Bunge la Katiba Haliko Kwa Ajili ya Kuboresha Rasimu ya Kina Warioba!

Bunge la Katiba Haliko Kwa Ajili ya Kuboresha Rasimu ya Kina Warioba!

Kwenu wajumbe wa bunge maalumu la katiba
Hv dodoma mmeenda kupoza kodi zetu za bure?
Maana sielewi,mjumbe anapoomba kuongezewa posho ya kujikimu
Laki tatu kwa maisha ya dodoma mbona its enough Sana????
Nani aje hapa hewani na kusema yeye anaendesha maisha yake kwa kilo tatu daily??
Mbona wengine hata. Tshs 50,000/= ni shida,?
Wengine wanakomaa wapewe hadi iPad
 
Km nilazima Serikali ya Mapinduzi iwepo Nikwanini pia TANGANYIKA icwepo! kwanini nyie watu wa CCM mnatufanya km Watt wadogo,,!

Ndugu yangu haya mambo yanaumiza sana moyo....hapa tumepigwa changa la macho that is why uteuzi wa wabunge wa katiba una maswali mengi na utata mkubwa sana....point ya msingi ni kua JK alikua anajua nini atakifanya na ana jua nini kinafuata kwenye hili bunge la katiba kifupi ni kuwa tume ya warioba bila kujua inahujumiwa na kile walicho kiandika kinaenda kutupwa chooni....Maskini watanzania kwa bahati mbaya sana hatutakua na ujasiri wa kupiga kura ya hapana kwa hiyo katiba itakayo andikwa upya na wabunge hawa ambao % kubwa ni maCCM.....yangu macho.....SO SAD.
 
Hili si tatizo kwani ndivyo sheria inavyotaka na ndivyo utaratibu uliokubaliwa. Kama walio wengi Bungeni wataamua kufanyia marekebisho vipengele vyovyote vya rasimu na ikaitwa kura na wakashinda basi vipengele hivyo vitakuwa katika Katiba Inayopendekezwa. Kama wananchi hawatakubaliana nayo basi wataikataa kwenye kura ya maoni.

Kwa hiyo MM unaposema hili sio tatizo maana yake ni kwamba unapenda na unafurahia kabisa uchakachuaji wa maoni ya wananchi na unajua wazi kua watanzania hawana ujasiri na hawawezi kamwe kupiga kura ya hapana.....daah inauma sana.
 
Hii nchi haina serikali, ina kigenge cha walanguzi tu! Ebbos kwaiyo zile billions za ukusanywaji wa maoni ya wananchi walizokuna Warioba na timu yake zimekwenda bure! Si ndio maana yake!
...
Maccm hayaridhiki hadi tuanze kuuana hapa!
 
Acha kupotosha we Mzee, kwa maana hiyo kulikuwa na maana gani ya sisi kutoa maoni yetu?

Akili zikizidi sana zinageuka kuwa hasara.

Mkuu hakuna kilichopotoshwa hapo! Hizi habari ni za kweli na vyombo vingi vya habari wametoa hiyo habari!
Pilika zote hizo ni njama ya maccm kupinga serikali tatu!
 
Maoni si yalikuwa ni maoni tu? Kwani sheria ilisema maoni ni lazima yakubaliwe? Hata kama maoni yalitolewa na watu wengi sheria haisemi maoni hayo ni lazima yakubaliwe! Yalikuwa ni maoni tu na mapendekezo. Yanaweza kukataliwa...

very well,,,Naunga mkono
 
Wakipitisha katiba isiyokidhi viwango basi haitadumu itabadilishwa tena ndani ya miaka kumi.
Mimi hata ije rasimu ingine bora tu iweke mbele maslahi ya nchi na haki ya mtanzania mmojamoja ipatikane.

Mkuu rasimu ikitoka bungeni, lazima ipitishwe na kura za wananchi!
Wananchi wakiikataa, rasimu inarudi bungeni kwa mara ya pili, na hapo ikikataliwa tena na wananchi, TUNATUMIA KATIBA HII HII TUNAYOTUMIA SASA!
 
Mkuu sijakupata vyeka unaposema Bunge la Katiba na Bunge la siku zote yapo sawa kwa kuwa yanatunga sheria. Lakini pia unasema hili Maalum linatunga sheria ambayo inaitwa Katiba. Kama ndivyo na unaikubali dhana ya Constitutional supremacy na kwamba sheria yoyote itakayotungwa na chombo chochote itakuwa batili kama itakinzana na Katiba (ambayo imetungwa na bunge maalumu) basi ukuu huu wa katiba unaipa ukuu pia Bunge la Katiba dhidi ya Bunge pa kawaida.

Umenipata vyema. Nilikuwa nakumbusha tu ukuu wa bunge lolote kutunga sheria, dhidi ya chombo chochote ambacho si bunge. Warioba naTume ya Katiba wanataka ukuu huo usiwepo. Lakini wazo kuwa bunge la aina moja ni juu ya lingine si lazima kimantiki, kinadharia na ki-uzoefu. Muhimu ni ukuu wa baraza la kutunga sheria. Naongezea kuwa ukuu wa Katiba unaozungumzwa mara nyingi haufikii ukuu wa Bunge. Ndiyo maana Waingereza hawautambui. Badala yake wanatambua parliamentary supremacy, lakini huu uwe mjadala mwingine.
 
