madini yatakuwa yake .mwenyewe , ataamua cha kuyafanya

Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)-Bara, Tundu Lisu ametaja mambo manne yatakayorekebishwa kwenye sheria ya madini pindi chama hicho kitakapoingia madarakani ili kuwanufaisha wachimbaji wadogo nchini.

Lissu amesema hayo leo Jumatano, Septemba 6, 2023 wakati akihutubia mkutano wa hadhara wa Operesheni +255 Katiba mpya, eneo la Kinyambiga, Bunda mkoani Mara.

Amesema licha ya sheria ya madini kusema madini yote nchini ni mali ya umma chini ya udhamini wa Rais kwa niaba ya Watanzania lakini amedai kiuhalisia madini ni mali ya Rais.

Lissu amesema suluhisho la kwanza, Chadema itakapoingia madarakani ni kubadilisha sheria hiyo akidai madini yanatakiwa yawe mali kwanza ya wenye ardhi ambaye ataelewana na atakaye yagundua kwenye ardhi yake.

Pili, sheria iseme machimbo ambayo yanatakiwa yawe kwaajili ya wananchi wa kwetu tu na ukweli ni kwamba sheria ndivyo inavyosema ya sasa lakini shida ni CCM...hizi zinazoitwa PMR remaining licence hizi ni leseni zinazotolewa kwaajili ya watanzania," alisema Lissu akihoji wageni wanakujaje mahali hapo.

Alisema wananchi, vijiji, halmashauri na Serikali kuu wanatakiwa kunufaika na rasilimali ya madini yaliyopo kwenye maeneo yao.

Tatu, linalohitaji mabadiliko ni Serikali inapotoa leseni kwa kampuni kubwa lazima kuwe na mgawanyo wa umiliki na faida zake.

Nne, ni kushugulika na mamlaka ya Rais, akidai Katiba iliyopo sasa siyo tu inamfanya Rais amiliki rasilimali za nchi yakiwemo madini, misitu na wanyama pori bali pia inampa nguvu ya kumiliki nchi na watu wake.
Wachagga na Walambya na Wasukuma na Waha watanunua ardhi yote hadi milele sasa itakuweje!
 
Kipaji cha Lisu ni kuwa MWANAHARAKATI!! Hawezi kuwa Rais!! Tutamfaidi vizuri akibakia mwanaharakati!! Chadema watafute mtu mwingine presidential material!! Lisu aje kuwa mwanasheria mkuu wa Serikali huku akiendeleza uanaharakati wake!!
Walikuwepo wenye chuki dhidi ya Lissu na sasa hawapo. Na wewe utapita.
 
Lissu kachanganyikiwa. Hicho anachokisema ni ujinga mtupu. Bora hata angesema kwamba madini yakigunduliwa kwenye ardhi yako na wewe unakuwa shareholder wa kampuni itakayochimba uwe unapata mrabaha.
We jamaa hata kama ni uchawa punguza kujiaibisha.

Yaani Ardhi ikiwa na Mawe na michanga ni yako ikiwa ma Dhahabu ni ya ccm😆😆
 
Back
Top Bottom