Bunge la Katiba Haliko Kwa Ajili ya Kuboresha Rasimu ya Kina Warioba!

Bunge la Katiba Haliko Kwa Ajili ya Kuboresha Rasimu ya Kina Warioba!

Wapinzani wamefanya kila wanaloweza kufanya . Ninayaona mapinduzi halisi yakifanywa na wananchi wakiongozwa na Baraza la katiba, achilia mbali CDM.

Watanzania wa sasa si wskundanganya na pelemende.
 
Hili limesemwa na wengine na limesemwa vizuri na Prof. Shivji kwamba Bunge la Katiba lina madaraka ya kuweza kufutilia mbali rasimu ya Katiba ya Tume ya Warioba ambayo kimsingi ni mahali pa kuanzia tu siyo mwisho. Kuna watu wanasema ati Bunge liko kwa ajili ya Kuboresha sijui wamepata wapi mawazo hayo; hayako kwenye sheria ya Katiba Mpya! Sheria ile - ambayo wengine tuliikosoa toka mwanzo - imelipa Bunge uwezo wa kufutia, kuongeza na hata kubadili rasimu ya Katiba ambayo ililetwa kwao na TUme ya Katiba chini ya Jaji Warioba.

Kwa vile madaraka ya Tume hiyo yamekoma, chombo pekee chenye madaraka ya kuandaa rasimu ya Katiba ambayo italetwa kwa wananchi kuulizwa ni Bunge la Katiba. Bunge la Katiba halitaleta rasimu ya Jaji Warioba bali rasimu yao ambayo wameiandaa kutokana na rasimu ya Warioba. Kama wajumbe wengi wanakubaliana na rasimu ya Warioba basi kitakacholetwa kwa wananchi kitafanana sana na ile; lakini kinyume chake ni kuwa Watanzania wanaweza kupigia kura rasimu ya Katiba tofauti.

Well.. habari ndiyo hiyo...

Well ,kumbe wamevaa mamlaka makubwa kiasi kile; basi watumie mamlaka hayo ya kisheria kubadilisha kipengele cha serikali tatu katika Rasimu ya Warioba na waje na mpango mzima wa serukali moja!!
 
Basi kama ni hivyo hapakuwa na haja ya kuunda Tume ya Warioba,tungeanza na Bunge la Katiba moja kwa moja ili kuepuka gharama zisizokuwa za msingi. Kwa sababu kama Bunge la Katiba lina uwezoa pia wa kutengeneza rasimu tofauti kabia na ile ya Jaji Warioba, maana yake ni kwamab litakuwa ni Bunge la kutunga Katiba kulingana na linavyoona lenyewe. Rasimu a Warioba ndiyo imebeba mapendekezo ya watanzaina wote, Bunge la Katiba likitengeneza rasimu nyingine tofauti na ile ya Warioba, litakuwa limetengeneza rasimu isiyotana na maoni ya watanzania, sasa je, in case ikitokea hivi kutakuwa kulikuwa na hjaa gani ya kuwa na tume ya Warioba?


Hoja yako unaweza kuigeuza upande wa pili vile vile; kama Bunge la Katiba halina uwezo ambalo naamini linalo - kwa mujibu wa sheria na mantiki - basi mapendekezo ya TUme ya Warioba yangekuwa ya mwisho na watu wangeenda kwenye kura ya maoni moja kwa moja. Ndio maana kilichotolewa na Warioba ni mapendekezo tu na mambo mengine ambayo yamo kwenye rasimu hayakutoka kabisa kwa wananchi yametoka kwa tume yenyewe! Bunge ndilo sasa lina wajibu wa kupima mapendekezo hayo na kuona kama watanzania wengi wanakubaliana nalo - wao wakiwa ni wawakilishi wa Watanzania hao.

