Bunge la Katiba Haliko Kwa Ajili ya Kuboresha Rasimu ya Kina Warioba!

Bunge la Katiba Haliko Kwa Ajili ya Kuboresha Rasimu ya Kina Warioba!



Hawa wasomi wa mambo ya katika kama akina Shivji wakati mwingine wanaonekana kuchanganya katika kuelimisha na ueleweshaji wa kawaida kuliko inavyotegemewa.

CC:
Mchambuzi,
JokaKuu, Bongolander, Pasco, Zakumi, MTAZAMO, zumbemkuu, Jasusi

CS, wewe kama wengine wanafanya kosa moja kubwa sana la kudhania (presumption). Wanadhania kuwa kwa vole tume ilizunguka nchi nzima na kukusanya maoni basi maoni yale yanatakiwa yaingizwe kwenye katiba na yakubaliwe. Kwanza, sheria haikuilazimisha tume kukubali maoni ya wengi - ndio maanayanaitwa maoni na vile vile sheria haijalazimisha Bunge la Katiba kukubali rasimu kama ilivyo.

TUme ilipewa jukumu la kukusanya maoni, kuyachambua na kuyapanga vizuri lakini haikuwa na amri ya "mambo yale yanayopendekezwa na wananchi wengi ndio yataingizwa kwenye rasimu". Kwa sababu hiyo utaona kuwa tume imeandika mambo mengine kwenye rasimu ambayo hayakuwa sehemu ya maoni yaliyokusanywa. Kwa mfano, wengi wanaamini kuwa serikali tatu ni mapendekezo ya wananchi wengi; hili laweza kweli lakini ni wananchi wangapi waliosema wanataka "Shirikisho" bila kujali idadi ya serikali? Ni wananchi wangapi walijadili suala la majaji, kugawa mikoa au idadi ya wizara?

Rasimu ni kianzio tu; ni wazi mambo mengi yaliyoko yataenda kwenye Katiba Inayopendekezwa lakini si lazima yawe yote na hakuna kitu kinachozuia Bunge la Katiba kubadili mambo ambayo yako kwenye rasimu.
 
Nakubaliana na wewe .Nakumbuka mwezi April mwaka 2012 nilipinga composition ya Bunge la Katiba.Nadhani nilikua nikichangia kwenye mjadala ulioanzisha na tulikua wachache sana tuliopinga huu mchakato tangu Mwanzo.Miaka 2 baadae tuko hapa

Historia ya Kenya ipo njia kujirudia hapa Tanzania

Historia ya alliance ya chama tawala cha MMD na chama cha UPND dhidi ya hoja za Patriotic Front na wanaharakati pamoja na wananchi wa Zambia kwenye katiba inajirudia na chama tawala wakajichimbia shimo kwenye uchaguzi mkuu uliofuata Upinzani ukashinda

Hofu ya chama tawala ilikua kuogopa reforms za tume ya uchaguzi na pendekezo la mshindi wa urais kupata 50%+1 ya kura zote.

Sasa uchaguzi mkuu uliofuata 2011 upinzani ukashinda ingawa hawakufikisha 50% + 1 .Wangekua na katiba mpya wasingetangazwa washindi

Wananchi waliungana na upinzani kwa kuwa walijua chama tawala hakina nia thabiti ya kushiriki mchakato wa katiba mpya kwa maslahi ya wazambia wote.

CCM hapa hawajifunzi.Nasi tuendelee kuwakumbusha wananchi historia na upinzani tujipange kuonyesha misimamo hata kama tumeshafanya makosa

Nilisema hatuwezi kufanya mazungumzo na watu wasio na nia njema.Wengine wakanikemia kuwa katiba mpya eti haipatikani barabarani

Msimamo wangu ni kuwa wasiotaka kukaa mezani kwa nia njema tukutane nao barabarani kisha turudishane mezani tukiwa na maumivu sasa tujadiliane kwa nidhamu.

ni kweli mzee...ila siasa imejawa na mazingaombwe sana unakuta wew/ninyi na misimamo yenu pia mnakuwa na hiden interst ambapo kama wananchi watafuata ni kheri kwao au itakuja kuwa shida baade kwao...huwa najaribu kufikir ni njia ipi bora kila siku ya kutenganisha siasa na mambo ya msingi na haswa haya yenye athar kubwa kwa jamii kwa baadae...
 