Hatua tuliyofikia ni

1:CCM wapitishe Rasimu yao kinyume na matakwa ya umma

2:Tusiwe na katiba mpya- Hii ni kwa sababu wanajua wakipitisha rasimu yao ni ama ikubaliwe au ikataliwe na hivyo tuendelee na katiba ya sasa


CCM hawataki katiba mpya sasa

Hiyo nö 2 ndio dhumuni la CCM, na logic yao ni kuendeleza muungano, but nakuhakikishia, wakifanya hivyo ndio wanaua Muungano na kusababisha machafuko ya kisiasa, kuna roho za Watz zitapotea kwa ujinga wao!
 
Mkuu rasimu ikitoka bungeni, lazima ipitishwe na kura za wananchi!
Wananchi wakiikataa, rasimu inarudi bungeni kwa mara ya pili, na hapo ikikataliwa tena na wananchi, TUNATUMIA KATIBA HII HII TUNAYOTUMIA SASA!

Wewe kwa mawazo yako unaona watanzania wana ujasiri kweli wa kupiga kura ya hapana? inshort imekula kwetu.
 
Maoni si yalikuwa ni maoni tu? Kwani sheria ilisema maoni ni lazima yakubaliwe? Hata kama maoni yalitolewa na watu wengi sheria haisemi maoni hayo ni lazima yakubaliwe! Yalikuwa ni maoni tu na mapendekezo. Yanaweza kukataliwa...

Kwaiyo zile billioni zilizotumika pale, kazi bure?
 
Wewe kwa mawazo yako unaona watanzania wana ujasiri kweli wa kupiga kura ya hapana? inshort imekula kwetu.

Mkuu kuna sintofahamu hapo mbele yetu! Kwa sababu Wazenji watapiga kura kivyao na wa Tz bara watapiga kura kivyao!
Just imagine Tz bara wamekubali wakati Zbar wamekataa!
...
Kwa mawazo yangu, ikipitishwa serikali mbili, ni lazima itapingwa na wananchi, na kwa mawazo yangu, naskia kaharufu kadamu kwa mbaaali!
 
I am trying to make sense of what you wrote, but I am not getting it. What exactly did you want to say?

Muhimu ni kuwa sheria, ikiwemo Katiba, hutungwa na baraza la kutunga sheria, liwe kwa muundo na jina lolote lile. Tume au serikali au chombo kingine hupendekeza tu sheria iweje. Ndiyo maana katika mjadala wa Shivji na Warioba nilisema Shivji yuko sahihi.
 
Hili limesemwa na wengine na limesemwa vizuri na Prof. Shivji kwamba Bunge la Katiba lina madaraka ya kuweza kufutilia mbali rasimu ya Katiba ya Tume ya Warioba ambayo kimsingi ni mahali pa kuanzia tu siyo mwisho. Kuna watu wanasema ati Bunge liko kwa ajili ya Kuboresha sijui wamepata wapi mawazo hayo; hayako kwenye sheria ya Katiba Mpya! Sheria ile - ambayo wengine tuliikosoa toka mwanzo - imelipa Bunge uwezo wa kufutia, kuongeza na hata kubadili rasimu ya Katiba ambayo ililetwa kwao na TUme ya Katiba chini ya Jaji Warioba.

Kwa vile madaraka ya Tume hiyo yamekoma, chombo pekee chenye madaraka ya kuandaa rasimu ya Katiba ambayo italetwa kwa wananchi kuulizwa ni Bunge la Katiba. Bunge la Katiba halitaleta rasimu ya Jaji Warioba bali rasimu yao ambayo wameiandaa kutokana na rasimu ya Warioba. Kama wajumbe wengi wanakubaliana na rasimu ya Warioba basi kitakacholetwa kwa wananchi kitafanana sana na ile; lakini kinyume chake ni kuwa Watanzania wanaweza kupigia kura rasimu ya Katiba tofauti.

Well.. habari ndiyo hiyo...
Mzee Mwanakijiji, kwanza asante kwa hii!. Naomba nikiri sasa nimeanza tena kumuona Mzee Mwakijiji yulee niliyemfahamu wakati nilipojiunga JF!, yule Mzee Mwanakijiji wa KLH News!, Mzee Mwakijiji wa "Cheche za Fikra!", ndio huyu Mwanakijiji wa leo!, ambaye amekuja na ukweli halisi as it is, not as it ought to be!, no matter ni mchungu kiasi gani kumeza, kilichopakuliwa ndicho hiki, watu wameze, wateme ni shauri yao ukweli huu ndio utasimama!.