Angalau kinadharia.
 
moja ya sifa KUU ya bunge maalum la katiba lazima liwe na full sovereignty ya kufanya chochote juu ya katiba mpya..tofaut na hapo halitakuwa na sifa ya kuitwa bunge maalum la katiba.Kama kunaframework nyingine inayohinder sovereignty ya bunge maalum bas hilo sio bunge maalum la katiba. kutokana na mantiki hiyo upo uwezekanao wa hata baadhi ya wajumbe kutosoma rasimu ya 'warioba' na bado mawazo yake yakaheshimiwa.
 
Nchi yenye watu masikini wa akili. Nadhani haya mambo tusiwe tunayasema tena hadharani. Tunachekwa...
 
Na ikiwa itatokea watafanya kubadili maoni ya rasimu ya katiba kutoka kwenye tume ya Warioba ambayo yametokana na wananchi halafu wakaweka madudu yasiyo na chembe ya utaifa bali vyama vyao kwenye kura ya maoni lazima tuiteme, NI HERI KUWA NA PENGO KULIKO KUWA NA JINO BOVU LITAKALOKUSUMBUA USIKU NA MCHANA KWA MAUMIVU

WAHEED SUDAY;
Laiti kiu yako ingekuwa kwa wengi, mambo mbona yangenyooshwa tu? Angalia magharama yoote waliotumia kuiandaa, angalia hasara zoote tunazoendelea kuzipata. Mwisho wa siku waje na mawazo ya vyama vyao kama kwamba mawazo yao ndo sahihi kuliko wengine.
Tatizo ni pale wanapowaletea sasa wananchi na lugha yao ya kisiasa kuwa lichama letu limeamua hivi, wananchi nao wanasema zidumu fikra sahihi za m/kiti wetu.
HOYEEEEEEE. Zipite hizo fikraaaaa. Itaitwa Katiba mpya kwisha. Jamani, Tanganyika yangu iko wapi? Natamani hao Wazenj wakomae na utaifa wao na MAMLAKA KAMILI. Nitaona hao Watanganyika watakavyo tuambia sisi kuwa wamempa nani ile nchi yetu. Muungano ni baina ya nchi 2 au zaidi, iweje huu wetu uwe kati ya nchi moja na hewa?
Wabunge waheshimiwa, fanyeni mfanyavyo lakini kumbukeni huku nako kuna watu wenye akili. Hamkuchaguliwa, mliteuliwa kwa sababu anazozijua yeye aliye wateua. Zikiwa nzuri itapendeza
 
Wazo hili ndilo lilikuwepo tangia mwanzo, kuwa mtawala ambaye amekuwa akikumbushwa mara zote kusimamia na kufuata katiba iliyopo huku akipuuza hawezi hata siku moja kuanzisha mfumo wa kuzirekebisha sheria zile zile ili zimbane yeye.
Wanaodhani kuwa hili linawezekana wakumbuke kuwa katiba mpya lilikuwa wazo la wapinzani na watawala walilidandia. Kutokana na nia yao kutokuwa halisi (sincerely) ndio maana limezungukwa na usanii ili 'lionekane limefanyika'.
Kinachoendelea hadi sasa ni ushahidi wa MMK kuwa mawazo feki yalizaa mchakato feki ambao umepelekea sheria feki, bunge feki (kama alivyoliita Mtikila) na mwisho itakuwa product feki.


Pia usisau wapinzania wanaona kundelea kwa katiba ya sasa mbali ya mapunufu yake inwanyima nafasi yakushika dola,na hilo ndilo linalowavuta katika mchakato mzma huu.
 
