Bunge lajadili juu ya adhabu ya Mbunge Luhaga Mpina. Laamua kumfungia vikao 15

Bunge lajadili juu ya adhabu ya Mbunge Luhaga Mpina. Laamua kumfungia vikao 15

baada ya kuadhibiwa inavyostahili na bunge kwa mujibu wa kanuni za bunge, na baadae adhabu kali sana ya ccm,

naungana na hoja muhimu na ya maana sana, aliyoitoa kaka yangu ninae muheshimu sana comrade Dr.Kasheku Msukuma mbunge wa jimbo la Geita, kwamba vyombo vya ulinzi na usalama vianzishe uchunguzi zaidi wa kina, kuona kama kuna wahusika wengine zaidi juu ya uzushi na uongo wa tuhuma hizi, alizobuni Mh.Mpina dhidi ya waandamizi wa serikali hususani Mh.Husen Bashe, waziri wa kilimo... :pulpTRAVOLTA:

hadi anaona aibu,
muongo na mzushi yupo mwenyewe tu :pedroP:
Kila mtu anataka uwaziri.
 
Bunge kibogoyo lisilo na faida yeyote.wazalendo wakihoji bunge kibogoyo linachukia.
Nilipomsikia supika akisema mimi ni mtu ninayeheshimika sana duniani hivyo mtu hawezi kuniletea dharau!! Nikajua hapa tayari kinachofuata ni mtu kuliwa kichwa tuu!! Tayari maamuzi yalishapita.
 
baada ya kuadhibiwa inavyostahili na bunge kwa mujibu wa kanuni za bunge, na baadae adhabu kali sana ya ccm,

naungana na hoja muhimu na ya maana sana, aliyoitoa kaka yangu ninae muheshimu sana comrade Dr.Kasheku Msukuma mbunge wa jimbo la Geita, kwamba vyombo vya ulinzi na usalama vianzishe uchunguzi zaidi wa kina, kuona kama kuna wahusika wengine zaidi juu ya uzushi na uongo wa tuhuma hizi, alizobuni Mh.Mpina dhidi ya waandamizi wa serikali hususani Mh.Husen Bashe, waziri wa kilimo... :pulpTRAVOLTA:

hadi anaona aibu,
muongo na mzushi yupo mwenyewe tu :pedroP:
Wajinga mpo wengi sana, huyo Musukuma zile za DPW ziliisha au bado anaendelea kuzitumia?

Hiyo kamati haijajibu hoja yoyote ya Mpina, imejibu utoto mtupu. Badala iundwe kamati ya kuchunguza ufiasadi wa Bashe na mama Abdul, wajinga wanamuundia kamati Mpina!.

Huyo Musukuma atakuwa ameshapangwa awe wa kwanza kuongea baada kuvuta mpunga wake, mfano takataka zilizojaa bungeni.
 
Wabunge week ijayo wanamtukana Bashe

Mafisadi yamejipanga kweli. Yanateteana kama ilivyotarajiwa. Uzuri ni kwamba uhuni wa wabunge hawa wevi wa kura hauwezi kubadilisha mtazamo dhidi ya hawa yao. Haya ndiyo majitu yaliyouza na bandari zetu. Hawa ni maadui namba 1 wa Taifa.

Jongera Mpina, wananchi wamekuelewa. Ulifanya vizuri sana kuongea na vyombo vya habari ili wananchi waujue vizuri iharamia wa hawa mafisadi.
 
Nilipomsikia supika akisema mimi ni mtu ninayeheshimika sana duniani hivyo mtu hawezi kuniletea dharau!! Nikajua hapa tayari kinachofuata ni mtu kuliwa kichwa tuu!! Tayari maamuzi yalishapita.
anasema mbele ya maitiza Taifa hili, hili ni taifa mfu
 
Unafiki gani, umethibitishwaje, je hoja zake zimejibiwa? Mtuhumiwa kajitetea? Iweje ahukumiwe?
Kweli nchi ya ajabu sana hii...Watu wote wanasema uwongo hadharani...Gwajima umenisikitisha sana...Unalitukana jina la Mungu, acheni unafiki nyie watu
 