Nilipo waambia , [h=3]Katiba: CHADEMA mlikosea! Kubalini yaishe, Tusonge mbele![/h]ulinibeza sana humu! sasa unaelekea kuukubali ukweli huu mchungu!, na maandalizi ya kuukubali ule ukweli wangu mwingine mchungu kabisa kuwa 2015 ni CCM tena!, utafuatia!. Uzuri wa ukweli, huwa unasimama no matter what!.

Namalizia kwa ule ule msisitizo wangu kwenye ile mada tuliyobishana sana na Mkuu Mzee Mwanakijiji, kuwa "Japo Watanzania walitaka "Katiba Bora!", lakini kitakachopatikana kwa mchakato huu ni "Bora Katiba!" nikasema "maji ukiisha yavulia nguo!", kwa misingi ya "if you can't get what you want (Katiba Bora", then take what you get "Bora Katiba" kwa msingi wa na "moja shika sii kumi nenda rudi!", kuliko kukosa yote tukarudia katiba ya zamani, nikawasisitiza watu humu, tukubali matokeo na kwenye kura ya maoni, tuipigie kura ya ndio hii "Katiba Mpya!".


Pasco.
 
Umenipata vyema. Nilikuwa nakumbusha tu ukuu wa bunge lolote kutunga sheria, dhidi ya chombo chochote ambacho si bunge. Warioba naTume ya Katiba wanataka ukuu huo usiwepo. Lakini wazo kuwa bunge la aina moja ni juu ya lingine si lazima kimantiki, kinadharia na ki-uzoefu. Muhimu ni ukuu wa baraza la kutunga sheria. Naongezea kuwa ukuu wa Katiba unaozungumzwa mara nyingi haufikii ukuu wa Bunge. Ndiyo maana Waingereza hawautambui. Badala yake wanatambua parliamentary supremacy, lakini huu uwe mjadala mwingine.

Hapo sasa ndipo kuna tofauti kati ya sisi na waingereza japo system yetu ni ya Westminster. Waingereza ni kweli wao wanatambua Parliamentary Supremacy na mfumo wao wa kiserikali ni wa Kibunge kulinganisha na wa kwetu ambao ni wa Kijamhuri. Pia nadhani unafahamu kwamba composition ya Bunge lao ni tofauti na composition ya Bunge letu ama Mabunge yetu. Kwao wao mihimili yote mitatu inaingia Bungeni na ndio maana kwao Bunge linakuwa na ukuu.

Huku kwetu Katiba ndio kuu kwa kuwa pia ndio inazaa Bunge na mihimili mingine.

 
Maoni si yalikuwa ni maoni tu? Kwani sheria ilisema maoni ni lazima yakubaliwe? Hata kama maoni yalitolewa na watu wengi sheria haisemi maoni hayo ni lazima yakubaliwe! Yalikuwa ni maoni tu na mapendekezo. Yanaweza kukataliwa...

Maoni si yalikuwa maoni tu? Ina maana hayana maana? Ni nani mwenye madaraka ya kuyakubali au kuyakataa maoni?
 
Tukumbuke na tuzitafakari kwa mapana,marefu na kina zile billion 480 zilizotoweka ghafla hazina.1.Zimetowekaje? 2.kwanini zitoweke? 3.Ziko wapi kwa sasa? 4.Zinafanya kazi gani?.Siamini kama inawezekana hiki kinachotokea kuanzia sasa ni tume ya warioba Vs 480bil.Duuuh mara nikaamka tayari asubuhi.
 
Inawezekana mimi ndiye mwenye matatizo ya utambuzi au tuko wengi kwenye kapu hili.

Hivi inawezekanaje, watu wenye fikra angavu (sober mind), wakaitegemea CCM na serikali yake kutupa katiba yenye kukidhi matakwa ya wananchi? Hao CCM walikuwa wapi siku zote? Kwa nini hawakufanya hivyo mwaka 1992 wakati wa kuingia kwenye mfumo wa vyama vingi?

Najua kwa sababu watu walikuwa na mihemuko (frustrations), walikumbatia uamuzi na nia ya Kikwete bila kuangalia mambo katia uhalisia wake. Poor JK, atajivunia kitu gani katika uongozi wake wa nchi hii toka ukatibu wa chama dola, uwaziri na hadi kuwa Amiri Jeshi, endapo hata hili limemshinda? The doom for him is immesurable!

Toka mwanzo na hadi sasa naamini kuwa hakuna katiba mpya itakayoandaliwa chini ya CCM. Ila kutakuwa na mapambazuko mengine, tena makubwa sana kwani hizi pesa za walipa kodi na masihara waliyofanyiwa Watanzania lazima CCM wayalipie siku moja!
 
Hatua tuliyofikia ni

1:CCM wapitishe Rasimu yao kinyume na matakwa ya umma

2:Tusiwe na katiba mpya- Hii ni kwa sababu wanajua wakipitisha rasimu yao ni ama ikubaliwe au ikataliwe na hivyo tuendelee na katiba ya sasa


CCM hawataki katiba mpya sasa

Umma ndio CCM ni kitu usichoelewa mganga njaa wewe???????
 
Back
Top Bottom