Hayawi hayawi, sasa yamekuwa...Watanzania kama hatutachukua tahadhari mapema, tumeliwa! Huu ni mwanzo tu na bado; CCM haina nia wala sababu ya kuheshimu maoni ya Watanzania walio wengi kama yalivyoanishwa kwenye rasimu ya Katiba mpya. Muundo wa Bunge la Katiba pekee unaonesha taswira ya wapi CCM inataka kutupeleka kuhusu upatikanaji wa katiba itakayokidhi matakwa ya wananchi bila kujali itikadi, dini, jinsia, rangi wala uwezo wa mali. Toka mapema walianza kujitokeza watu wa ajabu ajabu na kuanza kuhoji wakibeza ripoti ya Tume ya Katiba wakimlenga Mwenyekiti wake Jaji Joseph Sinde Warioba. Wengine pamoja na kushangaa tulijiuliza ni wapi wana CCM hawa walikuwa wanapata ujasiri huo wa kumrushia madongo kada wao, Waziri Mkuu Mstaafu na mteuliwa wa Mwenyekiti wa chama tawala CCM!
October said:
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi CCM Abdallah Bulembo amemshambulia kwa maneno makali Mwenyekiti wa Tume ya Katiba Jaji Joseph Warioba. Akihutubia mkutano wa CCM Tanga Bulembo amesema Warioba hana haki wala mamlaka ya kuwasemea Watanzania kuhusu Katiba mpya.

Bulembo ambaye pia ni mjumbe wa Kamati Kuu CCM amesema Warioba anapaswa kukaa mbali na kuwaamulia Watanzania Katiba aitakayo yeye. Huku akisisitiza kupinga kinachofanywa na Warioba aliwauliza wananchi kwa msisitizo..'Kwani Warioba ni Nani?' ....

Na kama vile hiyo haikutosha...
Januari said:
MBUNGE wa Kwimba (CCM), Shanif Mansoor, ameishambulia Tume ya Mabadiliko ya Katiba inayoongozwa na Jaji mstaafu, Joseph Warioba. Akizungumza jimboni kwake juzi alipokutana na wazee na waganga wa tiba za asili katika Kata ya Mankulwe, alimtaka Warioba na wenzake kuacha mara moja kuwa wapiga debe katika vyombo vya habari kuhusu Serikali tatu.
Bado nakumbuka msimamo wa serikali ya CCM toka mwanzo kabisa...Alianza Waziri wa Sheria na Katiba wakati huo, Celina Kombaine, akafuatia Mwanasheria mkuu wa Serikali Jaji Fredrick Werema, akafuatia Waziri Mpya wa Sheria na Katiba Mathias Chikawe na viongozi wengine wa Chama na serikali, wote wakidai hakuna umuhimu wa katiba mpya. Sasa lazima sote tujiulize na kujitafakari saana tu ndugu zangu, je kweli uongozi wa CCM uko tayari kuukubali rasimu hii kama ilivyotolewa na Tume ya Katiba? Jibu ni hapana. Mpango wote huu mpaka sasa ni kama danganya toto ila kuna kitu wanasahau; Tanzania ya sasa ni kitu kingine kabisa! Somebody is in for a rude shock!

Now enter Mwanazuoni na Mwanasheria nguli Profesa Issa Shivji! Shivji hakuachwa kwenye Bunge la Katiba kwa bahati mbaya, hapana; Shivji, muumini wa serikali mbili, ama aliachwa makusudi ili wakati muafaka ukifika CCM imtumie kulivuruga Bunge hilo kwa kupinga mapendekezo ya tume au hizi tetesi za kuwepo Katiba mbadala iliyoandaliwa na kikundi kisichojulikana (chini ya Shivji?) huenda ikawa kweli. Hivi sasa kuna juhudi kubwa zinazofanyika kuonesha mapungufu ya rasimu kama ilivyotolewa na Tume na kama asemavyo Mzee Mwanakijiji, si ajabu rasimu itakayofikishwa kwa wananchi ikawa tofauti kabisa na ya tume. Je Shivji naye kanunuliwa? Yangu macho.
 
Hili limesemwa na wengine na limesemwa vizuri na Prof. Shivji kwamba Bunge la Katiba lina madaraka ya kuweza kufutilia mbali rasimu ya Katiba ya Tume ya Warioba ambayo kimsingi ni mahali pa kuanzia tu siyo mwisho. Kuna watu wanasema ati Bunge liko kwa ajili ya Kuboresha sijui wamepata wapi mawazo hayo; hayako kwenye sheria ya Katiba Mpya! Sheria ile - ambayo wengine tuliikosoa toka mwanzo - imelipa Bunge uwezo wa kufutia, kuongeza na hata kubadili rasimu ya Katiba ambayo ililetwa kwao na TUme ya Katiba chini ya Jaji Warioba.