Hapana kuna mambo mawili ambayo lazima tuyangalie elimu na ufahamu unaweza kuwa na elimu kubwa ukakosa ufahamu ukaenda ukanywa sumu ukafariki sioni mankiti ya baadhi ya wasomi wa taifa hili kuwa eti bunge maalum kwa maana yao halina mamlaka ajabu pahali ambapo thuluthi mbili ya wabunge wa bunge maalum wanatapiga kura kuamua hatma ya rasimu yenyewe wanaambiwa hawana mamlaka ya kubadilisha ajabu sana.
 
Sitaki kuamini tumepeleka watu wengi waganga njaa huko Bungeni. Hoja wanazoleta na kazi wanayotakiwa kuifanya wala havilingani. Ila ukiwauliza wanajiita wazalendo. Wazalendo sisi tumekuwa wanafiki kweli. Matendo yetu yako tofauti na maneno tunayosema.
 
CS, wewe kama wengine wanafanya kosa moja kubwa sana la kudhania (presumption). Wanadhania kuwa kwa vole tume ilizunguka nchi nzima na kukusanya maoni basi maoni yale yanatakiwa yaingizwe kwenye katiba na yakubaliwe. Kwanza, sheria haikuilazimisha tume kukubali maoni ya wengi - ndio maanayanaitwa maoni na vile vile sheria haijalazimisha Bunge la Katiba kukubali rasimu kama ilivyo.

TUme ilipewa jukumu la kukusanya maoni, kuyachambua na kuyapanga vizuri lakini haikuwa na amri ya "mambo yale yanayopendekezwa na wananchi wengi ndio yataingizwa kwenye rasimu". Kwa sababu hiyo utaona kuwa tume imeandika mambo mengine kwenye rasimu ambayo hayakuwa sehemu ya maoni yaliyokusanywa. Kwa mfano, wengi wanaamini kuwa serikali tatu ni mapendekezo ya wananchi wengi; hili laweza kweli lakini ni wananchi wangapi waliosema wanataka "Shirikisho" bila kujali idadi ya serikali? Ni wananchi wangapi walijadili suala la majaji, kugawa mikoa au idadi ya wizara?

Rasimu ni kianzio tu; ni wazi mambo mengi yaliyoko yataenda kwenye Katiba Inayopendekezwa lakini si lazima yawe yote na hakuna kitu kinachozuia Bunge la Katiba kubadili mambo ambayo yako kwenye rasimu.

Unachokisema wewe ni sawa kwa ile version ya Kiswahili 25 (i) hadi (iii). Lakini kwa Version ya English, 25 (i) hadi (iii) inakataza Bunge la Katiba kubadilisha chochote. Na kwa mujibu wa Jaji Werema, kama kuna ukakasi katika kutafsiri sheria kati ya Kiingereza na Kiswahili ilevya Kiingereza ita prevail.
 
CS, wewe kama wengine wanafanya kosa moja kubwa sana la kudhania (presumption). Wanadhania kuwa kwa vole tume ilizunguka nchi nzima na kukusanya maoni basi maoni yale yanatakiwa yaingizwe kwenye katiba na yakubaliwe. Kwanza, sheria haikuilazimisha tume kukubali maoni ya wengi - ndio maanayanaitwa maoni na vile vile sheria haijalazimisha Bunge la Katiba kukubali rasimu kama ilivyo.

TUme ilipewa jukumu la kukusanya maoni, kuyachambua na kuyapanga vizuri lakini haikuwa na amri ya "mambo yale yanayopendekezwa na wananchi wengi ndio yataingizwa kwenye rasimu". Kwa sababu hiyo utaona kuwa tume imeandika mambo mengine kwenye rasimu ambayo hayakuwa sehemu ya maoni yaliyokusanywa. Kwa mfano, wengi wanaamini kuwa serikali tatu ni mapendekezo ya wananchi wengi; hili laweza kweli lakini ni wananchi wangapi waliosema wanataka "Shirikisho" bila kujali idadi ya serikali? Ni wananchi wangapi walijadili suala la majaji, kugawa mikoa au idadi ya wizara?

Rasimu ni kianzio tu; ni wazi mambo mengi yaliyoko yataenda kwenye Katiba Inayopendekezwa lakini si lazima yawe yote na hakuna kitu kinachozuia Bunge la Katiba kubadili mambo ambayo yako kwenye rasimu.

Katiba ni ya wananchi na wabunge ni wawakilishi wa wananchi na wanachotakiwa kufanya ni kile kufanya waliyotumwa na wananchi na kutetea yanayowahusu wananchi na taifa.