Aseee nchi ngumu saana hii, yaani anayepambania wananchi anasulubiwa! Aseeeee!
Ndugu yangu haya majitu ya ccm yamevimbiwa madaraka! Haya ma mantu yamechepusha mpaka madaraka ya rais kwamba yana uwezo wa kufanya jambo lolote na yasi shitakike! Na sisi tumekuwa kama maiti tu hatuwezi hoji chochote tupo kimya tu! Tulichobakiwa nacho ni kuandika hivi tu! Yani maandishi yetu kwao wanaota kama vile ndoto za mizimu ambazo kuna za kutisha na nyingine za kufurahisha kama maandish ya kina lucas mwamshambwa sijui! Nayakumbuka maneno ya jomo kenyata aliwah kusema yeye anaongoza wagonjwa mahututi ipo siku watapata nafuu watainuka kuhoji kenya yao ila kuna mwenzake jiran anaongoza maiti lini zitaamka zihoji kuhusu nchi yao?
 
Tulisema humu,mpina anasumbuliwa na chuki binafsi dhidi ya bashe hana vithibitisho vyovyote,leo yametimia,naomba achukuliwe hatua kali sana ili iwe funzo kwa wapuuzi wengine kama yeye
 
Awamu ya kutetea mafisadi.

Kusambaza habari ni swala la hatari zaidi kwa watanzania kuliko kuuwa viwanda vya ndani na kulisha watu sukari isiyopitia TBS?
Tatizo sio awamu, tatizo ni Maiti za hii nchi, ni kosa sana kutetea maiti
 
Kweli nchi ya ajabu sana hii...Watu wote wanasema uwongo hadharani...Gwajima umenisikitisha sana...Unalitukana jina la Mungu, acheni unafiki nyie watu
Wanasiasa nchi hii wanatutusi hadharani ni matusi makubwasana kwetu haya.
 
Kwa mujibu wa Kanuni ya # Bunge 84 (3) (a) za mwaka 2023 amekutwa na hatia na Kamati ya Hadhi na Madaraka ya Bunge.

Tuendelee kufuatilia bunge
≈=====================

"Mheshimiwa Luhaga Mpina (Mbunge wa Kisesa) alimtuhumu Mheshimiwa Waziri (Hussein Bashe, Waziri wa Kilimo) kuwa amelidanganya Bunge kwa kusema wamebadili kanuni za Nation Food Reserve Agency (NFRA) kuruhusu NFRA kuwa na mandate ya kuingiza sukari wakati hakuna tangazo la serikali lililotangazwa kuipa NFRA mandate ya kuingiza sukari, Waziri (Hussein Bashe, Waziri wa Kilimo) aliieleza kamati kuwa walitumia sheria ya usalama wa chakula sura ya 249 kukabiliana na uhaba wakati wa dharura kupitia NFRA ambapo alisema kuwa wameanza mchakato wa kubadilisha sheria ili NFRA waruhusiwe kuagiza, kuhifadhi na kusambaza sukari hata kwa kipindi kisicho cha dharura na mchakato huo ulianza kwa kutoa tangazo serikalini namba 225 (b) la tarehe 01 Aprili 2024" -Makoa

"Kamati ilipitia kifungu cha 14 cha sheria ya tasnia ya sukari kuhusu wanaoruhusiwa kuingiza sukari na kupitia kifungu cha 15 cha sheria ya usalama wa chakula ya mwaka 1991 na kubaini kuwa wakati wa dharura kama ilivyojitokeza sheria ya usalama wa chakula inakuwa na nguvu zaidi kuliko sheria ya tasnia ya sukari" -Makoa

"Kamati ilipata nafasi ya kujiridhisha kuhusu GN namba 25 (b) ya tarehe 01 Aprili 2024 na kupitia muswada wa sheria ya fedha iliona mapendekezo ya marekebisho yaliyoelezwa na Waziri kupitia kumbukumbu za Bunge na maelezo ya Waziri kamati ilikuwa na maoni kuwa hakuna uwongo uliozungumzwa na kwamba hakuna ukiukwaji wowote wa sheria uliofanywa" -Makoa

Ni sehemu ya maelezo ya Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Haki, maadili na madaraka ya Bunge Ally Makoa akiwasilisha Bungeni kuhusu tuhuma zilizotolewa na Mbunge wa Kisesa (CCM) Luhaga Mpina dhidi ya Waziri wa Kilimo Hussein Bashe
View attachment 3024970
Daah kweli nchi imeingiliwa!
 
Back
Top Bottom