Kwa vile madaraka ya Tume hiyo yamekoma, chombo pekee chenye madaraka ya kuandaa rasimu ya Katiba ambayo italetwa kwa wananchi kuulizwa ni Bunge la Katiba. Bunge la Katiba halitaleta rasimu ya Jaji Warioba bali rasimu yao ambayo wameiandaa kutokana na rasimu ya Warioba. Kama wajumbe wengi wanakubaliana na rasimu ya Warioba basi kitakacholetwa kwa wananchi kitafanana sana na ile; lakini kinyume chake ni kuwa Watanzania wanaweza kupigia kura rasimu ya Katiba tofauti.

Well.. habari ndiyo hiyo...

Ndg. Mwanakijiji,

Mimi si Mwanasheria lakini ni msomaji mzuri na makini wa nyaraka mbalimbali. Mzee Shivji na wewe mko sahihi sana. Sitaki kuchangia huko, ila nataka kuweka sawa jambo moja kidogo hapo kwenye post yako, kwamba; Bunge la Katiba halitozalisha 'Rasimu ya Katiba' tena, bali kwa mujibu wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, Sura ya 83 ya Sheria za JMT ya Mwaka 2013, kifungu cha 25 (1), Bunge la Katiba litazalisha kitu kingine kabisa kinachoitwa 'Katiba inayopendekezwa'. Hii si lazima ifanane na ile ya Jaji Warioba na wenzake, hii ni zao la mijadala na maridhiano na hatimaye maazimio ya Bunge hili. Na hii ndiyo itapata uhalali wake kutoka kwa wananchi kupitia kura zao za ndiyo ama hapana. Kura zitapigwa kwa mujibu wa utaratibu unaopewa masharti na sheria ya kura za maoni ya mwaka 2013.

Wakatabahu,
HK.
 
Well ,kumbe wamevaa mamlaka makubwa kiasi kile; basi watumie mamlaka hayo ya kisheria kubadilisha kipengele cha serikali tatu katika Rasimu ya Warioba na waje na mpango mzima wa serukali moja!!

Pole sana. Serikali moja imefungwa na sheria. Huwezi kuijadili. Na ni kwa sababu moja tu. Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar lazima iwepo kwenye picha!
 
Ndg. Mwanakijiji,

Mimi si Mwanasheria lakini ni msomaji mzuri na makini wa nyaraka mbalimbali. Mzee Shivji na wewe mko sahihi sana. Sitaki kuchangia huko, ila nataka kuweka sawa jambo moja kidogo hapo kwenye post yako, kwamba; Bunge la Katiba halitozalisha 'Rasimu ya Katiba' tena, bali kwa mujibu wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, Sura ya 83 ya Sheria za JMT ya Mwaka 2013, kifungu cha 25 (1), Bunge la Katiba litazalisha kitu kingine kabisa kinachoitwa 'Katiba inayopendekezwa'. Hii si lazima ifanane na ile ya Jaji Warioba na wenzake, hii ni zao la mijadala na maridhiano na hatimaye maazimio ya Bunge hili. Na hii ndiyo itapata uhalali wake kutoka kwa wananchi kupitia kura zao za ndiyo ama hapana. Kura zitapigwa kwa mujibu wa utaratibu unaopewa masharti na sheria ya kura za maoni ya mwaka 2013.