Dhana ya ushirikishwaji wananchi haitakuwa na maana pale maoni ya na matakwa ya wananchi walio wengi yakija kuchomolewa na kutupwa nje kisha kuingizwa yasiyotoka kwa wananchi.

Pamoja na wananchi kutokuwa wataalamu katika mambo ya sheria, jopo la wakusanya naoni ya wanayanchi ya kuwayaweka sawa iliundwa kwa weledi likiwa limesheheni wataalamu ambao wengi walikubaliana na uteuzi wao, ndio tunashuhudida hata chama tawala baada ya kuona wale walioshughulikia mswada huo kufaya kadiri ya matakwa ya wananchi na kuweka itikadi za kisiasa kando wamekuja na mitazamo ya kuja na rasimu yao kwa mlango wa uani.

Tukubali kwamba kazi ya bunge hili si kubuni katiba tunayoitaka, mswada umeshaandaliwa na kinachotakiwa sasa ni kuyachambua yaliyomo ndani ya katiba hiyo kuona kasoro zilizomo na kuzifanyia kazi. Hili jukumu ni sawa na mwandishi wa habari akileta habari kwa mhariri mwandamizi anachofanya ni edditing (kuhariri) wala si kuibadilisha habari. Huu ndio ukweli na hali halisi.
 
Watu milioni moja waliofikiwa katika kutoa maoni isichukuliwe ndio msingi mkuu wa wananchi ingelikiwa watu wameshatoa maoni wao kwa tume na ndio maoni yao sasa kwa nn mwisho wa mchakato wanayapigia kura maoni yao tena? Nguvu za wananchi ni kura ya maoni si mapendekezo ya tume
 
Natabiri nchi kuingia ktk migogoro,migomo,maandamano na kesi mahakamani ktk kipindi cha 08/2014 -08/2016 ktk kipindi hiki wengi watafungwa,watajeruhiwa na kuuwawa kwa sbb hizo hapo juu kwa kuwa serikali itatumia nguvu kudhibiti hali hizo
 
However, Mzee Mwanakijiji unatuchanganya kidogo pale unapotumia practical failures to justify theory and principle katika suala husika, je should practice justify theory and principle au theory/principle should justify practice in our context?

Naamni both theory na practice are equally important. All must be taken into account. Theory inasaidia kutumia tulichojifunza kutatua tatizo moja kwa njia mbalimabli. For example, a social worker working toward the protection of a vulnerable child itambidi a-justify practice yake kwa kutumia theories. Kama akiamua kutumia systems theory in their practice, then they must show kwa nini wamechagua hiyo approach instead of others approaches kama task-centred approach.

Most of the practical failures zinakuwa hazina foundations. Hazina basis au zina-adopt wrong approaches. Kama nyumba haina msingi mzusiri sidhani kama itadumu. Huu mchakato wa Katiba mpya uliibuka from nowhere. Hata mchoro wa ramani haukuwepo kwenye Ilani ya CCM. Kabla ya mchakato kuanza CCM hawajawhi kukaa chini na kufanya hata background study ya kuwa na Katiba mpya and how this should be achieved. Hata hivyo, watu wengi bado hawajiulizi how come CCM walifanya U-turn kubwa hivyo tena bila indicators na kuja na gia ya katiba mpya? Hawa akina Jaji Werema si walishasema hatuhitaji katiba mpya? If so, how come, wamekuwa entrusted kutengeneza katiba mpya ambayo walisema hatuhihitaji? How do you trust these sort of people?

It is well known na haihitaji hata theory kusema kuwa process ya kutengenza katiba lazima iwe participatory in nature na lazima infanywe na constituent assembly ambalo ni specialiased, liliyoundwa mahususi kwa ajili ya kutengeneza katiba mpya.

Of course, constitution making should not be idealised. Kuna umuhimu pia wa ku-take into account historia na tamaduni za nchi husika. Mfano, nchi za Amerika ya Kusini huwa zinatumia mabunge ya katiba, nchi za Afrika Magharibi hasa zile zilizotawaliwa na Ufaranza zinatumia constitutional conferences, Nigeria inatumia tume ikifuatiwa na aina fulani ya "Bunge la Katiba". Hii practice inatumika pia Afrika Mashariki kama tunavyoina sasa hapa nchini.

Hata hivyo, lazima kuwe na basis ya hiyo practice. Ni muhimu hiyo approach kuwa na misingi. Vinginevyo, kama nguvu za kisiasa kwenye process mzima zikiachwa kama zilivyo zinaweza kushape siasa na kuleta authoritarian regime kama ilivyotokea Venezuela au nguvu hizo za kisiasa kulazimisha aina ya katiba inayotakiwa na kikundi fulani na kusababisha mchakato mzima kuanguka kama ilivyotokea Bolivia.