Wakatabahu,
HK.
Mheshimiwa kabisa HKigwangalla, naomba nikuulize tuswali tuwili;

  1. Nini mawazo yako kuhusiana na muundo wa hili Bunge la Katiba?
  2. Kwa uzoefu wako una imani na matokeo ya hiyo kura katika mazingira tuliyo nayo?
Pole sana. Serikali moja imefungwa na sheria. Huwezi kuijadili. Na ni kwa sababu moja tu. Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar lazima iwepo kwenye picha!
Kumbe tunajadili katiba mpya huku tumefungwa pingu; nilidhani Katiba ndiyo sheria mama!
Natanguliza shukhrani.
 
Basi kama ni hivyo hapakuwa na haja ya kuunda Tume ya Warioba,tungeanza na Bunge la Katiba moja kwa moja ili kuepuka gharama zisizokuwa za msingi. Kwa sababu kama Bunge la Katiba lina uwezoa pia wa kutengeneza rasimu tofauti kabia na ile ya Jaji Warioba, maana yake ni kwamab litakuwa ni Bunge la kutunga Katiba kulingana na linavyoona lenyewe. Rasimu a Warioba ndiyo imebeba mapendekezo ya watanzaina wote, Bunge la Katiba likitengeneza rasimu nyingine tofauti na ile ya Warioba, litakuwa limetengeneza rasimu isiyotana na maoni ya watanzania, sasa je, in case ikitokea hivi kutakuwa kulikuwa na hjaa gani ya kuwa na tume ya Warioba?

Tume ya Warioba ilikuwa ni usanii na usanii huo unaanza kujidhihirisha taratibu.

Kwa kawaida Katiba huwa inatengenezwa na Bunge la Katiba lililochaguliwa na wananchi directly.

Rasimu ya Warioba haijabeba mapendekezo ya Watanzaina wote. Tume yenyewe was not the representative of the people.

Pia inavyoonekena Watanzania wengi, aidha kwa kutokuwa na elimu ya uraia, hawajui hata maana ya Bunge la Katiba.

Kwa kawaida wajumbe wa Bunge la Katiba hawateuliwi. Pia wabunge wa bunge la kawaida hawawezi kuwa converted automatically kuwa wajumbe wa Bunge la Katiba.

The so called "Bunge la Katiba" linaloendelea huko Dodoma halipo pale kwa ajili ya kupitisha rasimu ya Warioba.

Rather, it is there to merely rubber-stamp the decisions of the ruling party.
 
Naona unajichanganya tuu. Unasema

Mzee Shivji na wewe mko sahihi sana.

Hoja kuu ya Prof. Shviji ni kuwa Bunge la Katiba lina madaraka kuliko Bunge la kawaida. Hata hivyo, pamoja na kukubaliana nae unajichanganya kwa kuandika

Serikali moja imefungwa na sheria. Huwezi kuijadili. Na ni kwa sababu moja tu. Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar lazima iwepo kwenye picha!

Sasa kama unakubalina na Prof. kuwa Bunge la Katiba lina madaraka kuliko Bunge la kawaida inakuaje Bunge la Katiba kuwa bounded na sheria iliyotungwa na Bunge la kawaida?

Kati ya Bunge la Katiba na Bunge la Kawaida, which is one is superior to the other?

Bunge la katiba linatakiwa kuwa na unlimited power ya kuamua nini kiwepo na nini kisiwemo kwenye Katiba.

Bunge la Katiba haliwezi kuwa bounded either na rasimu ya Warioba or sheria iliyopitishwa na Bunge la kawaida.

Ndiyo maana wachache tukasema the so called "Bunge la Katiba" is not in fact Bunge la Katiba linalotakiwa kwa sababu halijachaguliwa na wananchi na liko pale for the interests of a particular group. Ndiyo maana Bunge hilo limekatwa kilimilimi kuongelea serikali moja.
 
Hayo ni mawazo yako na Ben, lakini sio lazima wabunge ''kama unavyowaita wabunge wa CCM'' wapinge maoni yote ya Jaji Warioba, tusipende sana kuongea na kutabiri na kufikiri kwamba mna akili za kugundua mawazo na hisia za watu wengine, Ngoja tusubiri tuone! tatizo lako MM,Ben nk ni wanaharakati na sio wanasiasa............naamini baada ya Bunge tutakutana JF!