Hivyo, ni muhimu process ya kutengeneza ya katiba mpya iongozwe na some normative principles. Vinginevyo, ni sawa na kuwa na sheria ambayo haina policy backing. Hizo normative principles ni pamoja na

  • Process ya kutengeneza katiba lazima ifanywe na bunge la katiba lililochaguliwa na wananchi moja kwa moja.
  • Hili bunge la katiba lazima liwe na unlimted power in the constitutional making. Litakuwa na unlimited power kwa sababu ilitakuwa limechaguliwa directly na wananchi ambao ndiyo wenye mamlaka ya mwisho na nchi yao.
  • Mchakato mzima wa kutengeneza katiba mpya lazima uwe inclusive and participatory.
Hoja ya Jaji Warioba imejikita on the fact kuwa kwa vile the so called "Bunge la Katiba" is not Bunge la Katiba per se, basi halina unlimited power ya kubadilisha rasimu ya tume yake ambayo anadai imebeba maoni ya Watanzania. Anaweza kuwa sahihi kwa sababu hilo bunge la katiba halichaguliwa na wananchi. Wapo wanaosema kuwa wabunge wa bunge la kawaida wamechaguliwa na wananchi lakini pamoja na kuwepo pia kwa wabunge walioteuliwa, hao waliochaguliwa hawakuchaguliwa muhsusi kwa ajili ya kutengeneza katiba. Laiti tungekuwa na job descrption za wabunge wa kawaida ndo tungejua kama moja ya kazi yao ni kutengeza katiba mpya. Tunaposema katiba ni sheria mana inajumuisha pia na the way inavyotengenezwa.

On the other hand, the fact kuwa bunge hili la katiba halijachaguliwa, haina maana kuwa tume ya Jaji Warioba inakuwa superior, simply because hata tume yake haikuchaguliwa na wananchi. Neither maoni iliyokusanya yanawakilisha maoni ya Watanzania wote kwenye masuala yote yanayowagusa. Tume yake si ilipewa terms of reference na ilitakiwa kuchukuwa maoni ya watu kulingana na hizo terms of reference?

Yaani jinsi mchakato mzima ulivyokuwa designed is highly political. Uteuzi wa Tume ya Jaji Warioba ulikuwa highly debatable na mpaka sasa Warioba anajaribu ku-justify kilichofanywa na tume yake. Was the Commission representative of the people? The terms of reference za hiyo tume are much debatable. Kwa ni wananchi wawe dictated na terms of reference katika kutoa maoni yao?

Tukija kwenye hilo Bunge la Katiba, nchini Brazil Bunge lao la Katiba lilikuwa directed kujadili na kuipitia tuu rasimu ya katiba kama anavyotaka Jaji Warioba, lakini hili lilikataliwa kwa sababu ingefanya bunge hilo kuwa rubber stamp ya kupitisha rasimu kuwa katiba bila hata kujadiliwa. Lakini kule East Timor, chama cha Fretilin, ambacho ni chama kilichokuwa na nguvu kwenye Bunge la Katiba kiliweza kulitumia bunge hilo na kuubadilisha kabisa mchakato mzima kwa faida yake kwa kuhakikisha kuwa Bunge la Katiba linajadili na kupitisha rasimu iliyowekwa mezani na chama hicho.
 
Katiba ni ya wananchi na wabunge ni wawakilishi wa wananchi na wanachotakiwa kufanya ni kile kufanya waliyotumwa na wananchi na kutetea yanayowahusu wananchi na taifa.

Dhana ya ushirikishwaji wananchi haitakuwa na maana pale maoni ya na matakwa ya wananchi walio wengi yakija kuchomolewa na kutupwa nje kisha kuingizwa yasiyotoka kwa wananchi.

Pamoja na wananchi kutokuwa wataalamu katika mambo ya sheria, jopo la wakusanya naoni ya wanayanchi ya kuwayaweka sawa iliundwa kwa weledi likiwa limesheheni wataalamu ambao wengi walikubaliana na uteuzi wao, ndio tunashuhudida hata chama tawala baada ya kuona wale walioshughulikia mswada huo kufaya kadiri ya matakwa ya wananchi na kuweka itikadi za kisiasa kando wamekuja na mitazamo ya kuja na rasimu yao kwa mlango wa uani.

Tukubali kwamba kazi ya bunge hili si kubuni katiba tunayoitaka, mswada umeshaandaliwa na kinachotakiwa sasa ni kuyachambua yaliyomo ndani ya katiba hiyo kuona kasoro zilizomo na kuzifanyia kazi. Hili jukumu ni sawa na mwandishi wa habari akileta habari kwa mhariri mwandamizi anachofanya ni edditing (kuhariri) wala si kuibadilisha habari. Huu ndio ukweli na hali halisi.

Kwa hiyo kazi ya bunge la katiba ni kupiga tuu "rubber-stamp" kwenye hiyo rasimu ya tume? Kwa maana hiyo, hao wananchi waliotoa maoni yao kupitia tume watakuwa wajinga sana. Yaani wamewatuma wabunge wao na kuwalipa fedha zote hizo kwa ajili ya kwenda kuweka "rubber-stamp" tuu kwenye hiyo rasimu? Kama ni hivyo, hao wananchi si wangemalizana na tume huko huko?

On the other hand, hao wananchi waliwachagua hao wabunge kwa ajili ya kuwatengenezea katiba mpya? Vipi wale wabunge wa kuteuliwa watakuwa wanamwakilisha akina nani kwenye hilo bunge la katiba? Miaka minne imeshapita tokea hao wabunge wachanguliwe na bado unadhani waliowapigia kura bado wanawa-trust kama siku ile walipowapigia kura?

Madhumuni ya mchakato wowote wa katiba mpya, ambayo ndiyo itakuwa sheria mama ya nchi ni kuhakikisha kuwa kila mwananchi anahusika na kuchangia katika process nzima. Mchakato wa katiba unasaidia kuhusisha watu ambao mara nyingi wanatengwa kwenye siasa za kawaida kwa kigezo eti watawakilishwa na wabunge wao.

Kuwepo kwa watu hao walitengwa kwenye siasa ndiyo kunasaidia kutajirisha mchakato mzima wa katiba na kuimarisha ubora wa demokrasia. Of course, matokeo ya wananchi kujihusisha moja kwa moja kwenye mchakato, hayatatatua matatizo yao moja kwa moja, lakini maazimio waliyofikia yatasaidia kuiweka nchi kwenye nafasi nzuri zaidi tofauti na ilivyokuwa zamani. Pia hao watu wataiheshimu katiba itakayopatikana kwa sababu ya kujihusisha kikamilifu katika kuitengeneza.

Hao wabunge unaodai wanawakilisha wananchi wameshapitisha sheria kibao tuu ambazo hata hawakutumwa na wananchi kuzipitisha. Lakini leo unawa-trust kuwa watapitisha kile kinachotakiwa hao wananchi? Vipi wakipitisha mambo mengine unaweza kuwa-hold accountable? Maana hukumchagua mbunge wako kwa ajili ya kukutengenezea katiba mpya. Pia sidhani kama kwenye kampeni zao walihaidi kukutengenezea katiba mpya.

Hata kama kungekuwa na job descriptions za wabunge, kusingekuwa na role ya kutengeneza katiba mpya. Kazi zao kubwa ni kutengeneza sheria za kawaida za nchi. Sheria mama inajadiliwa na kutengenezwa na wananchi wenyewe kupitia Bunge la Katiba walilolichagua mahususi kwa ajili ya kutengeneza katiba mpya. By Bunge la Katiba sina maana ya hili "Bunge la Katiba" linaloendelea sasa ambalo kwa maoni yako linaenda kupiga ruber stamp the so called "maoni ya Watanzania wote" yaliyomo kwenye rasimu ya Jaji Warioba.
 
...kinachotakiwa kujadiliwa kwenye bunge hili la katiba ni rasimu ya katiba itakayosomwa bungeni na jaji Warioba...period.....maana ndie nchi ilimtuma kukusanya maoni y wananchi.....Btw watu nashangaa hawajiulizi ni wananchi gani hao waliotoa maoni yao kwenye tume ya Warioba...watu wanasahau kuwa wananchi makundi yote walishirikishwa kwenye utoaji wa maoni yao ...wakiwemo wajumbe wooote(kupitia vyama vyao)..na pia makundi yao....na mawazo hayo yooote ndio yalitumika kutengeneza rasimu ya Warioba.....