Watu wa hatari katika jamii yoyote inayojaribu kujenga demokrasia ni wale ambao wanasubiri vitu vitokee ndio waanze kufikiria!
 
Mwanakijiji, naomba tafsiri ya kifungu cha 25(2) cha sheria ya mabadiliko ya katiba.

Tuangalie kifungu chote hicho cha 25:

25.-(1) Bunge Maalum litakuwa na mamlaka ya kujadili na kupitisha masharti ya katiba inayopendekezwa, kutunga masharti ya mpito na masharti yatokanayo kama Bunge Maalum litakavyoona inafaa.
(2) Mamlaka ya Bunge Maalum ya kupitisha masharti ya Katiba inayopendekezwa yatatekelezwa baada ya Rasimu ya Katiba kuwasilishwa na Mwenyekiti wa Tume na kupitishwa na Bunge Maalum.

Kifungu hicho cha pili kinaelezea mamlaka yanayotajwa kwenye kifungu cha kwanza; kwamba mamlaka hayo ya kifungu cha kwanza yataanza kutekelezwa baada ya tume kuwasilisha rasimu yake. Kimsingi, Bunge la Katiba lisingeweza kuanza kazi yake ya kifungu cha kwanza kama TUme ya Warioba isingewasilisha rasimu.

Kifungu cha pili hakina maana Bunge kazi ya ni kupitisha rasimu kama ilivyo.
 
Well ,kumbe wamevaa mamlaka makubwa kiasi kile; basi watumie mamlaka hayo ya kisheria kubadilisha kipengele cha serikali tatu katika Rasimu ya Warioba na waje na mpango mzima wa serukali moja!!

Hili wanaweza kabisa; ila kama ilivyotokea huko nyuma wengi wa wajumbe wanaiogopa Zanzibar. Ukisema serikali "moja" jibu lao litaanzia na "Zanzibar..."
 
Pole sana. Serikali moja imefungwa na sheria. Huwezi kuijadili. Na ni kwa sababu moja tu. Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar lazima iwepo kwenye picha!

HK, hili si sahihi; hata kwenye Serikali Moja bado Zanzibar inaweza kuwa na serikali yake... kama vile inavyowezekana tukaanzisha serikali za Kanda au za mahali fulani. Tatizo sasa hivi tumetengeneza kitu kisicho na mantiki kabisa; Katiba ya JMT inasema Tanzania ni Nchi Moja halafu Katiba ya Zanzibar nayo inasema "Zanzibar ni Nchi"! Na JK akatauambia Zanzibar "ni nchi ndani ya nchi"! the epitome of absurdity!

Suala la "Serikali Tatu" kwa baadhi ya watu wanaona ni suluhisho lakini nitajaribu kuonesha in few days - inshaallah, kile ninachokiita "Tatizo la Serikali Tatu"... ni zaidi ya gharama.
 
Ndg. Mwanakijiji,

ila nataka kuweka sawa jambo moja kidogo hapo kwenye post yako, kwamba; Bunge la Katiba halitozalisha 'Rasimu ya Katiba' tena, bali kwa mujibu wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, Sura ya 83 ya Sheria za JMT ya Mwaka 2013, kifungu cha 25 (1), Bunge la Katiba litazalisha kitu kingine kabisa kinachoitwa 'Katiba inayopendekezwa'.
HK.

I stand corrected.
 
Kwa kawaida wajumbe wa Bunge la Katiba hawateuliwi. Pia wabunge wa bunge la kawaida hawawezi kuwa converted automatically kuwa wajumbe wa Bunge la Katiba.

The so called "Bunge la Katiba" linaloendelea huko Dodoma halipo pale kwa ajili ya kupitisha rasimu ya Warioba.

Rather, it is there to merely rubber-stamp the decisions of the ruling party.

right on! right on!
 
  • Thanks
Reactions: EMT
Back
Top Bottom