....Sasa nami nasikitika sana napoona watu wanajadili etu possibility ya ku reject sehemu kubwa ya rasimu ya Warioba!!...eti na kuja na rasimu mbadala!!!(haya mawazo ya rasimu mbadala yanakujaje bungeni)????na rasimu mbadala inamwakilisha nani????haya ni mambo wajumbe makini wanatakiwa wahoji bungeni .........ina maana Warioba na tume yake walikuwa wanatafuna kodi zetu kuzunguka nchi nzima wakiongea na wanyama ama Watanzania????......hivi tume ya Warioba ilitoa views zao hewani ama??...

....to me ..at this stage...people should focus more on contents in the Warioba's draft na jinsi ya kuziboresha.....na si kuanza kujaribu kurudishana nyuma kwenye stage hii muhimu....One gets a feeling kwamba kuna watu wana motives za kuyumbisha constructive inputs kwenye draft y Warioba.....maana ikikwama kupita kwa wananchi (baada ya kunyewa bungeni)..then tunabaki na hii katiba ya zamani.....na hapa CCM will be happier than ever.....
 
Nakubaliana na wewe .Nakumbuka mwezi April mwaka 2012 nilipinga composition ya Bunge la Katiba.Nadhani nilikua nikichangia kwenye mjadala ulioanzisha na tulikua wachache sana tuliopinga huu mchakato tangu Mwanzo.Miaka 2 baadae tuko hapa

Historia ya Kenya ipo njia kujirudia hapa Tanzania

Historia ya alliance ya chama tawala cha MMD na chama cha UPND dhidi ya hoja za Patriotic Front na wanaharakati pamoja na wananchi wa Zambia kwenye katiba inajirudia na chama tawala wakajichimbia shimo kwenye uchaguzi mkuu uliofuata Upinzani ukashinda

Hofu ya chama tawala ilikua kuogopa reforms za tume ya uchaguzi na pendekezo la mshindi wa urais kupata 50%+1 ya kura zote.

Sasa uchaguzi mkuu uliofuata 2011 upinzani ukashinda ingawa hawakufikisha 50% + 1 .Wangekua na katiba mpya wasingetangazwa washindi

Wananchi waliungana na upinzani kwa kuwa walijua chama tawala hakina nia thabiti ya kushiriki mchakato wa katiba mpya kwa maslahi ya wazambia wote.

CCM hapa hawajifunzi.Nasi tuendelee kuwakumbusha wananchi historia na upinzani tujipange kuonyesha misimamo hata kama tumeshafanya makosa

Nilisema hatuwezi kufanya mazungumzo na watu wasio na nia njema.Wengine wakanikemia kuwa katiba mpya eti haipatikani barabarani

Msimamo wangu ni kuwa wasiotaka kukaa mezani kwa nia njema tukutane nao barabarani kisha turudishane mezani tukiwa na maumivu sasa tujadiliane kwa nidhamu.

Nawewe tulitaka uende bunge la katiba tuaogopa unaweza kwenda kumaliza watu na sumu zako..., au umeacha?
 
In my humble view, Warioba na Shivji, aidha wote wanatafsiriwa vibaya au hawakujieleza vya kutosha, if not both:

Ukweli unabakia kuwa - Bunge la katiba linatakiwa ku-base its discussions kutokana na rasimu ya katiba iliyoandaliwa na tume ya katiba na sio vinginevyo. Suala la bunge la katiba kuondoa yaliyopendekezwa ndani ya rasimu iliyowasilishwa na tume ya katiba ni suala ambalo sio black and white kama makada wa CCM na wengine of the same political persuasion wanapenda iwe. In order for the constituent assembly kuondoa au kufuta kipengele au vipengele vyovyote ndani ya rasimu iliyowasilishwa na tume ya katiba, inatakiwa zipatikane two thirds ya kura za wajumbe wa bunge la katiba, vinginevyo yaliyowasilishwa na tume ya warioba yanatakiwa kubakia kama yalivyo au kuboreshwa zaidi. Hali hii ndio inatoa uhalali, haja na umuhimu wa tume ya katiba na bunge la katiba.Kumezuka mjadala mkubwa sana juu ya umuhimu wa tume ya katiba vis a vis bunge la katiba huku wengi wakihoji iwapo kulikuwa na maana ya kuwa na tume ya katiba in the first place na wengine wakihoji iwapo basi kulikuwa na maana ya bunge la katiba kuketi baada ya kazi ya tume ya katiba. Nadhani ufafanuzi huo hapo juu utasaidi to shed some light katika sula hili unfolding before us;

Mchambuzi umeelezea vizuri sana hili na nadhani ndio kiini cha mjadala uliopo. Kuna watu wanaamini kuwa Bunge la Katiba limefungwa na rasimu kwamba linaweza kuboresha tu lakini si kufuta vipengele au masharti yaliyomo kwenye rasimu. Nadhani hii inatokana na kutoielewa kauli ya Warioba. Shivji, mimi na wengine tunadai - kwa kuangalia sheria - kuwa Bunge lina madaraka ya kukubali vipengele vilivyo au kuvibadilisha visomeke vizuri, kuviongozea vitu au hata kuvifuta alimradi - kile unachosema wewe - kuna utaratibu unaotakiwa kufuatwa ili kufanya hivi.


Hata hivyo, sidhani kuwa kauli yako ya:

In order for the constituent assembly kuondoa au kufuta kipengele au vipengele vyovyote ndani ya rasimu iliyowasilishwa na tume ya katiba, inatakiwa zipatikane two thirds ya kura za wajumbe wa bunge la katiba, vinginevyo yaliyowasilishwa na tume ya warioba yanatakiwa kubakia kama yalivyo au kuboreshwa zaidi.(msisitizo wangu)

Si sahihi.

Sheria haijaweka utaratibu wa jinsi ya kupitisha vipengele kwa vipengele - labda utakuwepo kwenye kanuni. Sheria inasema tu kuwa Katiba Inayopendekezwa itapitishwa kwa wingi wa 2/3 (absolute majority) ya wajumbe wa Bunge hili Maalum. Ninavyoona mimi utaratibu utakaotumika utakuwa ni 'voice vote' ya kuwauliza wajumbe kama kipengele kinapita au kisipite na wale "watakaaonekana" kuungwa mkono zaidi watashinda. Mwisho wa siku ndiyo kura ya kuamua kupitisha Katiba Inayopendekezwa ndio itapigwa kukidhi masharti ya Kifungu cha 26(2) cha Sheria ya Katiba Mpya.

Niko tayari kusahihishwa.
 
Katiba ni ya wananchi na wabunge ni wawakilishi wa wananchi na wanachotakiwa kufanya ni kile kufanya waliyotumwa na wananchi na kutetea yanayowahusu wananchi na taifa.n

Ukiangalia kwa karibu utaona kuwa hakuna mjumbe hata mmoja wa Bunge la Katiba aliyechaguliwa na Wananchi kuwawakilisha katika hili la kuandika Katiba Mpya. Kama yupo nani?
 
Wa Tanzania ni wavivu sana wa kusoma then wajenge hoja, wanaacha mtu mmoja afikiri halafu majority wanageuka wapiga debe wa mawazo au Comments za mtu mmoja! Wakati hii sheria inatungwa watu walikuwa bize kubishana nani ateuwe tume, then yakaja mabishano nani ateuwe wajumbe wa bunge la Katiba, Sasa watu wako bize kubishana Idadi ya Serlkali.
Mijadala hii ya kishabiki inaacha watu kuwa bize na vitu vidogo na kupuuza mambo makubwa sana.
Nani anazungumzia mjadala juu ya sheria ya umiliki Rasilimali zetu? Tume huru ya uchaguzi?, Mwananchi wa Ilulanguru Tabora, Tukuyu, Manyovu, Kiabakari wote wanalazimishwa kujadili Idai ya serikali wakati hata wakati wa utoaji maoni ni watu 47,820 pekee ndio waliogusia mambo ya Muungano. Tabia ya Taifa zima kujishughulisha na jambo moja tena lenye Interest na wanasiasa limeshai Cost nchi hii na itaendelea sana kui cost nchi kwa kuwa watu hawapendi kusoma.
Hata Professor Shivji alipokosoa Madai ya Warioba kwa ku base kwenye sheria iliyounda Tume hiyo kuna wale wavivu wa kusoma ila mabingwa wa kuchangia walimshambulia sana huyo Gwiji wa Sheria.
Kama hatutaki kuachana na Ujinga hakuna mwenye ubavu wa kututoa Ujingani
 
WArioba hatasoma rasimu ya Katiba; ataitwa tu kama anahitajika kutoa maelezo kwa wajumbe.
...nilimaanisha kukabidhi rasimu kwa bunge la katiba (si kuisoma kwao)...i hope kutakuwepo hii occasion..kwa mwenyekiti wa tume ya katiba kukabidhi rasimu bungeni ili ianze kujadiliwa....na hopefully Warioba will be given a chance to speak kwenye makabidhiano....na hopefully he will be given a last chance to clarify some of the burning issues in the draft before the parliament starts the deliberations.....hili nadhani litakuwepo kwenye ratiba yao...na kama halipo ..i wish them to do so...
 
...Na kwa wale wanaobeza kazi ya tume ya katiba........Kuna watu walitaka huu mchakato wa katiba uchelewe....c'mon!! .....this country needs a new constitution now.....in fact tumechelewa kuwa na katiba mpya.....nchi hii inahitaji ASAP katiba mpya kama njia mojawapo ya kututoa kwenye mgando huu.....hatuwezi kuendelea kusubiri....eti sijui michakato.....mnataka tuendelee kusubiri (huku tukipiga kelele)hadi pale watu watakapokatana mapanga ya kimbali (kama Kenya) ndipo tuamke kudai katiba mpya!!..c'mon kwangu huu ni upuuzi mkubwa....nchi hii inahitaji katiba mpya sasa......kuliko wakati mwingine wowote....


....kwa wale wafuasi wa vyama wanaofikiri nchi hii itakombolewa na vyama vyao ..ama taasisi flani ...hii ni short sight na upuuzi mkubwa sana....Nchi hii itakombolewa na RAIS makini.....jasiri ...mzalendo wa kweli...na muadilifu..atakayesimamia na kuilinda vema KATIBA iliyotokana na WATU wote.....Rais atakayesimamia misingi ya haki..usawa..na sheria za nchi.....na haitajalisha mtu huyu atatoka chama au taasisi gani....

....Watu wanaoshabikia matakwa ya vyama kwenye rasimu ya katiba yetu wanatakiwa wajue kuwa history ya dunia inaonyesha kuwa nchi hazikombolewi na vyama wala taasisi...bali watu mahiri(marais) wanaoongoza nchi mataifa yao kwa ujasiri mkubwa....kwa kufuata misingi imara ya katiba za mataifa yao.........This country (TZ)needs such a role model individual....ambaye simuoni hata leo hii....

...wale waobeza kazi ya Warioba sikubaliani nao...kwa kuwa namwona huyu mzee kama mzalendo wa kweli wa taifa hili.....ambaye ameweza hata kutofautiana na wenzake CCM kwenye kuandaa hii rasimu ya katiba....huu ni uzalendo mkubwa...na naweza kusema watu kama kina Warioba na Dr.Salim ni wazee wachache wazalendo na waadilifu sana ambao taifa hili limebaki nao na tunahitaji sana nasaha zao.....na nina uhakika kuwa mustakabali wa taifa hili hauwapi usingizi (as opposed to majority of CCM members)...maana unaelekea kupokwa na wajanja na matapeli wachache wa kisiasa....Wazee hawa wameishi na kuuona uadilifu na uzalendo wa wakina Nyerere..na kina Sokoine...ambao ni aina ya role models ambao taifa hili linawahitaji sana sasa kuliko wakati mwingine wowote......



...Tunahitaji katiba mpya sasa....theere is no going back at this stage....kama twataka kutoka kwenye mgando huu kama nchi...hatuwezi kusubiri vyama vya siasa vije vituletee katiba mpya....maana nchi hii haitakombolewa na vyama vya siasa...never....
 
Mkuu kuna sintofahamu hapo mbele yetu! Kwa sababu Wazenji watapiga kura kivyao na wa Tz bara watapiga kura kivyao!
Just imagine Tz bara wamekubali wakati Zbar wamekataa!
...
Kwa mawazo yangu, ikipitishwa serikali mbili, ni lazima itapingwa na wananchi, na kwa mawazo yangu, naskia kaharufu kadamu kwa mbaaali!

Wananchi gani wanaoweza kukataa Mawazo yanayoletwa na CCM hata km niyakiBWEGE unajua hao wapiga KURA huku mtaani Wanajadili wabunge wanavyopiga laki3 tu!
 
Kwa kifupi mpaka hapa wale mnaodhani CCM watawapa KATIBA itakayokidhi Mawazo ya wengi hesabuni MAUMIVU yaani mtangoja sana,,! Huko bungeni CHENGE atakuwa SPIKA Katiba itakuja Mtaani na waTZ wataipisha kwa kiSHINDO huo ndo ukweli chakujifunza hapa 2we 2nawaamini Viongozi wa Vyama vya UPIZANI tungewaunga MKONO Tangu kutoka Bungeni hadi kumuona RAIS 2cngefika hapa cc tukaishia kuwakejeli kwamba wamefata JUICE IKULU really? kwa haya wanayo2fanyia ccm NI stahili ye2 Ngoja watunyoe,,!!
 
Back
Top Bottom